Waafrika tulipotoshwa kuhusu Chifu Mangungo wa Msovero sio mjinga, Watanzania tuiombe familia yake msamaha na tumuenzi kama shujaa wa uwekezaji

Waafrika tulipotoshwa kuhusu Chifu Mangungo wa Msovero sio mjinga, Watanzania tuiombe familia yake msamaha na tumuenzi kama shujaa wa uwekezaji

Chifu mangungo hakuwa mjinga, watanzania tulipotoshwa, tunapaswa kuiomba familia yake msamaha

Kwa miaka mingi sana chifu mangungo ameendelea kuonekana kama mfano wa kiongozi mjinga hasa pale linapotokea swala la mikataba. Lakini je Mangungo alikuwa mjinga kweli?

Chifu mangungo ni nani?

Naomba ninukuu kidogo kipande cha historia fupi kuhusu chifu Mangungo kutoka katika uzi wa ndugu humu Jf KILABA

"Mangungo simultaneously for all his people and Dr. Peters for alt his present and future associates hereby concluded a treaty of Eternal Friendship.

Mangungo offers all his territory with all its civil appurtenances to Dr. Karl Peters, as the representative of the Society for German Colonization, for the exclusive and universal utilization for German colonization.

Dr. Karl Peters, in the name of the Society for German Colonization declares his willingness to take over the territory of the Sultan Mangungo with all rights for German Colonization subject to any existing suzerainty of Mwenyi Sagara.

In pursuance thereof, Sultan Mangungo hereby cedes all the territory of Msovero, belonging to him by inheritance or otherwise for all time, to Dr. Karl Peters, making over to him at the same time all his rights.

Dr. Karl Peters in the name of the Society for German Colonization undertakes to give special...attention to Msovero when colonizing Usagara.

This treaty has been communicated to the Sultan Mangungo by the interpreter Ramzan in a clear manner and has been signed by both sides, with the observation of the formalities valid in Usagara the Sultan on direct enquiry having declared that he was not in anyway dependent upon the Sultan of Zanzibar, and that he did not even know the existence of the latter.

Sgd. Dr. KARL PETERS
Sgd. MANGUNGO

This contract has been executed legally and made valid for all time before a great number of witnesses, we testify herewith:
Kwagakinga (mark);
Sultan Mangungo’s son of Golola (mark);
Sultan Mangungo’s second son of Draman (mark);
Graf Pfeil August Otto;
Mark of the intepreter Ramazan etc.
Dr. Karl Juhlke.
Msovero Usagara November 29, 1884.

Kwa tafsiri isiyo rasmi, kwa Kiswahili unasomeka hivi:
Mangungo, Sultan wa Msovero katika Mwenyisagara, na Dk. Karl Peters. Mangungo sambamba na watu wake wote na Dk. Peters kwa niaba yake na washirika wake wengine wajao kwa pamoja wanaweka mkataba wa Urafiki wa Kudumu.

Mangungo amekubali kutoa himaya yake yote pamoja na watu wake na hadhi yake kwa Dk. Karl Peters, kama mwakilishi wa Umoja wa Ukoloni wa Kijerumani (Society for German Colonization), kwa ajili ya matumizi ya moja kwa moja ya koloni la Kijerumani.

Dk. Karl Peters, kwa niaba ya jina la Umoja wa Ukoloni wa Ujermani anatangaza dhamira yake ya kuitwaa himaya yote ya Sultan Mangungo na haki zote kwa ajili ya Koloni la Ujerumani inayohusisha kila kona na amali za Mwenyi Sagara.

Katika kutekeleza hilo, Sultan Mangungo anakabidhi himaya yote ya Msovero, inayomilikiwa na yeye mwenyewe kwa urithi au kwa namna yoyote ile kwa nyakati zote, kwa Dk. Karl Peters, na wakati huo huo kumkabidhi haki zake zote.

Dk. Karl Peters kwa niaba ya Umoja wa Ukoloni wa Kijerumani anakusudia kuweka mkazo maalum kwa eneo la Msovero wakati wa kuitawala Usagara.

Mkataba huu umewasilishwa kwa Sultan Mangungo na mkalimani Ramzan katika dhana ya wazi kabisa na umesainiwa na pande zote, kwa kuzingatia taratibu zilizopo katika Usagara, Sultan baada ya kuhojiwa moja kwa moja alikiri kwamba hakuwa na ushirika ama kutegemea kwa namna yoyote Sultan wa Zanzibar, na kwamba hakuwa hata akimfahamu.

Imesainiwa. Dk. KARL PETERS
Imesainiwa. MANGUNGO

Mkataba huu umefanyika kihalali kabisa na umehuishwa kwa nyakati zote mbele za mashahidi wengi, ambao tunakiri hapa:
Kwagakinga (dole gumba);
Golola mtoto wa Sultan Mangungo (dole gumba);
Draman mtoto wa pili wa Sultan Mangungo (dole gumba);
Graf Pfeil August Otto.
Dole gumba la mkalimani Ramazan etc.
Dk. Karl Juhlke.
Msovero Usagara Novemba 29, 1884.



KWANINI MANGUNGO ALIONEKANA MJINGA?

Historia ilipoandikwa baada ya kupata uhuru , iliwahesabu watu wote waliopambana na wazungu kama mashujaa mfano Mkwawa. Bila kujali utawala wa hao machifu kama ulikuwa wa haki au laa. Historia haikutazama watawala hawa machifu kama watu walio pambania madaraka yao bali inawahesabu kama mashujaa kwa kuwa ilipambana tu mzungu.

Baada ya uhuru watu walisoma hadithi kama "KIBANGA AMPIGA MKOLONI". waliosoma kwa kipindi hicho walimuona Kibanga kama shujaa kwa kumpiga mzungu ( mkoloni). Lakini je Kibanga wa mwaka 1960 bado ni shujaa leo hii au ataonekana anafukuza "WAWEKEZAJI" ?

