Wabunge tuache kufananisha awamu ya Tano na ya Sita, tunakosea sana

Wabunge tuache kufananisha awamu ya Tano na ya Sita, tunakosea sana

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
13,778
Reaction score
14,214
Awamu ya Tano haikuwa awamu ya Sayansi, Sheria na Demokrasia. Ilikuwa ni awamu ya mambo yaende yatake yasitake, utake usitake. Awamu ya Tano iliamini kuwa sayansi, sheria na demokrasia ni nyenzo za kuchelewesha mambo kwa kuongeza ukiritimba.

Awamu ya Tano iliendesha nchi kama vile dereva anaendesha gari bovu limfikishe angalau sehemu salama hata kama kwa kuendelea kuliharibu zaidi na kuzidisha gharama za matengenezo baadaye kwa atakaetaka kulitengeneza.

Lazima tukubali kuwa awamu ya Tano kuna mambo imeyafanya vizuri sana, lakini Kuna ambayo imeyaharibu zaidi pia na yanaongeza gharama kwa awamu ya Sita na pengine na zijazo nyingi.

Baadhi ya mambo iliyoyaharibu zaidi ni demokrasia, utawala wa sheria, uhusiano wa kimataifa, kuhamia Dodoma, TANESCO, korosho, baadhi ya miradi mikubwa na biashara.

Awamu iliamini kuwa awamu zilizopita hazikuwa makini kwenye kila kitu hivyo ilitaka kurekebisha mapungufu ya awamu zote zilizopita kwenye awamu ya Tano. Rais wa Awamu ya tano aliamini kuwa aliletwa na Mungu kuikomboa Tanzania ili ifike kule walipo wazungu na pengine kuwapita. Kazi hii isingekuwa sawa na rahisi hata kidogo kwakuwa shida nyingi za Tanzania zinatoka nje ya Tanzania (neo colonialism, world trade market, IMF, UN, WB, EU, religions, NATO, etc.) ambazo zinautafuna uchumi na maisha yetu.

Hata kama hutaki na wala hupigani ni lazima ukanunue silaha kali na ya kisiasa kwa bei kubwa sana kwao hata kama silaha hiyo hutaitumia, maana jirani zako unaamini kuwa wanayo silaha ya aina hiyo. Maghala yetu ya silaha yamejaa silaha nyingi zilizonunuliwa kwa fedha nyingi sana ambazo zingetosha kusomesha watoto wote vyuo vikuu bure, kutoa ruzuku kwa wakulima na hata kujenga zahaniti kila kijiji. Silaha hizi zinakaa mpaka zina expire na kuagiza nyingine
 
Naomba kujibiwa unapo sema awamu ya sita na awamu ya tano una manisha nini .... umetumia vigezo gani kutofautisha hizi awamu ... sheria ipi ... msaada tafadhali
 
Awamu ya tano tanesco na kuhamia dodoma kuliharibu kitu gani mkuu?
Sababu za kuhamia Dodoma alizozieleza Nyerere enzi zake bado zina umuhimu ktk zama hizi? Jiwe alikuwa anapoteza fedha za walipa kodi tu.

Kujenga bwawa la Nyerere likalogharimu trilioni kumi na tatu kwa miaka 13 halafu akatelekeza mradi wa kuzalisha umeme kwa kutumia gesi anabo upo hatua nzuri, unaona alikuwa na akili yule jiwe?
 
Awamu ya Tano haikuwa awamu ya Sayansi, Sheria na Demokrasia. Ilikuwa ni awamu ya mambo yaende yatake yasitake, utake usitake. Awamu ya Tano iliamini kuwa sayansi, sheria na demokrasia ni nyenzo za kuchelewesha mambo.

Awamu ya Tano iliendesha nchi kama vile dereva anaendesha gari bovu limfikishe sehemu salama hata kwa kuendelea kuliharibu zaidi na kuzidisha gharama za matengenezo baadaye.

Lazima tukubali kuwa awamu ya Tano kuna mambo imeyafanya vizuri sana lakini Kuna ambayo imeyaharibu zaidi na yanaongeza gharama kwa awamu ya Sita na pengine na zijazo nyingi.

Baadhi ya mambo iliyoyaharibu zaidi ni demokrasia, utawala wa sheria, uhusiano wa kimataifa, kuhamia Dodoma, TANESCO, korosho, baadhi ya miradi mikubwa na biashara.

