Wabunge wataka Umri wa kugombea Urais uwe 35; Zitto asema umri mkubwa ni ushamba

Wabunge wataka Umri wa kugombea Urais uwe 35; Zitto asema umri mkubwa ni ushamba

Mimi nataka ushushwe.Mataifa mengi yanatambua mtu mwenye miaka 35 anaweza kuwa Rais.Sisi kwa nini tunaweka vizuizi? je watanzania tunachelewa kukomaa?Mbona umri wa ukomavu kisheria katika kufanya maamuzi na kupiga kura ni miaka 18 kama ilivyo kwa nchi nyingine?

Mbona Nyerere alikua Rais akiwa under 40?

Nakubali kuna watu walikua marais wakiwa under 40 lakini walifanikiwa kuongoza kwa weledi na kuna wengine waliofeli vibaya.

Come on Filipo!

Bila kuja na ushahidi wa kibaioloia, kisaikolojia au kisosholojia utakaoonyesha kwamba umri wa miaka 35 ndo umri muafaka wa kugombea urais, hoja hii itakuwa na ni ya ushabiki tu. Binafsi ningependa umri ushushwe hadi miaka 18 maana ndo umri ambao mtu anaweza kupiga kura na inaleta maana kwa mpiga kura naye kuweza kupiga kura.

Binafsi ningependa tuandike katiba ya wananchi wote, sio katiba ya kumwezesha Zitto au kikundi chochote kuwa rais. Kufanya hivyo ni aina fulani ya udikteta na mfano mzuri ni Mseveni anayebadilisha katiba kila anapojisikia ili aendelee kugombea. Tunatakiwa tujiulize tunataka rais mwenye sifa zipi ndipo tujaribu kuoanisha na umri mwafaka na sio kuanza na maslahi ya kundi au watu ndipo tupendekeze umri.
 
Me naona hata 18 and above anaweza kufaa pia kuwa rais lakini sisi swala la umri linaweza lisitusaidie sana:

*Tuna hitaji kiongozi mwadilifu.
*Tuna hitaji kiongozi mchapakazi.
*Tuna hitaji kiongozi aliye komaa kiakili.
*Tuna hitaji kiongozi aliye tayari kufanya maamuzi magumu kwa maslai ya taifa.
*Tuna hitaji kiongozi ambaye ana jua nini maana ya kuwa rais.
*Tuna hitaji kiongozi ambaye hato yumbishwa bali mwenye msimamo.
 
Ajabu! Huu mjadala umefanywa kama vile kigezo pekee au cha muhimu zaidi kwa mgombea urais ni umri. Hebu tujikumbushe sifa zinazotajwa kwa nafasi za baadhi ya kazi muhimu kwenye mashirika makubwa ya kimataifa, k.v. multinationals, UN, n.k. Wakati mwingine hata umri hautajwi. Kinachoainishwa ni mtiririko wa sifa za kitaaluma, kiutendaji na kiuzoefu (idadi ya miaka kwenye ngazi/nafasi/majukumu fulani) kiasi kwamba walioziandaa wanajua kabisa mwenye kuwa na sifa hizo lazima atakuwa amefikia au amevuka umri fulani (unaopendelewa). Sanasana wanaweza tu kuweka umri wa mwisho kwa muombaji.

Ni kweli tukifuata demokrasia ya kweli hata mtu wa miaka 18 ana haki ya kugombea. Lakini reality haitakuwa naye. Kwanza, kupata digrii ya kwanza tu chini ya miaka 23 si rahisi kwa wengi nchini. Sasa, tuje tuweke miaka ya kazi na/au harakati za kisiasa hadi kufikia ngazi ya juu yenye vielelezo vizito kuhusu mchango wa muombaji, si rahisi kwa idadi kubwa ya vijana. Kwa miaka 35 inawezekana na ni reasonable.

