Wafanyabiashara Kariakoo wameiomba serikali iwaondoe raia kigeni (Wachina) wanaofanya umachinga

Wafanyabiashara Kariakoo wameiomba serikali iwaondoe raia kigeni (Wachina) wanaofanya umachinga

Kiuchumi ni bora wazawa wauze kwa bei kubwa wananchi wa kawaida wataumia ila mwisho wa siku mzunguko wa biashara na hela utabaki nchini na ile faida ya wafanyabiashara itatumika kwenye shughuli nyingine za kiuchumi ndani ya nchi. Haohao wakipata faida kubwa ndio watasaidia wengine, wataajiri, watahonga, watalipa ada, watanunua nyama, watafuga na kulima, watanunua simenti na mbao wajenge.

Ni bora hivyo kuliko Wachina waje na bei ndogo zaidi, waue soko la wazawa na viwanda vya ndani kisha faida yote waipeleke kwao huku wazawa ndani wakibaki vibarua. Singapore ina gharama kubwa za kuishi na sio nchi maskini, Burundi ina gharama ndogo sana za kuishi na biashara zao zinapata faida kidogo mno ila bado ni maskini wa kutupwa.

Namibia wana biashara zina faida na zina bei kuliko sisi ila wana maisha mazuri kutuzidi.
Wewe unataka kutuchota na uongo.
Ni bora mchina auze bei ndogo kuliko mzawa auze Bei juu. Bei juu inachochea inflation, inaangusha sarafu

Uchumi wetu sio wa bei juu, pia hata hao wazawa wakiuza bei juu bado atayefaidika sana ni hao hao wachina na wengine wa nje sababu sisi ni waagizaji wakubwa mno kuliko kuzalisha. Atanunua range ambalo atapeleka pesa nje, atanunua mafuta kila siku ambayo nayo tunatoa nje

Mchina akiuza bei ndogo ni faida kwetu sababu pesa nyingi tutabaki nayo mfukoni hapahapa na pia atasaidia kucontrol inflation
 
Hilo swala nalielewa vizuri sana. Issue yangu ni kwanini huyo Mtanzania asiende China au India akawanyonye ili awaplekee hela watanzania wenzake, baala yake na yeue anaungana nao kwenye kuwaumiza?
Wenzake wanaumiza ugenini, yeye anawaumiza wa nyimbani?
Mtu aje kukumiza Usukumani kisa hapeleki hela nje bali anaenda kujenga uchagani?
Unajua cost of loan kwa China na kwa Tanzania ni tofauti mkuu.

Mtanzania wa kawaida kukopa benki hawezi, mpaka uwe na ardhi iliyopimwa tena potential. Ardhi ikiwa ya 50M wanaikadiria 25M alafu riba, kodi ya mkopo na gharama nyingine lukuki juu. Unaanza kukatwa kabla hujazalisha. Hivyo faida kwa Mtanzania inabidi iwe kubwa kidogo kuliko mgeni mwenye government support kwao.

Meanwhile kuna raia wa kigeni anakuja na mapumbu na makatarasi anapewa mradi wa Mlimani City anakuwa financed na mabenki. Au anatokea Mwarabu anakabidhiwa mradi wa mwendokasi anaitwa mwekezaji ila hapohapo serikali inakopa NMB ikanunue mabasi 100 ambayo italipa yenyewe na mwekezaji ataweka mapumbu tu apate faida akafuge ngamia jangwani.

Bora wapate faida Wahindi na Waarabu wanaoishi bongo kina GSM na Mo Dewji kuliko wapate faida kina Meng Xian wanaotokea Wuah na hawana mpango wa kuwa hata na beki tatu hapa bongo. Kila senti wanairudisha kwao.
 
Work permit ya mgeni kufanya kazi Tanzania kwa mwaka ni mil 2 mpaka 5. Nakazi zenyewe nizile Professional, sasa naomba uniambie kama Kuna Mchina anapewa Work-permit yakua Chinga kaliakoo.

Na mtu akishakua machinga maana yake anauza bila kutoa risiti, Je tumeruhusu wageni kuuza bidhaa bila kutoa risiti?. Watalipaje Kodi stahiki?.

