Tetesi: Wachezaji watano wa Simba wasimamishwa kupisha uchunguzi kwa kichapo kikali cha goli 5 kutoka kwa Yanga

Tetesi: Wachezaji watano wa Simba wasimamishwa kupisha uchunguzi kwa kichapo kikali cha goli 5 kutoka kwa Yanga

Ila Inonga ni kama simuelewi siku hz toka aje huyu Chemalone amekua anacheza kizembe zembe...au macho yangu..

Onyango alikuwa anafunika makosa ya Inonga. Onyango alikuwa anajilipua hata kucheza rafu isiyo na maumivu kutetea makosa ya walinzi wenzake.

Sasa Onyango hayupo Inonga anaonekana makosa yake
 
Badala ya kujifukuza wao viongozi eti wanawafukuza wachezaji ili wanachama wao wasione uzembe wa viongozi wao kwa kusajili hovyo .

Chama alitaka kusawazisha kwa free kick Diarra akafanya save ya maana ikawa kona iliyoleta goli !

Dakika 20 za mwisho wachezaji wa simba walikuwa hoi poor fitness maanake maandalizi yalikuwa duni uwezo wa mwili ulikuwa umefika Kikomo zingeongezwa dakika 30 wangepigwa 5 nyingine jumla ikawa 10!, lakini hapo sio kosa la mchezaji ni kosa la Mwalimu wa viungo.

Kwahiyo mwalimu wa viungo sawa ni halali kufukuzwa.
 
Gamondi kayataka yote haya
 

Attachments

  • 20231106_131200.jpg
    20231106_131200.jpg
    52.2 KB · Views: 2
Kama kuna kiongozi yoyote wa simba alikua anafikiri ataifunga yanga nayeye aondoke haraka.Kwani wakikubali kua yanga iko vizuri zaidi kuliko simba ili wapate nafasi yakujipanga upya watapungukiwa nini.Wanakimbilia kuwaza hujuma wakati mpira wenyewe unaonekana tulizidiwa kila mahali.Ata kama kuna hujuma na viongozi watakua wanahusika pia.

Sent using Jamii Forums mobile app
Wacha washupaze shingo umbwa Hawa,Badala ya kujikita kwenye ubora wa scauting Yao Ili kupata usajiri bora.yapo na jazba ya 🖐️yanapaluana.
 

Wachezaji watano wa Simba Sc akiwemo Enock Inonga na Clatous Chota Chama wamesimamishwa kazi kupisha uchunguzi dhidi yao baada ya kufungwa na Yanga SC mabao 5-1 siku ya Jumapili.

Wachezaji hao wanatuhumiwa kuihujumu timu kitendo kilichopelekea kupoteza kwa idadi kubwa ya mabao.

Maamuzi hayo yamefanyika katika kikao cha bodi ya Wakurugenzi ya Simba kilichofanyika jana jijini Dar es salaam.

Chanzo cha uhakika kutoka Simba SC kimeiambia Kishamba Media kuwa uongozi umeshapata ushahidi wa awali kuhusu tuhuma dhidi ya wachezaji hao na sasa imeanza uchunguzi wa kina ili kujiridhisha.

Wachezaji hao watakua nje ya kambi ya timu mpaka hapo maamuzi mengine yatakapofanyika.

Chanzo hicho kimesema huwenda leo klabu ya Simba ikatoa taarifa ya wazi kwa Umma juu ya maamuzi waliyofikia kuhusu wachezaji hao au wasitoe ila wahusika wamepewa taarifa.

Maamuzi mengine yaliyofikiwa na bodi ni kufutwa kazi kwa kocha mkuu Robertinho, msaidizi wake pamoja na kocha wa viungo.

Kishamba Updates
Yanga tulifungwa na Ihefu Kwa makosa ya kocha kupanga timu mbovu lakini tulivumilia. Kwa hiyo Simba isifungwe wao ni Nani ? Kweli madunduka ni shida
 
Moderators waniombe Radhi kwa kufuta Uzi wangu wa Juzi kuwa Inonga, Kapombe, Manula, Chama na Baleke Wameihujumu Simba SC na Kufungwa 5 kwa 1 na Yanga SC
Moderator hawawezi kukuomba radhi wewe . Sema Uongozi wa Simba ndio Ukushukuru kwa kutoa wazo litakalosaidia KUWAAMINISHA MASHABIKI KUWA SIMBA ILIHUJUMIWA.

KIMSINGI SIMBA WAMECHUKUWA JUNGU LAKO
 
Back
Top Bottom