Robert Heriel Mtibeli
JF-Expert Member
- Mar 24, 2018
- 28,297
- 68,017
- Thread starter
- #21
Omy kanifurahisha sana
Hivyo ndivyo watoto wakiume ukiwatelekeza wanavyo-act.
Wapo wengi mtaani ambao sio mashuhuri na karibu wote wanamtazamo Kama wa Ommy
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Omy kanifurahisha sana
Angewekewa ukaribu, inawezekana angebweteka na asingekuwa alivyo leoNi kweli Kabisa.
Lakini kitu ambacho watoto wanacholalamika ni ukaribu na upendo WA mzazi,
Yaani usipompa mtoto hayo mambo umekwisha.
Wanawake ndio utoa lecture ya kumdis mshua iliaonekana shetani namba mbili.
Ndio hivyo mkuu niliachaga mbegu pale stand kuu Mbeya.. sasa sijui mtoto atanitafuta au itakuaje😂😂😂
Nimejikuta nimecheka MKUU
Angewekewa ukaribu, inawezekana angebweteka na asingekuwa alivyo leo
Ndio hivyo mkuu niliachaga mbegu pale stand kuu Mbeya.. sasa sijui mtoto atanitafuta au itakuaje
Na wanakuwa hivyo, kutokana na kutelekezwa; ukijisogeza tu, vyote vinapotea.Sio kweli.
Watoto wengi waliokataliwa ni talented na Gifted
Acha apambane kivyake tumetumwa kuijaza dunia..😀😀
Mtafute dogo acha kukimbia majukumu.
Baba ni Provider, Leader, and protector
Alafu ninachowakubali watoto waliotelekezwa ni makauzu kichizi😂😂
Acha apambane kivyake tumetumwa kuijaza dunia..
Mimi nikishajaza mimba naendelea mbele sigeuki nyuma nadhan ntakua na watoto wengi wasionijua km mimi ndio baba yao...
Na wanakuwa hivyo, kutokana na kutelekezwa; ukijisogeza tu, vyote vinapotea.
Mimi nikishajaza mimba naendelea mbele sigeuki nyuma nadhan ntakua na watoto wengi wasionijua km mimi ndio baba yao...
Ukiwakumbatia hao wa nje, hawatafanikiwa kama inavyotakiwa, kwa sababu utakuwa unafukuza baraka za kufanikiwa kwaoSio kweli.
Watoto wengi waliotelekezwa huja kwa kusudi maalumu, ni Kama unavyomuona Yesu wa Nazareth.
Ukiwakumbatia hao wa nje, hawatafanikiwa kama inavyotakiwa, kwa sababu utakuwa unafukuza baraka za kufanikiwa kwao
Wanawake ndio wanamezesha sumu. Mtoto wangu wa kwanza mama yake anampa sumu sana kuhusu mimi wakati huwa namtafuta kwenda kumjulia hali na hela natoa ila mama sababu tuna ugomvi anaihamisha hadi kwa mtoto.Watoto wanaakili Wewe!
Usifikiri hawajui kile wanachokiona
Umegunduaje? Labda alijipa kabila la mama aiseeLe ndio tumegundua Ommy dimpoz ni mfipa na sio Muha Wala mmanyema
Hio situation ipo na kwangu,nimeamua kutulia na mwisho wa siku nimemwambia huyo mwanamke acha mm nibaki baba jinaWanawake ndio wanamezesha sumu. Mtoto wangu wa kwanza mama yake anampa sumu sana kuhusu mimi wakati huwa namtafuta kwenda kumjulia hali na hela natoa ila mama sababu tuna ugomvi anaihamisha hadi kwa mtoto.
Nami kwa jeuri hata akinikataa huko mbele ni poa tu.
Na sisi tuliolea watoto wa wanaume wenzetu kisha wakatukimbia baada ya kufanikiwa, wakawatafuta baba zao halisi, unatushauri nini?Anaandika, Robert Heriel
Sakata la Ommy Dimpoz na baba yake linanifanya na mimi nipigilie msumari kusisitiza.
