Wadogo zangu, kabla TV hazijaja enzi hizo mgeni alikuwa anapewa album atazame picha za zamani. Yaani umpe Mtanzania album asichomoe picha hata moja?

Wadogo zangu, kabla TV hazijaja enzi hizo mgeni alikuwa anapewa album atazame picha za zamani. Yaani umpe Mtanzania album asichomoe picha hata moja?

Woow..hii safi sana,niyakumbukayo;
1. Ndala za "Skyway"
2.Raba za "DH"
3.Suruali za "Tokyo & Beauct"
4.Mafuta ya kujipaka "Rays"
5.Tanbond sio blue band
6.Soda ya double cola na fahari.
7.Negro arushaa aliitwa " Masawee"
8.Peugeot 403 & 404[emoji3]

Viatu vya Cha Cha Cha unavijua?? Mwisho kuvivaa saa sita mchana.
 
Mama yangu mdogo alienda kusoma Ulaya akaja na TV, deki pamoja na mikanda ya akina Michael Jackson pamoja na Lionel Richie.

Zamani hata ukienda japani,china au marekani watu wanasema ameenda ULAYA au amerudi Kutoka ulaya.

Kuna jirani yetu alitoka Japani around 1994 au 95 akarudi na Hiace,TV na mziki mnene wakasema amerudi tajiri kwasababu alikuwa Ulaya.
 
Nasema uongo ndugu zanguuu.....
IMG_20210203_083647.jpg
 
Alikuwa anaitwa FOTOMII. Nkajua ndio jina lake kumbe ni PHOTO ME.. Aisee zamani raha na zile pipi kidonge zimepotelea wapi siku hizi
 
Album ni kitu Cha juz tu mtu alie zaliwa 2003 anaijua vizur sana maana pcha tumepiga sana had 2010 camera za simu nyingi za bei rahisi tulizoweza kuzimiliki ilikua ukipiga pcha inakua kituko
Hapo labda tu hawakukutana na usumbufu wa wapiga pcha, nakumbuka hata mm mwaka 2012 nilivyoenda kwa shangazi dodoma nilipewa album niangalia picha zao na baba wakiwa vijana wadogo ilikua ni Kama utamaduni flani hivi
 
Enzi hizo upige picha ukishindwa kuikomboa basi jamaa ataibandika kwenye kuta za studio yake kama adhabu, hivyo tulihakikisha tunazikomboa kuepuka kuanikwa.
Nakumbuka pozi lilikuwa kuchuchumaa au kushika maua au kusimama miguu sawa kama upo paredi ya jeshi
Nakumbuka ni juzi tu miaka ya 2007 Mara yangu ya kwanza kushonewa suti na shangazi ambayo hainitoshi ili nikue nayo nilipiga picha na dada yeye akiwa amechuchumaa nyingine tukapiga karibu na ua hivi vitu labda mtoto alie zaliwa mwaka 2009+ ndo anaweza kuwa hajakutana navyo[emoji16][emoji16]
 
Nishawahi fatilia picha almost mwezi mzima af nikaja ambiwa et zilivyosafishwa zilipeperuka
Mkuu hili neno "Unju bin Unuq" ina maana moja na hilo jina lako/ID? Kwa maana ndio a.k.a ya rapper mmoja hapa bongo anaitwa Nikki Mbishi.
 
Ila bongo tumetoka mbali, kitambo hata kutafuna bubble gum ilikuwa ni ufogo...
 
Ukiachana na haya ya album, hivi hawa watoto waliozaliwa juzi juzi wanajua kwamba hawa tunaowaita Wapiga debe jina lilitokana na kitu flani cha pembe nne kinachioitwa debe? Waliwahi kuliona debe? Siku hizi yapo wapi madebe wahenga?

Yanaitwa Madebe Lidai![emoji276]
 
Sasa utamu na uharisia ni upi hapa hivi watanzania wanaweza sifia uzamani hata kama ulikuwa wakipuuzi au ndio niko serious sana.
Mkuu, bila shaka jamaa alikuwa anajaribu kusisitiza kwamba maisha ya enzi hizo hayakuwa digital sana kama sasa hivi.
 
Hapo kwenye picha, utasikia hii siwezi kukupa kwa sababu nega yake haipo.
Na ilikuwa inachukiza kweli, umepiga picha leo unaipata baada ya mwezi, kila ukikutana na mpiga picha anakwambia mkanda haujajaa.
Hahahahaaa na mkanda kujaa ni baada ya weeks kadhaa kupita...
 
Enzi hizo hamna cd wala USB flash watu walikua mwendo LP au santoro kwa jina jingine na tapes,mtu unamwaazima tape unaringishia na Walkman
 
Back
Top Bottom