Wababa mliotelekeza watoto subirini mpaka mtafutwe na watoto wenu, acheni usumbufu!

huu msumari wa moto sana natamani baba yangu angekuja kuusoma... amenivuruga utotoni baadae nishakuwa mkubwa amekuja kusikia mwanaye nipo zangu canada nakula maisha anahangaika kuwasumbua ndugu kutaka nimtafute how comes? ikiwa alinitelekeza mimi na mama yangu mzazi ? ubarikiwee
 

Unafikiri Ommy Dimpoz ni mjinga au Hana haki au Hana akili Kama wewe?

scenario yako na ommy ni mbingu na Ardhi.
Umemaliza Chuo lakini unashindwa kuona utofauti wa Stori ya Ommy Dimpo na yako. Kweli elimu haimfanyi mtu kuwa na uwezo wa kuchambua Mambo.

Wewe Baba yako alikuwa anania na anaonyesha Nia yake na upendo wako kwako lakini Mama alikuwa anakataa,
OmmyDimpo maelezo yake ni kuwa Mzee Hakuwa na time naye.

Ommy Dimpo yupo wazi Kabisa kuwa yupo tayari kupata Laana kama anakosea wewe bado huoni tuu.
 

Yaani mtoto umhudumie alafu apandikizwe chuki ikubali? Hiyo haliwezekaniki!
WATOTO wanaakili, wanaona, wanasikia,
Wanajua Mama anakosea, au Baba anakosea.

Ukionana na mwanao mpe pesa yeye, mpe vitu yeye alafu uone mama hizo sumu za Mama yake zitafanya kazi.

Mama akimuambia Baba yako hakuhudumii alafu kweli humhudumii hiyo sio sumu, huo ni ukweli anamuambia ili aone kuwa anababa asiyejielewa.

Wanaume lazima tubadilike
 
Ndio mama yako alivyofanya?

Muulize Mama yake akifanya Jambo Baya au Baba yake akifanya Jambo Baya Hana uwezo wa kuliona?

Ni kweli mtoto anaweza kudanganywa lakini kuna umri akifika hasa umri wa kupevuka anaanza kujua mbivu na mbichi.

Tukubali tuu kuwa kama kuna watoto tumetelekeza iwe Kwa sababu yoyote basi tukubali matokeo tuu
 
Nimemuuliza makusudi najua hajalelewa na mama ila watu kama huyu ndio wanaongeza kusema akina mama wanapandikiza chuki Kwa watoto.
 
Na wewe mama yako alikupandikiza chuki?
Sana tu! Tena ilifikia hatua wakishirikiana na baba wa kambo ambaye nilikuwa natumia majina yake shuleni,walikuwa wananimbia negative kuhusu mzee,mara mshirikina,nikimuona nisimsalimie,na kweli ilifika kipindi nikienda likizo kumuona auncle,akija nilikuwa simsalimii kabisa! Na nilikuwa namkimbia.hahahaha
 

Hii ndio comment ya kikubwa kabisa imekaa poa sana wengine wanakoment kwa mihemko tu
 
Omy dimpoz atakua anaujua ukweli, achukue hatua stahiki kulingana na ukweli wake.Na inaonekana media ndo zimewaunganisha tunamuachia yeye ndo mwanuzi wa mwisho.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…