Na kigezo Cha Work-permit nikufanya kazi zile professional ambazo wazawa hawaziwezi. Sasa niambie umachinga umewashinda watanzania?.
hao tuliowapa mamlaka hawajatengeneza au kuweka mfumo sahihi naamini hizi hoja viongozi wameambiwa sana ila chura ni chura siku zote
 
Auze bei ndogo dukani kwake lkn sio auze kama machinga mtaani.
Hoja yako haikua mtaani Wala dukani Bali ulikua unapinga jumla vitu kuuzwa Bei ndogo.

Tukija suala la mtaani, wewe umemuona wapi anauza mtaani kama machinga? Hapo wanazungumzwa wanaouza dukani
Lakini hata Kama watakuja kuuza mtani tunapswa tuwaruhusu maana wanatusaidia kupunguza inflation. Nchi maskini kama Tanzania mama anayeuza vitumbua ikifika sikukuu ili anunulie Watoto wake nguo lazima aandae zaidi ya laki. Hapo Kuna uchumi gani unainuka?
 
Unajua cost of loan kwa China na kwa Tanzania ni tofauti mkuu.

Mtanzania wa kawaida kukopa benki hawezi, mpaka uwe na ardhi iliyopimwa tena potential. Ardhi ikiwa ya 50M wanaikadiria 25M alafu riba, kodi ya mkopo na gharama nyingine lukuki juu. Unaanza kukatwa kabla hujazalisha. Hivyo faida kwa Mtanzania inabidi iwe kubwa kidogo kuliko mgeni mwenye government support kwao.

Meanwhile kuna raia wa kigeni anakuja na mapumbu na makatarasi anapewa mradi wa Mlimani City anakuwa financed na mabenki. Au anatokea Mwarabu anakabidhiwa mradi wa mwendokasi anaitwa mwekezaji ila hapohapo serikali inakopa NMB ikanunue mabasi 100 ambayo italipa yenyewe na mwekezaji ataweka mapumbu tu apate faida akafuge ngamia jangwani.

Bora wapate faida Wahindi na Waarabu wanaoishi bongo kina GSM na Mo Dewji kuliko wapate faida kina Meng Xian wanaotokea Wuah na hawana mpango wa kuwa hata na beki tatu hapa bongo. Kila senti wanairudisha kwao.
Kukopa bank sio lazima uwe na ardhi. Mimi nimekopa bank na sikuweka ardhi. Rekebisha hili kwanza
 
Hii nimekumbuka mbali Sana ,niliwahi kwenda kutafuta chumba Cha kupanga keko ,Sasa mwanangu mmoja wa mitaa hiyo akanipa namba eti huyo ni dalali wa uhakika na atanipa chumba kizuri .

Doh salale nakuja kukutana na mchina ndiye dalali ana kiswahili Cha wandengereko ,nilikuwa nazunguka naye huku nikipata chance ya kukaa nyuma yake nacheka weeee ,alafu akiniuliza mbona unacheka nasema nimemkumbuka mama anavyonitaniaga .

Ila nilimgomea vyumba vingi ili nimtembeze zaidi kulipiza manyanyaso waliyopata mababu zetu .

Mpaka nakuja kukubali chumba ,macho yake yameumuka mpaka sio poa na amekuwa mwekundu 🤣
 
Hoja yako haikua mtaani Wala dukani Bali ulikua unapinga jumla vitu kuuzwa Bei ndogo.

Tukija suala la mtaani, wewe umemuona wapi anauza mtaani kama machinga? Hapo wanazungumzwa wanaouza dukani
Lakini hata Kama watakuja kuuza mtani tunapswa tuwaruhusu maana wanatusaidia kupunguza inflation. Nchi maskini kama Tanzania mama anayeuza vitumbua ikifika sikukuu ili anunulie Watoto wake nguo lazima aandae zaidi ya laki. Hapo Kuna uchumi gani unainuka?
Ndio malalamiko ya machinga haya ,wachina wanauza kaliakoo kama machinga, wanapanga vitu chini kama machinga.