Kwahiyo kama KIBANGA alionekana shujaa kwa kumpinga mkoloni kipindi cha kutaka kujitawala ni wazi historia yoyote iliyoandikwa kwa kipindi hiko ingemtazama mtu yeyote yule aliyeshirikiana na wakoloni kipindi wanaingia Afrika kama mtu mjinga na msaliti kwa jamii yake.


KWANINI NASEMA MANGUNGO SIO MJINGA?


Kilichotokea kati ya Mangungo na machifu wengine waliopigana na wazungu ni uelewa tu. Mangungo aliona mbali ambapo wengine hawakuona kwa kipindi kile. MANGUNGO aliwaona wazungu kama wawekezaji mapema sana kuliko machifu wenzake. Kile alichokifanya Mangungo kuwaona wazungu kama wawekezaji ndio hiki tunakiona leo na sisi kuwa wazungu wanauwezo wa kuwekeza katika nchi zetu za kiafrika na uchumi ukakua.

JE MANGUNGO ALIAHIDIWA NINI KWA WAZUNGU?

Binafsi naamini tofauti na mkataba wa kuichukua ardhi na kiutawala tunaoambiwa kuwa ndio huo MANGUNGO alisaini lakini inaonesha wazi kwamba Mangungo alielezwa kuwa kama wazungu watalichukua eneo basi watakuja na mamba yafuatayo ;

mashine ( matreka) za kilimo kama treka nk

Ujenzi wa hospital za kisasa kwa (kipindi hicho)

Ujenzi wa shule

Ujenzi wa maghala ya kuhifadhia chakula

Ujenzi wa barabara

Ujenzi wa mabwawa ya kuzalisha umeme

Ujenzi wa reli ya kisasa kwa wakati huo

Ujenzi wa madaraja katika maeneo yasiyopitika kipindi cha masika

Upatikanaji wa huduma za maji safi .

Je upi unaweza kuwa uthibitisho wa hizo ahadi hadi kupelekea MANGUNGO kukubali?

Ukilitazama vizuri hilo eneo la Msovero ambalo ndio inaelezwa kuchukua eneo kubwa la KILOSA ya leo utagundua yafuatayo.

Maeneo mengi ya wilaya hiyo yana mashamba makubwa ya mkonge yaliyolimwa na mwekezaji wa Mangungo. Kuanzia Msowero ya leo , Gairo, Kimamba, Ludewa, Kilosa mjini ya leo, Chanzuru, Kivungu, Zombo , Mikumi, Kilangali , Malangali ,Ngaite, Melela Mvomero inayopakana na kilosa , ILONGA had maeneo ya dumila nk

Hayo ni maeneo machache sana yanayoonesha mwekezaji alitekeleza kweli ahadi yake ya kuinua kilimo.

Maeneo ya Kilosa mengi yalijegwa hospital. Mfano hospital ya Kilosa , Kimamba , vituo vya afya kama maeneo ya Ludewa , Mkata , na vingine ambavyo vilijegwa na wajerumani . Hivyo vitu havikuwepo kabla ya mkataba wa MANGUNGO.

Uwepo wa barabara kama ya kutoka Kilosa hadi Mikumi kupitia Zombo, barabara ya kutoka Kilosa hadi Morogoro mjini kupitia Mkata na ile kupitia Ludewa ni ushahidi tosha kuwa mwekezaji alifanya yale aliyoahidi mbele ya chifu Mangungo.

Uwepo wa njia ya reli inayopita tokea Morogoro mjini pale kichangani na kupita maeneo kama Mkata, Kimamba, Kilosa mjini ya sasa, Mkadage huko hadi Pwaga na kuingia Mpwapwa hii inaonedha jinsi gani mkataba wa chifu Mangungo na machifu wa kiluguru na wa kizingua ulizaa matunda kwa maeneo yao kiuwekezaji.

Uwepo wa shule ya KIZUNGUZI (kizu boys)

Ajira kwa vijana Uwepo wa huduma za malazi kwa wafanyakazi. Ajira ilipatikana kwa manamba japo mshahara haukuwa mkubwa lakini ukibadili thamani ya mshahara wa kipindi hicho unafanana na baadhi ya mishahara ya baadhi ya watu wanaolipwa hivi leo. Si kwamba hata hivi leo watu hawalalamiki udogo wa mishahara.

Nyumba za watumishi zilijegwa kila kwenye stesheni , kwenye kila kituo chao cha kukusanyia mikonge mfano Kimamba, ludewa , Chanzuru Msiwero , Kivungu nk. Hapa inaonesha ni jinsi gani mkataba aliosaini abwana mangungo haukuwa mbaya kama tunavyoaminishana leo hii.


Bado kama hayo hayatoshi ukipita maeneo ya Ilonga utaona jinsi wajerumani walivyopaendeleza katika kilimo na vituo vya utafiti wa kilimo walijenga ( hapa mtanikosoa kama walijenga wajerumani au waingereza).


Kwa wale watu walio bahatika kuishi Sagara ya zamani au Kilosa ya leo wanaweza kuwa mashahidi . Mji wa kilosa wa leo unaoneka ni mji uliokuwa wa kifahari enzi ya wawekezaji wa Mangungo ( ambao waliitwa wakoloni hapo awali) kabla ya kubadilishwa jina tena na kuitwa wawekezaji kama alivyowaita Mangungo na kizazi cha sasa . Kilosa ulikuwa mji kimbilio la wageni toka mikoa mbali mbali Tanzania. Usifikiri katika "engo" ya manamba kupata mchanganyiko wa kabila katika eneo la kilosa bali hata huduma ziliwavuta vijana wa zamani kwenda kuishi Kilosa.

Je kunyonywa kiuchumi ndio kunatufanya tumuone Mangungo alikuwa mjinga?


