Wabunge wataka Condester Sichwale aliyetolewa nje kisa mavazi aombwe radhi

Wabunge wataka Condester Sichwale aliyetolewa nje kisa mavazi aombwe radhi

Sakata la kutolewa nje kwa mbunge wa Momba, Condester Sichwale (CCM) kuhusu mavazi, limeibuka tena leo jioni katika kikao cha Bunge baada ya wabunge wanawake kutaka aombwe radhi na aliyetoa hoja.

Hata hivyo mbunge Hussein Amar amesema hawezi kuomba radhi kwa sababu alichosema alikuwa sahihi kwakuwa mavazi aliyovaa mbunge mwenzake hayakuwa na staha ndiyo maana Spika wa Bunge Job Ndugai aliridhia hoja aliyoitoa yeye (Amar).

Katika kikao cha leo jioni wabunge Jacqueline Ngonyani na Stella Manyanya waliomba mwongozo wa Spika kwa madai mbunge aliyetolewa nje alionewa.

Mapema leo Sichwale alitolewa nje kwa amri ya Spika baada ya Amar kuomba mwongozo kwa kutumia kanuni 170 kuhusu mavazi ya staha.

Ngonyani amesema kilichotokea ni kwamba mbunge huyo alionewa kwani alikuwa na vazi la staha ambalo halikuwa na shida lakini akasema huenda Spika hakuona.

"Mimi ni mjumbe wa Baraza Kuu la wanawake wa CCM, ninapoona kuna uonevu lazima niseme na hili sikiungi mkono huyu mwanamke mwenzetu ameonewa,"amesema Ngonyani.

Mbunge huyo amesisitiza kuwa uonevu wa namna hiyo haupaswi kuvumiliwa kwakuwa umemdhalilisha mbunge huyo na wapiga kura wake jimboni.

Kwa upande wake Manyanya amesema tangu asubuhi alikuwa anafuatilia kwenye mitandao na amebaini kuwa Sichwale hakuwa na vazi baya.

Hata hivyo Manyanya amesema haiwezekani wabunge vijana wavae mavazi kama wanayovaa wabunge wanawake watu wazima.

Amesema katika siku za karibuni limeibuka suala la kutoa lugha za kuwadhalilisha wabunge wanawake ndani ya ukumbi ambako wakati mwingine hutamkwa kiungo cha mwanamke halafu wengine wanafurahi.

Naibu Spika Dkt. Tulia Akson amesema atatoa mwongozo baada ya kufuatilia jambo hilo.

Hakuna ulazima wa kusema mbuge wa ccm,maana binge zima ni ccm,inatosha tu kusema mbunge wa Jimbo gani basi
 
Kwa kumchukua Magufuli, Mungu ametenda haki kabisa. Huwezi kuwafanya watu wajinga kwamba wewe ndio mwenye akili wa kuwachagulia watu viongozi wa kuwaongoza tena huku ukiwakejeli.

Utukufu wa Mungu utadumu milele na milele, Amina.
 
Sketi ikibana sio shida ila suluali ikibana ni shida, mupitie upya kanuni ya mavazi! Pia naona mavazi yote yaruhusiwe tu, cha msingi suluali isibane kwenye lisani au kwa mbele, spika afutilie ilo tu!
Kwani ikibana huko mbele au nyuma kuna tatizo gani? Mbunge ameenda kujadili hoja au kuangalia matako?
 
Unamaanisha yule mzee ni muislamu?
Hivi wanawake wasiokuwa waislamu hawavai hijabu? Pale bungeni hapakuwa na wanawake wengine ambao hawakuvaa hijabu? Kwanini amseme yule tu
Hujamuona na barakashia?
 
Huyu mbunge wangu naona sasa kazi imemshinda, watu wake wa jimbo tuna changamoto nyingi mfano maji vijiji vingi havina maji mradi wa maji kutoka ziwa victoria pale nyamtukuza haujakamilia sasa kageukia kuangalia akinadada wamevaa nini bungeni badala ya kusimamia hoja za msingi juu ya wananchi wake
Kwa hiyo kila apatapo nafasi ya kuongea AONGELEE MRADI WENU WA MAJI hata kama hoja mezani ni MADINI ama WIZARA YA MICHEZO ?!!!
 
