Wafanyabiashara wa mikoani mnaochukua vitu Kariakoo, njooni tujuzane machimbo ya bidhaa

Wafanyabiashara wa mikoani mnaochukua vitu Kariakoo, njooni tujuzane machimbo ya bidhaa

Msaada wa dharura tafadhali natafuta chimbo au mtu anayejua mahali naweza pata spea za pikipiki aina zote kwa bei ya wholesale tafadhali
 
[emoji95]CHULight LED bulbs 5W
[emoji1666][emoji1666]TUNAUZA JUMLA:- Tsh.1,300/pc
[emoji597][emoji597]:- TUNATUMA HADI MIKOANI
BOOKING:- 0674 745 463
Screenshot_20231006-122315_1696586334316.jpg
 
Nahitaji viatu vya mtumba kwa bei ya jumla bei iwe 3,000/= mpaka 5,000/= kwa anayejua chimbo kwa Dar nichek whatsap 0744967478
 
Naona uzi umepoa. Ngoja nishushe vitu.
.
Unataka Kufanya Biashara ya Vyombo vya plastiki kama viti, meza, vikombe, majagi, mabeseni nk. maduka ya viwanda yapo kariakoo mtaa wa Livingstone na Aggrey mpaka mchikichi na mahiwa close huko utapata kwa bei nzuri na ukiuza utapata faida nzuri.
...
Vyombo vingine utavipata mtaa wa Aggrey na livingstone
.
Maua bandia utayapata mtaa wa Aggrey na sikukuu. Hapo kuna mchina yuko opposite na Bank ya NCBA.
.
Nguo za wanawake kama T_shirt skins, Bwanga, tops, gauni utapata mtaa wa Raha na Muhonda zaidi ingawa maduka ya nguo za wanawake yameganyika mitaa mbalimbali sana.
.
Vijora, Mitandio, Abaya na baibui utavipata mtaa wa nyamwezi na Narung'ombe jengo la Barcelona floor ya pili.
.
Nguo za wanaume kama suit, jeans, Track, shati, T_shirt, kadeti nk utavipata jengo la Mchikichi complex.
.
Shati quality za kiume chimbo ni kwa @welldone_turkish_fashions congo na narung'ombe
.
Pochi kariakoo makutano ya likoma na muhonda
.
Vifungashio kama makopo, chupa, mifuko, mabox ya bidhaa aina zote utapata mtaa wa Tandamti na sikukuu
.
Mnaulizia sana mtumba Grade A kuna marafiki zangu wanaleta mtumba mzuri ambao huwezi kujutia wako ilala Boma
.
Wale wa mtaji mdogo nenda ilala boma saa 11 asubuhi utapata mtumba ata nguo za 1000 ukauze minadani
.
Viatu vya kike vipo mtaa wa congo na narung'ombe, ukienda saa 11 asubuhi utajua machimbo ya wachina maana wengi wanashusha kutoka stoo asubuhi.
.
Viatu Vya kiume vipo Nyamwezi na Narung'ombe. Lakini ukihitaji viatu vya Mtumba hivyo utavipata mtaa wa Karume, nenda pia asubuhi saa 11.
.
Unahitaji Nywele, unahitaji rasta nenda mtaa wa jangwani na mafia. Huko kuna maduka mengi na mawakala wa viwanda vya rasta. Ni ule mtaa zinapopaki Daladala za makumbusho gerezani.
.
Kwa upande wa Vipodozi aina zote pia nenda huu mtaa wa Mafia na Jangwani hapo kuna duka maarufu la @kariakoovipodozi utapata vipodozi.
.
Lakini tusikalili kuna Machimbo mengine hayapo kariakoo ila wanashusha mizigo kwa bei ya chini na kuweka stoo.
.
Turudi kariakoo, mtaa huu wa mchikichi na nyamwezi kuna duka kubwa la vifaa na nguo za watoto wachanga, yaani nguo, mabeseni, matoroli, babyshioo, pot aina zote nk. Hilo jimbo kama una duka la watoto na wajawazito utanishukuru.
.
Mashuka ya uganda nenda kwa mchina opposite na Bank ya Crdb
.
Nguo za ndani Nenda makutano ya mtaa wa mchikichi na sikukuu. Hapo kuna duka kubwa mno utapata nguo za ndani jumla kwa aina zote.
.
Kuna Chimbo Waturuki wana vyombo imara vizuri vya kituruki pia wanakopesha kwa wenye maduka. Ni vizuri hata kwa matumizi binafsi
Chimbo gani lingine unaongeza lipi unatafuta? Endelea kwenye comments
.
Unataka number zao? Sijui kama hapa inaruhusiwa ila instagram kwenye page yangu ya @kelvinkibenje utapata machimbo yote na Number zao na updates.
 