Binafsi namuona Bwana Mangungo kama kiongozi aliyeuona uwekezaji tangu mapema. Kwani kama kuhusu kunyonywa bado hadi leo kama taifa bado tuna mikataba mingi ya kinyonyaji isiyoacha alama kwa taifa kuliko ile ya msovero iliyoacha hata reli ,magofu ya nyumba na hospital.
Wapo watakaosema ujinga wa Mangungo ni kuiachia ardhi kwa wazungu kulima pamba na mikonge huku wenyeji kuishi kwa njaa. Binafsi naamini kwa nyakati hizo kulikuwa na watu wachache sana wenye uwezo wa kulima mamia ya ekari kama wawekezaji. Wengi walilima kujikimu kwani ni miaka zaidi ya 70s sasa tangu Mzungu atuachie ardhi yetu lakini kuna maeneo tangu kuumbwa kwa dunia hayajawahi kulimwa na wazawa. Vijana wanashinda kwenye vituo vya kubeti huku redio zikihamasisha nguvu ya buku katika kushinda kamali. Kwa mawazo kama hayo hatuoni kama bwana Mangungo aluoba mbali kuingia mikataba na wawekezaji?

Wapo watakaosema ujinga ni kuwa alisaini bila kuelewa chochote . Binafsi naona si kweli, kwani kama ni kweli Mangungo alisaini kitu asichoelewa historia ingeonesha kutokea mgogoro baina ya mwekezaji na Mangungo. Katika hali ya kawaida mtu akwambie muingie makubaliano ya kulichukua eneo lako lote la ardi na kiutawala na ukakubali bila kumuuliza shughuri atakazofanyia eneo lako. Pili, mkata ulisainiwa kisha Karl na wenzake wakaondoka kurudi Ujerumani . Kama wangekuwa ni walaghai basi pale waliporudi kutekeleza uwekezaji wao lazima pangetokea ugomvi na kutoelewana. Maana katika hali ya kawaida ukimpa mtu eneo alime au akae alafu ghafla unamwona anakuja na fundi wake wanajenga nyumba , hospitali, reli bila kwenda kuwahoji.

MANGUNGO ALIKUWA KIONGOZI MWANADIPLOMASIA

Kwajinsi sasa jamii ya Kiafrika inavyomsifu kiongozi mwenye mahusiano mazuri na wazungu kama kiongozi bora na mwanadiplomasia basi ni wazi Mangungo alikuwa nguli zaidi kama mwanadiplomasia wa mwanzoni kabisa.

NINI WITO WANGU KWA JAMII

Niwakati sasa wa jamii yetu kubadili mtazamo juu ya chifu Mangungo kwa kumchukulia kama kiongozi mjinga na kumwona kama kiongozi wa mwanzoni kuhamasisha uwekezaji nchini. Kumwona Mangungo kama kiongozi mjinga kumeifanya hata familia yake isijulikane leo hii ksma zinavyojulikana familia za ma chifu wengine. Kwakuwa sasa viongozi wetu wamerudi kule kule kuwapokea wazungu na kufanya nao shughuri za maendeleo kama ujenzi wa miundombinu ya maji , barabara, reli, hospitali, na shule jambo ambalo hata Mangungo ndilo alilifanya kwa ustadi basi hatuna budi kumuenzi Mangungo kama mwasisi wa uwekezaji nchini.
Natamani sasa hata familia yake iliyobaki tuiombe msamaha kama taifa kwakuwa tulilewa mvinyo wa uhuru kiasi ya kuwaona waliopinga kushirikiana na wazungu kuwa ndio MASHUJAA.

Nawasaliim
Chifu Mangungo wa Msovero ni mmoja kati ya machifu wa Afrika ambao waliamua kushirikiana na wakoloni kama moja ya njia ya kukwepa kutawaliwa katika maeneo yao au kwa kufaidika na mgao ulokuwa ukipitishwa na wakoloni wa kijerumani baada ya kutuma mzigo wa malighafi kwenda kwao barani Ulaya.

Kama unavyofahamu moja ya malengo makuu ya wakoloni kuja Afrika pamoja na kututawala ilikuwa ni kufuata malighafi.

Wakoloni khasa wa kijerumani walipokuja Afrika walikutana na vikwazo vya aina tatu kutoka kwa waafrika wakiongozwa na machifu kama Mirambo wa Wanyamwezi, Mkwawa wa Wahehe , Chifu Machemba wa Wayao na Kinjekitile Ngwale wa Wangoni.

Kipingamizi cha kwanza ulohusisha ulihusisha mbinu kama kuharibu mashamba ya wakoloni au pia kuwaua. Kilingamizi hiki kiklitokana na mifumo imara ilojengwa na machifu kama Mkwawa na Mirambo ambao walikuwa ni viongozi imara waso legelege, wenye jeshi imara na umoja ulotukuka. Pia tawala hizi zilikuwa na mifumo imara ya uchumi, vyombo vya utawala na jamii zilokuwa zajielewa na pia kuwa na mbinu za hali ya juu za kivita. Kwa mfano machifu hawa waliweza kutumia milima kujilinda na kuiona adui atokea pande zipi.

Upinzani wa aina ya pili dhidi ya wakoloni ulikuwa ni kuwaacha wakoloni wafanye yao bila kushirikiana nao kwa maana ya kuwapatia vibarua wa mashambani na pia kutotumia vita kupigana nao. Pia aina hii ya upingaji ulohusisha kutolipa kodi ya kichwa, kutokuzalisha mazao ya biashara mashambani na kukataa kufanya kazi za mashambani.

Sasa hawa walokosa silaha, hawakuwa na jeshi imara, viongozi wao kuwa dhaifu, watu wao wenyewe kuwa waso na mshikamano na ushirikiano na pia kutokuwa na vyombo imara vya kusimamia jamii zao.

Kwanini Chifu Mangungo wa Msovero aliamua kushirikiana na wakoloni wa kijerumani kwa kuwauzia ardhi yake?

1. Alikuwa ni kiongozi ambae alikuwa ni dhaifu na pia hakuwa na jeshi imara ambalo lingeweza kukabiliana na jeshi la wajerumani. Wajerumani walikwishanya ujasusi wa kutosha ambao uliwapa taarifa au "dossier" yote juu ya udhaifu Chifu Mangungo na ndo maana wakamtuma Carl Peters.

2. Kwa kuwa Chifu Mangungo alikuwa ni dhaifu alitumia mwanya huo kushirikiana na wajerumani kwa minajili ya kutaka kunufaika kijeshi ili apate nguvu ya kupambana au kujilinda kwenye mipaka yao dhidi ya uvamizi wa machifu ambao walikuwa na nguvu kwelikweli kama Mkwawa, Machemba na wengine.

