Wachungaji na Maaskofu waiache CHADEMA ijipambanue kama chama cha siasa

Wachungaji na Maaskofu waiache CHADEMA ijipambanue kama chama cha siasa

Kwa mwaka huu 2024 imekuwa vigumu kujua kama CHADEMA ni chama cha siasa chenye nia ya kuhudumia Watanzania wote au ni Taasisi ndani ya taasisi ya dini katika madhehebu tofauti.

Miaka ya nyuma kulikuwa na minong'ono tu kuwa hiki ni chama kinadhaminiwa na Mlengo wa Kikristo.

Maneno hayo nilikuwa nayapinga mara kwa mara lakini leo hii, nashawishika kabisa kuwa maneno hayo yalikuwa na ukweli. Kwasababu kila tamko la CHADEMA linabaraka 100% ya maaskaofu na wachungaji na kila tamko au barua za kichungaji zote zina baraka ya CHADEMA kwa asilimia 100, Kulikoni?

ChADEMA ijikague, vinginevyo itapata kundi moja tu na kamwe huwezi kushika nchi kwa kundi moja tu. Bado mna nafasi.

Pia soma: Siasa na dini
Na CUF vipi???
 
Ukiona hivyo ujue kuwa Watu wema wamechoka kutawaliwa na watu waovu.
Tunatawaliwa na mashetani yasiyoshiba hata kwa kula nyama za watu.

Majitu yalejilimbikizia mali kila sehemu na hayana huruma kamwe . Majitu tunayalipa mishahara mikubwa na pensioni kubwa maisha yao yote lakini yanaiba kura ,yanabadili matokeo ya uchaguzi , yanauza rasilimali za umma.

Mashetani maovu yanakimbilia kujenga mahospitali majengo ya mabilioni ya pesa kwa sababu tu katika ujenzi ndipo wizi mkubwa wa pesa unapotokea .
Unajengaje Hospitali ya Bil.40 halafu hakuna madaktari .?
Hospitali zilizopo Tatizo sioajengo kwa sababu wafu wanahitaji madaktari zaidi. Hawaajiri.

Na hata CCM kwa muda mrefu sana imekua ikiwapumbaza waumini kwa rushwa na matokeo yake taasisi za dini zinaonekana kama zinabariki Ufisadi na mafisadi.

Na awamu hii tunataka mawakala wawe ni mashehe na Wachungaji na maaskofu na maustadhi wale walioshika dini ya haki kule ACT na Chadema ili wasikubali kununuliwa na waone uovu ya Watawala wahuni .

Lakini sio hivyo tu hata wagombea wote kwa sasa wanatakiwa kuwa ni watu wenye hofu ya Mungu.

Kuongozwa na watu wasiojali kuwa kuna kesho ahera ni sawa na kuongozwa na wanyama.
Tumechoka kuongozwa na wanayama.
Tunataka kuongozwa na binadamu sio watu wasioguswa hata na uhai wa watu. Watu wasiojali uhai wa binadamu hawafai kuongoza binadamu .Hao ni wanayama wakaongoze wanyama wenzao kule Loliondo.

Lakini sio taaisisi za dini tu zinaviunga mkono vyama vya ACT na Chadema bali hata Taasisi za kutetea haki za binadamu,wanasheria nguli , wafu huru, watu wenye heshima katika jamii na wasiopenda kuona wanayama na mashetani wakiongoza binadamu.

Hii ni Fursa nzuri sana kwa ACT na Chadema kuungana na kuwatoa madarakani hawa majitu yasiyo na huruma linapokuja suala la madaraka.

Chadema na ACT kaeni chini mjipange wakristo na waislam wapo tayari kuwapigia kura . CCM wamebaki na machifu na wachawi wao .
Ndio maana CCM walisema kuwa wao ushindi sio Mungu anayepanga bali ni lazima .

