macho_mdiliko
Platinum Member
- Mar 10, 2008
- 25,191
- 48,765
Una habari kuwa mdaiwa alikuwa nyumbani kwake na wao ndiyo walimvamia? Kuna sheria inasema uingie kwenye nyumba ya mdaiwa na kuiba vyombo vyake. Huu ni utetezi wa kijinga sana hauna ground yoyote.Yawezekana mdaiwa alitumia nguvu nyingi sana ikapelekea na wao kutumia nguvu zaidi Ili kumdhibiti vinginevyo pengine angewauwa wao ni bora afe mmoja kuliko wangekufa watu wanne
Wanaambiwa mshahara laki 240,000/= ikifika mwisho WA mwezi wanapigiwa mahesabu na kulipwa Kwa kuangalia wamedai kiasi gani. KIJANA wangu alipata kazi huko nikamkatalia. Alinishukuru Kwani wenzie waliompeleka wadhulumiwa. Vijana wasipodai hawalipwi ndio maana wanatumia Hadi NGUVU 😔Aiseeee kampuni inaajiri vitoto vidogo na kuwatwika majukumu makubwa.
Bosi wao naye aswekwe ndani
Wana roho mbaya sana hawa vijanaWafanyakazi wanne wa taasisi ya mikopo ya OYA wamefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Kibaha kwa tuhuma za mauaji ya kukusudia ya Juma Said Seif (45), mkaazi wa Kitongoji cha Mbagala Mlandizi Mkoani Pwani yaliyofanyika Oktoba 7. 2024.
Wakili wa Serikali, Monica Mwela amewataja watuhumiwa hao kuwa ni Dastan John Charles (23), Christopher John Charles (23), Emmanuel Joshua Olala(24) ambao ni wakazi wa Kilangalanga Mlandizi pamoja na Abdallah Felix Wendiliwe (32) mkaazi wa Janga Mlandizi.
Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Kibaha, Emmaeli Lukumai amesema ushahidi wa kesi hiyo iliyosomwa kwa mara ya kwanza bado haujakamilika, hivyo kesi hiyo imehairishwa hadi Oktoba 30 mkwaka huu.
Wakati wakisomewa kesi hiyo, watuhumiwa hawakutakiwa kujibu lolote kwa sababu mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza kesi ya mauaji. Watuhumiwa wote wamerudishwa rumande.
Chanzo: AZAM TV
Pia soma ~ Kampuni ya OYA watoa milioni 1 kwa familia Juma Mfaume ambaye alifariki baada ya kupigwa na wafanyakazi wa kampuni hiyo
Aiseee hii kesi mwajiri kujitoa si sawa.Wanaambiwa mshahara laki 240,000/= ikifika mwisho WA mwezi wanapigiwa mahesabu na kulipwa Kwa kuangalia wamedai kiasi gani. KIJANA wangu alipata kazi huko nikamkatalia. Alinishukuru Kwani wenzie waliompeleka wadhulumiwa. Vijana wasipodai hawalipwi ndio maana wanatumia Hadi NGUVU 😔
Kwa nini!?Huyu mwenye Bichwa Refu Anyongwe haraka
Basi wakibaliane na matokeoYawezekana mdaiwa alitumia nguvu nyingi sana ikapelekea na wao kutumia nguvu zaidi Ili kumdhibiti vinginevyo pengine angewauwa wao ni bora afe mmoja kuliko wangekufa watu wanne