Hakukuwa na shida na vazi la mbunge huyo...

Ni wazi kuna shida nyingine tu binafsi za baadhi ya wabunge wa kiume na baadhi ya wanawake na Spika pasipo kujiuliza mara mbili anakubali kuingia ktk mkenge huo...

Kuna wanawake wengine wana maumbo maalumu. Hata wavaeje tu, maumbo utayaona kwa uwazi sana na kama wewe ni mwanaume usiyeweza kudhibiti hisia zako za kingono, utamtamani tu mwanamke huyo huku ukijua huwezi kumpata...

Nadhani huyu mbunge wa kiislamu alitaka huyu mwanamke akavae ushungi au baibui - lile vazi maalumu la wanawake wa kiislamu
View attachment 1805717
Hao hapo wote ni wabunge na walikuwa ndani ya bunge Jana tarehe 1/6/202. Kulia ni Catherine Maggie na wa kushoto kwako kwenye picha ni Condester Schwale...

Sichwale aliyolewa nje lakini Catherine Magige alibaki ndani ya bunge akiendelea na shughuli kama kawaida kwamba, yeye yuko vizuri...

Mimi nasema, hili sakata halihusiani na mavazi. Kuna kitu nyuma ya pazia na bahati mbaya ni kuwa uongozi wa bunge unakubali kuyumbishwa na personal interests za baadhi ya wabunge kudhalilisha baadhi ya wabunge wanawake...
Kwa mtazamo wangu nimeona pana aidha:-
1. Ushabiki wa vilabu vya Simba na Yanga. Kumbuka Spika ni kama si mwanachama basi ni shabiki kindakindaki wa klabu ya Simba.
2. Mfumo dume. Hapa na maana mtoa hoja kwa sababu zake tu ni mwanaume na Spika ni mwanaume nae hakumwangusha, angelikuwa Spika ni jinsia ya kike angejiridhisha kwanza kabla ya kutoa maamuzi.
 
Hakukuwa na shida na vazi la mbunge huyo...

Ni wazi kuna shida nyingine tu binafsi za baadhi ya wabunge wa kiume na baadhi ya wanawake na Spika pasipo kujiuliza mara mbili anakubali kuingia ktk mkenge huo...

Kuna wanawake wengine wana maumbo maalumu. Hata wavaeje tu, maumbo utayaona kwa uwazi sana na kama wewe ni mwanaume usiyeweza kudhibiti hisia zako za kingono, utamtamani tu mwanamke huyo huku ukijua huwezi kumpata...

Nadhani huyu mbunge wa kiislamu alitaka huyu mwanamke akavae ushungi au baibui - lile vazi maalumu la wanawake wa kiislamu
View attachment 1805717
Hao hapo wote ni wabunge na walikuwa ndani ya bunge Jana tarehe 1/6/202. Kulia ni Catherine Maggie na wa kushoto kwako kwenye picha ni Condester Schwale...

Sichwale aliyolewa nje lakini Catherine Magige alibaki ndani ya bunge akiendelea na shughuli kama kawaida kwamba, yeye yuko vizuri...

Mimi nasema, hili sakata halihusiani na mavazi. Kuna kitu nyuma ya pazia na bahati mbaya ni kuwa uongozi wa bunge unakubali kuyumbishwa na personal interests za baadhi ya wabunge kudhalilisha baadhi ya wabunge wanawake...
Kwa nini mbunge huyo atake huyo dada tu ndio avae vazi la Kiislam ?!!!

Na kwanini iwe jana tu ikiwa siku zote huwa anamuona ?!!

Ama siku nyinginezo huyo mh.Condester huwa anavaa hilo vazi la Kiislam alitakalo mbunge wa Nyang'wahale kiasi kwamba huridhika nafsi yake ?!!!

