TANZIA Wafanyakazi watano wa TRA wafariki dunia kwenye ajali

TANZIA Wafanyakazi watano wa TRA wafariki dunia kwenye ajali

Wazee wa magendo Wana balaa, usiwafate hata kidogo. Hiyo road ya Tunduma-Mbeya kwenye milima mikali ya Iwambi,Songwe,senjere,chapwa,Old Vwawa wao ndio sehemu wanapokuacha wanafunguka hawaogopi malori yanayopita na gari wanatumia za kawaida.
Hatar

Ova
 
Hawa jamaa walikua wanakimbiza gari yenye mzigo wa magendo, mwenye hio gari aliovertake hilo lori kukawa na lori lingine linakuja face to face (mwenye magendo) akafanikiwa kulipita hilo lori, hii cruiser ikashindwa kupita maana lori lingine lilikua karibu tayari ikabidi jamaa apige hili lori kwa nyuma ndo akazama uvunguni..ila yote kwa yote hata tusemaje ndugu zetu hawa hawawezi kurudi tenda...pumzika kwa Amani mwanangu Saidi Buddy....jamaa alikua mwana kichizi....
Mkuu poleni sana.
 
Screenshot_2021-08-23-21-48-41-1.png
 
Hawa jamaa walikua wanakimbiza gari yenye mzigo wa magendo, mwenye hio gari aliovertake hilo lori kukawa na lori lingine linakuja face to face (mwenye magendo) akafanikiwa kulipita hilo lori, hii cruiser ikashindwa kupita maana lori lingine lilikua karibu tayari ikabidi jamaa apige hili lori kwa nyuma ndo akazama uvunguni..ila yote kwa yote hata tusemaje ndugu zetu hawa hawawezi kurudi tenda...pumzika kwa Amani mwanangu Saidi Buddy....jamaa alikua mwana kichizi....
Screenshot_20210823_215519.jpg
Dah inahuzunisha
 
Jamaa atakuwa alikandamiza brake bila shaka yani jamaa anataka kuitolea ubavuni tu jamaa akamtilia brake zote jamaa wakajaaa mazima 😂😂😂af Fuso unaita kiroli labda ikiwa tupu ila ikiwa fully loaded ni mziki mwengine!
Mmh aisee Kama kweli alikanyaga breki ili wajae Basi huyo dereva sio!
 
Wafanyakazi watano wa Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA) kikosi kazi cha Fast Track wamefariki dunia kwa ajali ya gari aina ya Landcluser lililogonga kwa nyuma Lori aina Fuso. Walikuwa wakifukuzana na gari iliyodhaniwa kubeba magendo

Ajali hiyo imetokea leo Agosti 23, 2021 saa 11 alfajiri katika barabara ya Mbeya Tunduma eneo la Hanseketwa Wilaya ya Mbozi Mkoani Songwe.

Kaimu Meneja wa Forodha wa TRA wa Tunduma, Omary Mnzava amewataja watumishi watano wa mamlaka hiyo kikosi kazi cha fast track waliofariki ajalini leo asubuhi Jumatatu mkoani humo ni Azari Shifonike ambaye ni dereva, Joel Mitondwa, Saidi Buddy, Fahad Hassan na Benard Mashingi.
Ninachojiuliza kwanini wafukukuzie gari wakati barabarani kuna askari wa usalama, kukimbiza gari barabarani kwa kuwa ni TRA ni hatari hata kwa usalama wa watu wengine na mwisho Mbeya na Songwe ni mikoa miwili tofauti ilikuwaje watumishi wa TRA wa mkoawa Mbeya wakafanye operesheni mkoa wa Songwe je waliruhusiwa na nani? je mkoa wa Songwe hawana TRA, je wakati wanaenda Mbozi waliwasiliana na wenzao wa Mkoa wa Songwe?
 
On a serious note, tunahitaji sheria kali dhidi ya magari mabovu barabarani. Hatuwezi kugeuza barabara kuwa garage, watu wengi sana wamekufa kwa sababu ya magari yaliyoharibika barabarani.
Umewaza vizuri, Mimi pamoja na kwamba huwa nawakubali Sana baadhi ya madereva wa maloli makubwa kwa umakini barabarani, lakini baadhi yao wana dosari katika parking hasa magari hayo yanapoharibika akiwa barabarani, endapo gari linapata breakdown. Wengi huwa analiacha ndani kabisa ya barabara "kicheche" Jambo ambalo ni hatari sana hususan miss ya giza. Niwashauri wawe wanapaki nje kabisa ya barabara.
 
Walikuwa wanawaza nini kufukuzia magendo?.. Unafukuzanaje na watu wamejitoa muhanga ??? ..

Halafu unazifukuzia kodi hivo, wenye nchi wanazigawanya kwenye posho za vikao.

Aisee wanaoifia hii nchi wana mioyo ya chuma
 
Ninachojiuliza kwanini wafukukuzie gari wakati barabarani kuna askari wa usalama, kukimbiza gari barabarani kwa kuwa ni TRA ni hatari hata kwa usalama wa watu wengine na mwisho Mbeya na Songwe ni mikoa miwili tofauti ilikuwaje watumishi wa TRA wa mkoawa Mbeya wakafanye operesheni mkoa wa Songwe je waliruhusiwa na nani? je mkoa wa Songwe hawana TRA, je wakati wanaenda Mbozi waliwasiliana na wenzao wa Mkoa wa Songwe?
Ni Kama Ole Sabaya alivyokua ana operate Hai,Arusha mjini,Dar kwa kutumwa na mamlaka iliyomteua,so nao Ni hivyo hivyo labda.
 
STL wanajionaga kings wa road kinoma. Mafuta wanachota bohari na spare wanapeleka tu kwa quotation. Yaani sema ndio ivo wapumzike kwa amani.

Kifupi ukiona gari ya megendo imekataa kusimama achana nayo. Ongea na polisi wa check point waweke kikwazo.
Wale madereva ni sawa na mtu asiyetumia kondom kwa mwanamke wa bar ya Kinondoni.
in short una maana wapo tayari kwa lolote lile na hawana kitu cha kupoteza kwa hiyo unapo changa karata zako kuwa makini.
 
Back
Top Bottom