Waafrika tuna uwezo mdogo wa kujiongoza kimaendeleo, Naomba unitajie nchi moja tu ya kiafrika inayoendeshwa na waafrika iliyo stable?

Labda kama Kuna Kenya nyingine tofauti na hii niliyoishi. Kenya na Tz hazitofautiani sana kimaendeleo.
 
Kenya walitakuwa kuwa juu zaidi ,nimeishi kenya maana pia nimekaa mpakani.

Kenya wana maendeleo ila sio nchi nzuri ...Kenya kuna ubaguzi wa wazi ndugu yangu kuna makabila ukizaliwa basi una nuksi mazima hata furaa hupati usiwe mkamba ,mkisii ,wakale
Huo ukabila wa Kenya ni story za kufikirika na propaganda zaidi,
Jaji mkuu wa saa wa Kenya ni Mmeru, Rais ni Mkale, mkuu wa majeshi ni Mjaluo, Speaker wa bunge ni Mluhya
 
Huo ukabila wa Kenya ni story za kufikirika na propaganda zaidi,
Jaji mkuu wa saa wa Kenya ni Mmeru, Rais ni Mkale, mkuu wa majeshi ni Mjaluo, Speaker wa bunge ni Mluhya
Nimeishi kenya na kukaa mpakani sehemu inaitwa Daluni ,kule ukabila ni hatari sio nchi ya kukaaa .kabisa kama umezoea Tanzania .


Kenya ni ovyo kabisa haswa unakuta mtu anapewa huduma kwa kuitwa jina la kabila "utasikia huyu mkikuyu"

Labda Mombasa na Nairobi ila kaunti zilizobaki ni chefu.
 
Wakenya hawana utu kabisa
 

Daluni ni Tanga, Tanzania
 
Daluni ni Tanga, Tanzania
Nimekaa hapo kenya wanaingilia sana na hayo maeneo walikuwa wanakuja sana ,tena wapo kibao tulikuwa tunachek nao mpira .

Pale wanaitana majina kwa makabila haswa wakisii wanadharaulika ,mtu akiwa mshiirikina utasikia mkamba huyo hata kama sio mkamba.
 
Naongezea pia Katiba bora.
 
Childish argument,
Hapa Tanzania yenyewe Wasukuma, Wachaga, watu wa pwani na karibia makabila yote yanataniana mambo ya ajabu ajabu tu. Kuna wanaosemwa ni wezi sana hata wakipewa nchi wataiuza, kuna wanaosemwa ni wavivu sana, kuna wanoitwa washamba sana, kuna wanaoitwa wachawi sana n.k
 
Sababu gani zinakufanya useme hawana utu kabisa?
Kenya huwezi kufananisha na Tanzania , wakenya wana roho mbaya wanafanana na watu wa kaskazini haswa kweny ubaguzi ..

Hakuna nchi ya Africa mashariki nzuri ya kuishi kuliko Tanzania ,kama kenya ningeshaishi tangu mwaka 2009 maana nilipata kazi huko ...Kiufupi kule ardhi ni ishu halafu wanasiasa wana nguvu sana labda kwa watu weupe.

Uchumi umeshikwa na watu kadhaa hata system sijajua baada ya mwaka 2010 ,ila sio pazuri hapa Tz ni mikoa miwili ndio unaweza kubaguliwa nadhani inajulika kwingine kote unaweza kupata ardhi pia kujali kabila na asili yako.

Kama hujui kenya kuna serikali ya majimbo ambayo inaleta utofauti mkubwa baina ya watu ...Kuna majimbo kama unatoka jirani basi kupata ajira ni shughuli .
 
Kenya hamna diversity kubwa makabila machache ndio tatizo ...Tanzania makabila kibao , narudia Tz ina mikao miwili yenye ubaguzi basi sasa nenda kenya kila jimbo lina sheria zake usije kushangaa
 
Watu wa Kaskazini wa nchi gani??
Tz wanafanana na wakenya kwa roho ,kenya sio sehemu nzuri kwanza wanatumaind sana sisi watanzania ilihali hatuna tatizo nao .

Wakenya wanapigana na somalia kutwa ila chuki zao zipo kwa watanzania ...Narudia tena Kenya huwezi kufananisha na Tz kweny maisha ya uhuru wa kiuchumi tena kaunti ya kisiii halafu mjaluo ukafanye biashara au kununua ardhi uone😅😅.

Maisha hayo washayazoea ila wewe mbongo hutoyaweza labda uishi Nairobi au Mombasa.
 
Kiufupi kule ardhi ni ishu halafu wanasiasa wana nguvu sana labda kwa watu weupe.
Tanzania ardhi sio ishu? Migogoro ya ardhi kila kona ya nini kama ardhi sio ishu??

Tanzania wanasiasa hawana nguvu?? Uchawa umeotokea wapi kama wanasiasa hawana nguvu?
 
Tanzania ardhi sio ishu? Migogoro ya ardhi kila kona ya nini kama ardhi sio ishu??

Tanzania wanasiasa hawana nguvu?? Uchawa umeotokea wapi kama wanasiasa hawana nguvu?
Sasa nakuambia hapa Tz vijana wanafanya biashara wadogo wanashika pesa ila sio kenya ...Kule kutoboa sio rahisi makampuni makubwa ya nje yana HQ zao hakuna biashara za kuchuuza kwa sana kutoka nje...Hata wanaofanya wengi wana mkono mrefu wa kisiasa.

Kenya ni kugumu hapa bongo madogo miaka 25 wanashika pesa ndefu ila kenya sio rahisi ,pesa ipo kenya ila inashikwa na watu wa juu sana ndio maana wanaandamana kisa ugali.
Tanzania biashara kibao mishemishe za kutosha ,hata udalali mtu anapiga pesa nyingi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…