Wafanyabiashara Stendi ya Magufuli wataka mabasi yote yashushe na kupakia abiria hapo stendi ili wapate wateja

Wafanyabiashara Stendi ya Magufuli wataka mabasi yote yashushe na kupakia abiria hapo stendi ili wapate wateja

Wanashauri ujinga fikiria mtu anaishi Boko au Mwenge basi Lina Toka Arusha au Moshi au Tanga linalopita Njia hiyo Kwa hiyo linapita hapo Boko na hapo Mwenge linakwenda na abiria Hadi stendi ya Magufuli linawashusha kule waanze kutafuta usafiri wa kurudi Mwenge na Boko basi linarudi tupu hata kama linapaki Mwenge au boko si.biashara kichaa hiyo

Au mtu anaishi mbagala anatoka Lindi na Mtwara basi linafika mbagala linapitiliza mbagala na huyo abiria Hadi stendi ya magufuli linamshusha atafute usafiri wa kurudi mbagala basi linarudi mbagala tupu hata kama linapaki mbagala huo ni wendawazimu

Hakuna abiria atakubali Hilo
Mkuu,
Kwanza kulikuwa na mpango wa kupiga Rami kutoka Bunju B hadi Msakuzi na kufika Mbezi Magufuli....

Pili kulikuwa na mpango wa stendi ya Njia za kusini kujengwa Mbagala....yani Dar kuwa na stendi kubwa mbili kama ilivyo Mwanza.

Ila hapa suala ni kwanini Mabasi yanaenda kupandishia watu Shekilango na vituo vya ndani....

Kuna barabara za ndani Mabasi hayaruhusiwi kupita....Mabasi yanafika mwenge kutafuta nini?
 
Kituo Chenyewe hakuna sehemu za kukaa, vituko vya binafsi kuna sehemu maalumu za kupumzika. Wanachojali ni mapato na si ustaarabu.
Pia jiji la Dar es salaam na ukubwa wake linahitaji Stand za Bus zaidi ya 3! Kigamboni, Mkuranga na Vingunguti...... aiji akilini mtu anaeishi Mbagala maji matitu bus aje apande Mbezi.....au yule anaekaa Masaki ya Pugu....aje Mbezi kupanda Bus la kwenda Lindi kwa mfano
 
Siku zote biashara haitakiwi kutegemea Stendi, bali stendi ndio inapaswa kutegemea biashara yako, shida ni hawa wafanyabiashara walidanganywa na ccm

Nimepita hapo stendi zaidi ya mara 50 lakini sikuwahi kununua chochote, hii ni kwa sababu si lazima abiria kununua kitu hapo stendi, sasa wanacholilia ni nini?

Ila nchi hii ina viongozi wa ajabu sana, hapo unakuta waziri anayehusika kwa kushirikiana na timu Msoga, kwakua tu stendi ina jina la Magufuli, basi kubadilisha jina, ikashindikana baada ya mchezo wao kuwekwa mitandaoni.

Wameona waje na mbinu ya kutofanya ulazima kwa wamiliki wa ma bus kuhakikisha wanashushia abiria na mizigo yao pale stendi...... Ili stendi ijifie yenyewe taratibu..... Jambo la aibu na linalopaswa kukemewa na jambo hili linaendelea kuonyesha kwa namna gani nchi hii inaongozwa wajinga waliopewa nafasi. Hivi JPM angekua hai, kuna mmiliki wa ma bus angeivimbia serikali namna hiii??.

Alafu hapo kuna dola, dola hiii hiii tunayosema kila siku iko mafunzoni kuhakikisha jicho lake linamulika kwa masilahi mapana ya taifa. Nadhani moja ya sehemu inayoitaji kufumuliwa ni mfumo mzima wa dola, umejaa wapigania matumbo tu .

