Wafuatao, wanaweza kuvivaa viatu vya Magufuli na vikawaenea

Ole wako Nchi ambayo kiongozi wako ni mwanamke au kijana mdogo!!

Ukiona hayo yameruhusiwa KUTOKEA, jua mnaadhibiwa.
Acha kuleta ubaguzi na mfumo dume. Kwanza wanawake ndio wengi Tanzania kuliko wanaume, pili watanzania 70% ni vijana chini ya miaka 35!! Sasa unategemea walio wengi wasiongoze?

Haupo serious
 
1 Bashilu Ally

2. Sabaya

3 Makonda

4 Mpina

5 Majaliwa
 
Wewe ni mpigaji obvious, kwa hiyo lazima uchukue watu ambao si wapigaji,si wataziba mianya?Huna lolote,na ndio maana mlimchukia JPM,shame on you.
Nlimchukia JPM sababu ya uongozi mbovu nothing personal. Huyo mpango kaziba mianya gani? Hivi kuna mwaka ripoti ya CAG haijawahi ona kuna ufisadi?
 
Nlimchukia JPM sababu ya uongozi mbovu nothing personal. Huyo mpango kaziba mianya gani? Hivi kuna mwaka ripoti ya CAG haijawahi ona kuna ufisadi?
Zitto JPM hakuwa na uongozi mbovu,he was the best President we have ever had.Nitalisema hili siku zote,watu waovu ndio waliomchukia JPM na hatimaye kumuua.
 
Kidogo majaliwa hao wengine ni comedians tu. Huyo namba 4 ndio zero kabisa, mropokaji tu aliyekosa ulaji hana uzalendo wowote ule.
Majaliwa hafai kuwa Rais,kwanza hana msimamo,pili sio mzalendo,tatu ni mwoga,nne he is easy to manipulate na tano hajui Dunia inavyoendeshwa.Ili isiwe rahisi Rais kuingizwa mkenge lazima ajue Dunia inavyoendeshwa.
 
Hapo nawaona wafuatao in descending order:
1.Phillip Mpango
2.Gwajina.

Tatizo ni NEC.Kwa kuwa imejaa wababaishaji haiwezi kuwapitisha.Kwanza si wenzao.
Mungu akawe msaada kwao japokuwa njia ni kama finyu kwao!!
 
Unajifanya hujamuona MAKONDA 🤣
 
Unajifanya hujamuona MAKONDA 🤣
Nimemwona,

Anakosa sifa kuu nne hapo juu, Hasa Uzalendo na ulipaji Kodi Kwa hiari.

Sifa ingine asiyo nayo ni Maono, ndo maana akampiga Mzee wetu mzalendo WARIOBA.
 
Acha kuleta ubaguzi na mfumo dume. Kwanza wanawake ndio wengi Tanzania kuliko wanaume, pili watanzania 70% ni vijana chini ya miaka 35!! Sasa unategemea walio wengi wasiongoze?

Haupo serious
Kwako kuwa serious, ni kuamini sawa nawe?
 
Mungu akawe msaada kwao japokuwa njia ni kama finyu kwao!!
Finyu sana mkuu.Kwa Tanzania ili NEC ikupitishe,lazima uwe mwenzao,yaani uwe na tabia za hovyo hovyo kama wao.Si uliona walivyokuwa wana mnyanyapaa Maguli.Magufuli CCM kumu-indorse was a decision of last resort.Waliona CCM will lose badly, so they saw Magufuli as their saviour because he is loved by most Tanzanians.
 
Na ndio maana wamemteua maana sio tishio kwa Rais kama ilivyo ada kwa makamu wote waliopita hawana impact.
Makamu wa Rais hawezi kuwa tishio kwa Rais kwa Katiba yetu.Yeye is sort of a ceremonial post,Rais ndiye mtendaji mkuu.
 
Hebu fanya marekebisho kidogo!
Namba 1 out weka namba 3
Namba 2 Ije namba 4 futa iliyopohivyo namba 4 weka Mpina Luhanga.
 
Tupo kwenye nchi ambayo wanasiasa ndio matajiri wa nchi. Hakuna nchi yenye maendeleo ambayo wanasiasa ni matajiri. Serikali inangaika kuongeza wilaya, mikoa na wizara ili watu wapate ajira. Nchi ambayo mtu ambaye hana elimu hata ya sekondari anakaa katika kamati kuu ya chama cha serikali kinachofanya maaamuzi ya nchi nzima. Tutafika kweli ? Huyo unayemtaja alitumia zaidi ya trillioni mbili katika ujenzi wa reli kutoka dar mpaka mwanza. Hio hela itarudi kivipi ?. Alifanya utafiti gani kuona kuna abiria na mizigo mingi inayoenda mwanza ambapo hio hela ingerudi. Je mwanza kuna foleni ya malori kama tunduma ? Hata mtoto wa shule ya msingi anaona kuna shida hapa. Kuna mambo mengi yanakatisha tamaa. Lakini tatizo kubwa ni watanzania hatujaamka sisi hatupo kama wakenya bado tumelala sana.
 
Hata sasa mazingira Yale Yale yanakinyemelea chama.

CCM imechokwa, turufu pekee ni mgombea mwenye sifa anayekubalika na wananchi asiye na makandokando.

Aliyepo CCM hauziki, akiteuliwa apeperushe bendera ya chama, upinzani utatoa mshindi hata Kwa kupiga mikwaju ya penalty.

Tusubiri.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…