Wafanyakazi wanne wa taasisi ya mikopo ya OYA wafikishwa Mahakamani kwa tuhuma za mauaji ya kukusudia

Wafanyakazi wanne wa taasisi ya mikopo ya OYA wafikishwa Mahakamani kwa tuhuma za mauaji ya kukusudia

Yawezekana mdaiwa alitumia nguvu nyingi sana ikapelekea na wao kutumia nguvu zaidi Ili kumdhibiti vinginevyo pengine angewauwa wao ni bora afe mmoja kuliko wangekufa watu wanne
Hawakutakiwa kutumia nguvu hata kidogo ni kinyume na sheria kwa taasisi ya fedha hii imekula kwao
 
Kumpeleka hospitali inaonesha hawakukusudia kuua. Wakipata mwanasheria mzuri anaweza kuwasaidia kubadili kesi, ila kifungo hakiepukiki.
 
Wakili wa Serikali, Monica Mwela amewataja watuhumiwa hao kuwa ni Dastan John Charles (23), Christopher John Charles (23), Emmanuel Joshua Olala(24) ambao ni wakazi wa Kilangalanga Mlandizi pamoja na Abdallah Felix Wendiliwe (32) mkaazi wa Janga Mlandizi.
Naona wote under 40, umri wa mihemuko kuliko busara. Mungu awavushe salama.
 
Kama ni hivyo,wote tungekufa au kupata dhahma mbaya kwenye umri mdogo.Ili twende sawa,tutumie neno AKILI isikuletee ukakasi kwenye tafsiri.
Siko hapa kukwepa ukakasi nipo hapa kusema ukweli,binadamu akifika miaka arobaini ndio anakuwa amekomaa,ndio maana wanasema maisha yanaanza kwenye miaka 40

Hata mitume wengi walipewa utume walipofikia miaka 40

Hata katiba ya tanzania raisi afikie miaka 40

Chini ya hapo ni kuokoteza tu
 
Siko hapa kukwepa ukakasi nipo hapa kusema ukweli,binadamu akifika miaka arobaini ndio anakuwa amekomaa,ndio maana wanasema maisha yanaanza kwenye miaka 40

Hata mitume wengi walipewa utume walipofikia miaka 40

Hata katiba ya tanzania raisi afikie miaka 40

Chini ya hapo ni kuokoteza tu
Ingekuwa hivyo hata kuoa/kuolewa ingekuwa ni hadi watu wafike miaka 40.Kuna mambo hayahitaji ubishi au kuonesha ukakamavu.Akili itangulie kwanza.Think before you do anything.
 
Na
Wafanyakazi wanne wa taasisi ya mikopo ya OYA wamefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Kibaha kwa tuhuma za mauaji ya kukusudia ya Juma Said Seif (45), mkaazi wa Kitongoji cha Mbagala Mlandizi Mkoani Pwani yaliyofanyika Oktoba 7. 2024.

Wakili wa Serikali, Monica Mwela amewataja watuhumiwa hao kuwa ni Dastan John Charles (23), Christopher John Charles (23), Emmanuel Joshua Olala(24) ambao ni wakazi wa Kilangalanga Mlandizi pamoja na Abdallah Felix Wendiliwe (32) mkaazi wa Janga Mlandizi.

Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Kibaha, Emmaeli Lukumai amesema ushahidi wa kesi hiyo iliyosomwa kwa mara ya kwanza bado haujakamilika, hivyo kesi hiyo imehairishwa hadi Oktoba 30 mkwaka huu.

Wakati wakisomewa kesi hiyo, watuhumiwa hawakutakiwa kujibu lolote kwa sababu mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza kesi ya mauaji. Watuhumiwa wote wamerudishwa rumande.

Chanzo: AZAM TV

Pia soma ~ Kampuni ya OYA watoa milioni 1 kwa familia Juma Mfaume ambaye alifariki baada ya kupigwa na wafanyakazi wa kampuni hiyo
Naendesha na kumiliki kampuni ya ukusanyaji wa madeni, huwa nahamasisha Sana collection instead of recovery haswa yenye utumiaji wa nguvu na pia inanisaidi kuondoa a na kesi za madai za kila leo, kwangu na kwa wateja wangu na bado inaacha mazingira ya urafiki na sio uadui
 
Ningekuwa hakimu ningewapata na kosa la involuntary manslaughter sio murder na kisha kuwapunguzia adhabu kwa sababu hawakukusudia na walimkimbiza hospital.
Sema maisha haya, hapo hakuna hata mmoja ambaye aliwahi fikiria ipo siku atashtakiwa kwa kuua aisee.
Walianza kuongea.Wakaja kufokeana.Wakaenda mbele kutukanana na kutishiana.Hawakuishia hapo,wakatafuta gongo.Wakampiga(sijajua ni mara ngapi).Baada ya kuona wamejeruhi na wametambulika ni wafanyakazi wa OYA na hawana ujanja tena wa kuhepa dhahma ndiyo wakamkimbiza hospitali.Sidhani kama huruma ndiyo iliwaongoza.Na,haijulikani kama mdaiwa alifia palepale,njiani au hospitali!
 
Ingekuwa hivyo hata kuoa/kuolewa ingekuwa ni hadi watu wafike miaka 40.Kuna mambo hayahitaji ubishi au kuonesha ukakamavu.Akili itangulie kwanza.Think before you do anything.
Akili ni kwa ajili ya kufikiri tu,kwahiyo ndio maana tunaoa kwasababu sisi sio wanyama,tunajua hatuwezi kuparamiana siku zote au katika maisha yetu yote

busara ni kuliweka kila jambo mahala pake hiyo ndio maana ndogo ya busara

sasa ni wachache sana wanaliweza hilo lkn at 40's unakuwa na nyenzo hiyo
 
Wafanyakazi wanne wa taasisi ya mikopo ya OYA wamefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Kibaha kwa tuhuma za mauaji ya kukusudia ya Juma Said Seif (45), mkaazi wa Kitongoji cha Mbagala Mlandizi Mkoani Pwani yaliyofanyika Oktoba 7. 2024.

Wakili wa Serikali, Monica Mwela amewataja watuhumiwa hao kuwa ni Dastan John Charles (23), Christopher John Charles (23), Emmanuel Joshua Olala(24) ambao ni wakazi wa Kilangalanga Mlandizi pamoja na Abdallah Felix Wendiliwe (32) mkaazi wa Janga Mlandizi.

Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Kibaha, Emmaeli Lukumai amesema ushahidi wa kesi hiyo iliyosomwa kwa mara ya kwanza bado haujakamilika, hivyo kesi hiyo imehairishwa hadi Oktoba 30 mkwaka huu.

Wakati wakisomewa kesi hiyo, watuhumiwa hawakutakiwa kujibu lolote kwa sababu mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza kesi ya mauaji. Watuhumiwa wote wamerudishwa rumande.

Chanzo: AZAM TV

Pia soma ~ Kampuni ya OYA watoa milioni 1 kwa familia Juma Mfaume ambaye alifariki baada ya kupigwa na wafanyakazi wa kampuni hiyo
Akili za kuambiwa changanya na zako
 
Back
Top Bottom