howardlite
JF-Expert Member
- Jul 16, 2016
- 242
- 392
Wazazi na walezi wenye watoto hiki kinawahusu,baadhi ya wadada wanaotusaidia kazi nyumbani(house girls) wamekuwa na tabia za kufukuza bila kusubiri mwezi uishe kwa namna inavyo kera.
Nilikuja kukagua shughuli za mradi Geita,baada ya kumaliza siku tatu nikampigia simu rafiki yangu anayeishi nyuma kidogo ya Geita karibu na shule ya Wajas Secondary,akaniomba nisiondoke nipite kupaona wanapoishi then nisafiri.
Nikaona ni kweli tunaishi kama ndugu akanipa ramani nilipo karibia akaja kunipokea.
Nikiwa ndio nimefika dada mmoja ambaye baadae nilijua ni mdogo wa mke wake alitoa nguo nje kufua na sehemu ya nguo zilikuwa za watoto wa rafiki yangu,alikuwa na watoto wa kike na wa kiume wawili mmoja ana mwezi tangu azaliwe.
Ghafla yule dada akabaki anashangaa kwa taharuki akiwa na nguo mkononi,sisi wote wawili tukaelewa kuna kitu hakiko sawa.
Tukasogea alipo kujua ni nini, na yule rafiki yangu akamuita jina lake ni nini?Hakujibu badala yake tukawa tumefika karibu yake zaidi na kuona mkononi akiwa na nguo ya binti wa rafiki yangu ikiwa na damu.
Nafikiri unaweza kuelewa mawazo yanavyokuwa,baba akauliza hii si ni damu?
Mama mwenye nyumba akatoka ndani na binti wa kazi wakaja wote nje,jamani kurudi tena ndani zikakutwa nguo nyingine kwenye tenga zimewekwa chini na juu ziko nguo za dada wa kazi na harufu mbaya kwenye kile chumba anachokaa dada wa kazi.
Baada ya kumuliza dada alikiri kutumia nguo za watoto kama pads (pedi).
Mama wa mji akamuuliza sinilikuuliza umevunja ungo ukasema ndio,unatumia nini kujisitiri ukasema pedi na nikakwambia ukiona dalili niambie imekuwaje unafanyia watoto ukatili wa aina hii?Uliniambia nisikupe pedi?Hali ikawa hivyo na makofi juu, mwisho wakasema lazima uondoke inaonekana ni tabia yako ya siku nyingi,dada akasema ni mara ya kwanza na ndio imeanza na kunishtukizia ikaonekana ni muongo wakawasiliana na ndugu zake wakamrudisha kwao.
Nilikuja kukagua shughuli za mradi Geita,baada ya kumaliza siku tatu nikampigia simu rafiki yangu anayeishi nyuma kidogo ya Geita karibu na shule ya Wajas Secondary,akaniomba nisiondoke nipite kupaona wanapoishi then nisafiri.
Nikaona ni kweli tunaishi kama ndugu akanipa ramani nilipo karibia akaja kunipokea.
Nikiwa ndio nimefika dada mmoja ambaye baadae nilijua ni mdogo wa mke wake alitoa nguo nje kufua na sehemu ya nguo zilikuwa za watoto wa rafiki yangu,alikuwa na watoto wa kike na wa kiume wawili mmoja ana mwezi tangu azaliwe.
Ghafla yule dada akabaki anashangaa kwa taharuki akiwa na nguo mkononi,sisi wote wawili tukaelewa kuna kitu hakiko sawa.
Tukasogea alipo kujua ni nini, na yule rafiki yangu akamuita jina lake ni nini?Hakujibu badala yake tukawa tumefika karibu yake zaidi na kuona mkononi akiwa na nguo ya binti wa rafiki yangu ikiwa na damu.
Nafikiri unaweza kuelewa mawazo yanavyokuwa,baba akauliza hii si ni damu?
Mama mwenye nyumba akatoka ndani na binti wa kazi wakaja wote nje,jamani kurudi tena ndani zikakutwa nguo nyingine kwenye tenga zimewekwa chini na juu ziko nguo za dada wa kazi na harufu mbaya kwenye kile chumba anachokaa dada wa kazi.
Baada ya kumuliza dada alikiri kutumia nguo za watoto kama pads (pedi).
Mama wa mji akamuuliza sinilikuuliza umevunja ungo ukasema ndio,unatumia nini kujisitiri ukasema pedi na nikakwambia ukiona dalili niambie imekuwaje unafanyia watoto ukatili wa aina hii?Uliniambia nisikupe pedi?Hali ikawa hivyo na makofi juu, mwisho wakasema lazima uondoke inaonekana ni tabia yako ya siku nyingi,dada akasema ni mara ya kwanza na ndio imeanza na kunishtukizia ikaonekana ni muongo wakawasiliana na ndugu zake wakamrudisha kwao.