Wahubiri wangu wa mfano Tanzania

Wahubiri wangu wa mfano Tanzania

Vp Kiboko ya wachawi ,mwenye kanisa Buza

Jamaa namskilizaga Furaha FM 90.9
 
Wapo pia mapadre wa kanisa katoliki na maaskofu walio wazuri sana katika kufundisha neno la Mungu ila kwa vile sio popular hawawezi kutajwa hapa .
Hawa ndio mkuu wao wa kanisa kasema ruksa jinsia moja kutinduana?.
 
Pastor Chris ndio Baba wa kiroho wa huyu tapeli na gold smuggler. Yeye nae akawa na kina Bushiri, makandiwa, mtalemwa, tonny na wengine kibao. Huyo jamaa ni charlatan wa kutupwa.
Baba wa kiroho wa Makandiwa sio huyo yuko Ghana na mwanzo walipoanza huduma walikuwa wanashare ila baadae mambo yaka badilika juu kwa juu...Ukiwa unawafuatilia utawaelewa tu.

Leo hii issue ya Fatherhood imenikumbusha jambo..Hivi unajia watumishi wengi wanasomeka sana katika ulimwengu wa roho kirahisi depending na Mababa wa Kiroho? Hata kushambiliwa hutegemea weakness za hao Mababa wa Kiroho..Choose your spiritual Father with full directives of Holy Spirit ukichagua kisa anafundisha na anawatu wengi au anawatoto wengi wa Kiroho inaweza kukupa shida mbeleni.

Hongera sana kwa vitabu ulivo visoma mtoa mada.Kuna njia nzuri sana kupitia hivi vitabu na mafundisho eidha ya audio au video vikiwa kwa uthabiti na kweli vimevuviwa na Master(Holy Spirit) kuwa imparted ndani ya spirit yamfuatiliaji ni kwa urahisi sana kama vile mapepo mengine yanavyo attack watu kupitia novels movies hata musics.

Hope namna yako ya kuamini sio ya kawaida maana watumishi hawa uliowataja wako deep mno katika issue za Faith.Hongera sana.
Wa Kimataifa/ toka Mataifa mengine ni hawa:
1. Kenneth Hagin
2. Kenneth Copeland
3. Smith Wigglesworth
4. Dr. David Oyedepo
5. Pastor Chris Oyakilome
6. Uebert Angel
7. T. L. Osborn
8. Gloria Copeland
9. F. F. Bosworth
10. Charles Capps
11. Norvel Hayes
12. Andrew Wommack
13. E. W. Kenyon
14. Jerry Savelle

Kwa Tanzania, ni hawa wafuatao:
1. Aaron B. C. Mabondo
Kwa sasa ni marehemu. Alikuwa katibu Mkuu wa Kanisa la Pentekoste Tanzania. Nilimfahamu kwa mara ya kwanza mwaka 2003, mwezi June, nilipohudhuria Camp iliyoandaliwa na NEW LIFE BAND ya jijini Arusha na kufanyikia katika shule ya Sekondari Moshi mkoani Kilimanjaro.

Nilibarikiwa na masomo yake ya Imani na jinsi alivyokuwa akiishi Imani yake. Baada ya kuaga dunia, nilifanikiwa kukisoma kitabu cha Historia ya maisha yake. Nimevutiwa na misimamo yake ya kiimani, kiasi cha kutokukubali kuwekewa mipaka ya kidhehebu.

Inasemekana, kupitia mafundisho yake, alichochea "uamsho" kwenye Makanisa yasiyokuwa ya Kipentekoste, kama Moravian, Anglikana, n.k. Huwa ninabarikiwa sana na wahubiri wanaolisambaza Neno la Mungu bila kuzingatia mipaka ya madhehebu yao. Msimamo wa Mabondo ulikuwa kwamba hakutumwa kuyahubiria madhehebu, bali kila kiumbe. Kwa hiyo alikuwa yupo tayari kuhubiri popote, bila kujali dhehebu litakalomwalika.

2. Dr. Mosses Kulola
Aliifanya huduma yake kwa uaminifu mkubwa sana. Hakuwa akitafuta maslahi yake binafsi. Alikuwa tayari kuhubiri hata katika mazingira magumu. Alikuwa ni mtu wa lengo moja tu maishani mwake, KUHUBIRI INJILI.

