Waafrika tunabaguliwa sana. Tupende vya kwetu. Mtoto huyu ilivyonyanyapaliwa

The Burning Spear

JF-Expert Member
Joined
Dec 23, 2011
Posts
4,118
Reaction score
9,864
Mtoto mweusi arukwa Kavalishwa medali mbele ya camera. Imagine what is happening behind the camera? hawa watu wa nje wanatubagua sana waafrica.

Ndo maana Magufuli alisema tupende n vya kwetu. .. huko nje hatupendwi hata kidogo

Your browser is not able to display this video.
 
Ni kweli huko nje tunabaguliwa sana na hata kutupiwa maganda ya ndizi. Lakini msiba mkubwa zaidi ni yale tunayotendeana sisi kwa sisi. Hatujaliani. Ubinafsi wa kinyama. Ni kila mtu na tumbo lake, familia yake na marafiki zake.

Fisadi mmoja anapoamua kukwapua mabilioni (na sasa tunaambiwa mpaka matrilioni ya shilingi) huku wananchi wenzake hawawezi kumudu hata mlo mmoja kwa siku; na wanaweza hata kukata roho kwa kukosa pesa ya kununua Aspirin huwa ni nini kama siyo unyani wetu na ubinafsi wa kihayawani? Kwa nini tunashangaa tukibaguliwa na hawa wazungu kama sisi kwa sisi tunatendeana unyama huu?

Halafu angalia tunavyojidharau. Utamaduni wetu hatuna. Dini zote za kuletewa. Lugha hali kadhalika. Hata rangi hii nyeusi kusema kweli hatuitaki. Yaani tupo tupo tu kama wasindikizaji hapa duniani.

Hili la kubaguliwa huko nje mimi wala halinishangazi (wala kunihuzunisha) kivile 😬

 
Mtoto mweusi arukwa Kavalishwa medali mbele ya camera. Imagine what is happening behind the camera? hawa watu wa nje wanatubagua sana waafrica...
Dah,hakika inaumiza sana. Hata hivyo binti kajitahidi kujikaza kwa umri wake angeweza kuangusha kilio.

Yani kweli jeuri mwenzio kusudi. Hawa wazungu wamekusudia kufanya ubaya ktk hili jambo ina maana hakuna wa kumkumbusha mtoa medani kuwa amemruka mtoto bila ya kumvalisha?
 
Ni kweli huko nje tunabaguliwa sana na hata kutupiwa maganda ya ndizi. Lakini msiba mkubwa zaidi ni yale tunayotendeana sisi kwa sisi. Hatujaliani. Ubinafsi wa kinyama. Ni kila mtu na tumbo lake, familia yake na marafiki zake...
Mkuu umenena vyema, acha tule matunda ya kile tulichopanda. Ubinafsi ndio unaotuua waafrika.
 
Nyinyi ndio wachokozi huko kwao Huwa mnafuata nini? Mtu akibaguliwa msinishirikishe maana mnapenda kujidai sana mkienda huko
#MWAAFRIKA HULALAMIKA MZUNGU HUTAJIRIKA
 
Thread closed
 
Tatizo wakifika huko huwa wanatuona Sisi tuliopo bongo kama manyani Acha wabaguliwe tuu
 
Hizo ni Chuki Mkuu,jaribu kuwa Moyo wa huruma hata kwa usiowajuwa utakuwa Blessd.
Wabadrike Kwanza , mtu anatupiwa ndizi huko alaf akija huku anatuona Sisi wote hatujastarabika, yaani back anawaona wazungu na tamaduni zao kuwa wa maana ,
 
Unatakiwa ufahamu kuwa chanzo cha ubaguzi wowote ule huwa ni HOFU; hofu inayotokana na aidha inferiority complex au superiority complex. Hivi viwili vyote huwa vinatokana na hofu na huwa vipo kwa mtu yule tu ambaye hayuko sawasawa kichwani
 
Sisi wengine tulisha ishinda iyo Khali tukibaguliwaga ni kama unatupa NEGATIVE MOTIVATION YA KU SUCCEED IN DIFFERENT ENVIRONMENT OCCASION & LIFE
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…