Sasa kama CCM itashinda aliyeshindwa ni Mungu sio Chadema wala ACT.
Watu wote wenye imani kwa Mungu Muumba wa mbingu na ardhi na ambaye akitaka jambo liwe linakua ,basi tuungane wote tuvichague vyama viwili Chadema na ACT ili kuhakikisha CCM haishindi kwa sababu CCM ikishinda Nchi hii itakua na watu waovu mara mia zaidi ya leo kwa sababu watu wengi wataamini kuwa CCM ni zaidi ya Mungu na ndiyo yenye kuamua hatima na uhai na maisha ya vitu vyote ikiwemo Mvua , Jua na mimea na wanyama.

CCM ikishinda uchaguzi ujao Mungu atadharauliwa sana.

Tunawashukuru sana Wachungaji ,maaskofu na mashekhe kwa sababu wameliona hilo . Kazi ya viongozi wa dini ni kuhakikisha kuwa haki inatamalaki lakini pia Mungu ndiye anayekula mkubwa wa wote na muamuzi na mpangaji wa kila kitu bila kushindwa.

Ndani ya Chadema kuna waislamu wengi sana lakini pia ndani ya ACT kuna wakristo wengi sana. Mbowe na Viongozi wa ACT kaeni muliangalie hili maana ushindi ni wa hivi vyama viwili kushirikiana japo Chadma ina wanachama wengi zaidi lakini haiwezi kushinda peke yake bila kushirikiana na ACT .

CCM kwisha ,kwisha kabisa
,mlalo wa chali ,kifo cha mende.mbendembende.🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣
Zamani wakati Shetani hajajiunga na CCM ,Kimbilio la CCM lilikua ni taasisi za dini sasa wamemuasi Mungu wanategemea machifu , waganga na wachawi kwenye uchaguzi ujao na makanisa ya kina Mungu Zumaridi na yanayofanana nayo.
Kwa kweli ujumbe huu unapendeza sana asante.
 
Mkuu, kwa hali kilivyo kwa sasa Chadema ni chama kinacho kubalika haswa. Kama uchaguzi ukiwa huru na haki kinashinda kabla ya saa 6.00 mchana.
Kwa hiyo Rais atakuwa ni Mzee Mbowe?
 
Kwa mwaka huu 2024 imekuwa vigumu kujua kama CHADEMA ni chama cha siasa chenye nia ya kuhudumia Watanzania wote au ni Taasisi ndani ya taasisi ya dini katika madhehebu tofauti.

Miaka ya nyuma kulikuwa na minong'ono tu kuwa hiki ni chama kinadhaminiwa na Mlengo wa Kikristo.

Maneno hayo nilikuwa nayapinga mara kwa mara lakini leo hii, nashawishika kabisa kuwa maneno hayo yalikuwa na ukweli. Kwasababu kila tamko la CHADEMA linabaraka 100% ya maaskaofu na wachungaji na kila tamko au barua za kichungaji zote zina baraka ya CHADEMA kwa asilimia 100, Kulikoni?

ChADEMA ijikague, vinginevyo itapata kundi moja tu na kamwe huwezi kushika nchi kwa kundi moja tu. Bado mna nafasi.

Pia soma: Siasa na dini
Kama Askofu Gwajima , Mch lwakwatare , Msigwa walivoicha Ccm ijipambanue chama Cha siasa sio ?
 
Huyu Alii ni mwanasiasa nguli sana .
Nimependa jinsi anavyo jenga hoja zake. Watu kama hawa Chadema inatakiwa iwe na fungu maalumu la kuwaendeleza katika elimu ya siasa ili wawe Makada wenye uwezo zaidi katika propaganda na mbinu za kuidhoofisha CCM na kupunguza kura za CCM kwa namna watakayokutana nayo iwe ya kijanja au ya kihuni au vyovyote.

..tunatakiwa tuwawezeshe Chadema waweze kufika kila mahali na kufanya kampeni za uhakika.
 
Mkuu, kwa hali kilivyo kwa sasa Chadema ni chama kinacho kubalika haswa. Kama uchaguzi ukiwa huru na haki kinashinda kabla ya saa 6.00 mchana.