3. Mwl Christopher Mwakasege
Tokea aanze huduma, amekuwa "focused" kwenye hiyo huduma. Angeweza kufanya shughuli zingine za kiuchumi, hasa ukizingatia kuwa ni msomi wa Uchumi, lakini kwa kuwa ameukubali wito wa KULIFUNDISHA Neno la Mungu, ameamua kuachana na vingine vyote na kubaki na kimoja tu, huduma aliyoitiwa.

Kingine ninachompendea, ni tabia yake ya kutokuendekeza "udini". Timu ya huduma yake inadhihirisha hilo. Ina wahudumu kutoka madhehebu mablimbali yaliyopo Tanzania.

Kwa ufahamu wangu, yeye ni miongoni mwa wahubiri wachache walioweza kukivuka kiunzi cha udhehebu nchini Tanzania.

4. Mch. Elyona Kimaro
Japo sijamfuatilia sana, lakini kwa vipindi vyake vichache nilivyovitazama kupitia Upendo TV, amenibariki kwa kweli. Ni kiongozi mzuri. Kiongozi huona hitaji na kutafuta kulitimiza kabla ya kuambiwa. Ndivyo alivyofanya Kimaro kwenye Kanisa analoliongoza, ametafuta jinsi ya kukata kiu ya kiroho ya watu wake.

5. Dr. Augustine Mpemba
Ni Mtanzania anayeishi Marekani. Alikuwa Askofu wa Kanisa la TFE Jijini Mwanza, lakini sijui kama angali kiongozi wa hilo Kanisa kwa sasa. Nilishakisoma kitabu chake kimoja, na nilishasikiliza mtandaoni mafundisho yake kadhaa. Ana uelewa mpana wa mambo ya kiroho na kijamii. Madhalani, yupo vizuri sana kwenye masomo ya IMANI, masomo ambayo ni adimu sana katika Makanisa mengi ya Tanzania.

6. Prosper Ntepa
Sijawahi kusikiliza mahubiri yake, lakini nimevisoma vitabu kadhaa alivyoviandika. Kuna kimoja kinachohusiana na uponyaji, nilikipenda sana. Ni Mwalimu mzuri sana kwenye somo la Imani. Na kama ilivyo kwa tabia ya walimu wengi, yeye naye ni msomaji mzuri sana wa Vitabu.

7. Pastor Famous
Huyu ni Mchungaji wa Winners Chapel Jijini Mwanza. Nafikiri ni Mnigeria, alikuwa akiliongoza Kanisa la Winners Chapel lililopo Pasiansi jijini Mwanza. Sijui kama bado yupo pale au la.

8. Dr. Barnaba Mtokambali
Ni Askofu Mkuu wa TAG na pia ni Rais wa Makanisa ya Assemblies barani Afrika. Kama hiyo haitoshi, ni Mwenyekiti wa Makanisa ya Kipentekoste Tanzania.

Ana maono ya kiuongozi. Si bure CPCT wamempa Uenyekiti.

NB. Naweza nisiwe nakubaliana na kila kitu kwa baadhi ya hao watumishi wa Mungu, lakini kwa kuamua kuwataja kama miongoni mwa wahubiri wangu wa mfano, ni kwa sababu kuna maeneo wamenibariki.

Na, katika wahubiri woote, "my favourite" ni KENNETH HAGIN. Japo alishaaga dunia tokea mwaka 2003, vitabu vyake vimenisaidia sana , hasa katika eneo la IMANI.

Hatujawahi kukutana ana kwa ana, lakini kupitia vitabu vyake, amekuwa kama baba kwangu. Nimeshavisoma zaidi ya vitabu vyake hamsini. Nimeshavisoma karibia vitabu vyote alivyoviandika. Ni vichache sana ndiyo bado.

Tuwekee na wewe watumishi au viongozi wa dini unaowachukulia kama watumishi wa Mungu au viongozi wa mfano kwako.

