Wahadhiri waliostaafu na kuajiriwa kwa mikataba ni kero vyuoni

Wahadhiri waliostaafu na kuajiriwa kwa mikataba ni kero vyuoni

Kuna vibabu vilishastaafu vikavuta mafao vikala vikamaliza bado vikarudi kupiga lecture jamani ni kero, sio kutisha watu huko vinatumia mifumo ya zamani. Kuna vingine haviingii darasani hadi TA akibebee vitabu, vingine vinajigamba eti katika somo lake hawajawahi kugraduate watano, wakijitahidi sana watatu. Kama sio kuvunjana moyo ni nini?

Ukweli, hivi vibabu ndio vikwazo vya uimara wa elimu yetu, basi vikikutana na wanafunzi wa masters ni shida kina hakikisha akigraduate hana hamu yakuendelea kukaa chuoni. Uwekwe utaratibu mtu akistaafu akalime sio kubaki chuoni kurandaranda.
Vijana kuweni wapole COVID-19 inawavizia hao maprofesa ile mbaya.
 
Umeandika kweli ma Prof wazee hawataki kubadilika Mimi nakumbuka Prof wangu wa somo la research alikuwa anatumia notes zake za research za mwaka 1970 tena kwenye daftari lake, wakati research ya sikuhizi ina mambo mengi Kuna software za kuchakata data ila yeye anatumia notes za kale zisizo relevant nowdays, ma Prof wengine hutumia videsa vyao miaka nenda rudi na ukitumia references nyingine tofauti na wanachoamini hata ukitumia books nyingine unafeli. Hivi vyuo vyetu viendane na masomo yanayoendana na dunia bana
 
Niko ndani ya taasisi hizi mleta mada ana hoja hata kama kaongeza chumvi.
Hawa wastaafu hawafai kurudi kufundisha wanafaa kuwa washauri zaidi.
Kwanza wengi sio wote hawamalizi courses unakuta topic 2 au 3 hazijafundishwa.
Pili hawasahihishi in detail. Siku hizi kuna appeals mkiremark unakuta mara
Nyingine swali zima hakusahihisha May be hakuliona.
Tatu kutumia systems hawajui mfano ARIS utakuta anachelewesha matokeo hata wiki au zaidi mpaka asaidiwe.
Tatizo wanadamu hatukubali tuna mwisho wetu na tuwaachie wengine. Mfumo wa kukaa Na wastaafu ni kujilemaza kama Taifa na kunyima damu mpya kuchangia maendeleo.
Na wengine hawajui kutumia computer pia wako too manual kwa kweli, unakuta hawasahihishi kazi za watu. Watu Wana mshambulia tu mleta mada ila vyuo vyetu wabadilike licha ya wazee pia Kuna vijana nao wako too manual na hawako proactive sasa sijui ndo wamebukizana mazoea.
 
He bado wapo....Kuna mmoja enzi zetu,late 1990s alikuwa anatumia notes za Mwaka 1977...
Sio utani niliziona mwenyewe live.
Prof.Ka....Mu....[emoji2960][emoji2960][emoji2960]
Dah kumbe na wewe ulikutana na WA aina hyo mwingine alikuwa anafundisha science and technology ila anatumia notice za 1990 huko you can imagine
 
Vyuo vikuu vyetu,viwe na utaratibu wa kuandaa wataalaam /vijana watakaochukua Majukumu ya maprofesa wanao tarajiwa kustasfu (Succession plan).
Maprofesa wameongezewa umri wa kustaafu.kutoka miaka 60 mpaka 65 lakini bado,wanashindwa kuwatayarisha vijana wa kuwakabidhi Majukumu yao muda wa kustaafu unapofika,wanajiumiza na kazi au la wanatumia notes za kizamani,zilizopitwa na wakati kufundishia
VIJANA HAWANA ADABU NA HAWAFUNDISHIKI.
 
Vyuo vikuu vyetu,viwe na utaratibu wa kuandaa wataalaam /vijana watakaochukua Majukumu ya maprofesa wanao tarajiwa kustasfu (Succession plan).
Maprofesa wameongezewa umri wa kustaafu.kutoka miaka 60 mpaka 65 lakini bado,wanashindwa kuwatayarisha vijana wa kuwakabidhi Majukumu yao muda wa kustaafu unapofika,wanajiumiza na kazi au la wanatumia notes za kizamani,zilizopitwa na wakati kufundishia
Hapo kwenye kuendelea kufundishia notes za zamani ...... nakubaliana na wewe. Kuna wale wavivu ambao hawajishugulishi kabisa kujiupdate na new things .... they are stuck in the past!!
 
Back
Top Bottom