Wachezaji watatu wenye uwezo wa kumdhibiti Aziz Ki uwanjani bila wasiwasi

Wachezaji watatu wenye uwezo wa kumdhibiti Aziz Ki uwanjani bila wasiwasi

Mwishokambi

JF-Expert Member
Joined
Nov 23, 2020
Posts
390
Reaction score
1,425
Aziz Ki ni mchezaji mzuri sana lakini akipata watu haonekani, ni mchezaji ambaye ukimwekea watu wenye kazi ya kukaba, humuoni, atabaki kulalamika tu kuwa anachezewa rafu.

Wachezaji watatu niliowashuhudia wakihangaika na Aziz Ki na akashindwa kabisa kufurukuta kwao ni kama ifuatavyo.

1. Kevin Nashon kiungo wa Ihefu. Huyu dogo balaa na nitafurahi mno akivaa jezi ya Simba msimu ujao. Anakaba sana, halafu hana masihara hata kidogo, ni moja ya viungo ambao wanacheza kama marehemu Idd Seleman Kibode.

2.Yussuf Kagoma, hii ni mashine nyingine ambayo ina uwezo wa kumzima kabisa Aziz Ki. Nimemshuhudia mara kadhaa akimdhibiti Aziz Ki bila matatizo yoyote. Nitafurahi sana nikimuona akiwa dimbani. Kagoma na Nashon hawapotezi pasi hovyo kama Mzamiru.

3.Yahya Zayd, hii mashine nimeikubali sana. Mashine hii ikisimama pale middle ya chini Simba aisee kila siku ntakuwa sikosi dimbani kumwangalia mnyama.

Hao ndio wanaume wanaoweza kutembea na yule raia wa Burkina Fasso.
 
Tafuteni wachezaji wa shirikisho yanga alishaweka kipimo huko Sasa muende muishie robo tena
 
Aziz Ki ni mchezaji mzuri sana lakini akipata watu haonekani, ni mchezaji ambaye ukimwekea watu wenye kazi ya kukaba, humuoni, atabaki kulalamika tu kuwa anachezewa rafu.

Wachezaji watatu niliowashuhudia wakihangaika na Aziz Ki na akashindwa kabisa kufurukuta kwao ni kama ifuatavyo.

1. Kevin Nashon kiungo wa Ihefu.Huyu dogo balaa na nitafurahi mno akivaa jezi ya Simba msimu ujao.Anakaba sana, halafu hana masihara hata kidogo, ni moja ya viungo ambao wanacheza kama marehemu Idd Seleman Kibode.

2.Yussuf Kagoma, hii ni mashine nyingine ambayo ina uwezo wa kumzima kabisa Aziz Ki.Nimemshuhudia mara kadhaa akimdhibiti Aziz Ki bila matatizo yoyote.Nitafurahi sana nikimuona akiwa dimbani.Kagoma na Nashon hawapotezi pasi hovyo kama Mzamiru.

3.Yahya Zayd, hii mashine nimeikubali sana.Mashine hii ikisimama pale middle ya chini Simba aisee kila siku ntakuwa sikosi dimbani kumwangalia mnyama.

Hao ndio wanaume wanaoweza kutembea na yule raia wa Burkina Fasso mwenye domo kama kinda la ndege
Una chuki binafsi
 
yule raia wa Burkina Fasso mwenye domo kama kinda la ndege
Umechambua vizuri mtazamo wako, ila hapa tu ndo umejidharaulisha.

Hivi huwa mnaanzaje kuwachambua wanaume wenzenu kwa chuki namna hii? Halafu unamchambua ovyo mtu ambaye kakuzidi mafanikio na umaarufu wewe na hao unaowakubali, na zaidi hakujui!

Anyway, siwezi jua labda wewe ni mdada
 
Yaani mawazo ya team za shirikisho bhn.
Sasa ukiwasajili Kwa akili ya Azizi ki na akahama Yanga.
Kumbuka Nabi alikuwa hamtumii sana Aziz ki na Yanga ilikuwa bingwa
 
Back
Top Bottom