Je "Work permit zao " zinawaruhusu kufanya umachinga?.

Sasa naomba nikuulize kinachosababisha kua na uchumi mbaya na pesa yatu kushuka thamani?.

Kwa nini vitu vinavyoagizwa nje vinakua na bei ndogo kuliko vinavyozalishwa ndani?.

Kwa nini nchi kama Burundi/Zambia/ Uganda wanapitisha vitu kwenye bandari yetu lkn wao wanauza bei ndogo kuliko sisi wenye bandari?.

Tatizo lakuimarisha uchumi wetu litafanikiwa pindi tutakapoweza kubadilisha malighafi zetu kuwa bidhaa na sio kuruhusu wachina kua wauzaji wa rejareja na machinga mtaani.
 
Ndio malalamiko ya machinga haya ,wachina wanauza kaliakoo kama machinga, wanapanga vitu chini kama machinga.

Je "Work permit zao " zinawaruhusu kufanya umachinga?.

Sasa naomba nikuulize kinachosababisha kua na uchumi mbaya na pesa yatu kushuka thamani?.

Kwa nini vitu vinavyoagizwa nje vinakua na bei ndogo kuliko vinavyozalishwa ndani?.

Kwa nini nchi kama Burundi/Zambia/ Uganda wanapitisha vitu kwenye bandari yetu lkn wao wanauza bei ndogo kuliko sisi wenye bandari?.

Tatizo lakuimarisha uchumi wetu litafanikiwa pindi tutakapoweza kubadilisha malighafi zetu kuwa bidhaa na sio kuruhusu wachina kua wauzaji wa rejareja na machinga mtaani.
Bado tunarudi palepale kama Bei zao nzuri hakuna mtu atanunua kwa mchina, wapunguze Bei

Work permit zao zinaruhusu kufanya umachinga? Unajua ukienda kwa tafsiri ya umachinga basi hutapata pa kuwashika maana tafsiri yake haipo rasmi

Kinachofanya tuwe na uchumi mbaya ni kutozalisha, pesa yetu inakosa nguvu sababu uzalishaji upo chini. Na wanaosababisha ni hao hao wanaolalamika, anaona bora aende kununua kitu China kwa 1000 alafu aje auze 8000 huku atapata faida kubwa

Viyu vinavyoagizwa nje vina bei ndogo sababu wenzetu wanatumia teknolojia rahisi kuzalisha kwa wingi

Burundi Zambia Uganda vitu bei chini kuliko kwetu, hii mbona unajifunga mwenyewe ambae unatetea bei tuuziwe kubwa kuliko uhalisia. Hapo ndio uone wachina wanaouza Bei chini wapo sahihi na ndio kitu nimekuambia

Hizo malighafi zetu tunabadilisha kuwa bidhaa kwa maneno? Kipi kianze tufukuze wachina ndio tubadiloshe malighafi zetu kuwa bidhaa au tuanze kubadilisha malighafi kuwa bidhaa alafu wachina watakimbia wenyewe sokoni? Ni sawa na utake kwenda peponi/mbinguni kabla ya kufa
 
Hii pia ni point muhimu, ni muunge mkono mtanzania anayenitia hasara wakati wafanyabiashara wa kitanzania wenyewe wanalalamikiana kama hapa
T14 Armata hapa unasemaje? Mimi kwangu naona bora ya mhindi na mchina wanaoniuzia kiatu kipya kwa shilingi 20,000 kuliko mbongo anayenunua kwa mchina halafu anaenda kuvisugua ngozi na soli vioneka ni european used halafu ananiuzia 70,000 hadi 90,000/-
Wachina walikuwa na protectionalism kwenye textile industry, hawakuruhusu kirahisi nguo kutoka nje kuingia kwenye masoko yao. Wakakua kwenye hiyp sekta.

Wachina walilazimisha partnership kwenye automobile industry. Ukitaka kuuza magari mengi kwao lazima ujenge assembly plant uzalishie kwao. Ukijenga plat lazima uwe na tech transfer na lazima ushirikiane na local firm matokeo yake ni magari kadhaa ya Kichina kufanana na ya makampuni ya kigeni yaliyoshirikiana nayo. Mfano hili JMC ni kama Isuzu
7bb1de95-0418-424c-8548-0d681c7b61e7.jpg


Sasa kwanini sisi tusiwe na protectionalism kisa eti tunawakomoa watu wa Kariakoo. Mwafrika anatumia akili gani sijui
 
Wachina walikuwa na protectionalism kwenye textile industry, hawakuruhusu kirahisi nguo kutoka nje kuingia kwenye masoko yao. Wakakua kwenye hiyp sekta.

Wachina walilazimisha partnership kwenye automobile industry. Ukitaka kuuza magari mengi kwao lazima ujenge assembly plant uzalishie kwao. Ukijenga plat lazima uwe na tech transfer na lazima ushirikiane na local firm matokeo yake ni magari kadhaa ya Kichina kufanana na ya makampuni ya kigeni yaliyoshirikiana nayo. Mfano hili JMC ni kama IsuzuView attachment 3150411

Sasa kwanini sisi tusiwe na protectionalism kisa eti tunawakomoa watu wa Kariakoo. Mwafrika anatumia akili gani sijui
Huko kote sikukatalii kaka, una make a very big point.
Mimi issue yangu ni yule aliyesema kuliko kununua kitu kipya kwa mchina ni heri kuibiwa na mtanzania mwenzangu sababu hela itabaki nchini kwa kuwa ataitumia hapahapa kufanya maendeleo. Yaani mimi niibiwe, nipate hasara, nidharirike kisa ataenda kusaidia ndugu zake ambao ni watanzania pia.
Yaani yeye anunue kitu kwa mchina kwa 30,000 anaenda kikikwangua kionekane used ya euro hala niuzie shilini 90,000 mimi nione ni sawa kuliko nikanunue kwa mchina wakati hata huyu anayenitapeli pia kanunua kwa mchina.
 
Wachina walikuwa na protectionalism kwenye textile industry, hawakuruhusu kirahisi nguo kutoka nje kuingia kwenye masoko yao. Wakakua kwenye hiyp sekta.

Wachina walilazimisha partnership kwenye automobile industry. Ukitaka kuuza magari mengi kwao lazima ujenge assembly plant uzalishie kwao. Ukijenga plat lazima uwe na tech transfer na lazima ushirikiane na local firm matokeo yake ni magari kadhaa ya Kichina kufanana na ya makampuni ya kigeni yaliyoshirikiana nayo. Mfano hili JMC ni kama IsuzuView attachment 3150411

Sasa kwanini sisi tusiwe na protectionalism kisa eti tunawakomoa watu wa Kariakoo. Mwafrika anatumia akili gani sijui
Sisi sio wachina kwa vitu vingi ila tunaweza kujifunza kwa wachina wamewezaje japo kazi nzito kweli kweli kwa sababu itahusisha mambo mengi

Nikuulize swali umewahi kufanya kazi na wachina ?
 
Bado tunarudi palepale kama Bei zao nzuri hakuna mtu atanunua kwa mchina, wapunguze Bei

Work permit zao zinaruhusu kufanya umachinga? Unajua ukienda kwa tafsiri ya umachinga basi hutapata pa kuwashika maana tafsiri yake haipo rasmi

Kinachofanya tuwe na uchumi mbaya ni kutozalisha, pesa yetu inakosa nguvu sababu uzalishaji upo chini. Na wanaosababisha ni hao hao wanaolalamika, anaona bora aende kununua kitu China kwa 1000 alafu aje auze 8000 huku atapata faida kubwa

Viyu vinavyoagizwa nje vina bei ndogo sababu wenzetu wanatumia teknolojia rahisi kuzalisha kwa wingi

Burundi Zambia Uganda vitu bei chini kuliko kwetu, hii mbona unajifunga mwenyewe ambae unatetea bei tuuziwe kubwa kuliko uhalisia. Hapo ndio uone wachina wanaouza Bei chini wapo sahihi na ndio kitu nimekuambia

Hizo malighafi zetu tunabadilisha kuwa bidhaa kwa maneno? Kipi kianze tufukuze wachina ndio tubadiloshe malighafi zetu kuwa bidhaa au tuanze kubadilisha malighafi kuwa bidhaa alafu wachina watakimbia wenyewe sokoni? Ni sawa na utake kwenda peponi/mbinguni kabla ya kufa
Tanzania utitili wa kodi ni kibao kwa wazalishaji.
 
