Wachezaji bora wa muda wote kipindi cha miaka 25

Naona mnatizama makombe tu!! Simkatai cr7 ila msimletee dharau andunje.. Hesabu medali za national team!! Ronaldo na timu yake kacheza fainali moja tu, messi anaedhihakiwa kacheza fainali 4(3)
 
2018 argentina yote ilikuwa mbovu na ubovu ulioletwa na kocha sio andunje!! Vipi umpe lawana messi wakati timu lote lilikuwa bovu.
 
Kumbe messi na ronaldo huwa wanajipasia wenyewe mpaka golini.hapa kila mtu ana mtizamo na mchezaji wake mwenyewe.Haishangazi kuitana wachambuzi uchwara.
 
Wivu unawatesa hawa
Wakati mwingine mjadiliane kama mlio balehe.Mtu atamwonea wivu messi ili apate nini?kumbukeni kila macho yana uoni wake na kila moyo una chaguo lake na si kila mtu atapenda kijani.mnachofanya ni iulazimishana mitazamo.Chukulieni huu kama mjadala tu.Acheni unafiki wa kitanzania.
 
Utamkubali vipi mtu ambae hujawai kumshuhudia live!! Nikikuuliza utaniambia umemcheki youtube.

Waswahili tuna safari ndefu sana.
Hapa ukiulizwa kuhusu kuona live kwenye swala jingine utarauka.Wakija watu wakakuuliza dini yako utasema muislam au mkristu je umewahi kuwaona yesu au muhamad.Wakati wewe hukumuona pelle wengine walimuona.Hatuwezi kuacha kujadili sababu wewe hukuwepo.
 
Mkuu hata mimi ni mpenzi wa pele ila siku nyingine jaribu kusoma maelezo kwanza..

Hapa wametajwa wachezaji bora ndani ya miaka 25 iliyopita.

bila kombe la dunia anaubora gani.......
Soma hiyoooo


 
Utamkubali vipi mtu ambae hujawai kumshuhudia live!! Nikikuuliza utaniambia umemcheki youtube.

Waswahili tuna safari ndefu sana.
Kama mesi ulimwangalia dk 90/ uwanjani, hata Pele nimemcheki dk 90/ uwanjani huko you tube ulikosema kuna full match za timu ya taifa ya Brazil enzi hizo.

Kacheki na wewe utajua kwa nini Pele ni king wa soccer duniani mpaka leo
 
Sasa MTU unashindwa kuisaidia nchi yako kwenye match saba tu za kombe la dunia mchukue kombe halafu unamwita mchezaji bora kwa kipindi cha miaka 25 huo ni ujinga, ubora wake uko wapi sasa

Narudia tena messi na ronaldo wa ureno sio wachezaji bora kwa kipindi hicho cha miaka 25
 
2018 argentina yote ilikuwa mbovu na ubovu ulioletwa na kocha sio andunje!! Vipi umpe lawana messi wakati timu lote lilikuwa bovu.
Mbona ureno ilibeba euro ikiwa mbovu tu? sasa kama mchezaji bora unashindwa kweli kuonyesha individual skills kuibeba timu na kusingizia eti anaocheza nao wabovu huu ni upuuzi basi tuamini hawezi kucheza timu nyingine tofauti na Barca na pengine hata Uefa hao Barca wasinyakue tena kwa kumtegemea Messi kwani nae anataka wachezaji wa viwango vikubwa awategemee ili yeye aonekane bora (eg. Xavi & Iniesta)
 
Itakuwa hauna akili timamu Baba ake alikuwa goalkeeper wa sub awekwe Kwa kigezo gani busquets aliyemuhamisha namba Alonso Spain ni huyu huyu kiungo mkaji mwenye udambwi dambwi dunia nzima
Matusi ya nini wewe fala..
 
Hawa watu wana sababu za hovyo... Timu ya Messi, di maria, aguero, maxi, zabaleta, otamendi, rojo, higuain, mascherano, dybala n.k unasema ni mbovu?
Inafungwa na timu ya Sanchez, medel, vidal n.k mara 2 fainali?
Tuongelee vingine sio kwa timu nzuri kama argentina
 
Mkuu kama kigezo ni kombe la dunia mbona hujamuweka POGBA, VARANE, MBAPPE, GIROUD, GRIEZMANN, OZIL, KROOS, MULLAR N.K
tuache ushabiki mkuu..sasa KANTE wa nini hapo?
 
Mviziaji mwenye Uefa 5, D'or 5, Euro, Top scorer Uefa... Unaleta mahaba ya hovyo mkuu.

NArejea tena. Iniesta na Xavi hawa majamaa ni ulimwengu mwengine kabisa kwenye football kwa last 12years. Jamaa walimnyanyasa kila aliyojitokeza karibu. Huwezi walinganisha na mtu anaesubiria krosi au kipa akitema.
 
Katika era ya CR7 na Messi usimuweke Zidane! Utakosea sana!

Zidane awekwe katika era za Ronaldo Lima, Henry, na wengineo bwana Gaucho.

Zidane na bwana Gaucho ni zama za watu wa udambwi udambwi!

Siku hizi ni nadra kuona maudambwi udambwi kama yale, ya kupiga kanzu watu wa 4!

Katika tik taka style ya barca utapiga kanzu watu wa 4 saa ngapi wakati wenzako wanataka pasi mpaka 500 half time tu.

Kwenye hii era ya andunje na Cr7 wawekwe watu ambao ni nguli wa kupiga mabao na watengeneza mabao,

Watu kama Sergio Busquet andaa headline ya kumuweka. Ipe Jina hili hapa Best Offensive Midfielders of all Time.

Hapa utamuweka Fabinho, Ng'olo Kante, Busquet, na wengineo wazee wa kukata umeme.

Mtoa mada umejaribu sana, lakini umefeli kutofautisha aina za hao watu.

Kuna mabenki bora wa kushoto duniani, mawinga bora duniani, na wengine wengi tu.
 
NArejea tena. Iniesta na Xavi hawa majamaa ni ulimwengu mwengine kabisa kwenye football kwa last 12years. Jamaa walimnyanyasa kila aliyojitokeza karibu. Huwezi walinganisha na mtu anaesubiria krosi au kipa akitema.
Bora uongelee mwingine sio Ronaldo.C,
Anaekataa Messi kuwepo kwenye list hii ni ushabiki, utoto na ujinga unamsumbua kama wewe unavyomkataa Ronaldo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…