Wadau Huyu Fei Toto Mnamuonaje??

Kama sio mzuri mbona wakati wa usajili mlimfukuzia hadi Tandika kwa Maguruwe na akawachomolea nje. Ki ukweli dogo anajua na anacheza mpira wa ku relax. Ebu mkuu Sembo jaribu kumwaangalia alivyocheza mechi ya Yanga Vs Mtibwa (Chuo cha Soka) ndio utaona utamu wake.
 
Hahaha... Feisal 'anajitahidi'.. Ila kufikia vile 'viwango' vya kuwa tegemeo la Taifa.. Inatakiwa asibweteke, aweke kichwa chini na ajifunze toka kwa kaka zake kina Mkude.
Kwani Mkude anacheza namba ngapi Taifa stars maana naona ajifunze kwa Mkude zipo nyingi!
 
Mkuuu we endelea kupiga porojo mtandaoni.. Ukija kushituka unaona picha ajibu akisaini Simba.

Achana na zile habari za ndani zilizopo ofisini juu ya makubaliano yaliyofikiwa.. Anza na hii..

Meneja wa Ajibu anena haya.. “Kutokana na uwezo ambao anauonyesha Ajibu, viongozi wa Simba wamenifuata ili niweze kuzungumza nao kwani hata msimu uliopita kabla hajajiunga na Yanga walikua wakimhitaji"

Source: SIMBA WAMFUATA STRAIKA HUYU YANGA - SALEH JEMBE
 

Hahaha.. Sawa Mkuu.
 
Jipe moyo,kuna mchezaji wa simba leo hii kaniambia kwa mdomo wake wameshauriwa kutumia vizuri mshahara wa mwezi uliopita,mkuu endelea kujipa moyo
 
Huo ndio ukweli,huyo ndemla mwenyewe tulishamtia kibindoni akawa anawazuga anaenda sweden,ndio maana hata walipoenda turkey yy alichelewa kwenda,kama si yule nyika kumzingua mtu aliyetaka kumsajili Yanga yule dogo saa hizi angekua jangwani

Hahaha... Mkuu nami nataka niwasajilie Alex Kitenge katika dirisha dogo.. Vipi mtampokea??
 
fei toto ni mchezaji mzuri sana, tatizo ni 'uzanzibar' a.k.a mdebwedo, ila ball 'dancing' na 'control' kwa fei ni nyumbani kwake!
 
Wabongo huwa tunaleta ushabiki sana kuliko uhalisia. Ni ile tu kutaka kuonesha timu yako ni bora kwenye kila sekta dhidi ya mtani wako. Nasikitika kusema hata mkubwa Sembo upo kundi hili.

Feisal ni mchezaji mzuri ila kufikia uwezo wa Mkude afanye mazoezi usiku na mchana.
 
Ni kweli Mkuu.. Na ushauri wangu kwa watani zangu.. Kulikua kuna Juma Seif Kijiko.. Kukikua kuna Godfrey Mwashiuya..n.k wote walipotea kwa sifa kama hizi hizi wanazompa Feisal kwa sasa. Wapunguze kumpamba.
kulikuwa na Kichuya
 
Kipindi cha mwisho Mkude anasaini Simba.. Tulimpa 80 milioni keshi + gari + mazagazaga kibao.. Safari hii tunadouble hilo dau.. Mna uwezo wa kupambana??
Mkude kalifanyia nini hili Taifa??? na Simba kacheza miaka 7 ubingwa Mara mbili..ujue anazidiwa medali na Makapu...
 
Mkude ni balaa, we mchezaji karibia misimu 10 yupo kwenye kiwango bora kabisa unadhan mchezo.. kundi la mkude wapo akina yondani, sure boy, nyoni, boko, himid, kapombe, na wengine wachache.
ana medali ngapi za ligi??? mbili tu..Pato Ngonyani 4
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…