Je alipoomba mwongozo wa kikanuni na ikiwa SPIKA hajaukubali ,mbunge Condester angetolewa nje?!!

Je mbunge Condester ametolewa nje na mbunge wa Nyang'wahale ama na KITI cha mh.Spika?!!!
 
Ungemuuliza kwani kuna dini inayoruhusu kuvaa uchi?
Tuache ya huyo mbunge, kuna dini inaruhusu?
Siwezi kumuuliza Kwani mimi si muumini wa hizo mada za "udini" anazozipenda sana huyo jaji mfawidhi....

Huyu angekuwa Jaji wa ukweli angehukumu na kubagua watu "kidini" 🤣🤣

Kweli Afrika imejaa "mateka" wa hayo mambo ya "udini"....
 
Hahahaaaa! Mzee wa Nyang'wale kaingia cha kike.

Hivi jimbo la Nyang'wale liko mkoa wa Kilimanjaro?!

Huyo Mbunge wakampime huenda akawa na matatizo ya mfadhaiko kila anapoona chura! haiwezekani mama wa watu kavaa kawaida kabisa yeye akamsagia kunguni kwa Sipika
 
Huyo Mbunge wakampime huenda akawa na matatizo ya mfadhaiko kila anapoona chura! haiwezekani mama wa watu kavaa kawaida kabisa yeye akamsagia kunguni kwa Sipika
🤣🤣mmh mbona hilo "lichura "usemalo sijaliona ?!!

Kwani humo ndani hakuna wenye hizo "chura" zaidi ya "mlengwa" ?!!
 
Sakata la kutolewa nje kwa mbunge wa Momba, Condester Sichwale (CCM) kuhusu mavazi, limeibuka tena leo jioni katika kikao cha Bunge baada ya wabunge wanawake kutaka aombwe radhi na aliyetoa hoja.

Hata hivyo mbunge Hussein Amar amesema hawezi kuomba radhi kwa sababu alichosema alikuwa sahihi kwakuwa mavazi aliyovaa mbunge mwenzake hayakuwa na staha ndiyo maana Spika wa Bunge Job Ndugai aliridhia hoja aliyoitoa yeye (Amar).

Katika kikao cha leo jioni wabunge Jacqueline Ngonyani na Stella Manyanya waliomba mwongozo wa Spika kwa madai mbunge aliyetolewa nje alionewa.

Mapema leo Sichwale alitolewa nje kwa amri ya Spika baada ya Amar kuomba mwongozo kwa kutumia kanuni 170 kuhusu mavazi ya staha.

Ngonyani amesema kilichotokea ni kwamba mbunge huyo alionewa kwani alikuwa na vazi la staha ambalo halikuwa na shida lakini akasema huenda Spika hakuona.

"Mimi ni mjumbe wa Baraza Kuu la wanawake wa CCM, ninapoona kuna uonevu lazima niseme na hili sikiungi mkono huyu mwanamke mwenzetu ameonewa,"amesema Ngonyani.

Mbunge huyo amesisitiza kuwa uonevu wa namna hiyo haupaswi kuvumiliwa kwakuwa umemdhalilisha mbunge huyo na wapiga kura wake jimboni.

Kwa upande wake Manyanya amesema tangu asubuhi alikuwa anafuatilia kwenye mitandao na amebaini kuwa Sichwale hakuwa na vazi baya.

Hata hivyo Manyanya amesema haiwezekani wabunge vijana wavae mavazi kama wanayovaa wabunge wanawake watu wazima.

Amesema katika siku za karibuni limeibuka suala la kutoa lugha za kuwadhalilisha wabunge wanawake ndani ya ukumbi ambako wakati mwingine hutamkwa kiungo cha mwanamke halafu wengine wanafurahi.

Naibu Spika Dkt. Tulia Akson amesema atatoa mwongozo baada ya kufuatilia jambo hilo.

Mbungi za mbunge za kijani

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom