Wafahamu kwa Majina Makamu Wenyeviti Tangia Kuasisiwa Kwa CCM 1977. Ujue Kwanini Ameteuliwa Mzee Stephen Wasira na wote wamezaliwa kabla ya Uhuru

Duuuuuh kweli ndo tumefika huku siamini hata kidogo naomba kufahamu japo kidogo mashiko ya utendaji wake toka enzi za Nyerere kweli nyota na uchawa huamua si utendaji
 
Haidhuru ukituwekea
Nina mambo mengi sana ya kuweka muda huu mpaka muda hautoshi kabisa.hapa bado sijaweka uchambuzi wa uteuzi wa Mheshimiwa Stephen Wasira,bado sijaweka nini watanzania watarajie baada ya uteuzi huo n.k.
 
Acha kudharau wazee.Wazee ni hazina.Usione tunaishi kwa amani ukadhani ni busara za vijana tu ndio zinaongoza nchi.Ina maana hata baba yako humuamini kuwa ana busara za kuweza kuongoza familia yenu?Mbona ukirudi kule kijijini kwenu unawapigia wazee wako magoti na kuwaomba wakumiminie baraka zote.Kwa hiyo kwenye siasa tu ndio uone wazee hawana thamani.
Ndoa zenu zikiyumba mnakimbilia wazee kuokoa jahazi.
 
Unasema, “Ni watu ambao hawawezi kulisaliti Taifa letu pamoja na chama chetu…” Really?

Hivi kwa Kinana kutelekeza meli katikati ya bahari sio kitendo cha usaliti? Mtu asiyekuwa Msaliti ataifikisha meli bandari salama na kuikabidhi kwa nahodha mwingine. Kinana pia amehusishwa na tuhuma za uwindaji haramu wa wanyamapori wetu. Kama hizo tuhuma ni za kweli, basi sio kweli kwamba Kinana ni mmoja wa watu ambao hawawezi kulisaliti taifa letu.

Kufanya usaliti kwa chama ni kufanya kitu gani hasa? Hivi wakati ule Wasira alipohamia NCCR Mageuzi na kuwa mpiganaji wa jeshi la adui yake CCM hakufanya kitendo cha usaliti kwa chama chake?
 
MUHIMU
HUYU MAKAMU MWENYEKITI WA SASA APEWE ULINZI ULIO NA NYONGEZA KIDOGO UKILINGANISHA NA WATANGULIZI WAKE WOTE
ULINZI WA HUYU WA SASA INABIDI UONGEZWE KIDOGO
 
MUHIMU
HUYU MAKAMU MWENYEKITI WA SASA APEWE ULINZI ULIO NA NYONGEZA KIDOGO UKILINGANISHA NA WATANGULIZI WAKE WOTE
ULINZI WA HUYU WA SASA INABIDI UONGEZWE KIDOGO
Mungu asipoulinda mji aulindaye akesha bure.
 
SIHITAJI KUYAFAHAMU MAJITU YALIYOFILISI NCHI
 
Wa Visiwani wako wapi!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…