Kuhusu Zitto, kuna matatizo mawili. Kwanza, ni kama ameathiriwa zaidi na mashambulizi ya wapinzani wake kiasi kwamba hataki kuielezea vizuri hoja hii ya umri, kwa utulivu na kwa namna inayoshawishi. Pili, alishawahi kunukuliwa kipindi fulani huko nyuma akidai kwamba anatembea na barua ya kujitoa Chadema na hata kuachana kabisa na siasa za vyama lakini anaendelea "kujishauri". Sasa, ukichanganya na nia yake aliyokwishaitangaza ya kugombea urais kupitia tena Chadema inakuwa vigumu kwetu wengi kumtilia maanani anapokuja na hoja ya kigezo (pekee) cha umri wa kugombea urais. He ends sounding a bit like a joker in the pack! Sorry.
 
Hata rais awe na miaka 10 ..zitto hafai na hana vigezo vya kuwa rais..hatuchagui rais asiye na maadili..kutwa yuko double tree ana kazi ya kugawa gawa namba kwa wanawake...hafai
 
Nikiwa kama mwanachadema na pia mzaliwa wa kijiji cha kimobwa wilaya ya kasulu(KIGOMA) sikubaliani na suala la umri wa miaka 35 kugombea urais coz kwa umri huo tunaweza kupata rais ambaye hajapevuka sawasawa kisiasa na kiakili na akaja kutupelekea utoto wake ikulu.
Zitto mara kwa mara amekuwa akitumia mifano ya akina paul kagame na meles zenawi wa nigeria kuwa walifanya makubwa wakiwa na umri mdogo,,hilo ni sawa lakini ilitokana na hali ya kisiasa kwenye nchi zao nikimaanisha kulikuwa na SINTOFAHAMU KWENYE NCHI ZAO then wakiwa kama vijana wakaanza harakati za kujitoa mhanga ili mambo yakae kwenye msitari,,so hali hiyo ya kisiasa iliyokuwepo kwao ni tofauti kabisa na hali ya kisiasa ilivyo tanzania.
Sasa ushauri wangu kwa zitto ni kuwa badala ya ku2mia muda mwingi kupigia debe suala la umri ni bora apigie chapuo la tume huru ya uchaguzi coz bila tume huru chadema twaweza kuendelea kuwasindikiza ccm kisha 2015 mje muanze kutuambia kuwa mmetambua dawa ya kuiondoa ccm 2020 hapo hatutaelewana.
Hivyo kabwe zitto vuta subira umri wako wa miaka 40 ukifika utagombea bila tatizo coz uongoz hautaki papara vinginevyo utaonekana una uchu wa madaraka na ubinafsi ndani yake.
 
Umri wa miaka 35 ni mdogo jamani. Tusifanye masihara na Ikulu. Vijana watatusababishia vurugu sababu akili zao zinakuwa hazijakomaa.
 
Wabunge wanataka kipindi cha rais kiwe ni miaka 7 - na hakuna term ya pili. Kwa maana hiyo kama mtu atachaguliwa kuwa rais akiwa na miaka 35, atastaafu urais (kisheria) akiwa na umri wa miaka 42! At 42 years of age anakuwa 'pensioner'! Huu ni umaalun. 42!!! Imagine tutakuwa na marais wastaafu wangapi?

Kama ni hivyo basi rais mstaafu naye asiruhusiwe kuchukuwa mafao yake hadi afikishe umri wa miaka 60!
Tatizo la hawa vijana ni kutokuwa na Hekima na Busara, hivyo hayo unayoyaona wewe wao hawakufikiria kabisa. Hizi ambition zao zinawaponza sana wananchi na inatupa picha mbaya sana kwamba wote hawa hawafikirii jambo kwa maslahi ya Taifa hata kidogo bali maslahi yao wao wenyewe ili kuweka njia safi wapite.
Swala hapa ni UONGOZI BORA na mahala pa kuanzia ni kutazama ili tupate uongozi bora ni maswala gani yanatakiwa kurekebishwa ama kuwekwa ktk katiba mpya badala ya kutazama UMRI ambao kesho utakuja tugharimu zaidi na hakuna guarantee yoyote ya ufanisi wao ktk maamuzi.
 
