Wahubiri wangu wa mfano Tanzania

Wahubiri wangu wa mfano Tanzania

Baba wa kiroho wa Makandiwa sio huyo yuko Ghana na mwanzo walipoanza huduma walikuwa wanashare ila baadae mambo yaka badilika juu kwa juu...Ukiwa unawafuatilia utawaelewa tu.

Leo hii issue ya Fatherhood imenikumbusha jambo..Hivi unajia watumishi wengi wanasomeka sana katika ulimwengu wa roho kirahisi depending na Mababa wa Kiroho? Hata kushambiliwa hutegemea weakness za hao Mababa wa Kiroho..Choose your spiritual Father with full directives of Holy Spirit ukichagua kisa anafundisha na anawatu wengi au anawatoto wengi wa Kiroho inaweza kukupa shida mbeleni.

Hongera sana kwa vitabu ulivo visoma mtoa mada.Kuna njia nzuri sana kupitia hivi vitabu na mafundisho eidha ya audio au video vikiwa kwa uthabiti na kweli vimevuviwa na Master(Holy Spirit) kuwa imparted ndani ya spirit yamfuatiliaji ni kwa urahisi sana kama vile mapepo mengine yanavyo attack watu kupitia novels movies hata musics.

Hope namna yako ya kuamini sio ya kawaida maana watumishi hawa uliowataja wako deep mno katika issue za Faith.Hongera sana.
You are right sir! Wanasema "like the father like the son". Kama niliona mhubiri ananitia mashaka, namfuatilia mentor/ baba yake wa kiroho. Nitakachobaini kwa hiyo ndicho kitskachonofanya niendelee kumfuatilia huyo au la.

Na kuhusu vitabu, they are very powerful. Kama ilivyo kwa maneno ya kutamkwa, ndivyo ilivyo kwa maandishi, ni roho.

Binafsi, nimeathiriwa sana na vitabu vya Kenneth Hagin. Nahisi vimeniambukiza "kitu", lakini kizuri.
 
Huyu ni mchungaji kweli ila hana Injili, huwezi kumweka kundi moja na Kulola aisee, Huyu, Mitimingi na Toni Kapola hawana tofauti

Pr Mbaga wa Adventista ni far better kuliko huyu

Haya ni maoni Yangu
🙏🙏🙏
 
Kimsingi umewataja wa mtandaoni na wanaosikika sana kwenye media ila bado wapo watumishi wazuri tu humu duniani. Kuna mzee mmoja nilimkuta huko Iringa niliendaga na kuiishi kikazi mwezi mmoja huko Vijijini Dabaga nikawa naabudu kanisa la TAG Kilolo Christian Centre lipo pale Kilolo Wilayani Anaitwa Mzee Lucas Mkuye. Huyo ndio Mtume wa kwanza wa kweli kumuona maishani mwangu.

Mzee alianza huduma 1979 kipindi hiko ukanda wote wa Dabaga hauna kanisa lolote la kipentecoste na alikuwa akitembea kwa miguu hadi Mapanda huko Mufindi na akaanzisha na kusimamisha makanisa ya TAG ukanda huo. Zaidi ya makanisa 60 yametokea mikononi mwake.

Kwa Walutheri tunaoishi au kukulia ulutheri Morogoro au kwa wale tuliosoma Lutheran Junior Seminary miaka ya 1990's tuna mkumbuka Marehemu Mchungaji Hebert Hafferman. Huyu ndio Mtume wa Pili wa kweli kumuona kwa macho yangu achana na akina Bashando na Daudi Mashimo.

Mzee yule alikuwa mzungu na alikuja TZ miaka ya 1950's na alisambaza Ulutheri kwa kiasi kikubwa kwenye jamii ya kimasai. Aliwekeza kwenye huduma ya Neno na masuala ya kijamii ikiwemo kuwasomesha wamasai wengi wa Morogoro. Zao lake mmojawapo ni Richard Mameo Askofu wa Lutheran hapa Morogoro. R.I.P HEBERT HAFFERMAN, tutakutana katika pambazuko lile katika siku ile ya kalamu ya mwanakondoo.