Karibu!!!
 
hakuna kupepesa macho kwa matapeli, wenyewe wanajijua. injili yao hata kwenye Biblia haipo. huyo kuhani mtoto wa yesu wa mkombo aliyefukuziwa congo huyo, na mwamposa anajua alikotoka. washindwe kwa Jina la Yesu.
Matapeli yamekuwa mengi sana. Waumini maamuma lazima wanaswe kwenye hizo vilinge vyao. Shetani naye anayo Mazingaombwe yake wengi wamekufa kwa kutafuta miujiza fake.
 
Baba wa kiroho wa Makandiwa sio huyo yuko Ghana
Oh its true, anaitwa prophet Victor kussi Boateng nimekumbuka.Hizi ni nyakati za mwisho. Bibilia inasema nyakati za mwisho zitakuwa za hatari, maana watu watayakataa mafundisho yenye uzima na kugeukia mafundisho ya mashetani na maagizo ya kibinadamu nao watajipatia waalimu makundi makundi kwa kuwa wana masikio ya utafiti. Siku hizo ndo siku hizi sasa
 
Hapo Kenyon ndio namuelewa kuliko list yote. Sio kwa kumsikiliza bali kwa kusoma vitabu vyake.
Wengine wote wale wazungu huwa wanatuhumiwa kuwa ni Fmasons 33° hivyo huwa nawasilikiza kwa umakini sana au nawaacha kabisa.
Uchumi nje namsikiliza mzee Myron Golden. Namuelewa maana hapayuki anaongea vitu kiakili alafu hatafuti sadaka ya mtu. Nikiona mtumishi anatafuta sadakasadaka sana kuliko kufukua neno huwa namkwepa. Sadaka ni matokeo ya mtu kushiba neno sio mkakati wa injili.

Kwa Bongo, namkubali Pr. Mbaga Mwakasefe kidogo ila vitabu sio kumsikiliza tena eneo la uchumi tu sio kiroho.
 
Nilisema hvo bse Aligawa pesa kwa waumini walouzuria crusade leaders akisema zinatoka Baharini... Na sote tunajua ufalme wa giza unamakao huko Baharini... Ila kibaya zaidi injili anayohubiri haiko balanced... Mafanikio kwa Sana ila swala la utakatifu hamna au kidogo.
😃😃😃
 
4. Mch. Elyona Kimaro
Japo sijamfuatilia sana, lakini kwa vipindi vyake vichache nilivyovitazama kupitia Upendo TV, amenibariki kwa kweli. Ni kiongozi mzuri. Kiongozi huona hitaji na kutafuta kulitimiza kabla ya kuambiwa. Ndivyo alivyofanya Kimaro kwenye Kanisa analoliongoza, ametafuta jinsi ya kukata kiu ya kiroho ya watu wake.

Huyu ni mchungaji kweli ila hana Injili, huwezi kumweka kundi moja na Kulola aisee, Huyu, Mitimingi na Toni Kapola hawana tofauti

Pr Mbaga wa Adventista ni far better kuliko huyu

Haya ni maoni Yangu
 
Kwangu mimi mpaka sasa kwa hapa Tanzania ni hawa.
1. Mwalimu Christopher Mwakasege
2. Pastor Carlos Kirimbai

Jamaa wanaijua bible fresh, wanaisoma kila siku, na wanatamani kila mtu aisome Bible fresh na kuitambua. Yote kwa yote wanakufanya umjue Yesu at personal level bila kubabaishwa na chochote au yoyote.

Naambiwa walifanikiwa kuukwepa upepo wa kidini (kidhehebu) uliokuwa ukivuma vilivyo miaka ya 90, na wamefanikiwa pia kuuvuka huu upepo wa sasa wa tamaa za mali na umungu mtu unaotikisa kanisa la Tz kwa zaidi ya 80%.

Yote kwa yote jamaa wanaweza kukushawishi umjue Yesu na kuijua Bible fresh hata kama wewe sio mkristo au wewe ni mpagani.
Z. Kakobe
 
Pastor Carlos Kirimbai ni wa wapi?
Pastor Carlos Kirimbai wa Tanzania, yuko hapo Dar, miaka mingi ya nyuma alikuwa akifanya kazi ya ukalimani katika mikutano ya Injili iliyokuwa inawaleta wahubiri mbali mbali wa kimaitafa hapa Tanzania mfano akina Bhonke. Kwa sasa muda mwingi anakuwa anafundisha na kuhubiri hapo Dar akitumia madarasa ya shule ya sekondari ya Kisutu, mjini kati na akishare free mafundisho yake kupitia mitandao ya kijamii ikiwemo whatsapp. Ni jamaa fulani hivi hana makuu lakini anapeo fresh wa bible na jamii.
 