Ni kweli ila kwa Hali ya Jamii ya Tanzania Chadema ikiungana na ACT Wazalendo ndio upinzani itaingia Ikulu zote za Tanganyika na Zanzibar vinginevyo hakuna chama kitakachoitoa CCM madarakani kwa karne hii. Japo patakuwa na mabadiliko sana ya kiutawala lakini ndani ya CCM. tutatawaliwa mpaka na madereva achilia mbali Makonda .

Mpaka Sasa ACT inatajwa kuwa ni chama chenye harufu ya kidini kama ilivyo chadema .

Sasa kama ACT ina mtaji mkubwa Zanziba, Kundi,Kigoma, Baadhi ya kata kwenye mikoa ya pwani basi hakuna namna ya kuacha kushirikiana nao ili CCM isipate mwanya wa kushinda hasa kwenye ubunge na udiwani na serikali za mitaa .

Cha msingi tu ni kuwapata wagombea wanaomuogopa na kujua kuwa kuna siku Mungu atahukumu wetu wote bila kujali cheo .

Kwa sababu tukiweza tu ikulu na kusahau nature ya watanzania kiimani basi ni wazi kabisa kuwa shetani kupitia CCM atakua ameshinda na Mungu atadhalilishwa sana Tanzania . Na ule usemi wao wa ushindi wa CCM sio Mungu anayeweza kuuzuia wala kuupanga bali ni lazima utatumia .

Kwa hiyo kwa sasa kazi iliyopo mbele yetu ni kuhakikisha kuwa SHETANI HASHINDI NA KUITAWALA TANZANIA KUPITIA Mgongo wa CCM . Kwa sababu ushindi wa CCM ni ushindi wa shetani na anavyopata ni damu za watu kuongezeka kumwagwa kama shukrani na malipo yake.

Sasa wapinzani wakuu ACT kule Zanzibar na Chadema Bara wasipoungana ni wazi kuwa Tutakuwa tumemkabidhi shetani nchi rasmi .Hivyo tujiandae tu kuona uovu wa kila aina ukifanywa ikiwemo ulawiti,ushoga ,bidhaa feki na zenye sumu, usagaji, magendo ,madawa , uonevu , mauaji ,migogoro mikubwa ya ardhi,kutorosha kwa wanyama na madini n.k .
kushirikiana na ACT ni jambo la Busara sana na litaleta baraka kwenye nchi na litabalance siasa na kuleta amani kati ya dini zote za Haki na wapenda haki dunia nzima .
 
..tunatakiwa tuwawezeshe Chadema waweze kufika kila mahali na kufanya kampeni za uhakika.

Chadema wanakosa maarifa ya ushindi sio wapiga kura .

Kwanza mpaka sasa hawana hamasa ya kujiandikisha .

Mimi hua sielewi tu kuwa rasilimali zote zilizopo na mapesaengi yanayopotea kila idara kuundwa kwa bodi zisizo na tija kwenye kila taasisi ya umma tena bodi ya wastaafu walioshiba asali na waliohujumu mashirika na tasisis hizo hizo ,kweli tunashindwa kudhibiti ufisadi wa wachache ,kupunguza matumizi ya serikali na kudhibiti fungu kubwa la wasiojulikana na kisha kuwapa posho hata elfu 50 mpaka 100k wenyeviti wa serikali za mitaa kwa kazi kubwa wanayoifanya ambayo ndiyo hasa msingi wa amani ya nchi yetu hasa Tanganyika ?!!
.Kwa nini Chadema wasije na sera ya kuwalipa posho ya kalamu na karatasi na chai kwa wenyeviti wa serikali za mitaa na pia kuvutia vijana wasio na ajira lakini waliosomea uongozi ili wajitokeze kugombea nafasi hizo dhidi ya wazee wa washirikina wa CCM wanaotegemea ndumba kushinda na kukalia ofisi na pia waliozoea kuhongwa wakati wa uchaguzi na kutumika tu kwa hisani ya mafisadi .
Chadema kije na sera ya kubadili hadhi ya Mwenyekiti wa serikali ya mtaa na kumfanya ajiamini na kusimamia amani na rasilimali za nchi ikiwemo ardhi na mipango miji . Wasomi wajitokeze kugombea
 
 
Back
Top Bottom