Enyi wavivu, wazembe, wala rushwa na mafisadi wakubwa, jina la John pombe Magufuli, hili halitakaa kufutika mioyoni wa taifa hili, historia itayasahau majina yenu pale tu mtakapokufa, lakini haitokaa kumsahau JPM.
Ebu wahurumie wananchi wewe, Kuna Ubaya gani ikiwa gari inalala Chanika,ikasema abiria aliyetoka nalo Mwanza ambaye anaishi Gongo la Mboto au Chanika asogezwe mpaka huko?

Unajua gharama ya mtu mwenye mizigo kutoka hapo stendi usiku saa nane kwenda Chanika au Mbagala au Kigamboni ni shilingi ngapi?.

Unataka watu wateseke eti ili wengine wafanye biashara kwenye miili yao!. Si wabadilishe aina za biashara?.
 
Mkuu,
Kwanza kulikuwa na mpango wa kupiga Rami kutoka Bunju B hadi Msakuzi na kufika Mbezi Magufuli....

Pili kulikuwa na mpango wa stendi ya Njia za kusini kujengwa Mbagala....yani Dar kuwa na stendi kubwa mbili kama ilivyo Mwanza.

Ila hapa suala ni kwanini Mabasi yanaenda kupandishia watu Shekilango na vituo vya ndani....

Kuna barabara za ndani Mabasi hayaruhusiwi kupita....Mabasi yanafika mwenge kutafuta nini?
Nadhani ni marketing strategy wa wenye mabasi.
 
Abiria wengi wanaishi maeneo nje ya stendi. Hivyo mabasi yanaanza kwanza kuwachukua huko nje ndipo yaje stendi ya Magufuli. Ni njia moja ya kupata abiria wengi.
  • Abiria wanaoishi nje ya stendi ya Magufuli,,,wanatakiwa wafike stendi kwa mfumo wa usafiri wa ndani ya jiji....(Daladala,bolt,Bajaaj,boda)
  • Kwani unafkiri Ubungo ilikuwa karibu kwa kila mtu,,,watu wa Bunju,Chanika,Mbande,Kibada,Ununio,Mbweni,Kimbiji....ushawahi kaa hayo maeneo ,,,nayo yapo mbali kutoka Ubungo.
 

Ila nchi hii ina viongozi wa ajabu sana, hapo unakuta waziri anayehusika kwa kushirikiana na timu Msoga, kwakua tu stendi ina jina la Magufuli, basi kubadilisha jina, ikashindikana baada ya mchezo wao kuwekwa mitandaoni.

Wameona waje na mbinu ya kutofanya ulazima kwa wamiliki wa ma bus kuhakikisha wanashushia abiria na mizigo yao pale stendi...... Ili stendi ijifie yenyewe taratibu..... Jambo la aibu na linalopaswa kukemewa na jambo hili linaendelea kuonyesha kwa namna gani nchi hii inaongozwa wajinga waliopewa nafasi. Hivi JPM angekua hai, kuna mmiliki wa ma bus angeivimbia serikali namna hiii??.

Alafu hapo kuna dola, dola hiii hiii tunayosema kila siku iko mafunzoni kuhakikisha jicho lake linamulika kwa masilahi mapana ya taifa. Nadhani moja ya sehemu inayoitaji kufumuliwa ni mfumo mzima wa dola, umejaa wapigania matumbo tu .

Enyi wavivu, wazembe, wala rushwa na mafisadi wakubwa, jina la John pombe Magufuli, hili halitakaa kufutika mioyoni wa taifa hili, historia itayasahau majina yenu pale tu mtakapokufa, lakini haitokaa kumsahau JPM.
Kwahiyo kwa akili yako kama gari linaanzia safari zake Mbagala na kuishia Mbagala unataka basi hilo likiingia Mbezi stendi lishushe abiria wote hata kama basi linaenda Mbagala liende tupu liwaache abiria Mbezi kisa tu watu fulani wauze biashara zao?

Kumbuka Mbezi ni stendi kuu tu ambapo kila basi litapita hapo kushusha ama kupakia abiria kisha litaendelea na safari yake linapoishia.