3. Walitaka utulivu na amani ili kila mmoja awe mpole katika aneo lake hivyo ilibidi kushirikiana na wakoloni hao katika kuhakikish amambo hayo mawili.

4. Hii ndo twasema kutojitambua au kujidharau au kwa kiingereza twasema ni "ignorance" na ambayo inamkumba kila mara Chifu Mangungo wa Msovero. Chifu Mangungo hakuelewa ulaghai wa walokoni khasa Carl Peters ambae ndie alietumwa kwenda kwake. Hivyo alipomuona aja na zawadi kemkem, mzee wa wtu akachanganyikiwa na alipopewa mkataba asaini haikuwa jabo gumu.

Na si tu Chifu Mangungo hata machifu wa washona na ndebele pia nao walikubali vijizawadi na kulaghaiwa kisha kutia saini mikataba hewa walopewa na jasusi mwingine aitwae John Moffat. Chifu Lobengula alisaini mikataba zaidi ya mitano katika vipindi tofauti kati ya mwaka 1850 na 1890 akisaini na majasusi kama huyo Moffat, Grobbler, Lippart na Rudd.

Ndo kusema hadi leo bado zawadi zaja kwa aina tofauti na ukishindwa kugundua nini kilicho nyuma ya zawadi hizo kinotokea mwisho ni majanga.

Lakini mwisho. sisi waafrika tuna mengi ya kujifunza na hadi leo bado twapata fursaq zaidi za kujifunza kuwa ni nani khasa alikuwa ni kiongozi imara aliekataa zijizawadi ka kuuza ardhi yake. Je, ni akina Mtemi Mirambo, Chifu Mkwawa na Kinjekitile Ngwale na kwamba je. ni kwanini Chifu Mangungo alikuwa ni kiongozi dhaifu ambae alikubali kulaghaiwa tena mbele ya washauri wake wa karibu na kuamua kutia saini mkataba wa kilaghai wa wawakilishi wa wakoloni wa kijerumani?
 
Mwafrika zamani alichukuliwa utumwani tena kwa msaada wa mwafrika mwenzake kwa nguvu kwenda utumwani leo hata kesho maelf ya vijana wa kiafrica wakishinda kwenye ofisi mbalimbali za ubalozi wakililia viza huku maelfu kwa maelfu wakihatarisha maisha yao baharini wakililia kwenda utumwani kwa hiari. SAsa UHURU una maana gani kama vijana wa kiafrica wanazikimbia nchi zao zenye fursa ya raslimali tele na kwenda kuwa ma cheap labour utumwani. Zamani waliitwa watumwa siku hizi jina limeadvance wanaitwa diasporas.
Yes hao ni watumwa tu
 
Kosa kubwa Sana la Mwalimu Nyerere ni kuacha mazuri ya mkoloni yaani alimchukia mkoloni na mazuri yake yote. Kwa hali ya SAsa Ili kumaliza tatizo la ajira nchini mfumo wa elimu wa mkoloni ndio jawabu, na sio mfumo huu wa elimu siasa. Mwalimu alikosea Sana kuingiza siasa kwenye mfumo wa elimu matokeo ni kuzalisha Jamii ya blah blah angalau Wakenya wao mfumo wao wa elimu ni ule tangu mkoloni kwa kufanyia maboresho tu.
Haujawasaidia kitu hao wakenya ndio maana bado kuna ukabila na wakenya wengi wanakimbilia ughaibuni kwenda kuwa watumwa mambo Leo (Diaspora )
 
Historia ya Tanzania haina ukweli hata chembe! Nilishangaa sana walipodanganya eti Nyerere alizaliwa Butiama? Eti Nyerere babake ni mzee Burito? Yule mzee siyo damu ya Mzanaki, sema wenzetu wakishatoa mahari mtoto yeyote atakayezaliwa anakuwa mali yao!😁😁😁
 
Ipi tofauti baina yao hali wote wanashikilia uchumi wa nchi.
Kwangu bora ya wakoloni kuliko wawekezaji
Mi nilishindwa kumjibu mana niliona kaja kama mwalimu wa history na anataka tujadili mambo kama anavyoyafundisha yeye huko shuleni.
 
Huyo mkalimqni alisoma wapi kijerumani? Mgeni au mwenyeji? Hapa ndipo tu narudi kule kule alisomeshwa tu
Muhimu jua

Karl peter aliishi London miaka mingi alikojifunza falsafa za ukoloni . Kwahiyo alijua kuongea kingereza vizuri. Alifijia Zanzibar na kumpata mkalimani anaitwa Ramadhani. Uwezekano wa Ramadhan kujua kingereza upo kutokana na Zanzibar kutembelewa na watu wa maeneo tofaut tangu karne za mwanzano. Pia Ramadhani kufaham kiswahili inawezekana kutokanana ushahidi unaonesha Zanzibar wameanza kizungumza kiswahili mapema sana
Ko mangungo tuseme tu alisaini kitu anachokielewa.
 
Na swali jingine ni hili: Hawa "wasomi" wetu wanaosaini mamikataba haya mabovu na kuuza madini, gesi na wanyama wetu kwa wazungu nao ni akina Mangungo? Hawajui kusoma na kuandika kama Mangungo?
Ukijadili mikataba ya sasa unatoka kwenye historia na kurudi kwenye siasa.
Na swali jingine ni hili: Hawa "wasomi" wetu wanaosaini mamikataba haya mabovu na kuuza madini, gesi na wanyama wetu kwa wazungu nao ni akina Mangungo? Hawajui kusoma na kuandika kama Mangungo?

