Wahitimu wengi wa Vyuo Vikuu vya Kitanzania hawawezi kufanya mjadala kama huu wa watoto wa shule

Wahitimu wengi wa Vyuo Vikuu vya Kitanzania hawawezi kufanya mjadala kama huu wa watoto wa shule

MALCOM LUMUMBA

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2012
Posts
21,113
Reaction score
65,124
Nimeangalia kwa makini sana huu mjadala na kama mtu niliyewahi kufundisha chuo nimeshangazwa sana na uwezo wa hawa wanafunzi wa Kiafrika. Kipindi wanafanya huu mjadala walikuwa ni wenye umri mdogo sana, lakini uwezo wao wa kujenga na kujibu hoja, kuzungumza lugha ngeni kwa ufasaha, ujasiri, pamoja na uwezo wa kumheshimu mzungumzaji mwingine umenishangaza.

Nafahamu fika kwamba hizo hoja zao walizijadili vizuri kabla ya mjadala, lakini kilichonifurahisha ni uwezo wao wa kuvaa vizuri uhusika na kuzijenga hoja ipasavyo. Nasikitika kusema kwamba wahitimu wetu wengi wa vyuo vikuu wanashindwa kujenga hoja kwa namna hii na kuzungumza lugha kwa ufasaha: Iwe ni Kiingereza au Kiswahili.

Kuna sehemu kubwa sana, sisi kama taifa tunakwama: Nasikika zaidi kusema kwamba hawa ndugu wa mwaka 1957, waliweza kufanya mjadala mzuri unaoeleweka kuliko wabunge wengi wa Tanzania wa mwaka 2021. Kibaya na kinachosikitisha ni kwamba wanasiasa wetu wamekuwa ni watu wanaoogopa mno mijadala, tena hadi wengine ni PhD....

Tuna kazi ya ziada kama taifa....
 
Hao wa 1957 walikuwa wanalipiwa hadi nauli za kwenda na kurudi likizo. Shuleni na vyuoni maisha yalikuwa matamu.. na ukimaliza chuo unapangiwa kazi sio kuomba.

Siku hizi wanafunzi wa chuo inabidi wafanye vibiashara vidogo vidogo ili kwenda sawa na gharama za chuo. Siku ya kumaliza unapewa invoice ya HESLB huku ajira hakuna. Mnaosifia zamani wote ni wa kupuuzwa.
 
Tatizo kubwa la nchi yetu ni kutoheshimu mifumo iliyopo na hivyo tunajikuta hulka binafsi za watawala kuathiri moja kwa moja taaluma na fikra za watu.

Yaani ni sawa na baba wa familia anayependa kuonekana yeye ndio aliye sahihi siku zote na hivyo kusababisha athari kubwa kwa watoto.

Mfano, ukiwa baba wa familia halafu 1+1 ukasema ni 5, na kwasababu hupendi challenge watoto wako watakaa kimya. Na wewe ili kuonesha umwamba zaidi utawaambia watoto wako kuwa waliotinga hesabu ni wajinga na hawawatakii mema na hivyo unawalazimisha watoto wasisome hesabu.

Hali hii tumeiona wakati wa Magufuli.

Hata wanasiasa wetu hawawezi mijadala ndio maana mtu akiwa na madaraka anaamua kujibu hoja kwa physical attacks.

Watu wenye uwezo wapo lakini je, wanapewa uhuru wa kufikiri !?

Na je kwa familia zetu tunawapa uhuru wa kufikiri watoto wetu au ndio mkubwa hakosei?
 
Katiba Mbovu ndo inatufelisha wabongo, inatunyima kujiamini na kufanya mambo mazuri kwa kujiamini, si umeona tunaenda kujenga sanamu la million 400 plus.

Ila kuwapa mikopo vijana isiyo na riba wafanye biashara wanashindwa, kuwadhamini wahitimu waendelee kupata ujuzi wa kazi uku wakiwalipa accomodations and transport fee wanashindwa.

