Wafanyabiashara Stendi ya Magufuli wataka mabasi yote yashushe na kupakia abiria hapo stendi ili wapate wateja

Wafanyabiashara Stendi ya Magufuli wataka mabasi yote yashushe na kupakia abiria hapo stendi ili wapate wateja

Hapo unakosea, nadhani mabasi yanaweza kushusha huko kote kakini safari ikianza lazima gari iingie stendi na ikiisha inapita stendi kabla ya kuelekea huko kwingine.
Nadhani hilo ndio la muhimu.
Na ndilo linalofanyika Sasa hivi mkuu
 
Sgr nayo iwe inafuata abiria. Mkuu utaratibu lazima uwepo na upo kila nchi. Hiyo ya mabus kufata abiria sio sahihi ni kulazimisha tu
imagine unakaa bunju ukisafiri kutokea Arusha au tanga via bagamoyo road inabid ukashushiwe Mbezi ili kumfurahisha shopkeeper wa stand kuu
hii aina ya uwazaji huwa inanishangaza sana
 
  • Abiria wanaoishi nje ya stendi ya Magufuli,,,wanatakiwa wafike stendi kwa mfumo wa usafiri wa ndani ya jiji....(Daladala,bolt,Bajaaj,boda)
  • Kwani unafkiri Ubungo ilikuwa karibu kwa kila mtu,,,watu wa Bunju,Chanika,Mbande,Kibada,Ununio,Mbweni,Kimbiji....ushawahi kaa hayo maeneo ,,,nayo yapo mbali kutoka Ubungo.
Ubungo kwa sasa ni kama hub ya mkoa wa dar,
 
Mimi mfano nakaa mbezi ila nikifika kituoni nataka kwenda Moro naambiwa usafiri wa mabasi ya Abood haupatikani hapo ...Yapo Urafiki. Basi linajazia urafiki then linapita juu kwa juu Mbezi bila ya kuingia ndani stendi!

Zaidi ya asilimia 75-80 ya basi zinazoondoka alfajiri haziingii ndani ya stendi ya Magufuli badala yake zinapita juu kwa juu.

Wamiliki wa mabasi wanaihijumu serikali , wanaikosesha serikali mapato yake ya getini. Pia wanawahujumu watanzania kwa kuwakosesha ajira
Hapo umemdanganya mabasi yanapitia ndani ya stendi hasa yanayotumia njia ya chalinze.
 
Tutaangalia interest ya abiria. Ndio maana huko kote Kuna mabasi yanaanza huko. Kwa watu wa mbande, kimbiji etc Kuna stendi Kigamboni, chanika, Temeke nk. Kwa bunju mabasi yanapitia njia ya bagamoyo au anaweza kukimbilia basi magomeni au urafiki Lazima tuwa appreciate wenye mabasi kwa kuwajali abiria baadala ya kulaumu.
Interest ya abiria au wateja ndiyo husababisha kuwe na
  • Nyumba za ibada hadi ufukwe wa Coco
  • Sheli hadi kwenye Masoko na makazi ta watu
  • Bar hadi kwenye makazi au maeneo ya shule.
  • Stendi za Mabasi kila chocho
Vitu lazima vikae kwa mpango...
Dar ni Jiji kubwa Serikali inapasa iweke stendi kubwa tatu...watu wazifuate stendi....
Aya magari ni makubwa hayatakiwi kabisa yapite kwenye njia za Tarura.
 
Utaratibu ni ustaarabu, wafuate utaratibu ma bus yote yapakie na kushusha abiria ndani ya stand ya ma bus na siyo vinginevyo. Kila siku tunalalamikia teuzi za rais, ni kwa sababu ya upuuzi kama huu.

Mkuu wa mkoa yupo, Mkuu wa wilaya yupo, Mkurugenzi yupo, afisa biashara wa mkoa na wilaya wapo, wachumi wa mkoa na wilaya wapo, Askari polisi na askari wa usalama barabarani wapo, kwanini bus lipakie abiria nje au kushusha abiria nje ya stand iliyojengwa kwa madhumuni hayo?

Wahusika wasimamie au watumbuliwe waje wengine wenye nia na kazi hizo.