  • Thanks
Reactions: FJM
Kweli kabisa tusiicheze ikulu kwa kupeleka vijana wadogowadogo wakati JK mwenyewe licha ya kufit kiumri bado anapwaya ndani ya ikulu.
Pili kwa kuwa zitto amekwishatangaza nia ya kugombea urais 2015 na atakuwa hajatimiza miaka 35,,kuendelea kuipigia debe hiyo hoja inaonesha mgongano wa kimaslahi kwake na pia anajiua kisiasa coz tunaanza kumuona mtu
anayekurupukia uongozi(tamaa za kisiasa)
 
Lengo ni kufuta viti maalum coz imeonekana viti maalum havina tija, ila kwa kuwa wanawake wanatakiwa kushiriki katika vyombo vya maamuzi kwa asilimia 50, ndo ikapendekezwa majimbo ya sasa yafutwe afu kila wilaya iwe jimbo..Na kila mwanaume akigombea jimbo basi awe na mgombea mwenza mwanamke na kama mwanamke atagombea asiwe na mgombea mwenza. Wanadai hii itapunguza ukubwa wa bunge kwa maana ya idadi ya wabunge hivyo kuokoa pesa nyingi lakini wakati huo huo kuwaempower wanawake...Pia wanadai hii itasaidia uwajibikaji kwani kutamfanya mgombea mweza kuona kachaguliwa na wanachi wa wilaya husika na si kikundi cha watu wachache..
Viti maalum hakika vivunjwe lakini itakuwa ujinga mwingine kuweka wabunge kwa sababu kwa uuwiano. Hii akili inatoka wapi jamani?... Bungeni ni mahala pa kuwalikisha Wananchi, mbunge anayechaguliwa ama kuteuliwa hutetea kundi ktk jimbo lake sasa kama swala ni kuwatetea wanawake basi lazima itazamwe ni jinsi gani wanawake wataweza kutetewa vizuri bungeni iwe kt sheria zetu na pengine maendeleo yao. Hivyo, la muhimu hapa kila chama kitachagua wanawake wake kutetea hoja za wanawake na watoto kwa kuwakilisa sera za chama chao kulingana na mahitaji yao. Sisi sote tumezaliwa na kina mama na ni jukumu letu sote kuwpa nguvu kubwa hasa ktk Uzazi jambo ambalo kwa miaka mingi limewekwa chini sana japokuwa kuna wabunge wengi wanawake..
 
Miaka 7? Kichekesho kingine hivi hawa mambo ya maana ya kujadili maendeleo ya nchi? temu ziwe 2 tu miaka 5 inatosha kujua umahiri wa kiongozi; uraia wa nchi 2 sio jambo la kujadili watake wasitake litakuwa tu; badala ya kujadili suala la umri wa wagombea wangeanza na elimu kwa wagombea kuanzia udiwani hadi ubunge; idadi ya wabunge ni kubwa sana ukiangalia uwiano kati ya idadi ya watanzania idadi ya wabunge ni wengi na wamegeuka mzigo mkubwa huku wakiwa hawana tija yoyote kwa maendeleo zaidi ya kuwa wapiga deal tu kwa kutumia vyeo; mawaziri hawana sababu ya kuwa wabunge wawe ni watendaji wa kuwahudumia wananchi; viti maalumu ni mzigo na sijaona wabunge wana maana gani mpaka sasa hivi; viongozi wote watendaji wa serikali lazima wathibitishwe na bunge kuondoa kupeana vyeo kwa misingi ya kirafiki tunataka watu wenye uwezo wa kuongoza ndio wapewe nafasi>

Chama
Gongo la mboto DSM
 
Jack Zoka ni naibu mkurugenzi mkuu wa usalama wa taifa anayeshughulikia siasa,huyu anashutumiwa kupanga njama kuwauwa akina Dr Slaa,Mnyika na Lema

Uzushi mwingine; hao kina Dr. Slaa; Mnyika na Lema kila wakialikwa ikulu kunywa chai wanakwenda leo iweje mje na uzushi wa kutaka kuuliwa?

Chama
Gongo la mboto DSM
 
Hata rais awe na miaka 10 ..zitto hafai na hana vigezo vya kuwa rais..hatuchagui rais asiye na maadili..kutwa yuko double tree ana kazi ya kugawa gawa namba kwa wanawake...hafai

Sasa unataka asiwasiliane na wapiga kura wake?

