Tetesi: Wabunge kumpigia kura Spika wa Bunge kutokuwa na imani

Stuka

JF-Expert Member
Joined
Jul 19, 2022
Posts
282
Reaction score
906
Kuna tetesi kuwa baadhi ya wabunge wamejipanga kuwasilisha hoja bungeni ya kutokuwa na imani na Spika wa Bunge, Dk. Tulia Ackson baada ya kuonekana wazi kushindwa kuuongoza mhimili huo kwa manufaa ya watanzania.

Hatua ya wabunge hao inakuja baada ya Spika kuzima ajenda za wananchi ambapo baadhi ya wabunge walitaka masuala hayo yajadiliwe bungeni yeye akayazuia yote wengine wakimlaumu kuwa ana mgongano wa maslahi na ya kifamilia kutokana na mumewe kuwa boss wa ewura.

Tetesi kubwa ni kwamba wabunge wanachukizwa na kitendo cha Spika kukalia ripoti ya CAG kwa sababu walioguswa ana mahusiano nao ya kifamilia na wengine kuwa na mgongano mkubwa wa maslahi.

Baadhi ya Wabunge wametetea kuwa suala la Mumewe Spika kuwa MD wa Ewura hailizuii Bunge kujadili matatizo yaliyoko kwenye Wizara ya Nishati eti kwa sababu ya mumewe wa Spika.

(i) Hoja ya kujadili Ripoti ya CAG (Mhe. Ole Sendeka)
(ii) Hoja ya kujadili uvamizi wa tembo kwa wananchi( Mhe. Bahati)
(iii)Hoja ya tatizo la mbolea na kufutiwa leseni mawakala wa mbolea( Mhe. Msambatavangu)
(iv)Hoja ya ajira kutolewa kwa upendeleo (Mh. Mwita Waitara)
 
Spika anapozuia bila kutoa maelezo ya maana huwa ana maana gani? Yeye anasimamia bunge la wananchi wa Nchi ya Wapi?
 
Hizo tetesi ni zako mwenyewe na hoja zilizotajwa hazina mashiko
 
Dde, ewe
 
Labda kama ni wabunge wa Kenya au Zambia,lakini hapa kwetu ni ndoto ya mchana,amka unaweza kukojoa kitandani.
 
Kiukweli yanayoendelea bungeni yanasikitisha sana.

Natamani Watanzania waamke kutoka usingizi wa pono tuwavue UWAZIRI mawaziri wote kudadeki.

Yaani jinsi Ndalichako alivyotetea KIKOKOTOO na Jenista Mhagama alivyotetea ajira ambayo ilikuwa hoja ya Esther Matiko INAUMIZA SANA.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…