Hapo nyuma tulilalamikia ndege binafsi kutua kila mahali biula taarifa wala ukaguzi, viwanja vya ndege vimepanuliwa na mamlaka husika walisimamia hili, bandari bubu zilizokuwa zikiingiza vitu vya magendo kama sukari na bidhaa zingine, tulilalamika mamlaka zikashughulikia, sasa kwanini hawa wa mamlaka za usafirishaji wasishughulikie hili la buses na abiria?

Tusipende vitu vya shaghalabaghala, tujenge tabia za kufuata taratibu sisi wenyewe, tunaposhindwa mamlaka husika zisimamie turudi kwenye mstari ndiyo majukumu yao. Na kama waliopewa dhamana hizo wameshindwa na watumbuliwe tu.

Na kama hii ndiyo sababu ya kutumbua watu basi atumbue asubui na jioni na ikiwezekana kila siku mpaka tupate watendaji wanaoelewa majukumu yao.

Nchi zilizoendelea zinatushinda kwasababu wao raia wao kwanza wanapenda utaratibu, na mamlaka zao zina enforce sheria zilizowekwa. Kama ni kutupa uchafu kwenye ndoo wote watatupa uchafu kwenye ndoo, na atakayefanya tofauti anachukuliwa hatua, hapa kwetu watu wanatetea ujinga.

Stand imejengwa kwa madhumuni gani, ikiwa kila mtu atafanya anavyopenda? Miafrika tuone aibu, hivi ni vitu vidogo tujielekeze wenyewe, tusisubiri kusukumwa.

Vijana wanakimbilia south Afrika na Ulaya, au Amerika kupata fursa, sasa bila utaratibu huku nani angeenda?

Nasi tujifunze matumizi mazuri ya akili na vitu , Stand ya bus, ma bus yote yangie stand, na abiria wote washukie stand na kupanda ma bus stand, kama ilivyo kwa ndege, habiria hupanda na kushukia airport na buses iwe hivyo.



Tuache hizi tabia tuendelee.
🤣 🤣 🤣
 
Interest ya abiria au wateja ndiyo husababisha kuwe na
  • Nyumba za ibada hadi ufukwe wa Coco
  • Sheli hadi kwenye Masoko na makazi ta watu
  • Bar hadi kwenye makazi au maeneo ya shule.
  • Stendi za Mabasi kila chocho
Vitu lazima vikae kwa mpango...
Dar ni Jiji kubwa Serikali inapasa iweke stendi kubwa tatu...watu wazifuate stendi....
Aya magari ni makubwa hayatakiwi kabisa yapite kwenye njia za Tarura.
Hapo nakubaliana na wewe.
 
Kwa hiyo na ndege zifuate abiria walipo? Kuna haja gani ya kutumia pesa nyingi kujenga stendi??
NB: Arusha mbaki na stendi yenu maana tumeona hazina umhimu.
Na Kwa iyo pikipiki ziwe na stendi Yao na abiria wazifuate huko na kuangukia huko!!
Elewa kila kitu kina namna ya huduma yake. Je, ulishawai kuona ndege imepaki mtaani kwenu au popote ale nje ya airport? Na je, ulishawai kuona meli inapakia abiria magogoni zaidi ya bandarini?? Lakini maboti na mitumbwi yanashusha abiria popote kando ya bahari/ maziwa au mtoni.
Acha kasumba hizo na utaratibu huu uendelee.
 
Maana ya Stend ni nini? Kahiyo abiria wote walazimishwe kushuka hapo Stendi ili wafanyabiashara wafanye biashara? Hiyo ni sehemu ya biashara?

Kwahiyo abiria wakiamua wanakuja kufuatwa na vyombo vya usafiri binafsi pia mtaanza kulia kuwa hakuna abiria kupanda gari binafsi bali ni bodaboda na taxi za stendi?

Iwapo makampuni wakaanzisha huduma ya kubeba abiria walioshuka kutoka kwenye mabasi yao bure kuelekea njia ya katikati ya mji pia mtaanza kulalamika?

Acheni lawama, wahimize serikali watengeneze njia nzuri kwa kila mwananchi kunufaika bila kutumia matatizo ya mwingine kama sehemu ya kuponea kwake....mbona Airport abiria wananunua kitu wakipenda na wala hawalazimishwi? Shida mnafanya vitu kiholela sana ndiyo maana hayo majengo mnayaaribu kabla ya kuanza kutumika.