Kuna wanaume wenye tabia za kizamani kuwa ati, anaacha kwa makusudi kabisa kulea mtoto wake halafu anakuwa na mtazamo kuwa; "Akikua atanitafuta, atamtafuta baba yake". Hiyo tabia ipo na baadhi ya sisi wanaume.
Mtoto haramu,
Mtoto wa uzinzi,
Mtoto wa single mother,
Mtoto chokoraa,
Mtoto asiye na baba,
Mtoto wa nje!
Na majina mengine kama hayo licha ya kuwa yalikuwa adhabu kwa mtoto wako, hukupata muda wa kumfariji na kumuonyeshea ukaribu wako kama baba. Wewe kama baba ukachangia kwa sehemu kubwa kumuumiza mtoto kwa kile kiitwacho kutafuta maisha, kile kiitwacho ujana, kile kiitwacho magomvi yako na mama yake na sababu zingine.
Leo mtoto anakuwa, anajiweza, unafikiri atakuheshimu, unafikiri atakupenda, unafikiri atakuchukulia wewe ni baba yake? Kama wewe hukumchukulia kama mtoto wake ni ngumu yeye kukuchukulia kama baba yake. Yeye anakuona kama watu wengine, kama wewe ulivyomuona kama watoto wengine.
Ooh! Hujajua maisha, ooh huyo ni baba yako. Ndiyo ni baba lakini simchukulii kama baba, kama yeye alivyokuwa hanichukulii kama mwanaye. Mila na desturi za kijingajinga kuendekeza upuuzi ndiyo zimeifikisha Afrika hapa ilipo. Unafiki unafiki kila mahali.
Kama ulisema mtoto atakutafuta kaa usubiri mpaka utafutwe na mwanao sio usubiri amekua na kujiweza ndio uanze kumsumbua dogo.
Na dunia ilivyombaya sasa, yule uliyemtelekeza ndio Mungu anapigilia baraka hukohuko, ili akufundishe.
Mtoto wako ambaye mara nyingi ulikuwa unamuona hana msaada kwako ndiye mara nyingi baadaye huwa jiwe kuu la msingi katika sehemu ambayo wengine wote hawana uwezo wa kukusaidia.
Wanaume tujitahidi kulea watoto wetu, iwe waliozaliwa kwa bahati nasibu au wale tuliopanga. Na kama tutaamua kutelekeza basi tusisumbue watoto wetu tuliowatelekeza.
Msamaha sio lazima. Msamaha ni neema tuu ambayo siyo haki ya mkosaji. Hivyo mtoto atakavyotuchukulia ni sawa tuu, tusiwe watu wa kulalamika.
Huwezi hukumiwa na Mungu kwa kushindwa kusamehe watu. Hakuna sheria ya hivyo. Kama vile Mungu anavyosamehe apendavyo ndivyo na wewe/mimi unatoa msamaha vile upendavyo na siyo kwa shinikizo.
Mwisho, watoto waliotelekezwa kama itawapendeza mnaweza wasamehe wazazi wenu. Ingawaje najua hakuna uwezekano wa kuwa na ukaribu au mazoea ya mzazi aliyekutelekeza. Siyo baba tu hata mama. Kama hajakulea ni ngumu kuwa na ukaribu na upendo naye.
Hivyo ndivyo karma inavyofanya kazi.
Robert Heriel,
Taikon wa Fasihi,
Kwa sasa Dar es Salaam.
Hizi mambo zimewahi kunikuta nikiwa mdogo,baada ya kuachana wazazi,mama yangu hakutaka msaada wowote ule wa baba,ilifikia hatua hata mshua akileta nguo alizichoma moto,baadae mshua akaamua kukaa pembeni na kutojihusisha na kutoa matunzo yoyote yale kwangu,ulipofika umri wa shule alinipa majina ya baba wa kambo aliyemuoa wakati huo,nilisoma mpaka chuo kikuu nikitumia hayo majina,nimebahtika kupata ajira,sasa nikipata kidgo namtumia biological father,hiyo hali ya kumtumia pesa baba yangu mzazi,mama yangu imekuwa inamkera mno ni vile tu nimekuwa mtu mzima anashindwa kunikemea au kunipangia ila anaumia sana! So wakati mwengine mama zetu huchangia hiyo hali,ndo maana mimi siwezi kutupa lawama kwa baba yake dimpoz,hatujui huko walikuwaje na mzazi mwenzake.Anaandika, Robert Heriel
Sakata la Ommy Dimpoz na baba yake linanifanya na mimi nipigilie msumari kusisitiza.
