Wachawi wanavyoiba nyota za watu wanafanyaje?

Wachawi wanavyoiba nyota za watu wanafanyaje?

Mimi ni mvivu wa kuandika ila nishakwambia nyota haiibiwi maana nyota ni malaika au jini linalomuongoza mtu au kumlinda na hii ni automatic tu kulingana na maagano yako pale ulipozaliwa wazazi wako walikuwa upande upi wa Mungu au waovu, na hili lilifanyika kwa vizazi vya zamani mtoto anapozaliwa walimfanyia maombi kwa malaika wake amulinde na kumuongoza na familia za kichawi nazo walikabidhi kwa jini wa nyota hiyo hiyo maana nyota ya siku Ina watu wawili wa kuiongoza malaika na jini Sasa mtu anachagua yupi awe mwelekeo wake Sasa hapo mtu ataibaje nyota ya mtu? Kinachopotezwa kwa mtu ni zile nguvu alizopewa na malaika wake yaani fortune ya mtu au bahati mtu kwa uchawi au wewe mwenyewe au kwa watu wa maarifa kukuzidi wanajisogeza karibu na wewe kujua bahati zako zipo wapi Ili wazizime na wewe usiendelee kuwatishio kwao au kukukomoa kama Samson alivyonyolewa nywele na ile bahati yake ya kuwa na nguvu nyingi ikaondoka, wachawi wao wanamaarifa yao ya kudhuru mtu, na wewe mwenyewe unaweza kujiweka mbali na nyota yako kwa tabia mbaya nyota yako isizozipenda, ila Sasa kizazi kinachozaliwa Sasa wengi walipozaliwa hawana maombi yoyote maalumu ya muelekeo wa ulinzi wao na tunuku zozote ndo maana hawaeleweki nini cha tofauti wanacho zaidi ya maarifa wanayotafuta kwa kupitia shule na maisha ya mtaani bila nguvu za ziada hivyo kuibiwa nyota haiwezekani ila unapotezewa bahati ulizotunikiwa wakati unazaliwa.
At least you are making sense!

Ahsante sana mkuu!
 
Kwahiyo Farao yule wa 40 aliyetumikisha Waebrania kule Misri Wachawi wake na Wanamazingaombwe wake walishindanisha miujiza yao dhidi ya ile ya Musa kwa uweza upi? Wa Mungu yupi? Maana umesema ni Mungu pekee ndiye awezakubadili alichokiumba, lkn maandiko yako wazi kuwa wale wa Farao nao walifanya miujiza ya kubadili, sasa kwa nguvu ya nani?

Hili somo gumu na tata!
Farao alitumia uchawi kufanya miujiza thus alishindwa kwa
 
Mambo meng yamekaaga kiimani tu usipo amini hayapo na huto yaona na wala hayatokuzulu wala kukusumbua

Wacawi ni watu gan ushawai kuwaona
Nyota ni nn unafanyaje kaz na inafanana vp iyo nyota na inatokana na nn

Ayo mambo yote ni mambo ya iman na kuamin na ndo maana ukiwahoji watu weng wanaoyatetea ayo mambo watakujibu tu ww sio mtu wa imani mara ww wakishua maana yake wachawi na nyota ni vtu vya maskini
 
Mambo meng yamekaaga kiimani tu usipo amini hayapo na huto yaona na wala hayatokuzulu wala kukusumbua

Wacawi ni watu gan ushawai kuwaona
Nyota ni nn unafanyaje kaz na inafanana vp iyo nyota na inatokana na nn

Ayo mambo yote ni mambo ya iman na kuamin na ndo maana ukiwahoji watu weng wanaoyatetea ayo mambo watakujibu tu ww sio mtu wa imani mara ww wakishua maana yake wachawi na nyota ni vtu vya maskini
Wachawi wapo na wanafanya kazi.

Lakini hizi habari za nyota zina utata.
 
Kama wanaiba nyota kwanini wasiibe nyota ya rais ili marais watoke vizazi vyao tu?

Kama wanaiba nyota kwanini wasiibe nyota za wanasayansi wagunduzi walioingia kwenye rekodi za dunia ili vizazi vyao viambukizwe uwezo huo wa ugunduzi?

Kama wanaiba nyota vipi nikiwalipa waniibie nyota za Warren Buffet, Amancio Ortega Gaona, Dangote, Messi, Zuckerberg, Bill Gate nk watafanya?

Wanaiba nyota kwa malipo ya mtetea-mweusi? Baghosha!