Picha ya Marehemu mzee Hebert Hafferman akiwa na mtoto wa mchungaji mmoja wa Kimasai Marehemu Lucas.
FB_IMG_1700366471163.jpg
 
Huyu ni mchungaji kweli ila hana Injili, huwezi kumweka kundi moja na Kulola aisee, Huyu, Mitimingi na Toni Kapola hawana tofauti

Pr Mbaga wa Adventista ni far better kuliko huyu

Haya ni maoni Yangu
Mkuu, binafsi simfahamu Pr Mbaga. Unaweza ukamwelezea kidogo? Huenda kuna mtu anaweza akawa anahitaji "huduma" yake.
 
Pastor Carlos Kirimbai wa Tanzania, yuko hapo Dar, miaka mingi ya nyuma alikuwa akifanya kazi ya ukalimani katika mikutano ya Injili iliyokuwa inawaleta wahubiri mbali mbali wa kimaitafa hapa Tanzania mfano akina Bhonke. Kwa sasa muda mwingi anakuwa anafundisha na kuhubiri hapo Dar akitumia madarasa ya shule ya sekondari ya Kisutu, mjini kati na akishare free mafundisho yake kupitia mitandao ya kijamii ikiwemo whatsapp. Ni jamaa fulani hivi hana makuu lakini anapeo fresh wa bible na jamii.
Nashukuru mkuu🙏

Kumbe ni huyo! Nilishawahi kumsikiliza kupitia YouTube. Yupo vizuri🙏🙏🙏
 
Huyu TAPELI nae yumo hivi huwa mmefungwa macho? Aljeeriza wameonyesha utapele wa huyu na nia ya kuhubiri bado umemuweka meza moja na Kulola
Mkuu, nilieleza kuwa hao niliowaweka ni ambao kwa namna Moja ama nyingine nimebarikiwa na huduma zao.

Nilivisoma vitabu kadhaa vya Uebert Angel, japo kuna baadhi ya mambo ambayo mwanzoni vilinitia mashaka kuhusu huduma yake, niliamua kupuuzia baada ya kubaini kuwa mentor wake ni Pastor Chris.

Pastor Chris naye nilikuwa nina mashaka naye, lakini mashaka yaliisha nilipogundua kuwa rafiki yake wa karibu ni Benny Hinn.

Hata Benny Hinn, nilikuja kumkubali vilivyo baada ya kugundua ukaribu alikokuwa nao na Reinhard Bonnke.

Unauona mnyororo ulivyo? Bonnke, Benny Hinn, Pastor Chris, Uebert Angel.

Lakini sivyo tu, huwa nina "falsafa" yangu kwa habari ya watumishi. Kwamba, katika mafundisho yao, nitatofautisha chuya na wali. Nikikutana na chuya, nitatema lakini wali nitaumeza.

"Sibugii" kila kitu kisemwacho na mtumishi. Nikijiridhisha kuwa akisemacho kipo nje ya Biblia, nakiweka kando nasubiria kingine.
 
Wa Kimataifa/ toka Mataifa mengine ni hawa:
1. Kenneth Hagin
2. Kenneth Copeland
3. Smith Wigglesworth
4. Dr. David Oyedepo
5. Pastor Chris Oyakilome
6. Uebert Angel
7. T. L. Osborn
8. Gloria Copeland
9. F. F. Bosworth
10. Charles Capps
11. Norvel Hayes
12. Andrew Wommack
13. E. W. Kenyon
14. Jerry Savelle

Kwa Tanzania, ni hawa wafuatao:
1. Aaron B. C. Mabondo
Kwa sasa ni marehemu. Alikuwa katibu Mkuu wa Kanisa la Pentekoste Tanzania. Nilimfahamu kwa mara ya kwanza mwaka 2003, mwezi June, nilipohudhuria Camp iliyoandaliwa na NEW LIFE BAND ya jijini Arusha na kufanyikia katika shule ya Sekondari Moshi mkoani Kilimanjaro.

Nilibarikiwa na masomo yake ya Imani na jinsi alivyokuwa akiishi Imani yake. Baada ya kuaga dunia, nilifanikiwa kukisoma kitabu cha Historia ya maisha yake. Nimevutiwa na misimamo yake ya kiimani, kiasi cha kutokukubali kuwekewa mipaka ya kidhehebu.

Inasemekana, kupitia mafundisho yake, alichochea "uamsho" kwenye Makanisa yasiyokuwa ya Kipentekoste, kama Moravian, Anglikana, n.k. Huwa ninabarikiwa sana na wahubiri wanaolisambaza Neno la Mungu bila kuzingatia mipaka ya madhehebu yao. Msimamo wa Mabondo ulikuwa kwamba hakutumwa kuyahubiria madhehebu, bali kila kiumbe. Kwa hiyo alikuwa yupo tayari kuhubiri popote, bila kujali dhehebu litakalomwalika.