Kitendo cha kuwapokea wazungu nimekizungumzia kama kukaribisha wawekezaj.
Kitendo cha kuishi nao vizuri tumekizungumzia kama mwanadiplomasia.
Kitendo cha kusaini mikataba mbele ya ramadhan na familia yake tunaona namna Mangungo alivyokuwa muwazi kwenye mikataba yake.
Kama mangungo mjinga kweli kama mnavyoamini na mkataba wake ulikuwa wa wazi sasa kwanini hawa wajanja wenu wa leo mikataba yao ni ya siri wakati ni mikataba ya KIJANJA ??
Jambo la msingi ni aidha tumtoe Mangungo kwenye kundi la viongozi wajinga tumweke kwenye kundi la viongoz walio harakisha uwekezaji ( viongoz wajanja) au viongozi wa kiafrika wa leo tuwaweke kundi moja na Mangungo jambo ambalo watu wanapinga kwa kusema ukolon si sawa na uwekezaji wa leo.
Na ikumbukwe tukisema hakuna maendeleo bila wazungu kama alivyoamini mangungo na viongoz wa leo, maana yake wapigania uhuru ni kama waliwafukuza wawekezaji. Kwasababu viongoz wa leo wanapata tabu kuwarudisha wazungu kufanya jambo lilelile walilokuwa wanashirikiana na mangungo. Au labda tuseme viongozi wa leo wao wanaboresha kwenye vipengele alivyopigwa Mangungo
 
Chifu mangungo hakuwa mjinga, watanzania tulipotoshwa, tunapaswa kuiomba familia yake msamaha

Kwa miaka mingi sana chifu mangungo ameendelea kuonekana kama mfano wa kiongozi mjinga hasa pale linapotokea swala la mikataba. Lakini je Mangungo alikuwa mjinga kweli?

Chifu mangungo ni nani?

Naomba ninukuu kidogo kipande cha historia fupi kuhusu chifu Mangungo kutoka katika uzi wa ndugu humu Jf KILABA

"Mangungo simultaneously for all his people and Dr. Peters for alt his present and future associates hereby concluded a treaty of Eternal Friendship.

Mangungo offers all his territory with all its civil appurtenances to Dr. Karl Peters, as the representative of the Society for German Colonization, for the exclusive and universal utilization for German colonization.

Dr. Karl Peters, in the name of the Society for German Colonization declares his willingness to take over the territory of the Sultan Mangungo with all rights for German Colonization subject to any existing suzerainty of Mwenyi Sagara.

In pursuance thereof, Sultan Mangungo hereby cedes all the territory of Msovero, belonging to him by inheritance or otherwise for all time, to Dr. Karl Peters, making over to him at the same time all his rights.

Dr. Karl Peters in the name of the Society for German Colonization undertakes to give special...attention to Msovero when colonizing Usagara.

This treaty has been communicated to the Sultan Mangungo by the interpreter Ramzan in a clear manner and has been signed by both sides, with the observation of the formalities valid in Usagara the Sultan on direct enquiry having declared that he was not in anyway dependent upon the Sultan of Zanzibar, and that he did not even know the existence of the latter.

Sgd. Dr. KARL PETERS
Sgd. MANGUNGO

This contract has been executed legally and made valid for all time before a great number of witnesses, we testify herewith:
Kwagakinga (mark);
Sultan Mangungo’s son of Golola (mark);
Sultan Mangungo’s second son of Draman (mark);
Graf Pfeil August Otto;
Mark of the intepreter Ramazan etc.
Dr. Karl Juhlke.
Msovero Usagara November 29, 1884.

Kwa tafsiri isiyo rasmi, kwa Kiswahili unasomeka hivi:
Mangungo, Sultan wa Msovero katika Mwenyisagara, na Dk. Karl Peters. Mangungo sambamba na watu wake wote na Dk. Peters kwa niaba yake na washirika wake wengine wajao kwa pamoja wanaweka mkataba wa Urafiki wa Kudumu.

Mangungo amekubali kutoa himaya yake yote pamoja na watu wake na hadhi yake kwa Dk. Karl Peters, kama mwakilishi wa Umoja wa Ukoloni wa Kijerumani (Society for German Colonization), kwa ajili ya matumizi ya moja kwa moja ya koloni la Kijerumani.

Dk. Karl Peters, kwa niaba ya jina la Umoja wa Ukoloni wa Ujermani anatangaza dhamira yake ya kuitwaa himaya yote ya Sultan Mangungo na haki zote kwa ajili ya Koloni la Ujerumani inayohusisha kila kona na amali za Mwenyi Sagara.

Katika kutekeleza hilo, Sultan Mangungo anakabidhi himaya yote ya Msovero, inayomilikiwa na yeye mwenyewe kwa urithi au kwa namna yoyote ile kwa nyakati zote, kwa Dk. Karl Peters, na wakati huo huo kumkabidhi haki zake zote.

Dk. Karl Peters kwa niaba ya Umoja wa Ukoloni wa Kijerumani anakusudia kuweka mkazo maalum kwa eneo la Msovero wakati wa kuitawala Usagara.

Mkataba huu umewasilishwa kwa Sultan Mangungo na mkalimani Ramzan katika dhana ya wazi kabisa na umesainiwa na pande zote, kwa kuzingatia taratibu zilizopo katika Usagara, Sultan baada ya kuhojiwa moja kwa moja alikiri kwamba hakuwa na ushirika ama kutegemea kwa namna yoyote Sultan wa Zanzibar, na kwamba hakuwa hata akimfahamu.

Imesainiwa. Dk. KARL PETERS
Imesainiwa. MANGUNGO

Mkataba huu umefanyika kihalali kabisa na umehuishwa kwa nyakati zote mbele za mashahidi wengi, ambao tunakiri hapa:
Kwagakinga (dole gumba);
Golola mtoto wa Sultan Mangungo (dole gumba);
Draman mtoto wa pili wa Sultan Mangungo (dole gumba);
Graf Pfeil August Otto.
Dole gumba la mkalimani Ramazan etc.
Dk. Karl Juhlke.
Msovero Usagara Novemba 29, 1884.



KWANINI MANGUNGO ALIONEKANA MJINGA?

Historia ilipoandikwa baada ya kupata uhuru , iliwahesabu watu wote waliopambana na wazungu kama mashujaa mfano Mkwawa. Bila kujali utawala wa hao machifu kama ulikuwa wa haki au laa. Historia haikutazama watawala hawa machifu kama watu walio pambania madaraka yao bali inawahesabu kama mashujaa kwa kuwa ilipambana tu mzungu.