JPM alitokomeza mauaji ya muda mrefu ya vikongwe wenye macho mekundu na wenye ulemavu wa ngozi.

Sorry for graphic images. Taswira kwa hisani ya google.

View attachment 2040666

Ofisi ya wenye biashara ya kuiba nyota.

View attachment 2040668
Kiganja cha Albino kikiwa kimekatwa.

View attachment 2040669
Albino aliyeuawa Burundi kunyofolewa mguu na mikono na masalia kutelekezwa porini.

Micah.3:2-3 2Who hate the good, and love the evil; who pluck off their skin from off them, and their flesh from off their bones; 3Who also eat the flesh of my people, and flay their skin from off them; and they break their bones, and chop them in pieces, as for the pot, and as flesh within the caldron.
Jiwe alikuwa mchawi balaa
 
Mambo ya nyota ni mambo ya kiroho na yako katika ulimwengu wa roho. Ni kweli mtu au watu uweza kuiba au kuchukua nyota ya mtu. Yaweza kuwa kwa njia za kichawi, majini, au nguvu zozote zile za giza katika ulimwengu wa roho. Haya mambo yamekuwepo enzi na enzi.
Katika Biblia Mathayo 2:1, 2. Kuna wise men( wenye hekima au Watabiri nyota) waliuliza

"yu wapi mfalme mpya alozaliwa, maana tumeona nyota yake tulipokuwa mashariki".

Hii haikumaanisha nyota kama nyota ya mwonekano. Na utajiuliza kwa nini hawa wisemen watatu ndo waliona hii nyota si wengine. Herode alituma watabiri wakaangalie yu wapi huyu Yesu alozaliwa. Hawa jamaa baada ya kufika kule walimwona Yesu na Mamake. Walipotaka kuondoka waliona nyota ya yule mtoto Yesu imechafuka ikionesha mauaji ya mtoto mdogo asie na hatia. Ndipo Mungu akawambia wasirudi kwa Herode. Mathayo 2:12.

Nimenukuu kutoka katika Biblia kuonesha binadamu tunanyota na nyota ndo muongozo wa maisha. katika nyota unaweza mjua mtu ni nani na atakuwa nani. Haya mambo yapo katika Ulimwengu wa roho. Hawa watabiri wa nyota tayari walishaona nyota ya mtoto aliezaliwa na walisema mfalme mpya alie zaliwa. Hivyo nyota ya Yesu ilionesha ni mfalme. Hii ilimuuzi Mfalme Herode na kuamru watoto wadogo miaka 2 hadi 0 kuuwawa.
Maswala ya wizi wa nyota ni somo refu saana. Kwa kifupi!
Viganja vya mkono uonesha nyota ya mtu. Hii ni pamoja na nyayo.
Paji na macho uonesha nyota ya mtu.

Kuwa makini na mtu anae kutazama sana katika paji lako au machoni huku kakaza macho yake. Na hasa anaweza kukuangalia wakati weye umeyumbisha macho umuoni uzuri. Kuna uchawi wa macho. Nchini Ethiopia, uchawi huu hutumika hasa mtu anapokuwa na kinyongo nawe, au kijicho. Hivyo uchukua nyota yako nawe kubaki unaangaika sana.

Kuna kitabu kinaitwa "Mind of an Eye" kama sijakosea ni kikubwa kwa wingi wa page. Na pia ni kipana. Kimeeleza mengi juu ya nguvu za jicho. namna binadamu unavyoweza kubadilika hata ukatoweka mfano upo Dar lakini ukafika Mwanza hata arabuni. kinafundisha uponyaji na mambo mengi katika ulimwengu wa roho.

Hivyo jicho linaweza chukua nyota ya mtu. Ndo maana mtu anaweza sema fulani kaniangalia kwa jicho baya. Jicho linanguvu za ajabu kwani uweza kuona hata yalofichika.
Nyayo au kiganja kimebeba mwili wa mwanadamu. Taswira ya mtu unaipata katika nyayo au kiganja chake. Ndo maana wengine, uchota nyayo za mtu ili kummaliza. Au uchukua maandishi ulioandika kwa viganja vyako. hata kama ni karamu ilikamatwa na kiganja hivyo ni rahisi katika ulimwengu wa roho kuchukua reflection yako.

Kuna kuchukua nyota yako kupitia jina la ukoo wako, jina la ukooo linanguvu na hasa kama ni la babu yako. haya majina hutumika kukujua vizuri wewe na ukoo wako. Nguvu zenu kiroho na nyota yako.
Mchawi hawezi kuroga kama yupo kawaida, mpaka ajibadili aingie katika ulimwengu wa roho. ndiyo maana huwezi mshika au hata kumuona.