Ila wao kubadili magari na kupeana zawadi za mabenzi ndo wanaona fashion.

Hakika zambi ya kumchungulia Nuhu inatutafuna, ubongo zetu zimejaa makasi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hao wa 1957 walikuwa wanalipiwa hadi nauli za kwenda na kurudi likizo. Shuleni na vyuoni maisha yalikuwa matamu.. na ukimaliza chuo unapangiwa kazi sio kuomba. Siku hizi wanafunzi wa chuo inabidi wafanye vibiashara vidogo vidogo ili kwenda sawa na gharama za chuo. Siku ya kumaliza unapewa invoice ya HESLB huku ajira hakuna. Mnaosifia zamani wote ni wa kupuuzwa.
Hahah nasema uongo ndg zanguuuuuuuuuu?
 
Hao wa 1957 walikuwa wanalipiwa hadi nauli za kwenda na kurudi likizo. Shuleni na vyuoni maisha yalikuwa matamu.. na ukimaliza chuo unapangiwa kazi sio kuomba. Siku hizi wanafunzi wa chuo inabidi wafanye vibiashara vidogo vidogo ili kwenda sawa na gharama za chuo. Siku ya kumaliza unapewa invoice ya HESLB huku ajira hakuna. Mnaosifia zamani wote ni wa kupuuzwa.
Haya hebu tuijdali hii hoja yako vizuri:

Mosi, wengi walisoma kwenye mfumo huo unaosema wewe wa kulipiwa kila kitu lakini bado wana matatizo makubwa. AU wewe huwaoni wasomi wetu wengi wenye umri kuanzia miaka 45 na kuendelea waliosoma kipindi cha Mzee Nyerere na Mzee Mwinyi ?

Pili, wengine wanasoma kuanzia shule hadi chuo-kikuu kwa pesa za wazazi wao lakini tatizo bado kubwa. Wanatafutiwa na ajira kabisa, lakini tatizo bado ni kubwa. AU mwenzangu huwaoni jinsi walivyo huko maofisini ?
 
Watu wenye uwezo wapo lakini je, wanapewa uhuru wa kufikiri !?

Na je kwa familia zetu tunawapa uhuru wa kufikiri watoto wetu au ndio mkubwa hakosei?
Mkuu umeongea jambo muhimu sana, uhuru wa kifikra (Intellectual Freedom) ni moja ya msingi imara kabisa unaoruhusu mtu kukua kiakili na kujitambua (Cognitive Growth). Nadhani mada kama hii mtu akiijibu kisiasa tu kwa kutoa sababu rahisi kabisa, nadhani hataweza kupata suluhu.
 
Mkuu umeongea jambo muhimu sana, uhuru wa kifikra (Intellectual Freedom) ni moja ya msingi imara kabisa unaoruhusu mtu kukua kiakili na kujitambua (Cognitive Growth). Nadhani mada kama hii mtu akiijibu kisiasa tu kwa kutoa sababu rahisi kabisa, nadhani hataweza kupata suluhu.
Yes, sometimes hata elimu yetu siyo ya kuilaumu kivile kwasababu kuna watu wamesoma nje huko lakini wakirudi hapa wanakuwa na fikra zile zile kama wengine wa hapa.

Binafsi naona Kama tumeshindwa ku-democratise siasa at least tungejitahidi kufanya hivyo kwenye taaluma.

Secondary schools kuna morning speeches/talks na vyuoni kuna masuala ya presentations lakini ni mambo ya hiari. Siyo kila mmoja anashiriki.

Suala la self confidence, public speaking na presentation ni matatizo kubwa sana nchi hii.

Tena hili ni tatizo mpaka kwa wanasiasa ambao shughuli zao kubwa zinahitaji hizi skills. Chukulia mfano wa yule Naibu Waziri wa Fedha alipokuwa anatoa majibu bungeni.