Baada ya uhuru watu walisoma hadithi kama "KIBANGA AMPIGA MKOLONI". waliosoma kwa kipindi hicho walimuona Kibanga kama shujaa kwa kumpiga mzungu ( mkoloni). Lakini je Kibanga wa mwaka 1960 bado ni shujaa leo hii au ataonekana anafukuza "WAWEKEZAJI" ?

Kwahiyo kama KIBANGA alionekana shujaa kwa kumpinga mkoloni kipindi cha kutaka kujitawala ni wazi historia yoyote iliyoandikwa kwa kipindi hiko ingemtazama mtu yeyote yule aliyeshirikiana na wakoloni kipindi wanaingia Afrika kama mtu mjinga na msaliti kwa jamii yake.


KWANINI NASEMA MANGUNGO SIO MJINGA?


Kilichotokea kati ya Mangungo na machifu wengine waliopigana na wazungu ni uelewa tu. Mangungo aliona mbali ambapo wengine hawakuona kwa kipindi kile. MANGUNGO aliwaona wazungu kama wawekezaji mapema sana kuliko machifu wenzake. Kile alichokifanya Mangungo kuwaona wazungu kama wawekezaji ndio hiki tunakiona leo na sisi kuwa wazungu wanauwezo wa kuwekeza katika nchi zetu za kiafrika na uchumi ukakua.

JE MANGUNGO ALIAHIDIWA NINI KWA WAZUNGU?

Binafsi naamini tofauti na mkataba wa kuichukua ardhi na kiutawala tunaoambiwa kuwa ndio huo MANGUNGO alisaini lakini inaonesha wazi kwamba Mangungo alielezwa kuwa kama wazungu watalichukua eneo basi watakuja na mamba yafuatayo ;

mashine ( matreka) za kilimo kama treka nk

Ujenzi wa hospital za kisasa kwa (kipindi hicho)

Ujenzi wa shule

Ujenzi wa maghala ya kuhifadhia chakula

Ujenzi wa barabara

Ujenzi wa mabwawa ya kuzalisha umeme

Ujenzi wa reli ya kisasa kwa wakati huo

Ujenzi wa madaraja katika maeneo yasiyopitika kipindi cha masika

Upatikanaji wa huduma za maji safi .

Je upi unaweza kuwa uthibitisho wa hizo ahadi hadi kupelekea MANGUNGO kukubali?

Ukilitazama vizuri hilo eneo la Msovero ambalo ndio inaelezwa kuchukua eneo kubwa la KILOSA ya leo utagundua yafuatayo.

Maeneo mengi ya wilaya hiyo yana mashamba makubwa ya mkonge yaliyolimwa na mwekezaji wa Mangungo. Kuanzia Msowero ya leo , Gairo, Kimamba, Ludewa, Kilosa mjini ya leo, Chanzuru, Kivungu, Zombo , Mikumi, Kilangali , Malangali ,Ngaite, Melela Mvomero inayopakana na kilosa , ILONGA had maeneo ya dumila nk

Hayo ni maeneo machache sana yanayoonesha mwekezaji alitekeleza kweli ahadi yake ya kuinua kilimo.

Maeneo ya Kilosa mengi yalijegwa hospital. Mfano hospital ya Kilosa , Kimamba , vituo vya afya kama maeneo ya Ludewa , Mkata , na vingine ambavyo vilijegwa na wajerumani . Hivyo vitu havikuwepo kabla ya mkataba wa MANGUNGO.

Uwepo wa barabara kama ya kutoka Kilosa hadi Mikumi kupitia Zombo, barabara ya kutoka Kilosa hadi Morogoro mjini kupitia Mkata na ile kupitia Ludewa ni ushahidi tosha kuwa mwekezaji alifanya yale aliyoahidi mbele ya chifu Mangungo.

Uwepo wa njia ya reli inayopita tokea Morogoro mjini pale kichangani na kupita maeneo kama Mkata, Kimamba, Kilosa mjini ya sasa, Mkadage huko hadi Pwaga na kuingia Mpwapwa hii inaonedha jinsi gani mkataba wa chifu Mangungo na machifu wa kiluguru na wa kizingua ulizaa matunda kwa maeneo yao kiuwekezaji.

Uwepo wa shule ya KIZUNGUZI (kizu boys)

Ajira kwa vijana Uwepo wa huduma za malazi kwa wafanyakazi. Ajira ilipatikana kwa manamba japo mshahara haukuwa mkubwa lakini ukibadili thamani ya mshahara wa kipindi hicho unafanana na baadhi ya mishahara ya baadhi ya watu wanaolipwa hivi leo. Si kwamba hata hivi leo watu hawalalamiki udogo wa mishahara.

Nyumba za watumishi zilijegwa kila kwenye stesheni , kwenye kila kituo chao cha kukusanyia mikonge mfano Kimamba, ludewa , Chanzuru Msiwero , Kivungu nk. Hapa inaonesha ni jinsi gani mkataba aliosaini abwana mangungo haukuwa mbaya kama tunavyoaminishana leo hii.


Bado kama hayo hayatoshi ukipita maeneo ya Ilonga utaona jinsi wajerumani walivyopaendeleza katika kilimo na vituo vya utafiti wa kilimo walijenga ( hapa mtanikosoa kama walijenga wajerumani au waingereza).


Kwa wale watu walio bahatika kuishi Sagara ya zamani au Kilosa ya leo wanaweza kuwa mashahidi . Mji wa kilosa wa leo unaoneka ni mji uliokuwa wa kifahari enzi ya wawekezaji wa Mangungo ( ambao waliitwa wakoloni hapo awali) kabla ya kubadilishwa jina tena na kuitwa wawekezaji kama alivyowaita Mangungo na kizazi cha sasa . Kilosa ulikuwa mji kimbilio la wageni toka mikoa mbali mbali Tanzania. Usifikiri katika "engo" ya manamba kupata mchanganyiko wa kabila katika eneo la kilosa bali hata huduma ziliwavuta vijana wa zamani kwenda kuishi Kilosa.