Wa Kimataifa/ toka Mataifa mengine ni hawa:
1. Kenneth Hagin
2. Kenneth Copeland
3. Smith Wigglesworth
4. Dr. David Oyedepo
5. Pastor Chris Oyakilome
6. Uebert Angel
7. T. L. Osborn
8. Gloria Copeland
9. F. F. Bosworth
10. Charles Capps
11. Norvel Hayes
12. Andrew Wommack
13. E. W. Kenyon
14. Jerry Savelle

Kwa Tanzania, ni hawa wafuatao:
1. Aaron B. C. Mabondo
Kwa sasa ni marehemu. Alikuwa katibu Mkuu wa Kanisa la Pentekoste Tanzania. Nilimfahamu kwa mara ya kwanza mwaka 2003, mwezi June, nilipohudhuria Camp iliyoandaliwa na NEW LIFE BAND ya jijini Arusha na kufanyikia katika shule ya Sekondari Moshi mkoani Kilimanjaro.

Nilibarikiwa na masomo yake ya Imani na jinsi alivyokuwa akiishi Imani yake. Baada ya kuaga dunia, nilifanikiwa kukisoma kitabu cha Historia ya maisha yake. Nimevutiwa na misimamo yake ya kiimani, kiasi cha kutokukubali kuwekewa mipaka ya kidhehebu.

Inasemekana, kupitia mafundisho yake, alichochea "uamsho" kwenye Makanisa yasiyokuwa ya Kipentekoste, kama Moravian, Anglikana, n.k. Huwa ninabarikiwa sana na wahubiri wanaolisambaza Neno la Mungu bila kuzingatia mipaka ya madhehebu yao. Msimamo wa Mabondo ulikuwa kwamba hakutumwa kuyahubiria madhehebu, bali kila kiumbe. Kwa hiyo alikuwa yupo tayari kuhubiri popote, bila kujali dhehebu litakalomwalika.

2. Dr. Mosses Kulola
Aliifanya huduma yake kwa uaminifu mkubwa sana. Hakuwa akitafuta maslahi yake binafsi. Alikuwa tayari kuhubiri hata katika mazingira magumu. Alikuwa ni mtu wa lengo moja tu maishani mwake, KUHUBIRI INJILI.

3. Mwl Christopher Mwakasege
Tokea aanze huduma, amekuwa "focused" kwenye hiyo huduma. Angeweza kufanya shughuli zingine za kiuchumi, hasa ukizingatia kuwa ni msomi wa Uchumi, lakini kwa kuwa ameukubali wito wa KULIFUNDISHA Neno la Mungu, ameamua kuachana na vingine vyote na kubaki na kimoja tu, huduma aliyoitiwa.

Kingine ninachompendea, ni tabia yake ya kutokuendekeza "udini". Timu ya huduma yake inadhihirisha hilo. Ina wahudumu kutoka madhehebu mablimbali yaliyopo Tanzania.

Kwa ufahamu wangu, yeye ni miongoni mwa wahubiri wachache walioweza kukivuka kiunzi cha udhehebu nchini Tanzania.

4. Mch. Elyona Kimaro
Japo sijamfuatilia sana, lakini kwa vipindi vyake vichache nilivyovitazama kupitia Upendo TV, amenibariki kwa kweli. Ni kiongozi mzuri. Kiongozi huona hitaji na kutafuta kulitimiza kabla ya kuambiwa. Ndivyo alivyofanya Kimaro kwenye Kanisa analoliongoza, ametafuta jinsi ya kukata kiu ya kiroho ya watu wake.

5. Dr. Augustine Mpemba
Ni Mtanzania anayeishi Marekani. Alikuwa Askofu wa Kanisa la TFE Jijini Mwanza, lakini sijui kama angali kiongozi wa hilo Kanisa kwa sasa. Nilishakisoma kitabu chake kimoja, na nilishasikiliza mtandaoni mafundisho yake kadhaa. Ana uelewa mpana wa mambo ya kiroho na kijamii. Madhalani, yupo vizuri sana kwenye masomo ya IMANI, masomo ambayo ni adimu sana katika Makanisa mengi ya Tanzania.

