Wahamiaji haramu toka Kenya watiwa mbaroni Tanzania

Wahamiaji haramu toka Kenya watiwa mbaroni Tanzania

Geza Ulole

JF-Expert Member
Joined
Oct 31, 2009
Posts
65,136
Reaction score
91,917



Vyombo vya Kamati ya Usalama Wilaya ya Rombo vimewakamata wahamiaji haramu kutoka nchi jirani ya Kenya ambao wameingia Nchini bila kufuata utaratibu kwa maana ya hawakupitia boda iliyo rasmi na hawakuwa na nyaraka zozote za kiuhamiaji

Wamekamatwa kupitia msako halali, na imeelezwa walikuwa watu 26 ambapo kati yao wanaume ni watatu na wanawake ishirini na tatu

Baada ya kukamatwa, wahamiaji hao walifikishwa kituo kikuu cha Polisi cha Rombo. Wakiwa hapo wamefanyiwa upekuzi pamoja na kuhojiwa

Pia wamefikishwa Mahakama ya Wilaya ya Rombo na wamekutwa na hatia baada ya kukiri makosa yao. Wamehukumiwa kifungo cha mwaka mmoja gerezani au kulipa faini ya 500,000

======

MYTAKE
Hii wanalipa gharama za wale wa Bodaboda! next watalipa gharama ya kuzuia Mahindi!


CC: Tony254
 
Mahakama ya wilaya ya Rombo imewahukumu kifungo cha mwaka mmoja jela au faini ya sh 500,000 kila mmoja raia 26 wa Kenya.

Raia hao kutoka Kenya wamekamatiwa Usseri Rombo na kufikishwa mahakamani chini ya ulinzi mkali.

Raia hao wote 26 wa jamii ya wafugaji wamekiri kosa la kuvunja sheria ya uhamiaji.

Washtakiwa wote wameshindwa kulipa faini na hivyo kutupwa jela.

Source ITV habari

Maendeleo hayana vyama!
 
Na bado msako uanze mara moja
Mkuu wa wilaya amesema wanawasaka kila kona ili sheria ichukue mkondo wake kwa sababu wachaga wakiingia upande wa Kenya bila kuvaa barakoa nao huwa wanakamatwa na kushtakiwa!
 
Doooh sasa itakuwaje wakati mungu mtu wenu anapumulia gas zao uko kwao Kenya.
 
Chokochoko mnazitafuta wenyewe, Mambo yakishaharibika mnaanza kuwasingizia WAPINZANI.

Wale wahamiaji haramu wa Ethiopia mbona waliachiwa bila masharti yoyote?

Unadhani Ni taifa lipi litafurahi raia wake wakionewa?

Hao wafugaji bila shaka Ni jamii ya wamasai, wamasai wapo Kenya na TANZANIA miaka na miakaa na hawajuagi kabisa habari za mipaka ya kimataifa.

Na tumekua tukiwachukulia hivyo miaka na miaka, Kwa maana Ni ndugu zetu pia.

Sasa hivi Ni visasi visivyo na msingi,

Mkiendelea hivi na kesho mtakuja kusema na wanyamapori wanaovuka kutokana Kenya kuja Tz wataifishwe au wachomwe Moto kwa kuvuka kinyemela

Kiukweli, watanzania tusifike huko.

Usichopenda ufanyiwe, nawe usimfanyie mwenzio.

Sio tu wee kidogo TU ukiguswa unataka mkae meza ya maridhiano.

Kama mtanzania mzalendo,
Siafikiani kabisa na hizi chokochoko zinazoendelea dhidi ya ndugu zetu wakenya.
 
Ukiwa huko rombo na sehemu za tarakea

Watu wa pnde zote mbili wanatembeleana

Kuna watu pia wanatoka upande wa tz wanaenda kenya kufanya shuguli wengine wanachukua

Bidhaa huko na kuleta Tanzania.

Kwa upande wa kenya hivyo hivyo

Ova
 
Serikali ya awamu ya tano inazidi kuharibu mahusiano ya kidiplomasia na nchi Jirani, zaidi tunaoumia ni Wananchi wa kawaida.
 
Back
Top Bottom