Je kunyonywa kiuchumi ndio kunatufanya tumuone Mangungo alikuwa mjinga?


Binafsi namuona Bwana Mangungo kama kiongozi aliyeuona uwekezaji tangu mapema. Kwani kama kuhusu kunyonywa bado hadi leo kama taifa bado tuna mikataba mingi ya kinyonyaji isiyoacha alama kwa taifa kuliko ile ya msovero iliyoacha hata reli ,magofu ya nyumba na hospital.
Wapo watakaosema ujinga wa Mangungo ni kuiachia ardhi kwa wazungu kulima pamba na mikonge huku wenyeji kuishi kwa njaa. Binafsi naamini kwa nyakati hizo kulikuwa na watu wachache sana wenye uwezo wa kulima mamia ya ekari kama wawekezaji. Wengi walilima kujikimu kwani ni miaka zaidi ya 70s sasa tangu Mzungu atuachie ardhi yetu lakini kuna maeneo tangu kuumbwa kwa dunia hayajawahi kulimwa na wazawa. Vijana wanashinda kwenye vituo vya kubeti huku redio zikihamasisha nguvu ya buku katika kushinda kamali. Kwa mawazo kama hayo hatuoni kama bwana Mangungo aluoba mbali kuingia mikataba na wawekezaji?

Wapo watakaosema ujinga ni kuwa alisaini bila kuelewa chochote . Binafsi naona si kweli, kwani kama ni kweli Mangungo alisaini kitu asichoelewa historia ingeonesha kutokea mgogoro baina ya mwekezaji na Mangungo. Katika hali ya kawaida mtu akwambie muingie makubaliano ya kulichukua eneo lako lote la ardi na kiutawala na ukakubali bila kumuuliza shughuri atakazofanyia eneo lako. Pili, mkata ulisainiwa kisha Karl na wenzake wakaondoka kurudi Ujerumani . Kama wangekuwa ni walaghai basi pale waliporudi kutekeleza uwekezaji wao lazima pangetokea ugomvi na kutoelewana. Maana katika hali ya kawaida ukimpa mtu eneo alime au akae alafu ghafla unamwona anakuja na fundi wake wanajenga nyumba , hospitali, reli bila kwenda kuwahoji.

MANGUNGO ALIKUWA KIONGOZI MWANADIPLOMASIA

Kwajinsi sasa jamii ya Kiafrika inavyomsifu kiongozi mwenye mahusiano mazuri na wazungu kama kiongozi bora na mwanadiplomasia basi ni wazi Mangungo alikuwa nguli zaidi kama mwanadiplomasia wa mwanzoni kabisa.

NINI WITO WANGU KWA JAMII

Niwakati sasa wa jamii yetu kubadili mtazamo juu ya chifu Mangungo kwa kumchukulia kama kiongozi mjinga na kumwona kama kiongozi wa mwanzoni kuhamasisha uwekezaji nchini. Kumwona Mangungo kama kiongozi mjinga kumeifanya hata familia yake isijulikane leo hii ksma zinavyojulikana familia za ma chifu wengine. Kwakuwa sasa viongozi wetu wamerudi kule kule kuwapokea wazungu na kufanya nao shughuri za maendeleo kama ujenzi wa miundombinu ya maji , barabara, reli, hospitali, na shule jambo ambalo hata Mangungo ndilo alilifanya kwa ustadi basi hatuna budi kumuenzi Mangungo kama mwasisi wa uwekezaji nchini.
Natamani sasa hata familia yake iliyobaki tuiombe msamaha kama taifa kwakuwa tulilewa mvinyo wa uhuru kiasi ya kuwaona waliopinga kushirikiana na wazungu kuwa ndio MASHUJAA.

Nawasaliim
Mkuu hongera kwako kwa kuielikisha jamii, na hapo watu hawata kuelewa kwasababu walishaminishwa tofauti
 
Nachangia kutokana na ulichoeleza, sijawahi kufika maeneo yote uliyoainisha.

Kwa mtazamo wangu na ulichoandika, mjerumani alikuwa akijinufaisha yeye. Chifu Mangyngo alifaidika binafsi na familia yake? Sijui.

Ila kwa watu wengine, ndio walikuwa manamba au watumwa. Kama kulijengwa hospitali, barabara na viwanda, vyote ni kuhakikisha uzalishaji wa uhakika kumnufaisha mjerumani. Sikuona ukieleza mambo ya shule, kama zilijengwa. Ila umetaja mambo ya shule katika mambo unayohisi aliahidiwa chifu.

Tukiangalia miundombinu iliyowekwa, chifu anaweza kusifiwa, japo kiuhalisia, inaonekana miundombinu yote, ilikuwa kwa lengo la kurahisisha shughuli na maisha ya mjerumani na kujitajirisha.

Na ukiangalia mazingira ya eneo lake kulinganisha na sehemu walikowapinga wakoloni, utasema kuna maendeleo ya vitu, kutokana na miundombinu hiyo iliyokuwa ikisaidia wizi wa mjerumani.
Hapana mkuu, mtazamo tu kuwa miundombinu kurahisisha uzalishaji wake bali kuwahudumia wafanyakazi wake hata sasa ukienda Mtibwa kuna zahanati ndani ya kiwanda kwa jamii iliyopo ndani ndio hunufaika.
Kwamifano hai kuonesha kunufaika kwa wakazi wake watu wengi kutoka iringa walikuja wao kwa hiari yao kuja kufanya kazi na walipo rudi walirudi na majina ya huko km Ludewa, Mlangali na malangali
 
Shida ni kwamba kila walichokuwa wanakizalisha kilipelejwa Nje kwenda kutengeneza material ya kutumia. Vibarua wa Kiafrika walifanya kazi Kwa mazingira magumu na ujira mdogo. Kila walichokifanya ni Kwa manufaa Yao na sio Kwa mwafrica
Ulitaka wanufaike vipi zaidi ya Mshahara?
 