Na too bad, watu wasiokuwa na contents za maana ndio wamekuwa na ujasiri mkubwa mno kuanzia kwenye siasa, burudani, biashara kiasi kwamba sasa taaluma zimeanza kuonekana hazina maana.

Kuna makampuni sasa hivi hasa media hayaangalii tena taaluma katika kuajiri, when it comes to public speaking na confidence.
 
Nimeiangali hiyo video kuanzia mwanzo hadi mwisho. Nimegundua kwamba tumetka mbali sana, hasa huyo mbwa jike wa kizungu, kanaongea ushuxi mtupu
 
Nimeiangali hiyo video kuanzia mwanzo hadi mwisho. Nimegundua kwamba tumetka mbali sana, hasa huyo mbwa jike wa kizungu, kanaongea ushuxi mtupu
Ndiyo mijadala ilivyo, lazima tupingane kwa hoja ili wasikilizaji waamue nini waondoke nacho mwishowe. Pia mijadala inasaidia hata wazungumzaji kujifunza na kubadilisha mitazamo yao. Lengo kuu la mijadala ni kuijenga jamii, na binafsi naamini mijadala ya wazi kama hii ndiyo huwezesha jamii kung'amua wapi tatizo lipo na lirekebishwe.

Taifa ambalo halifanya mijadala katika ngazi zote au kupiga marufuku mijadala ya wazi ni taifa ambalo halijastaarabika na linaenelekea korongoni.
 
Katiba Mbovu ndo inatufelisha wabongo, inatunyima kujiamini na kufanya mambo mazuri kwa kujiamini, si umeona tunaenda kujenga sanamu la million 400 plus.

Ila kuwapa mikopo vijana isiyo na riba wafanye biashara wanashindwa, kuwadhamini wahitimu waendelee kupata ujuzi wa kazi uku wakiwalipa accomodations and transport fee wanashindwa.

Ila wao kubadili magari na kupeana zawadi za mabenzi ndo wanaona fashion.

Hakika zambi ya kumchungulia Nuhu inatutafuna, ubongo zetu zimejaa makasi.

Sent using Jamii Forums mobile app
Aisee nimekuamini
 
Vyuo vikuu vya Tanzania sio chem chem ya fikra teena!!,kama ilivyokuwa60s,70s,80s and 90s Bali vimekuwa ni chem chem ya kijipwndekeza ili wapate teuz za UDC na URAS
 
Nimeangalia kwa makini sana huu mjadala na kama mtu niliyewahi kufundisha chuo nimeshangazwa sana na uwezo wa hawa wanafunzi wa Kiafrika. Kipindi wanafanya huu mjadala walikuwa ni wenye umri mdogo sana, lakini uwezo wao wa kujenga na kujibu hoja, kuzungumza lugha ngeni kwa ufasaha, ujasiri, pamoja na uwezo wa kumheshimu mzungumzaji mwingine umenishangaza.

Nafahamu fika kwamba hizo hoja zao walizijadili vizuri kabla ya mjadala, lakini kilichonifurahisha ni uwezo wao wa kuvaa vizuri uhusika na kuzijenga hoja ipasavyo. Nasikitika kusema kwamba wahitimu wetu wengi wa vyuo vikuu wanashindwa kujenga hoja kwa namna hii na kuzungumza lugha kwa ufasaha: Iwe ni Kiingereza au Kiswahili.

Kuna sehemu kubwa sana, sisi kama taifa tunakwama: Nasikika zaidi kusema kwamba hawa ndugu wa mwaka 1957, waliweza kufanya mjadala mzuri unaoeleweka kuliko wabunge wengi wa Tanzania wa mwaka 2021. Kibaya na kinachosikitisha ni kwamba wanasiasa wetu wamekuwa ni watu wanaoogopa mno mijadala, tena hadi wengine ni PhD....

Tuna kazi ya ziada kama taifa....

Wewe kama mwalimu wa chuo ulichukua hatua gani kutatua hii changamoto? Hatua ulizochukua zilifanikiwa kiasi gani?
 
Back
Top Bottom