Chinga One
JF-Expert Member
- May 7, 2013
- 11,469
- 12,391
hivi wenzako wote wangeenda PM we ungejua chochote kuhusu huu uzi?Huyu mtu bado yupo kweli? Maana namchek pm inashindikana,, nataka madini zaidi ya machimbo kkooo
Sent using Jamii Forums mobile app
Nmetafuta sijaona
Karibu na ule msikiti wa wasuni sijui waleZinapatikana wapi Madame B? Nimetoka bilabila
Kituo cha msimbazi pale yanapopaki magari ya mabibo ndio chimbo la sabuni,mafuta ya aina zote,pafyumu na makolokolo kibao ya urembo yanapatikana mitaa ileChimbo la sabuni zile za kunukia (za kuogea) hapo k/koo,msaada jamani nimeona fursa huku chalinze
Kuanzia 100kMidoli ya kuuzia nguo ile ya plastic inapatikana kwa bei gan?
Midoli ya kuuzia nguo ile ya plastic inapatikana kwa bei gan?
Contact na hao watuKuanzia 100k
Mambo Charty,hahhahah sasa wewe mie mkali wa hizi kazi tokea nipo chuo kitamboo nimeivuruga sana hiyo k.koo hahah hadi leo nipo yaani na sibanduki ng'ooo inabidi tuwasaidie wenzetu bana maana haya maisha mtu akikuongezea jero kwenye product ni kubwa sanaaaa.Na hivi vyuma vimekaza acha tu na wenyewe wale.Ila si unajua mjini wasioujua bado wengi utawapata tu maana hawapo humu JF .
Ngoja niwape chimbo la pochi za bei rahisi zile ronya na za kati 6000,8000,12000 lipo maeneo ya nyamwezi karibu na soko la shimoni kale kamtaa cha kati uje utokee msimbazi kota,karibu wanapouza maturubali, lingine lipo mtaa wa congo na aggrey kwa juu ghorofani kama unataka kutoka congo kituo cha basi pale wanauza high quality PU zao 22k,25k,28k,30 nk ambazo ukikuta kwenye botique ni mwendo wa 50k,70k hadi 100k. Pia tena hiyohiyo congo/mchikichi pale katikati kwa ghorofani wanauza pochi eh bei chee tatizo lenu mnapita juu juu tu ingieni maduka ya ndani na chini yana mambo mazuri Wallet nazo mchikichi zipo za kumwaga za kiume na za kike bei chee hakikisha unaingia ndani kabisa kwenye vichochoro. Haya kwa wale wa mabegi ya kusafiria kuna mchina anazalisha mwenyewe maeneo ya Veta karibu na sofia house kule anakutengeneezea design unayotaka eh,pesa yako tu. Kuna kingine nimesahau? Danhappy
sawa vingine ukitaka unasema tu nakuelekeza! ninavyovijua pia nitakua nakuongezea machimbo mapya maana supplier wengine wanafilisikaga hahaaahaa
Yeees nimeshalipata mkuu dah utajiri si huu jamani!!!πππKituo cha msimbazi pale yanapopaki magari ya mabibo ndio chimbo la sabuni,mafuta ya aina zote,pafyumu na makolokolo kibao ya urembo yanapatikana mitaa ile
2017 huyu mchina atakuwepo bado Kiukweli nilipatafuta sikupaona kabisaNgoja nikupe machimbo eh best kizuri kula na mwenzio...Vitenge mara nyingi machimbo yake yapo NIDA kule mnazi mmoja wengi wanaouza k.koo wanaenda kufata huko, Viatu navyo vinapatikana huu mtaa wa Narung'ombe na congo pale nenda straight kwenye maduka ya wachina yaani sio wale machinga wanaomwaga chini nop unazama dukani utakuta zile simple wanauza 4000/pc na vile visandles wanauza 2500/pc. Cheni zama mchikichi katikati kuna mchina anauza mpaka 2000-3000/dz na hazipauki.Magauni nayo ingia ndanindani kule congo na aggrey wanauza nayo bei chee 6000-8000-1000-16000/pc. Vingine siku ingine nitakwambia nimechoka kutype ah.
Mkuu nielekeze na MimiYeees nimeshalipata mkuu dah utajiri si huu jamani!!!πππ
Naomba namba na Mimi nipajueMi kuna machinga nilikuwa nachukua mzigo kwake,hivyo nampa pesa ye anazunguka kwenda kuchukua mzigo.Ukimuuliza asemi,siku nilienda na vijana wangu watatu ambapo yeye hakuwaona.Hivyo nilivyomkabidhi pesa akaondoka,vijana wangu wakamfuatilia mpaka wakajua maduka yote aliyoingia.Tangia siku hiyo hajaniona na majamaa wa madukani washanizoea hats bila pesa wananipa mzigo au wanatuma mkoani.
2017 huyu mchina atakuwepo bado Kiukweli nilipatafuta sikupaona kabisa
Nataka wanapouza cheni na urembo wa kike please nisaidieWapo sana tena wamekua wengi cha msingi,uwe unadamka mapema ikiwezekana kabsa saa 1 asubuhi ikukute mtaa wa Narung'ombe na Congo.Wafanyabiashara wenzako wanapokua wanakusanya oda ya kuchangia box nawe uwepo ili upate kwa bei nafuu.Inakua kama mnada fulani hivi sample zinazungushwa.Ila angalia usitapeliwa usitoe pesa ako hadi uone mzigo sawa.
Huu uzi umesonga sana kitambo sana sijapita humu.Kila la kheri.
Ukifika pale msimbazi kituo cha polisi si kuna kituo cha mwendokasi,ukiwa kama unaelekea fire mwisho wa kile kituo cha mwendokasi kuna barabara inaelekea kushoto kwenye maduka ya jumla ya rasta, nenda na hiyo barabara ikiwezekana ulizia kwa watu yalipo maduka ya rasta,ukifika kwenye hayo maduka ya rasta...maeneo hayohayo we ulizia duka la vipodozi kwa bei ya jumla,watu watakuelekeza maana ni chimbo haswaaa huwezi kupajua kirahisiMkuu nielekeze na Mimi