Wafanyabiashara wa mikoani mnaochukua vitu Kariakoo, njooni tujuzane machimbo ya bidhaa

Wafanyabiashara wa mikoani mnaochukua vitu Kariakoo, njooni tujuzane machimbo ya bidhaa

Samahani waheshimiwa, kwa wazoefuvwa biashara ya nguo za kuchukulia kariakoo ni nguo zipi ziwaweza zikawa na fata faida kubwa kati ya mtumba au za dukani.
 
Ngoja nikupe machimbo best. Kizuri kula na mwenzio. Vitenge mara nyingi machimbo yake yapo NIDA kule Mnazi Mmoja wengi wanaouza Kariakoo wanaenda kufuata huko. Viatu navyo vinapatikana huu Mtaa wa Narung'ombe na Congo pale nenda straight kwenye maduka ya Wachina yaani sio wale machinga wanaomwaga chini, nop. Unazama dukani utakuta zile simple wanauza 4000/pc na vile vi-sandles wanauza 2500/pc. Cheni zama Mchikichi katikati kuna Mchina anauza mpaka 2000-3000/dz na hazipauki. Magauni nayo ingia ndanindani kule Congo na Aggrey, wanauza nayo bei chee 6000-8000-1000-16000/pc. Vingine siku ingine nitakwambia nimechoka ku-type ah! .
MMkuu una utu sana ,nmependa uungwana wako aiseee
 
Jamani anayefahamu chimbo LA mapazia Yale wanayouza kwa jola snipe mwongozo please. Kuna mahali yanahitajika.
 
Jamani anayefahamu chimbo LA mapazia Yale wanayouza kwa jola snipe mwongozo please. Kuna mahali yanahitajika.
Kama unaenda Posta upande wa chuo cha DIT na CBE, Ukishavuka ule ukuta kuna duka la mfanyabiashara ana asili ya india anauza bei nzuri na mara nyingi Jumamos anakua na bei ya SALE kwahyo unaweza kupata majora ya mapazia kwa bei chee na kila design.
 
Wakuu msaada wapi kariakoo wanauza hizi bidhaa kwa jumla na bei nafuu, na material nyingine zinazohusiana na mihuri/stamps?

828D.jpg

images.jpg
 
Naombeni kuelekezwa machimbo/mtaa wa nguo kali za watoto wa kiume na viatu ya bei nafuu reja reja
 
Naombeni msaada wanapouza yake mabazee kama yaki nigeria au alovaa DIAMOND kwenye nyimbo yake ile 2amevaa costume kama za KIFALME na kama mtu anafahamu bei yake.Ahsanteh
 
Abar zenu jamani, m nipo pemba Zanzibar naomba kujua Maduka ya jumla ya nguo za wanawake, like pencil skate, vikoti, nai nai and other pls
 
Naomba kujua maduka ya taa za urembo na lampshades . bei za jumla.
 
Back
Top Bottom