Kuna wanaume wenye tabia za kizamani kuwa ati, anaacha kwa makusudi kabisa kulea mtoto wake halafu anakuwa na mtazamo kuwa; "Akikua atanitafuta, atamtafuta baba yake". Hiyo tabia ipo na baadhi ya sisi wanaume.
Mtoto haramu,
Mtoto wa uzinzi,
Mtoto wa single mother,
Mtoto chokoraa,
Mtoto asiye na baba,
Mtoto wa nje!
Na majina mengine kama hayo licha ya kuwa yalikuwa adhabu kwa mtoto wako, hukupata muda wa kumfariji na kumuonyeshea ukaribu wako kama baba. Wewe kama baba ukachangia kwa sehemu kubwa kumuumiza mtoto kwa kile kiitwacho kutafuta maisha, kile kiitwacho ujana, kile kiitwacho magomvi yako na mama yake na sababu zingine.
Leo mtoto anakuwa, anajiweza, unafikiri atakuheshimu, unafikiri atakupenda, unafikiri atakuchukulia wewe ni baba yake? Kama wewe hukumchukulia kama mtoto wake ni ngumu yeye kukuchukulia kama baba yake. Yeye anakuona kama watu wengine, kama wewe ulivyomuona kama watoto wengine.
Ooh! Hujajua maisha, ooh huyo ni baba yako. Ndiyo ni baba lakini simchukulii kama baba, kama yeye alivyokuwa hanichukulii kama mwanaye. Mila na desturi za kijingajinga kuendekeza upuuzi ndiyo zimeifikisha Afrika hapa ilipo. Unafiki unafiki kila mahali.
Kama ulisema mtoto atakutafuta kaa usubiri mpaka utafutwe na mwanao sio usubiri amekua na kujiweza ndio uanze kumsumbua dogo.
Na dunia ilivyombaya sasa, yule uliyemtelekeza ndio Mungu anapigilia baraka hukohuko, ili akufundishe.
Mtoto wako ambaye mara nyingi ulikuwa unamuona hana msaada kwako ndiye mara nyingi baadaye huwa jiwe kuu la msingi katika sehemu ambayo wengine wote hawana uwezo wa kukusaidia.
Wanaume tujitahidi kulea watoto wetu, iwe waliozaliwa kwa bahati nasibu au wale tuliopanga. Na kama tutaamua kutelekeza basi tusisumbue watoto wetu tuliowatelekeza.
Msamaha sio lazima. Msamaha ni neema tuu ambayo siyo haki ya mkosaji. Hivyo mtoto atakavyotuchukulia ni sawa tuu, tusiwe watu wa kulalamika.
Huwezi hukumiwa na Mungu kwa kushindwa kusamehe watu. Hakuna sheria ya hivyo. Kama vile Mungu anavyosamehe apendavyo ndivyo na wewe/mimi unatoa msamaha vile upendavyo na siyo kwa shinikizo.
Mwisho, watoto waliotelekezwa kama itawapendeza mnaweza wasamehe wazazi wenu. Ingawaje najua hakuna uwezekano wa kuwa na ukaribu au mazoea ya mzazi aliyekutelekeza. Siyo baba tu hata mama. Kama hajakulea ni ngumu kuwa na ukaribu na upendo naye.
Hivyo ndivyo karma inavyofanya kazi.
Robert Heriel,
Taikon wa Fasihi,
Kwa sasa Dar es Salaam.
Hahahaha!Na sisi tuliolea watoto wa wanaume wenzetu kisha wakatukimbia baada ya kufanikiwa, wakawatafuta baba zao halisi, unatushauri nini?