Waafrika tulipotoshwa kuhusu Chifu Mangungo wa Msovero sio mjinga, Watanzania tuiombe familia yake msamaha na tumuenzi kama shujaa wa uwekezaji

Kwahiyo nawewe unaamini sasaihivi tupo huru?
 
Mkuu, umetuliza akili sana. Huwa najisikia amani sana nikikutana na mtu anayekwenda tofauti na kinachokubaliwa na wengi na bado akaweza kutengeneza hoja inayofikirisha.
 
Sawa, nimekupata. Nilitaka nipate uhakika wa hili. Okay poa mjadala uendelee...
 
Mkuu kuhusu mkata wa mangungo kuchukuliwa Tanganyika yote sio kweli
Naomba niseme hivi

1 mkuu si kweli kwamba mkataba wa mangungo na Peter ndio uliowawezesha kuitawa Tanganyika yote.
2 Mangungo alitoa eneo lake tu na machifu wengine walitoa maeneo yao kwa ridhaa yao na kwa mikataba yao ipo pia kama chifu wa uzingua huko alikopita bwana Peter katika milima ya usambara.
4 Mkataba wa Pita na Mangungo unatumika kama mfano tu ingawa alisainisha machifu wengi kiasi cha kurudi ujerumani na furushi la mikataba.
5 Ndio maana machifu wasio kubali vita ilipiganwa kama Iringa kwa chifu Mkwawa
6 Binafsi siamini kama Mangungo kasaini kitu asichokijua kwasabu hii pia
Kabla kufika Msovero bwana Pita alikuwa masomoni Londoni huko alijifunza pia kingereza. Wakati anafika msovero alifikia Zanzibar ambapo ndipo alipompata mkalimani huyo. Uwezekano wa bwana Ramadhani kujua kiswahi upo kutokana na uwepo wa ushahid wa kimaandishi kuonesha Zanzibar walianza kuongea kiswali tangu karne nyingi nyuma.
Pia uwezekano wa ramadhani kujua kingereza upo kutokana na kisiwa hiko kuwa na uthibitisho wa kutembelewa a watu wa mmataifa mbalimbali.
Hivyo kwa hoja hizi najiridhisha kusema bwana Ramazani alifaham kingereza kutoka kwa Pita na kumtafsiria Mangungo kwa kiswahili.
Na hili linaweza kuwa ndio sababu pita na rafiki yake kufikia Zanzibarkwanza kabla kuja bala kwa kigezo cha lugha.
 
Asante sana kwa ufafanuzi Mkuu. Mbona mikataba ya hizo chiefdoms nyingine haizungumziwi kama ule wa Sultan Mangungo? What was so special with it?
 
Mkuu, umetuliza akili sana. Huwa najisikia amani sana nikikutana na mtu anayekwenda tofauti na kinachokubaliwa na wengi na bado akaweza kutengeneza hoja inayofikirisha.
Ahsante mkuu na twendele kujadili
 
Mangungo offers all his territory with all its civil appurtenances to Dr. Karl Peters, as the representative of the Society for German Colonization, for the exclusive and universal utilization for German colonization.
Nisaidie kuuona huo ushujaa hapa!
 
Mkuu ulishawaisikia mjerumani anamponda Hittler popote pale?
Bila Hittler Ujerumani ingekuwa shithole kabisaaa
Kosa lake ni ubabe wa kipumbavu ukiwa mbabe huwezi kuwa na akili.Angeacha kuvamia mataifa mengine asingepigwa
 
Hakuna tofauti kubwa Kati ya wakoloni na wawekezaji wa sasa, kama unaruhusu wawekezaji toka nje means tulikurupuka kudai UHURU
 
Kwa miaka mingi sana chifu mangungo ameendelea kuonekana kama mfano wa kiongozi mjinga hasa pale linapotokea swala la mikataba. Lakini je Mangungo alikuwa mjinga kweli?
Alikuwa mjinga hujui kusoma wala kuandika unakubali kuingia mikataba ya kijinga
 
Mkataba wa Mangungo na Carl ni Bora mara elfu kuliko ule wa serikali ya JK na Wachina kwenye gesi ya asili.

Nje ya mada: mapato ya muvi ya "Royal Tour " yamefika dola ngapi kule Amazon? au wabongo kwa usahaulifu tumeishasahau kuhusu hii sinema?
 
Alikuwa mjinga hujui kusoma wala kuandika unakubali kuingia mikataba ya kijinga
Alikuwa na mkalimani wake aliyemsomea,achana na somo la historia lina upotoshi mwingi Sana kwa interest za kina Nyerere na wapigania UHURU wengine waliandika zaidi kuhusu negative
 
Kwa miaka mingi sana chifu mangungo ameendelea kuonekana kama mfano wa kiongozi mjinga hasa pale linapotokea swala la mikataba. Lakini je Mangungo alikuwa mjinga kweli?
Na swali jingine ni hili: Hawa "wasomi" wetu wanaosaini mamikataba haya mabovu na kuuza madini, gesi na wanyama wetu kwa wazungu nao ni akina Mangungo? Hawajui kusoma na kuandika kama Mangungo?
 
Alikuwa na mkalimani wake aliyemsomea,achana na somo la historia lina upotoshi mwingi Sana kwa interest za kina Nyerere na wapigania UHURU wengine waliandika zaidi kuhusu negative
Huyo mkalimqni alisoma wapi kijerumani? Mgeni au mwenyeji? Hapa ndipo tu narudi kule kule alisomeshwa tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…