Wafanyabiashara wa mikoani mnaochukua vitu Kariakoo, njooni tujuzane machimbo ya bidhaa

Huo ndio ujanja na dawa ya mjanja kama dalali anataka mkubaliane kabisa na usiende kumuona mwenye kwianja utamuona mkishakubaliana naye ahaha.
 
Nimefanikiwa kwa asilimia zote, nmesoma between lines. Naingia chimbo namimi nifanye kwa manufaa yangu.
Wachangiaji wote Mungu awabariki sana. Haya maarifa huwa tunayatafuta lakini tunakosa pa kuyapatia. Ubarikiwe pia wewe uliyeanzisha thread hii!!
 
Tanzania nchi ya ajabu sana, miwani za tiba wanauza waha kwa jumla ambapo hata shule hawakwenda. Wakati wenye profession wamelala kwenye ajira, unakuta jamaa anakupa mzigo hata kuandika jina kwenye risiti anambwela. Bongo wasomi wakishtuka biashara itanoga.
 
Nimefanikiwa kwa asilimia zote, nmesoma between lines. Naingia chimbo namimi nifanye kwa manufaa yangu.
Wachangiaji wote Mungu awabariki sana. Haya maarifa huwa tunayatafuta lakini tunakosa pa kuyapatia. Ubarikiwe pia wewe uliyeanzisha thread hii!!
Usisahau kutupatia mrejesho mkuu
Kila la kheri
 
Mkuuu samahani, unaweza nisaidia wanakojumua viatu vya mtumba vya akina dada kwa pande za kariakoo..
Samahani kwa usumbufu lakini
 
Uzi madini sana huu.

Jamani nami naombeni mawazo yenu wandugu...

Nimepata mkopo wa Tsh Milioni MOJA kamili. Ni mkopo usio na riba. Nimepewa MIEZI MITATU niwe nimerejesha yote.

Nipeni ushauri ndugu zangu. Nifanye biz gani ya kukimbiza chap chap? any ideas please. Kwa sasa nipo Dar, ila ni kijana ambaye nipo tayari kuingia kokote penye fursa ya biashara kwa mtaji huo. Nipeni mawazo wapendwa, maisha yamenichapa mno ndugu zangu, sasa naukataa umasikini kwa nguvu zote!

CC: charty , Danhappy , na wachangiaji wengine wote. Natanguliza shukrani
 
Ndo nimesha subscribe kininja......following
 


Mkuu Dimma, hongera kwa kupata mkopo usio na riba. Maana daah you are lucky, wengine akina sie tunatamani sana kupata mtaji (hata nusu ya hiyo) ili tukimbize mishe town, but hatukopesheki.

Kuhusu bizina ideas za kufanya kwa mtaji huo, hebu jaribu kusearch humu JF, kuna a lot of threads with several bizna ideas. Naamini utapata cha kufanya. Huo mtaji unatosha kabisa for a start up... bidii, nidhamu, na honesty... ndo mambo ya msingi.

-Kaveli-
 
Naishi nairob vitu vinafanana saingine ila pochi huku hamna wala vitenge best hadi dar

Sent from my Fire2 3G using JamiiForums mobile app

Binafsi nilishaacha kwenda dar na mzigo naagiza hapo hapo mix narudia fanya utafiti


Nakubaliana na Danhappy. Nadhani kweli Nai wana uhaba wa vitege/Khanga, and the like.

I have a lady friend in Nai. Mara kwa Mara huwa ananiagiza kumnunulia Vitenge na kumtumia kwa Bus... na ni aina moja tu: 'Makenzie' ya kitenge.

So it seems kweli Kenya either wana uhaba wa vitenge/khanga or zilizopo hazina quality kama za Tz.

-Kaveli-
 
Hazina ubora mkuu ukitaka kula hela leta vitenge huku vinaenda...
 
Hazina ubora mkuu ukitaka kula hela leta vitenge huku vinaenda...


Kumbee, now I know. Thanks mkuu kwa kunipa hiyo tip. I will explore further with her on this.

Hivi Makenzie ndo yana soko zaidi huko eeh? maana huwa ananiagiza aina hiyo tu.

Na mpakani siku hizi wanasumbua sana? Mie huwa namtumia kwa Dar Express na mzigo unafika poa tu.

-Kaveli-
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…