6. Prosper Ntepa
Sijawahi kusikiliza mahubiri yake, lakini nimevisoma vitabu kadhaa alivyoviandika. Kuna kimoja kinachohusiana na uponyaji, nilikipenda sana. Ni Mwalimu mzuri sana kwenye somo la Imani. Na kama ilivyo kwa tabia ya walimu wengi, yeye naye ni msomaji mzuri sana wa Vitabu.

7. Pastor Famous
Huyu ni Mchungaji wa Winners Chapel Jijini Mwanza. Nafikiri ni Mnigeria, alikuwa akiliongoza Kanisa la Winners Chapel lililopo Pasiansi jijini Mwanza. Sijui kama bado yupo pale au la.

8. Dr. Barnaba Mtokambali
Ni Askofu Mkuu wa TAG na pia ni Rais wa Makanisa ya Assemblies barani Afrika. Kama hiyo haitoshi, ni Mwenyekiti wa Makanisa ya Kipentekoste Tanzania.

Ana maono ya kiuongozi. Si bure CPCT wamempa Uenyekiti.

NB. Naweza nisiwe nakubaliana na kila kitu kwa baadhi ya hao watumishi wa Mungu, lakini kwa kuamua kuwataja kama miongoni mwa wahubiri wangu wa mfano, ni kwa sababu kuna maeneo wamenibariki.

Na, katika wahubiri woote, "my favourite" ni KENNETH HAGIN. Japo alishaaga dunia tokea mwaka 2003, vitabu vyake vimenisaidia sana , hasa katika eneo la IMANI.

Hatujawahi kukutana ana kwa ana, lakini kupitia vitabu vyake, amekuwa kama baba kwangu. Nimeshavisoma zaidi ya vitabu vyake hamsini. Nimeshavisoma karibia vitabu vyote alivyoviandika. Ni vichache sana ndiyo bado.

Tuwekee na wewe watumishi au viongozi wa dini unaowachukulia kama watumishi wa Mungu au viongozi wa mfano kwako.

Karibu!!!
Mwamba huyu mchambuzi wa Bible na misimamo mikali

Unaitwa FULL GOSPAL
. Z.Kakobe
 
Mzee Mabondo umenikumbusha mbali sana mkuu, Mungu ampumzishe salama. [emoji120]
Unamfahamu Aaron B. C. Mabondo? Hebu dadavua kidogo mkuu! Ni kati ya watumishi wa Mungu niliowakubali sana.

~ Alimpenda sana Mungu

~ Aliwaheshimu watumishi wenzake bila kujali utofauti wa madhehebu yao

~ Alikuwa mnyenyekevu sana

~ Alikuwa na imani katika NENO la Mungu. Japo hakuwa mtu wa media na hakupenda kujitangaza, kuna watu wengi walisaidika sana kupitia huduma yake, mfano:
1. Kumfufua Kanali wa JWTZ mkoani Arusha. Siku hiyo alikuwa Arusha katika Kanisa la KLPT Kaloleni alipopigiwa simu na mke wa marehemu ili akamsaidie kuupeleka mwili mochwari. Lakini alipofika, alimwamuru ainuke na ikawa hivyo, tena, akiwa hana hata chembe ya maumivu.

2. Dar Es Salaam nako pia alimfufua mtu.

3. Alipopelekwa hospitalini baada ya kivunjika mguu kwa ajali ya gari, daktari alipomwambia atakaa hospitalini mwezi mmoja alikataa. Alisema ana kazi nyingi hivyo atatoka baada ya siku tatu. Na kweli, siku ya tatu iligundulilka kuwa mguu ulishaunga na akaruhusiwa kwenda nyumbani.

Alikuwa ni mtu wa imani hasa. Alimwombea mwanamke aliyekuwa katolewa kizazi na hatimaye akaweza kubeba mimba, alimwombea muathirika wa VVU akapona, n.k.

Ukiweza, soma kitabu cha Historia yake, kinaitwa A WALK OF FAITH.
 
Back
Top Bottom