2. Dr. Mosses Kulola
Aliifanya huduma yake kwa uaminifu mkubwa sana. Hakuwa akitafuta maslahi yake binafsi. Alikuwa tayari kuhubiri hata katika mazingira magumu. Alikuwa ni mtu wa lengo moja tu maishani mwake, KUHUBIRI INJILI.

3. Mwl Christopher Mwakasege
Tokea aanze huduma, amekuwa "focused" kwenye hiyo huduma. Angeweza kufanya shughuli zingine za kiuchumi, hasa ukizingatia kuwa ni msomi wa Uchumi, lakini kwa kuwa ameukubali wito wa KULIFUNDISHA Neno la Mungu, ameamua kuachana na vingine vyote na kubaki na kimoja tu, huduma aliyoitiwa.

Kingine ninachompendea, ni tabia yake ya kutokuendekeza "udini". Timu ya huduma yake inadhihirisha hilo. Ina wahudumu kutoka madhehebu mablimbali yaliyopo Tanzania.

Kwa ufahamu wangu, yeye ni miongoni mwa wahubiri wachache walioweza kukivuka kiunzi cha udhehebu nchini Tanzania.

4. Mch. Elyona Kimaro
Japo sijamfuatilia sana, lakini kwa vipindi vyake vichache nilivyovitazama kupitia Upendo TV, amenibariki kwa kweli. Ni kiongozi mzuri. Kiongozi huona hitaji na kutafuta kulitimiza kabla ya kuambiwa. Ndivyo alivyofanya Kimaro kwenye Kanisa analoliongoza, ametafuta jinsi ya kukata kiu ya kiroho ya watu wake.

5. Dr. Augustine Mpemba
Ni Mtanzania anayeishi Marekani. Alikuwa Askofu wa Kanisa la TFE Jijini Mwanza, lakini sijui kama angali kiongozi wa hilo Kanisa kwa sasa. Nilishakisoma kitabu chake kimoja, na nilishasikiliza mtandaoni mafundisho yake kadhaa. Ana uelewa mpana wa mambo ya kiroho na kijamii. Madhalani, yupo vizuri sana kwenye masomo ya IMANI, masomo ambayo ni adimu sana katika Makanisa mengi ya Tanzania.

6. Prosper Ntepa
Sijawahi kusikiliza mahubiri yake, lakini nimevisoma vitabu kadhaa alivyoviandika. Kuna kimoja kinachohusiana na uponyaji, nilikipenda sana. Ni Mwalimu mzuri sana kwenye somo la Imani. Na kama ilivyo kwa tabia ya walimu wengi, yeye naye ni msomaji mzuri sana wa Vitabu.

7. Pastor Famous
Huyu ni Mchungaji wa Winners Chapel Jijini Mwanza. Nafikiri ni Mnigeria, alikuwa akiliongoza Kanisa la Winners Chapel lililopo Pasiansi jijini Mwanza. Sijui kama bado yupo pale au la.

8. Dr. Barnaba Mtokambali
Ni Askofu Mkuu wa TAG na pia ni Rais wa Makanisa ya Assemblies barani Afrika. Kama hiyo haitoshi, ni Mwenyekiti wa Makanisa ya Kipentekoste Tanzania.

Ana maono ya kiuongozi. Si bure CPCT wamempa Uenyekiti.

NB. Naweza nisiwe nakubaliana na kila kitu kwa baadhi ya hao watumishi wa Mungu, lakini kwa kuamua kuwataja kama miongoni mwa wahubiri wangu wa mfano, ni kwa sababu kuna maeneo wamenibariki.

Na, katika wahubiri woote, "my favourite" ni KENNETH HAGIN. Japo alishaaga dunia tokea mwaka 2003, vitabu vyake vimenisaidia sana , hasa katika eneo la IMANI.

Hatujawahi kukutana ana kwa ana, lakini kupitia vitabu vyake, amekuwa kama baba kwangu. Nimeshavisoma zaidi ya vitabu vyake hamsini. Nimeshavisoma karibia vitabu vyote alivyoviandika. Ni vichache sana ndiyo bado.

Tuwekee na wewe watumishi au viongozi wa dini unaowachukulia kama watumishi wa Mungu au viongozi wa mfano kwako.