Majengo mengi ya stendi watu wamejianzishia maduka uchwara tofauti na ubunifu ilivyokuwa awali.
✍️📝👍👌👏👊🤝🙏
 
Wanashauri ujinga fikiria mtu anaishi Boko au Mwenge basi Lina Toka Arusha au Moshi au Tanga linalopita Njia hiyo Kwa hiyo linapita hapo Boko na hapo Mwenge linakwenda na abiria Hadi stendi ya Magufuli linawashusha kule waanze kutafuta usafiri wa kurudi Mwenge na Boko basi linarudi tupu hata kama linapaki Mwenge au boko si.biashara kichaa hiyo

Au mtu anaishi mbagala anatoka Lindi na Mtwara basi linafika mbagala linapitiliza mbagala na huyo abiria Hadi stendi ya magufuli linamshusha atafute usafiri wa kurudi mbagala basi linarudi mbagala tupu hata kama linapaki mbagala huo ni wendawazimu

Hakuna abiria atakubali Hilo
Usitumie matako kufikiria...hakuna aliyesema kuwa abiria wa njiani asishushwe kabla ya basi kufika Magufuli bus terminal....kinachogusiwa hapa ni magari kugoma kupakia abiria hapo Magufuli
 
Wanashauri ujinga fikiria mtu anaishi Boko au Mwenge basi Lina Toka Arusha au Moshi au Tanga linalopita Njia hiyo Kwa hiyo linapita hapo Boko na hapo Mwenge linakwenda na abiria Hadi stendi ya Magufuli linawashusha kule waanze kutafuta usafiri wa kurudi Mwenge na Boko basi linarudi tupu hata kama linapaki Mwenge au boko si.biashara kichaa hiyo

Au mtu anaishi mbagala anatoka Lindi na Mtwara basi linafika mbagala linapitiliza mbagala na huyo abiria Hadi stendi ya magufuli linamshusha atafute usafiri wa kurudi mbagala basi linarudi mbagala tupu hata kama linapaki mbagala huo ni wendawazimu

Hakuna abiria atakubali Hilo
🙋‍♂️📝✍️👍👌👏👊🤝🙏
 
Hakika hata mimi nilipita stendi nilishangaa kwenye lile ghorofa wanauza andazi sh 100 alafu na chai kwenye kikombe cha plastic. Waliotokea mikoani vijijini wameelewa hii code.
Lakini DC na mbunge wake wanaweza kumaliza tatizo hili.
 
Mimi mfano nakaa mbezi ila nikifika kituoni nataka kwenda Moro naambiwa usafiri wa mabasi ya Abood haupatikani hapo ...Yapo Urafiki. Basi linajazia urafiki then linapita juu kwa juu Mbezi bila ya kuingia ndani stendi!

Zaidi ya asilimia 75-80 ya basi zinazoondoka alfajiri haziingii ndani ya stendi ya Magufuli badala yake zinapita juu kwa juu.

Wamiliki wa mabasi wanaihijumu serikali , wanaikosesha serikali mapato yake ya getini. Pia wanawahujumu watanzania kwa kuwakosesha ajira
Unadanganya kwa faida ya Nani sasa, wengi tunatumia hicho kituo, Abood kwa mfano ana basi zinaanzia hapo magufuli,, ila kimsingi ya Magufuli haijai mapema kuliko Ile inayopaki Engen Ubungo, ndo maana watu wanaona ni bora kupandia basi Ubungo,.
 
Interest ya abiria au wateja ndiyo husababisha kuwe na
  • Nyumba za ibada hadi ufukwe wa Coco
  • Sheli hadi kwenye Masoko na makazi ta watu
  • Bar hadi kwenye makazi au maeneo ya shule.
  • Stendi za Mabasi kila chocho
Vitu lazima vikae kwa mpango...
Dar ni Jiji kubwa Serikali inapasa iweke stendi kubwa tatu...watu wazifuate stendi....
Aya magari ni makubwa hayatakiwi kabisa yapite kwenye njia za Tarura.
🙋‍♂️📝✍️👍👌👏👊🤝🙏
 
Hassan Bomboko, Dc wa wilaya ya Ubungo aache kuhangaika na machangudoa wa Riverside na Sinza badala yake ajikite hili suala linalotokea katika kata yake ya Mbezi na ubungo.

Aamke alfajiri akafunge ofisi za haya Mabadi pale urafiki na shekilango ayaamuru yakapakie mbezi, magufuli bus terminal
 
Back
Top Bottom