Attachments

  • Screenshot_20231012-005812.jpg
    Screenshot_20231012-005812.jpg
    240.5 KB · Views: 56
Wakuu naombeni machimbo ya belo za nguo za watoto na yebo za mtumba zenye muundo wa sendo
 
Hakuna chimbo zuri kama alibaba...utatengeneza faida mara 2 na kuendelea kwa bidhaa unazonunua Kariakoo...ukiona unanunua bidhaa kariakoo elfu 5 ujue china ni 1,500 kusafirisha na kodi etc elfu 1 jumla 2,500..kwahiyo hapo umeokoa 2,500 ambayo ulitakiwa uitoe kariakoo.
 
Hakuna chimbo zuri kama alibaba...utatengeneza faida mara 2 na kuendelea kwa bidhaa unazonunua Kariakoo...ukiona unanunua bidhaa kariakoo elfu 5 ujue china ni 1,500 kusafirisha na kodi etc elfu 1 jumla 2,500..kwahiyo hapo umeokoa 2,500 ambayo ulitakiwa uitoe kariakoo.
Sio mitumba, mitumba mingi inatoka Nchi za ulaya ulaya, Dubai na kwengineko.
 
Wakuu naombeni machimbo ya belo za nguo za watoto na yebo za mtumba zenye muundo wa sendo
Sina uhakika Exactly ila mitumba mingi nguo nguo inakua baina ya Lumumba na Livingstone, mfano Narung'ombe na Livingstone mpaka Narung'ombe na Lumumba Kuna maduka mengi yanauza mabelo, na mtaa unafuata mahiwa,

Pia Mafia na Livingstone kama unaenda Mafia na sikukuu ipo mitumba ya mabelo.

Ukifika maeneno hayo hata kama utakosa watakuelekeza wenzao.
 
Hakuna chimbo zuri kama alibaba...utatengeneza faida mara 2 na kuendelea kwa bidhaa unazonunua Kariakoo...ukiona unanunua bidhaa kariakoo elfu 5 ujue china ni 1,500 kusafirisha na kodi etc elfu 1 jumla 2,500..kwahiyo hapo umeokoa 2,500 ambayo ulitakiwa uitoe kariakoo.
Mkuu sasa china si mpaka uwe na mtaji mkubwa ?
 
Mkuu sasa china si mpaka uwe na mtaji mkubwa ?
Namaanisha kununua kwenye mtandao wa Alibaba na SIO KWENDA CHINA physically.. Alibaba haiitaji mkubwa unaweza kupata supplier akakufungia mzigo hata wa laki moja au hata chini ya hapo inategemeana na bidhaa.Cha msingi ujifunze namna ya kuutumia Kwa kusearch bidhaa, kuwasiliana na supplier, kulipia na kusafirisha..
 
Ni wapi kariakoo naweza pata chupa hizi na bei yake kwa jumla
 

Attachments

  • Screenshot_20231107_140407_Gallery.jpg
    Screenshot_20231107_140407_Gallery.jpg
    74.5 KB · Views: 51
Back
Top Bottom