Wafanyakazi wanne wa taasisi ya mikopo ya OYA wafikishwa Mahakamani kwa tuhuma za mauaji ya kukusudia

Wafanyakazi wanne wa taasisi ya mikopo ya OYA wafikishwa Mahakamani kwa tuhuma za mauaji ya kukusudia

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
Snapinsta.app_463405039_1088676905948653_6371951213833624637_n_1080.jpg
Wafanyakazi wanne wa taasisi ya mikopo ya OYA wamefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Kibaha kwa tuhuma za mauaji ya kukusudia ya Juma Said Seif (45), mkaazi wa Kitongoji cha Mbagala Mlandizi Mkoani Pwani yaliyofanyika Oktoba 7. 2024.

Wakili wa Serikali, Monica Mwela amewataja watuhumiwa hao kuwa ni Dastan John Charles (23), Christopher John Charles (23), Emmanuel Joshua Olala(24) ambao ni wakazi wa Kilangalanga Mlandizi pamoja na Abdallah Felix Wendiliwe (32) mkaazi wa Janga Mlandizi.

Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Kibaha, Emmaeli Lukumai amesema ushahidi wa kesi hiyo iliyosomwa kwa mara ya kwanza bado haujakamilika, hivyo kesi hiyo imehairishwa hadi Oktoba 30 mkwaka huu.

Wakati wakisomewa kesi hiyo, watuhumiwa hawakutakiwa kujibu lolote kwa sababu mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza kesi ya mauaji. Watuhumiwa wote wamerudishwa rumande.

Chanzo: AZAM TV

Pia soma ~ Kampuni ya OYA watoa milioni 1 kwa familia Juma Mfaume ambaye alifariki baada ya kupigwa na wafanyakazi wa kampuni hiyo
 
Wafanyakazi wanne wa taasisi ya mikopo ya OYA wamefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Kibaha kwa tuhuma za mauaji ya kukusudia ya Juma Said Seif (45), mkaazi wa Kitongoji cha Mbagala Mlandizi Mkoani Pwani yaliyofanyika Oktoba 7. 2024...
Ona sasa vijana kabisa, safari yao ya uraiani inaishia hapa. Sababu ya misconduct na kutumia too much force
 
Unapoagizwa kufanya jambo hata kama umeambiwa utumie nguvu,tanguliza busara zaidi.Utaharibu maisha yako kwa mambo ya kumtetea tajiri.
Yawezekana mdaiwa alitumia nguvu nyingi sana ikapelekea na wao kutumia nguvu zaidi Ili kumdhibiti vinginevyo pengine angewauwa wao ni bora afe mmoja kuliko wangekufa watu wanne
 
Yawezekana mdaiwa alitumia nguvu nyingi sana ikapelekea na wao kutumia nguvu zaidi Ili kumdhibiti vinginevyo pengine angewauwa wao ni bora afe mmoja kuliko wangekufa watu wanne
Mdaiwa anatumiaje nguvu? Kwamba alikua anakataa kwa maneno kutolipa kwa kutumia nguvu kubwa ama sijakuelewa na wanaodai na wao walikuja kudai ama kuua kwamba walidai kwa kutumia nguvu kubwa ya kuua?
 
Yawezekana mdaiwa alitumia nguvu nyingi sana ikapelekea na wao kutumia nguvu zaidi Ili kumdhibiti vinginevyo pengine angewauwa wao ni bora afe mmoja kuliko wangekufa watu wanne
Naamini ulichokiandika ni jambo umedhani/hisi tu.Bado kuna mambo hao vijana walipaswa kuenenda kwa akili.Naamini tena kwamba hawakuenda na lile gongo(rungu?)walilompigia.

Sasa,hadi wakaokota gongo kumtwanga mvutano ulikuwa wa muda gani?Mdaiwa alifanya fujo au alihatarisha nini kwao?Vijana wanne walishindwa kumdhibiti mdaiwa bila kuleta madhara?

Walienda na uongozi wowote kama wenyeji wao?Sheria inawaambiaje kwa wateja wakorofi/ wasumbufu?

Anyway, hatukuwepo ngoja tuone.
 
Back
Top Bottom