Chama
Gongo la mboto DSM
 
Wasisahau kujadili suala la AFYA ya wagombea tumeingia kwenye mzigo mkubwa sana wa kuwahudumia wabunge wagonjwa kila kukicha safari za matibabu India

Chama
Gongo la mboto DSM
 
Wabunge wa Bunge la Jamuhuri ya Muungano, pamoja na mambo mengine..Wataka Umri wa mgombea uraisi upunguzwe tka miaka 40 hadi 35...Wataka Mawaziri wateuliwe nje ya wabunge...Uteuzi wa viongozi wa juu uthibitizhwe na Bunge...Idadi ya Wizara ijulikane kikatiba na ziwe chache...

Wataka matokeo ya rais yapingwe mahakamani...Muungano wa kimkataba (treaty-based union)...Rais wa Zanzibar awe Makamu wa rais...Majina matatu ya jaji mkuu yapendekezwe kwa rais kwa uteuzi na jaji athibitishe na Bunge na Rais asiwe na mamlaka ya kuwaondoa mpaka ridhaa ya wabunge, Hapa inahusu pia uteuzi wa CDF,IGP, Mkuu wa TISS, Magereza, Uhamiaji nk....

Wataka pia ubunge na udiwani uwe na kikomo...Viti maalumu vifute na badala yake majibo yawe ni wilaya na kuwe na mgombea ubunge na mgombea mwenza wake..Kama mgombea ni mwanaumwe, mgombea mwenza awe mwanamke na akichaguliwa mmoja wote wameshinda kama kwa rais...Uraisi uwe wa Kipindi kimoja cha miaka 7.....

Pia uraia wa nchi mbili (Dual Citizenship)...Kuwe na tume kikatiba itakayo shunghulikia kero za Muungano...Chiligati ataka Articles of Unioni zirejee kama ilivyokuwa mwanzo mambo 11...Mafuta gesi visiwe vya Muungano (hapa ni wabunge wa CCM na CUF bara na Visiwani waliungana)....Ubunge na Udiwani uwe na kikomo cha vipindi viwil (Miaka mitano kila kipindi)....Na mambo mengine mengi...
Source Mimi Mweneyewe Bungeni Dodoma leo...

Hata huo bado mkubwa sana bora uwe miaka mitano (5)
 
Hata rais awe na miaka 10 ..zitto hafai na hana vigezo vya kuwa rais..hatuchagui rais asiye na maadili..kutwa yuko double tree ana kazi ya kugawa gawa namba kwa wanawake...hafai

Wamchague hao hao
 
Inawezekana vijana akili haijakomaa,mtu akishafikisha miaka 41 anaweza kuwa rais mpaka miaka 150+,kwanini vijana wanabaguliwa wakati mzee anapofika miaka 65 hawezi kuwa sawa na 41? Ingependeza kukawa na mwisho wa kugombea urais mtu akifikisha 65 apumzike kwa amani ata kama ana uwezo gani nadhani hapo tutatendeana haki la sivyo vijana wataendelea kuitwa taifa la kesho.
 
Ubinafsi ndicho kitu kinamsumbua huyu Bwana mdogo Zitto,
Ana uwaza sana U-Rais, sijui ni akili yake au kashikiwa?
Kama ana nia ya kuwa Rais wetu aendelee kuonyesha uwezo wake wa Kiuongozi, sio kutaka kukimbilia IKULU
Hapa ndio nakumbuka yale maneno ya yule Marehemu Mzee Mwalimu "wanaokimbilia ikulu waogopwe kama ukoma"
Kwani ni lazima saaaaaaaaaaaaaaana awe Rais 2015?
Kwani akisubiri hadi 2020 itakuwaje? Hata hivyo kwani kwake ni lazima awe Rais wetu? Kuna nini?
Hapo ndio napata wasi wasi na kijana Zitto Kabwe
 
Watanzania vijana mnalipeleka taifa mahali pabaya, kwa hiyo JK na mkapa kwa umri wao wameipeleka nchi mahali gani? Huu ni unafiki wa baadhi ya vijana kutumika kwa maslahi ya watu,maoni yangu mtu yeyote Yule kuanzia umri wa kuwa mtu mzima anaweza kuwa rais, urais ni taasisi sio mtu binafsi. Watu wengine ovyo kabisa na mawazo Yao mgando
 
Back
Top Bottom