Siku hizi biashara ni akili mabasi yameanza kuwafuata abiria huko huko kwenye makazi yao mfano yapo yanayoanzia safari Chanika, Kigamboni, Mbagala, Shekilango na maeneo mbalimbali.
 
Binafsi nashauri hi!! Bus lazima ipite stendi husika, then inaweza kuendelea na ruti za ofsini kwake. Kutokupita kabisa si suala la kushabikia, huko ni kutumia pesa za watanzania ovyo. Na vitu kama stendi vinawapa ajira watanzania wengi sasa mkigeuza kuwa magofu wale walioko pale wakaibe??
Hakuna basi isiyoingua stand zote zinaingia stand ila hao wafanyabiashara wanachotaka ni kwamba hata kama inaelekea abiria wanakuoelekea iwaache hapo stand. Mimi naunga mkono basi kuanzia inakoanzia na abiria kama wapo na kuingia na kutoka na abiria ambao wanaelekea linapoelekea.
Kama ambavyo wao wanalalamika hara abiria basi kumwacha hapo wakati ana mizigo na linaelekea anakoelekea abiria naye anapata shida.
 
Mbona ndege huwa hamuombi mshushwe kwenu mnakubali kwenda airport? Utaratibu wa vituo ni muhimu sana, mkifanya shaghala baghala msilalamikie mfumo na utaratibu wa serikali.

Sasa Stand ya bus ya nini kama unaweza panda na kushuka popote?
Ww tumia akili ona aibu basi ndege aitport unafanisha na stend hata majina tu yanapishana ile inaitwa airport ...Hata pale airport kuna hotel zimejiongeza kutoa usumbufu kwa wateja wao wanao fika hapo wanamagari kabisa yanasubiri abiria.Siwezi kushuka magufuri wakati najua nikishuka shekilango hata bei ya bajaji kunipeleka ferry ni chini pia sitasbuka kubeba mizigo kutafuta sijui mwendo kasi..
 
Nadhani ni marketing strategy wa wenye mabasi.
Sasa wenye Mabasi hawatakiwi waachwe huru kiasi hiko....
Lazima wafuate utaratibu,,,
Mana sasa hayo Mabasi hadi Chanika na Vijibweni nisha yaona.....

Hatakama tupo Soko huru lakini lazima vitu vifanyke kwa utaratibu...
 
Abiria wanaingia hiyo Stendi wakiwa wameshiba ama wamechoka, unataka wanunue nini saa 10 alfajiri? wakinunua mavyakula hovyo watachimba dawa njia nzima

Wakifika jioni wamechoka na kwao ni hapo kimara tu sasa wananunua nini hapo stendi ambacho nyumbani kwao hakipo? Wauzaji wenyewe afya zao ni mashaka matupu, unanunua ili ukaharishe?
Mbona wakati ipo Ubungo shughuli zote zilikuwa zikifanyika pale? Tulikuwa tukila na kununua bidhaa kabla ya safari
 
Wanashauri ujinga fikiria mtu anaishi Boko au Mwenge basi Lina Toka Arusha au Moshi au Tanga linalopita Njia hiyo Kwa hiyo linapita hapo Boko na hapo Mwenge linakwenda na abiria Hadi stendi ya Magufuli linawashusha kule waanze kutafuta usafiri wa kurudi Mwenge na Boko basi linarudi tupu hata kama linapaki Mwenge au boko si.biashara kichaa hiyo

Au mtu anaishi mbagala anatoka Lindi na Mtwara basi linafika mbagala linapitiliza mbagala na huyo abiria Hadi stendi ya magufuli linamshusha atafute usafiri wa kurudi mbagala basi linarudi mbagala tupu hata kama linapaki mbagala huo ni wendawazimu

Hakuna abiria atakubali Hilo
Hapo unakosea, nadhani mabasi yanaweza kushusha huko kote kakini safari ikianza lazima gari iingie stendi na ikiisha inapita stendi kabla ya kuelekea huko kwingine.
Nadhani hilo ndio la muhimu.
 