Nilishawahi kusikia kule China Bank za China ukishakuwa na Yard umefence vizuli basi wanakufata unawapa business Plan yako wanakupa pesa ya kununulia machine mpaka malighafi ni chench kidogo ya kutaftia Soko ulejeshaji utaanza pale tu utakapoanza Uzalishaji
Njoo Bongo sasa ile umepewa mkopo kabla hujatoka dirishani wanafyeka mara Bima,sijui Amana mara sijui vitu gani Yaani ukiomba million kumi jua laki tano unawaachia siku ya kwanza tu, na tarehe kama hiyo mwezi unaofata wanaanza kuchukua Chao, Kwakweli unaweza kujikuta Mtanzania unamuonea huruma tu
 
Sisi sio wachina kwa vitu vingi ila tunaweza kujifunza kwa wachina wamewezaje japo kazi nzito kweli kweli kwa sababu itahusisha mambo mengi

Nikuulize swali umewahi kufanya kazi na wachina ?
Mifumo yetu hairuhusu Mjasiliamali kukua kidogo kidogo, ili ukue inabidi kuwe na nguvu ya ziada ndo maana miaka nenda miaka Ludi wazalishaji ni wale wale na wachuuzi ni wale wale, kuhama kutoka Mfanyabiashara mpaka kuwa Mzalishaji ni kipengele sana ongezea na soko huria ushindani wa wafanyabiashara wanaoagiza nnje bidhaa. Wenzetu protectionism waliifanya serious sasa sisi tumeshajifunga na mikataba ya kila aina unazuiaje bidhaa zao
 
Mifumo yetu hairuhusu Mjasiliamali kukua kidogo kidogo, ili ukue inabidi kuwe na nguvu ya ziada ndo maana miaka nenda miaka Ludi wazalishaji ni wale wale na wachuuzi ni wale wale, kuhama kutoka Mfanyabiashara mpaka kuwa Mzalishaji ni kipengele sana ongezea na soko huria ushindani wa wafanyabiashara wanaoagiza nnje bidhaa. Wenzetu protectionism waliifanya serious sasa sisi tumeshajifunga na mikataba ya kila aina unazuiaje bidhaa zao
Tunahitaji kubadili fikra zetu kwa kweli hasa kwa wale wenye maamuzi ya kisera,sheria
 
Sisi sio wachina kwa vitu vingi ila tunaweza kujifunza kwa wachina wamewezaje japo kazi nzito kweli kweli kwa sababu itahusisha mambo mengi

Nikuulize swali umewahi kufanya kazi na wachina ?
Siri ya wachina inabidi ujue historia yao.

China ni nchi ya watu wenye akili nyingi kitambo, kuna majengo yamejengwa miaka 3000 iliyopita mpaka leo wapo.


Kwa nini China kwa sasa ipo vizuri?
Jibu: Deng Xiaoping
Alikuwa "Rais" wa pili wa China,Huyo mzee ndio chanzo cha utajiri wa china. Yaani ni kama zali za mentali kupata kiongozi mjanja kama huyo. Kafatilie historia yake ndio utaelewa.

Ila Mchina ni mwizi wa teknolojia, mjanja sana halafu mchina anafanya kazi kwelikweli


Pia mchina anatafuta jinsi ya kuzalisha kwa bei ndogo mno ili kuvutia dunia nzima kununua vitu kwake. Nguo na viatu, mapochi ni synthetic materials za nguo, ngozi e.t.c


Mchina anapata mkopo kwa masharti nafuu ni rahisi biashara kukua kwa haraka.

Kuanzisha kiwanda china ni bei nafuuu na rahisi sana ndio maana viwanda ni vingi sana.
 
Back
Top Bottom