Wachawi na magereza

Wachawi na magereza

Root hii si kweli uchawi upo tena live kabisa hata vitabu na misahafu vimeelezea uwepo wa uchawi ningejua uko wapi na una nafasi ningekualika uje huku niliko ujionee....niko field ya utambuzi wa kiroho na nguvu za kishirikina karibu sana

Mkuu tunaweza kujiunga pamojaa?.maana hata mimi nahitaji sana hii elimu kwa maslahi ya wengi
 
wanshindwa kwasababu ndumba zao huwa wameziacha nje si unajua jera huingii na kitu chochote ndo maana wanavuliwaga nguo zote na kusachiwa hadi matakoni sow hawawezi toroka lakini kama wangengia nazo wangesepa tu maana hamna namna
 
wanshindwa kwasababu ndumba zao huwa wameziacha nje si unajua jera huingii na kitu chochote ndo maana wanavuliwaga nguo zote na kusachiwa hadi matakoni sow hawawezi toroka lakini kama wangengia nazo wangesepa tu maana hamna namna
sasa kwa nini wasizifiche kimazingara ili askari wasizione? au uchawi huwa unafanyika usiku tu?
 
me ningesikia mzungu karogwa hapo ningeamini uchawi upo..usichokiamini hakiwezi kuwepo!

Sasa mkuu si kuna stori za kina Otango Osale,si waliroga wazungu mkuu.au bado huamini.

Kwa mawazo yangu ni kuwa swala la kuamini au kuto kuamini haimaanishi kuwa kitu akipo,ila mkuu sema kuwepo kipo ila ukiamini uchawi haukupati wala hautokudhuru basi ni kweli hauwezi kukudhuru ila kuwepo upo.

Ni hayo tuu mkuu
 
Trela ya uchawi ni mazingaombwe! karatasi kuwa fedha,mayai mabichi kuiva kwa maneno ya kimazingara wewe achaa ni noma!
 
wanapo kuwa gerezani kumbuka wanakuwa hawana tunguli,hirizi wala ungo..kabla ya kuingia lazima usachiwe.kwa ufupi wanakuwaga hawana vitendea kazi

Kwanini wasiagize wachawi wenzao wakati wa kuwatembelea wawapelekee hivyo vitendea kazi ili watoke?
 
Serikali haiamini katika uchawi lakini ofisi na majengo ya serikali yana zindiko balaa ikiwa ni mchanganyiko wa mazindiko na dawa mbalimbali za watumishi waliopita na kufanya kazi katika ofisi/majengo hayo.
Nasema haya nikiwa naelewa ninachokisema kutokana na majengo ya serikali niliyokulia.
Magereza nayo imezindikwa balaa hivyo kuingia wala kutoka kichawi si rahisi hata siku moja. Waulize wachawi waliokamatwa na kufungwa enzi za teacher.
 
Uchawi ni mental state au ujanja ujanja in reality hukuna kitu kama hicho, ndo maana na uchawi wito hamewezi kushinda mechi kubwa hawezi kutumika kimaendeleo, waafrika tunakana mapanga na kupigana bunduki wakati wa vita badala ya kurogana, ukichukulia kiundani sana angali kama kuna rafiki yako wa karibu yeyote ambae ni mchawi, jibu kwa wengi hapana kwa wachache je umemshudia akifanya yake jibu kwa wengi hapana kwa wachache badaa ya kufanya alipata matokeo?
 
iliwahi tokea muheza niliwahi hadithiwa na uncle jamaa alikuwa anaitwa msenga ni mganga wa kienyeji(amefariki tayar) alikamatwa na makosa fulani fulani akawekwa lupango......siku ilifuata polisi walipoenda kufanya uchunguz nyumbani kwake kijijini wakamkuta yupo shambani na mkewe analima.....wale polisi wakauliza wewe vipi mbona uko huku alichojibu nimekuja kufanya kazi zangu za kila siku ila jioni ntarudi kituoni ilibidi wamuachie tu na kesi ilipotea kimizengwe tu
 
Nimekutana na wawili walioweza kutoka gerezani kwa nguvu za kichawi.

Mmoja alifungwa kama leo, kesho yake asubuhi askari wakakuta kinyesi mbele ya mlango huku kufuri zito bado lipo mlangoni, walipofungua wakauliza, ni nani kanya mbele ya mlango na huku ulikuwa umefungwa, jamaa akajibu ni yeye. Akaulizwa alitokaje mpaka akaenda kunya kwa nje akajibu "niliamka usiku nikajikuta tu nimetoka nje ya gereza na kujisaidia kisha nikarudi ndani tena"

Siku hiyo hiyo akaachiwa huru asitoroshe wafungwa wengine. Alipoachiwa alienda kituo cha polisi na gunia la nyoka kulipiza kisasi kwa waliomkamata...ilikuwa patashika


Kamanda umetisha kama Ukawa.


swissme
 
Osale Otango alikuwa ni mwizi maarufu enzi za wakoloni huko Tanga yeye alikuwa anaibia wazungu halafu anaenda kuwagaiya waafrika maskini, na ilikuwa akitaka kwenda kuwaibia alikuwa anawapa taarifa kwanza kwa kupiga simu zile za kukoroga kwamba ataenda muda fulani kuiba au kula nao
Wazungu walikuwa wanaweka ulinzi wote wa wakati huo lakini ukipita ule muda aliosema anawapigia simu na kuwaambia kuwa keshachukua kitu fulani

African Robin Hood
 
Back
Top Bottom