Utaratibu ni ustaarabu, wafuate utaratibu ma bus yote yapakie na kushusha abiria ndani ya stand ya ma bus na siyo vinginevyo. Kila siku tunalalamikia teuzi za rais, ni kwa sababu ya upuuzi kama huu.

Mkuu wa mkoa yupo, Mkuu wa wilaya yupo, Mkurugenzi yupo, afisa biashara wa mkoa na wilaya wapo, wachumi wa mkoa na wilaya wapo, Askari polisi na askari wa usalama barabarani wapo, kwanini bus lipakie abiria nje au kushusha abiria nje ya stand iliyojengwa kwa madhumuni hayo?

Wahusika wasimamie au watumbuliwe waje wengine wenye nia na kazi hizo.

Hapo nyuma tulilalamikia ndege binafsi kutua kila mahali biula taarifa wala ukaguzi, viwanja vya ndege vimepanuliwa na mamlaka husika walisimamia hili, bandari bubu zilizokuwa zikiingiza vitu vya magendo kama sukari na bidhaa zingine, tulilalamika mamlaka zikashughulikia, sasa kwanini hawa wa mamlaka za usafirishaji wasishughulikie hili la buses na abiria?

Tusipende vitu vya shaghalabaghala, tujenge tabia za kufuata taratibu sisi wenyewe, tunaposhindwa mamlaka husika zisimamie turudi kwenye mstari ndiyo majukumu yao. Na kama waliopewa dhamana hizo wameshindwa na watumbuliwe tu.

Na kama hii ndiyo sababu ya kutumbua watu basi atumbue asubui na jioni na ikiwezekana kila siku mpaka tupate watendaji wanaoelewa majukumu yao.

Nchi zilizoendelea zinatushinda kwasababu wao raia wao kwanza wanapenda utaratibu, na mamlaka zao zina enforce sheria zilizowekwa. Kama ni kutupa uchafu kwenye ndoo wote watatupa uchafu kwenye ndoo, na atakayefanya tofauti anachukuliwa hatua, hapa kwetu watu wanatetea ujinga.

Stand imejengwa kwa madhumuni gani, ikiwa kila mtu atafanya anavyopenda? Miafrika tuone aibu, hivi ni vitu vidogo tujielekeze wenyewe, tusisubiri kusukumwa.

Vijana wanakimbilia south Afrika na Ulaya, au Amerika kupata fursa, sasa bila utaratibu huku nani angeenda?

Nasi tujifunze matumizi mazuri ya akili na vitu , Stand ya bus, ma bus yote yangie stand, na abiria wote washukie stand na kupanda ma bus stand, kama ilivyo kwa ndege, habiria hupanda na kushukia airport na buses iwe hivyo.



Tuache hizi tabia tuendelee.
Kwamba mimi ni mkazi wa Bunju halafu basi linatoka Arusha linapita njia ya Bagamoyo kwahiyo nisishuke Bunju bali nije hadi Magufuli stendi ndiyo nishuke halafu nianze kupambania usafiri wa kurudi Bunju ambapo nilipapita?

Hizi akili ni za kipumbavu kupita kiasi. Yaani mtu asishushwe kituo chake bali aletwe hadi Magufuli stendi kisa tu kuwanufaisha wafanyabiashara?
 
1. Kwani mtu anayeshuka uwanja wa ndege na anakaa Kunduchi huwa anafikaje nyumbani...?

2.Kwanini gari ziende Shekilango au Mnazi mmoja .....?
Kitu ambacho huelewi ni kwamba abiria wanaooelekwa urafiki au shekilango ni kama offer ya mwenye basi na sio sheria. Ni mwenye basi kumjali mteja wake na kumpunguzia gharama zisizo za lazima.
 
Back
Top Bottom