Karibu!!!
KUNA KAUKOMAVU FULANI NA KAUTUBUZIMA NIMEKAONA NILIPOKUWA NASOMA LINE TO LINE YA HAYO ULIYOANDOKA.WEWE SIYO WALE WA SURIALI NI DHAMBI AU SIYO DHAMBI .GRAND MALT NI DHAMBI AU SIYO DHAMBI.
NATAMANI TUNGEKUTANA ANA KWA ANA,NINGETOKA KATIKA MKWAMO.
BE BLESSED.
 
Wa Kimataifa/ toka Mataifa mengine ni hawa:
1. Kenneth Hagin
2. Kenneth Copeland
3. Smith Wigglesworth
4. Dr. David Oyedepo
5. Pastor Chris Oyakilome
6. Uebert Angel
7. T. L. Osborn
8. Gloria Copeland
9. F. F. Bosworth
10. Charles Capps
11. Norvel Hayes
12. Andrew Wommack
13. E. W. Kenyon
14. Jerry Savelle

Kwa Tanzania, ni hawa wafuatao:
1. Aaron B. C. Mabondo
Kwa sasa ni marehemu. Alikuwa katibu Mkuu wa Kanisa la Pentekoste Tanzania. Nilimfahamu kwa mara ya kwanza mwaka 2003, mwezi June, nilipohudhuria Camp iliyoandaliwa na NEW LIFE BAND ya jijini Arusha na kufanyikia katika shule ya Sekondari Moshi mkoani Kilimanjaro.

Nilibarikiwa na masomo yake ya Imani na jinsi alivyokuwa akiishi Imani yake. Baada ya kuaga dunia, nilifanikiwa kukisoma kitabu cha Historia ya maisha yake. Nimevutiwa na misimamo yake ya kiimani, kiasi cha kutokukubali kuwekewa mipaka ya kidhehebu.

Inasemekana, kupitia mafundisho yake, alichochea "uamsho" kwenye Makanisa yasiyokuwa ya Kipentekoste, kama Moravian, Anglikana, n.k. Huwa ninabarikiwa sana na wahubiri wanaolisambaza Neno la Mungu bila kuzingatia mipaka ya madhehebu yao. Msimamo wa Mabondo ulikuwa kwamba hakutumwa kuyahubiria madhehebu, bali kila kiumbe. Kwa hiyo alikuwa yupo tayari kuhubiri popote, bila kujali dhehebu litakalomwalika.

2. Dr. Mosses Kulola
Aliifanya huduma yake kwa uaminifu mkubwa sana. Hakuwa akitafuta maslahi yake binafsi. Alikuwa tayari kuhubiri hata katika mazingira magumu. Alikuwa ni mtu wa lengo moja tu maishani mwake, KUHUBIRI INJILI.

3. Mwl Christopher Mwakasege
Tokea aanze huduma, amekuwa "focused" kwenye hiyo huduma. Angeweza kufanya shughuli zingine za kiuchumi, hasa ukizingatia kuwa ni msomi wa Uchumi, lakini kwa kuwa ameukubali wito wa KULIFUNDISHA Neno la Mungu, ameamua kuachana na vingine vyote na kubaki na kimoja tu, huduma aliyoitiwa.

Kingine ninachompendea, ni tabia yake ya kutokuendekeza "udini". Timu ya huduma yake inadhihirisha hilo. Ina wahudumu kutoka madhehebu mablimbali yaliyopo Tanzania.

Kwa ufahamu wangu, yeye ni miongoni mwa wahubiri wachache walioweza kukivuka kiunzi cha udhehebu nchini Tanzania.

4. Mch. Elyona Kimaro
Japo sijamfuatilia sana, lakini kwa vipindi vyake vichache nilivyovitazama kupitia Upendo TV, amenibariki kwa kweli. Ni kiongozi mzuri. Kiongozi huona hitaji na kutafuta kulitimiza kabla ya kuambiwa. Ndivyo alivyofanya Kimaro kwenye Kanisa analoliongoza, ametafuta jinsi ya kukata kiu ya kiroho ya watu wake.

5. Dr. Augustine Mpemba
Ni Mtanzania anayeishi Marekani. Alikuwa Askofu wa Kanisa la TFE Jijini Mwanza, lakini sijui kama angali kiongozi wa hilo Kanisa kwa sasa. Nilishakisoma kitabu chake kimoja, na nilishasikiliza mtandaoni mafundisho yake kadhaa. Ana uelewa mpana wa mambo ya kiroho na kijamii. Madhalani, yupo vizuri sana kwenye masomo ya IMANI, masomo ambayo ni adimu sana katika Makanisa mengi ya Tanzania.