Awamu iliamini kuwa awamu zilizopita hazikuwa makini kwenye kila kitu hivyo ilitaka kurekebisha mapungufu Yao yote kwenye awamu ya Tano. Kazi hii isingekuwa sawa na rahisi hata kidogo kwakuwa shida nyingi za Tanzania zinatoka nje ya Tanzania (neo colonialism, world trade market, IMF, UN, WB, EU, religions, etc.) ambazo zinautafuna uchumi wetu.

Hata kama hutaki lazima ukanunue silaha kali na ya kisiasa kwa bei kubwa sana kwao hata kama silaha hiyo hutaitumia, maana jirani zako wanayo silaha ya aina hiyo.
Kwani uwongo awamu zilizopita zilikaribia kuuza nchi, na ya sasa wanamalizia kabisa
 
Awamu ya Tano haikuwa awamu ya Sayansi, Sheria na Demokrasia. Ilikuwa ni awamu ya mambo yaende yatake yasitake, utake usitake. Awamu ya Tano iliamini kuwa sayansi, sheria na demokrasia ni nyenzo za kuchelewesha mambo.

Awamu ya Tano iliendesha nchi kama vile dereva anaendesha gari bovu limfikishe sehemu salama hata kwa kuendelea kuliharibu zaidi na kuzidisha gharama za matengenezo baadaye.

Lazima tukubali kuwa awamu ya Tano kuna mambo imeyafanya vizuri sana lakini Kuna ambayo imeyaharibu zaidi na yanaongeza gharama kwa awamu ya Sita na pengine na zijazo nyingi.

Baadhi ya mambo iliyoyaharibu zaidi ni demokrasia, utawala wa sheria, uhusiano wa kimataifa, kuhamia Dodoma, TANESCO, korosho, baadhi ya miradi mikubwa na biashara.

Awamu iliamini kuwa awamu zilizopita hazikuwa makini kwenye kila kitu hivyo ilitaka kurekebisha mapungufu Yao yote kwenye awamu ya Tano. Kazi hii isingekuwa sawa na rahisi hata kidogo kwakuwa shida nyingi za Tanzania zinatoka nje ya Tanzania (neo colonialism, world trade market, IMF, UN, WB, EU, religions, etc.) ambazo zinautafuna uchumi wetu.

Hata kama hutaki lazima ukanunue silaha kali na ya kisiasa kwa bei kubwa sana kwao hata kama silaha hiyo hutaitumia, maana jirani zako wanayo silaha ya aina hiyo.
@Kinuju Crimea Magonjwa Mtambuka Nyani Ngabu na Nigrastratatract watakujibu
 
Sababu za kuhamia Dodoma alizozieleza Nyerere enzi zake bado zina umuhimu ktk zama hizi? Jiwe alikuwa anapoteza fedha za walipa kodi tu.

Kujenga bwawa la Nyerere likalogharimu trilioni kumi na tatu kwa miaka 13 halafu akatelekeza mradi wa kuzalisha umeme kwa kutumia gesi anabo upo hatua nzuri, unaona alikuwa na akili yule jiwe?
Bwawa la nyerere trillion 13?? Ni trillion 6.5
 
Hii yaweza kuwa Chupa Tofauti Mvinyo ule ule AU Mvinyo Tofauti Chupa ile ile....

Si hawa hawa ndio walikuwepo hizo so called Awamu Tofauti ?
 
Bwawa la nyerere trillion 13?? Ni trillion 6.5
Weee! Kakwambia nani? Soma ripoti mpya. Wanakwambia mpk kukamilka litatumia trilioni 13 na kukamilka ni miaka 13.

Jiwe alikuwa mpotoshaji na mlipuaji. Unakumbuka mabweni ya bilioni kumi yalivyokuwa na expansion joint??
 
Awamu ya tano👇🤡🤡🤡
16454615872191.jpg
 
Awamu ya Tano haikuwa awamu ya Sayansi, Sheria na Demokrasia. Ilikuwa ni awamu ya mambo yaende yatake yasitake, utake usitake. Awamu ya Tano iliamini kuwa sayansi, sheria na demokrasia ni nyenzo za kuchelewesha mambo.

Awamu ya Tano iliendesha nchi kama vile dereva anaendesha gari bovu limfikishe sehemu salama hata kwa kuendelea kuliharibu zaidi na kuzidisha gharama za matengenezo baadaye.

Lazima tukubali kuwa awamu ya Tano kuna mambo imeyafanya vizuri sana lakini Kuna ambayo imeyaharibu zaidi na yanaongeza gharama kwa awamu ya Sita na pengine na zijazo nyingi.

Baadhi ya mambo iliyoyaharibu zaidi ni demokrasia, utawala wa sheria, uhusiano wa kimataifa, kuhamia Dodoma, TANESCO, korosho, baadhi ya miradi mikubwa na biashara.