Zamani za Nyerere tuwalifukuzilia kwa mbali hukoo! wakafanyie ujinga wao hukooo km kina Faza Thom na kundi lake! Leo akifanya hovyo tunaua! km Korimba si unawajua? Mtikila nk?! tupilia mbali kule! ....

Then .tuna subiria kwanza kumuandika vibaya! Nikuulize tuu nani kafanya ujinga na bado tuka mvumilia sisi wabongo??? Bashite unajua?, Sabaya ndo kabisaa, au yule mrafi na Mtekaji? km hujui aliko nenda chato?..

hao wooote si unajua hali zao weye lkn bana ! au huishi Bongo kijana! tena huyo wa Msovero ashukuru tu ni zamani lkn laiti angefanya hayo leo heee!!...wewe/yeye woote manzi ga nyanza!

Nakuuliza weye hujui Bazil Mramba na wenzake walivochapwa mpaka wakawa wanaokota takataka/ usafi Hospitali ya Sinza! ulikuwa wapi??? yaani hiyo huoni ni adhabu tosha kwa viongozi km huyo wa Msovero??

au ulitaka tuwauwe ndo ujue kuwa tumechukia??? ...Well! adhabu tuliyompa kambona , Bibi tii, Mohamed Babu, na yule komandoo aliye fia Msumbiji umesahau mara hii??......kweli weye kichwa chako bOga sana......

ndo tatizo lenu wana vijiji mnaleta mada wkt hata hujui kinachoendelea nchini! kifupi tumeaadhibu wengi sana na weye unastahili adhabu kushadadia waarifu!

Tatizo lako unadhani kuwekeza ni dhambi kwa kuwa hujui maana yake!......wanalipa kodi tunayotaka sisi!! na tunachagua sisi nani awekeze na nani asiwekeze! na kwa wakati gani!! tuna uwezo huo!

Mangungo yeye hakuwa na uwezoo wa kupinga alikuwa dhaifu! na chifu mzima na baraza lake looote alidanganywa sisi hatudanganywi

ikitokea wa ivo yeye huyo aliye mkaribisha na huyo mwekezaji wataipata fresh ile yenyewe!! mifano ni mingi tu!! ....ebu funguka bana weee!...huyo mzee wako ni moja ya mifano mibaya Africa ever!

hata Idd amini, Bokasa, Banda wa Malawi walikuwa ni mifano mibaya Africa, lkn wana wafuasi wao waliokuwa wana faidika nao! lkn wanaficha aibu zao! mbali kabisaaaa!...sasa weye mbraaaa!!
Mbona Nyerere bado anatukuzwa na madudu yake
 
Maisha ya mwafrika yalikuwa bora Sana enzi ya ukoloni kuliko baada ya UHURU, kwa maana wakulima awakuwaza kuhusu soko wao jukumu lao lilikuwa ni kulima tu ishi ya soko sio wao, wafanyabiashara wa kiafrica walifanya biashara pasipo bughudha, ajira zilikuwa tele viwandani na mashambani, elimu na afya ilikuwa bora.
Ni tamaa tu ya wapigania UHURU ndio imeleta shida zote hizi, wao walipigania maslai yao binafsi kwa kuwahadaa waafrika wawape sapoti lakini lengo lilikuwa wao ndio walambe asali.
Sio wapigania uhuru sema wachumia tumbo
 
Tukiruhusu fikra huru tuna sababu za msingi za kuhoji ujinga wa Chief Mangungo kama historia inavyodai.

Tunahitaji kuheshimu maamuzi ya Mangungo na labda kumuweka kwenye kundi la mashujaa waliochagua amani na sio vita..Kuchagua amani sio ujinga.

Historia imewapa ushujaa viongozi waliopambana na kumwaga damu na wengine kujiua kabla ya kushikwa na wakoloni kama Mkwawa, Isike, Abushiri, Bwana kheri, Makung'anya, Mangi Meli, Mangi sina, na Kinjekitile Ngwale. Huku ikiwanyima ushujaa viongozi waliochagua amani na diplomasia kama Mangungo na Rumanyika....zaidi Mangungo ati alisaini mkataba wa kilaghai.

Kwanini tunatakiwa kumjadili upya Mangungo?

Mangungo alikuwa muwazi...Mkataba na Carl Peters ulisainiwa mchana kweupe mbele ya mashahidi wa pande zote na mkalimani aliyeongea kiswahili ambacho upande wa Mangungo ulikielewa...sasa vitabu vingi vya historia yetu vinasema Mangungo alisaini mkataba asioelewa maana yake na kwa lugha ya kigeni ambayo hakuielewa...Kuna upotoshaji hapa au utafiti hafifu.

Baada ya Carl Peters kurudi kutoka Ujerumani akiwa ameiunda GEACO na ukoloni kuanza, mangungo na watu wake hawa kuanzisha vita kupinga ukoloni kwa muda huo. Hii ina maana kwamba baadhi ya makubaliano yalitimizwa ikiwamo ujenzi wa miundo mbinu na huduma nyingine za kijamii hata kama interest kubwa ilikuwa kwa mkoloni...Kama Mangungo angestuka kuona makubaliano hayatekelezwi basi ni wazi angeanzisha mapigano kama walivyofanya Samori Toure wa Mandika na Lobengula wa Washona wa Zimbabwe...hawa waliingia makubaliano baadae wakagundua dhuluma na kuanzisha vita.

Mkondo aliouchukua Mangungo ni kama ule aliouchukua Nyerere wakati wa kudai uhuru...Mangungo alitumia diplomasia, hakutaka bloodshed kama Nyerere alivyofanya. Wakati kina Mwai Kibaki, Ahmed Sekou Toure, Samu Nujoma, Eduado Mondlane, Samora Machel nk wakidai uhuru kwa nguvu, Julius Nyerere alichagua diplomasia na hakutaka bloodshed. Tunamuitaje Mangungo mjinga hapa?

Tofauti ni zama tu lakini content ya mkataba wa Mangungo na mikataba mingi ya sasa ni yaleyale...Mangungo alisaini kuukubali ukoloni, viongozi wa sasa wanasaini kuukubali Ukoloni mamboleo.


Guevara Jr
 
Back
Top Bottom