Anapoamua kuonekana kuna jambo au pia wewe katika ulimwengu wa roho unanguvu. Hivyo kuichukua nyota yako itahitajika kwanza aifahamu, na afahamu ukoo wako kisha katika ulimwengu wa roho anaiiba au kuichukua nyota yako.

Na mara nyingi hawaichukui wawe nayo wao lah asha. Wanaiondoa tu kwako ili pengine usifanikiwe, uteseke, au tu uangaike. Kwani ni ngumu nyota ya mtu kutumika kwa mwingine. Hivyo wakiichukua maana yake wanaondoa baraka zako, wanakufunga. isipokuwa hawawezi kuitumia nyota yako.

Narudia tunatumia tu neno nyota uchukuliwa, si kwamba wanaichukua waitumie hapana. Uwezi tumia nyota ya mtu mwingine kwa sababu kila mtu anapozaliwa uzaliwa na nyota yake. Kikubwa wanaiondoa ile nyota kwako, kwa sababu za husuda, roho mbaya, na mengineyo ili ubaki ukiteseka na usifikie ambacho nyota yako inaonesha hapa duniani ungekuwa nani, au mtu wa namna fulani.
Hivyo nyota yako ufichwa mahala. Ndo maana katika maisha omba, ombea wanako au familia. Ili Mungu akulinde weye na familia yako. Unajua kuna watu wa ajabu ktk hii dunia, mtu akiona weye ni mzuri ktk jambo fulani au umefanikiwa kiasi fulani basi anakumaliza kwa ulimwengu wa roho.
Japo kuna watu wanajifanya hawaamini haya mambo lakini yapo. Yana nguvu sana. Kuwa makini na watu ulionao karibu. Hao ndo wakwanza kwa kijicho na husuda. Mtu hata kama si mchawi atakuendea kwa wataalamu au waganga ili waiharibu nyota yako. Usifanikiwe! Kila siku utajiona ni mtu wa mikosi na balaa. Au unajitahidi kufanya hiki hakiendi. Wanafunga nyota yako!
Asante sana mkuu, umemaliza Kila kitu. Kuna watu hawaamini uwepo wa mambo ya roho mchafu kwa sababu tu hawajawahi kukutana na changamoto za kiroho. Ipo pia mtu kumtazama mtu mwingine kwenye utosi. Ogopa sana mtu mkiwa mnaongoea halafu akawa anakuangalia kwenye utosi Kama Kuna kitu vile
 
Namba zako za bahati ni
2, 4, 6, 11, 20, 29, 37, 47, 56

Nyota yako inaendana vizuri na kazi zifuatazo > mambo yanayohusiana na bustani, vyakula (catering) , muziki, mapenzi , mitindo ya nguo , kazi yoyote ya ubunifu kwa kutumia mikono

Pia una mvuto wa asili

Vyovyote itakavyokuwa lazima uwe na hela sababu ulishapewa hela na asili yenyewe

Una wachawi wengi lakini Mchawi wako mkubwa ni KUPENDA VITU VYENYE THAMANI SANA (LUXURY GOODS)
Asante Sana Mkuu Ulivosema yote ni Kweli ila Sikujua Kuhusu Mambo ya bustani Mengine yote ni Kweli Shukrani
 
Wewe ni Taurus (Ngombe)

Ni mtu usiependa kuingiliwa kwenye maamuzi yako na unakua mkaidi sana mtu anapojaribu kufanya hivyo.

ni mfanyaji kazi mzuri na ukiamua jambo lako na kuliamini ni ngumu sana kuyumbishwa na mitazamo ya watu wengine

Shida yako kuu ni Ukaidi (stubborn)
Umetisha Mkuu[emoji23][emoji23][emoji106]
 
Namba zako za bahati ni
2, 4, 6, 11, 20, 29, 37, 47, 56

Nyota yako inaendana vizuri na kazi zifuatazo > mambo yanayohusiana na bustani, vyakula (catering) , muziki, mapenzi , mitindo ya nguo , kazi yoyote ya ubunifu kwa kutumia mikono

Pia una mvuto wa asili

Vyovyote itakavyokuwa lazima uwe na hela sababu ulishapewa hela na asili yenyewe

Una wachawi wengi lakini Mchawi wako mkubwa ni KUPENDA VITU VYENYE THAMANI SANA (LUXURY GOODS)
Naomba niangalizie na me mkuu tar 1/9
 
Back
Top Bottom