6. Prosper Ntepa
Sijawahi kusikiliza mahubiri yake, lakini nimevisoma vitabu kadhaa alivyoviandika. Kuna kimoja kinachohusiana na uponyaji, nilikipenda sana. Ni Mwalimu mzuri sana kwenye somo la Imani. Na kama ilivyo kwa tabia ya walimu wengi, yeye naye ni msomaji mzuri sana wa Vitabu.

7. Pastor Famous
Huyu ni Mchungaji wa Winners Chapel Jijini Mwanza. Nafikiri ni Mnigeria, alikuwa akiliongoza Kanisa la Winners Chapel lililopo Pasiansi jijini Mwanza. Sijui kama bado yupo pale au la.

8. Dr. Barnaba Mtokambali
Ni Askofu Mkuu wa TAG na pia ni Rais wa Makanisa ya Assemblies barani Afrika. Kama hiyo haitoshi, ni Mwenyekiti wa Makanisa ya Kipentekoste Tanzania.

Ana maono ya kiuongozi. Si bure CPCT wamempa Uenyekiti.

NB. Naweza nisiwe nakubaliana na kila kitu kwa baadhi ya hao watumishi wa Mungu, lakini kwa kuamua kuwataja kama miongoni mwa wahubiri wangu wa mfano, ni kwa sababu kuna maeneo wamenibariki.

Na, katika wahubiri woote, "my favourite" ni KENNETH HAGIN. Japo alishaaga dunia tokea mwaka 2003, vitabu vyake vimenisaidia sana , hasa katika eneo la IMANI.

Hatujawahi kukutana ana kwa ana, lakini kupitia vitabu vyake, amekuwa kama baba kwangu. Nimeshavisoma zaidi ya vitabu vyake hamsini. Nimeshavisoma karibia vitabu vyote alivyoviandika. Ni vichache sana ndiyo bado.

Tuwekee na wewe watumishi au viongozi wa dini unaowachukulia kama watumishi wa Mungu au viongozi wa mfano kwako.

Karibu!!!
PAST Elingarami Munishi,namuona yuko objective sana.
 
KUNA KAUKOMAVU FULANI NA KAUTUBUZIMA NIMEKAONA NILIPOKUWA NASOMA LINE TO LINE YA HAYO ULIYOANDOKA.WEWE SIYO WALE WA SURIALI NI DHAMBI AU SIYO DHAMBI .GRAND MALT NI DHAMBI AU SIYO DHAMBI.
NATAMANI TUNGEKUTANA ANA KWA ANA,NINGETOKA KATIKA MKWAMO.
BE BLESSED.
Karibu mkuu, lakini mimi si Mchungaji wala kiongozi wa dini. Lakini ukipenda kunitafuta sitakuzuia.
 
Mkuu, nilieleza kuwa hao niliowaweka ni ambao kwa namna Moja ama nyingine nimebarikiwa na huduma zao.

Nilivisoma vitabu kadhaa vya Uebert Angel, japo kuna baadhi ya mambo ambayo mwanzoni vilinitia mashaka kuhusu huduma yake, niliamua kupuuzia baada ya kubaini kuwa mentor wake ni Pastor Chris.

Pastor Chris naye nilikuwa nina mashaka naye, lakini mashaka yaliisha nilipogundua kuwa rafiki yake wa karibu ni Benny Hinn.

Hata Benny Hinn, nilikuja kumkubali vilivyo baada ya kugundua ukaribu alikokuwa nao na Reinhard Bonnke.

Unauona mnyororo ulivyo? Bonnke, Benny Hinn, Pastor Chris, Uebert Angel.

Lakini sivyo tu, huwa nina "falsafa" yangu kwa habari ya watumishi. Kwamba, katika mafundisho yao, nitatofautisha chuya na wali. Nikikutana na chuya, nitatema lakini wali nitaumeza.

"Sibugii" kila kitu kisemwacho na mtumishi. Nikijiridhisha kuwa akisemacho kipo nje ya Biblia, nakiweka kando nasubiria kingine.
Hao wote hapo juu sina shaka nao,hasa pastor Chris oyakhilome
20231118_204016.png
 
Back
Top Bottom