Awamu iliamini kuwa awamu zilizopita hazikuwa makini kwenye kila kitu hivyo ilitaka kurekebisha mapungufu Yao yote kwenye awamu ya Tano. Kazi hii isingekuwa sawa na rahisi hata kidogo kwakuwa shida nyingi za Tanzania zinatoka nje ya Tanzania (neo colonialism, world trade market, IMF, UN, WB, EU, religions, etc.) ambazo zinautafuna uchumi wetu.

Hata kama hutaki lazima ukanunue silaha kali na ya kisiasa kwa bei kubwa sana kwao hata kama silaha hiyo hutaitumia, maana jirani zako wanayo silaha ya aina hiyo.

Wewe bana, panua kwanza uwezo wa kufikili ndo uandike uzi.

Umejiandikia tu bila kudadavua vizuri. Kicha cha babari ni tofauti na ulichoandika. Huna uwezo wa kuunganisha mawazo.
 
Awamu ya Tano haikuwa awamu ya Sayansi, Sheria na Demokrasia. Ilikuwa ni awamu ya mambo yaende yatake yasitake, utake usitake. Awamu ya Tano iliamini kuwa sayansi, sheria na demokrasia ni nyenzo za kuchelewesha mambo.

Awamu ya Tano iliendesha nchi kama vile dereva anaendesha gari bovu limfikishe sehemu salama hata kwa kuendelea kuliharibu zaidi na kuzidisha gharama za matengenezo baadaye.

Lazima tukubali kuwa awamu ya Tano kuna mambo imeyafanya vizuri sana lakini Kuna ambayo imeyaharibu zaidi na yanaongeza gharama kwa awamu ya Sita na pengine na zijazo nyingi.

Baadhi ya mambo iliyoyaharibu zaidi ni demokrasia, utawala wa sheria, uhusiano wa kimataifa, kuhamia Dodoma, TANESCO, korosho, baadhi ya miradi mikubwa na biashara.

Awamu iliamini kuwa awamu zilizopita hazikuwa makini kwenye kila kitu hivyo ilitaka kurekebisha mapungufu Yao yote kwenye awamu ya Tano. Kazi hii isingekuwa sawa na rahisi hata kidogo kwakuwa shida nyingi za Tanzania zinatoka nje ya Tanzania (neo colonialism, world trade market, IMF, UN, WB, EU, religions, etc.) ambazo zinautafuna uchumi wetu.

Hata kama hutaki lazima ukanunue silaha kali na ya kisiasa kwa bei kubwa sana kwao hata kama silaha hiyo hutaitumia, maana jirani zako wanayo silaha ya aina hiyo.
Umeme (Tanesco) na kuhamia Dodoma ni kati ya project bora za awamu ya 5 na hakuna ambaye angeweza kufanya zaidi ya pale kwa sababu zifuatazo;

Umeme Tanzania ulikuwa jipu lisilotumbulika lakini JPM aliweza kadili nalo na Tanesco wakakaa sawa, umeme haukukatika hovyo hovyo kama awamu ya 4 na sasa hivi ya 6. Hapa usije na sababu zenu ooh haikufanyiwa matengenezo na blabla kibao ukweli ni kuwa mitambo yote kama hufanyi matengenezo ita knock down tu sasa kwanini haikunock kipindi cha JPM? Sababu ni kuwa matengenezo yalifanyika kwa wakati na kwa weledi wa hali ya juu. Ila awamu ya 4 na 6 umeme umekuwa na utaendelea kuwa chocho za kupigia dili ukizingatia Waziri ni wa mchongo.

Kuhamia Dodoma, hakuna Rais angekuwa na uthubutu zaidi ya JPM kuhusu Selikari kuhamia Dodoma. Mnachotafuta sasa ni justification na sympathy za kurudi Dar mlete foleni. JPM amewaachia mji mzuri kazi kwenu kufanya finishing ili mji upendeze ila msije Dar mtaongeza joto na tuliopo huku tunatosha msije Dar kama hamtaki Dodoma amieni Zanzibar.
 
Hakuna awamu ya sita kwani tumefanya uchaguzi lini ? Mama anamalizia ngwe ya mwendazake.
Rais wa Zanzibar Abood Jumbe kama sikosei by then alipojiuzulu wakati kipindi chake kikwa bado hakijamalizika na akaapishwa Rais mwingine,aliyeapishwa alibaki kuwa wa awamu ya Jumbe ama alikuwa na awamu yake?
 
Back
Top Bottom