Wahubiri wangu wa mfano Tanzania

Wahubiri wangu wa mfano Tanzania

Unamfahamu Aaron B. C. Mabondo? Hebu dadavua kidogo mkuu! Ni kati ya watumishi wa Mungu niliowakubali sana.

~ Alimpenda sana Mungu

~ Aliwaheshimu watumishi wenzake bila kujali utofauti wa madhehebu yao

~ Alikuwa mnyenyekevu sana

~ Alikuwa na imani katika NENO la Mungu. Japo hakuwa mtu wa media na hakupenda kujitangaza, kuna watu wengi walisaidika sana kupitia huduma yake, mfano:
1. Kumfufua Kanali wa JWTZ mkoani Arusha. Siku hiyo alikuwa Arusha katika Kanisa la KLPT Kaloleni alipopigiwa simu na mke wa marehemu ili akamsaidie kuupeleka mwili mochwari. Lakini alipofika, alimwamuru ainuke na ikawa hivyo, tena, akiwa hana hata chembe ya maumivu.

2. Dar Es Salaam nako pia alimfufua mtu.

3. Alipopelekwa hospitalini baada ya kivunjika mguu kwa ajali ya gari, daktari alipomwambia atakaa hospitalini mwezi mmoja alikataa. Alisema ana kazi nyingi hivyo atatoka baada ya siku tatu. Na kweli, siku ya tatu iligundulilka kuwa mguu ulishaunga na akaruhusiwa kwenda nyumbani.

Alikuwa ni mtu wa imani hasa. Alimwombea mwanamke aliyekuwa katolewa kizazi na hatimaye akaweza kubeba mimba, alimwombea muathirika wa VVU akapona, n.k.

Ukiweza, soma kitabu cha Historia yake, kinaitwa A WALK OF FAITH.
Naweza nikakipata wapi
 
Mkuu, nilieleza kuwa hao niliowaweka ni ambao kwa namna Moja ama nyingine nimebarikiwa na huduma zao.

Nilivisoma vitabu kadhaa vya Uebert Angel, japo kuna baadhi ya mambo ambayo mwanzoni vilinitia mashaka kuhusu huduma yake, niliamua kupuuzia baada ya kubaini kuwa mentor wake ni Pastor Chris.

Pastor Chris naye nilikuwa nina mashaka naye, lakini mashaka yaliisha nilipogundua kuwa rafiki yake wa karibu ni Benny Hinn.

Hata Benny Hinn, nilikuja kumkubali vilivyo baada ya kugundua ukaribu alikokuwa nao na Reinhard Bonnke.

Unauona mnyororo ulivyo? Bonnke, Benny Hinn, Pastor Chris, Uebert Angel.

Lakini sivyo tu, huwa nina "falsafa" yangu kwa habari ya watumishi. Kwamba, katika mafundisho yao, nitatofautisha chuya na wali. Nikikutana na chuya, nitatema lakini wali nitaumeza.

"Sibugii" kila kitu kisemwacho na mtumishi. Nikijiridhisha kuwa akisemacho kipo nje ya Biblia, nakiweka kando nasubiria kingine.
Mkuu uko sawa. Uebert Angel nimemfuatilia tangu 2018. mara ya kwanza kumwona mtandaoni nilijua mhuuni fulan wa kiinjili,nilijaji kitabu kwa kuangalia cover. Baada ya kumsikiliza deeply alisababisha nishindwe kuwasikiliza wahuburi wengine mitandaoni mpka nilipomsikia akisema Pastor Chris ni baba yake,kumfuatilia naye wa moto pia. Lakini yote kwa yote uebert Angel bado ndio nilishaganda. Wakati anakuja Dar June mwishoni,nilisafiri kutoka Geita just kuhudhuria live,sijuti kumfahamu huyu mtumishi.
 
Benny Hinn mzee wa Roho Mtakatifu,hiki ni chuma
Mkuu, fahamu kuwa imeandikwa, USIHUKUMU USIJE UKAHUKUMIWA.

Kama Bonnke aliamini kuwa Benny Hinn ni mtumishi wa Mungu, si vizuri wewe kumwita tapeli.

Angalia video Bonnke akimwombea Benny Hinn na mkewe.
 
Mkuu uko sawa. Uebert Angel nimemfuatilia tangu 2018. mara ya kwanza kumwona mtandaoni nilijua mhuuni fulan wa kiinjili,nilijaji kitabu kwa kuangalia cover. Baada ya kumsikiliza deeply alisababisha nishindwe kuwasikiliza wahuburi wengine mitandaoni mpka nilipomsikia akisema Pastor Chris ni baba yake,kumfuatilia naye wa moto pia. Lakini yote kwa yote uebert Angel bado ndio nilishaganda. Wakati anakuja Dar June mwishoni,nilisafiri kutoka Geita just kuhudhuria live,sijuti kumfahamu huyu mtumishi.
Mwanzoni nilitaka kumtilia mashaka kutokana na kilichoonekana kama miujiza iliyozidi kiasi kwenye huduma yake. Lakini kadiri nilivyomfuatulia, ndivyo nilivyozidi kugundua kuwa hayupo kinyume na Maandiko. Nilisikiliza mahubiri yake kadhaa na kusoma vitabu vyake kadhaa, vikiwemo GENETICS OF WORDS, PRAYING FOR THE IMPOSSIBLE, PRAYER BANKS, SPIRITUAL WARFARE, etc.

Nilipofahamu kuwa mentor wake ni Pastor Chris, na kwamba anawakubali akina Benny Hinn,David Oyedepo, Kenneth Hagin, T. L. Osborn, n.k., mashaka yote yaliniisha.
 
Naweza nikakipata wapi
Mwandishi wake ni Dr. Charles Sokile. Mimi nilikinunua Dodoma mjini mwaka 2010. Nafikiri, kinaweza kupatikana kwenye maduka ya vitabu, hasa Dar Es Salaam. Ukikikosa, wasiliana na huduma ya New Life Band. Mkurugenzi wa hiyo huduma ni Hondo ambaye ni mtoto wa Mabondo. Kwa vyo vyote, wanajua kinapopatikana.
 
Wa Kimataifa/ toka Mataifa mengine ni hawa:
1. Kenneth Hagin
2. Kenneth Copeland
3. Smith Wigglesworth
4. Dr. David Oyedepo
5. Pastor Chris Oyakilome
6. Uebert Angel
7. T. L. Osborn
8. Gloria Copeland
9. F. F. Bosworth
10. Charles Capps
11. Norvel Hayes
12. Andrew Wommack
13. E. W. Kenyon
14. Jerry Savelle

Kwa Tanzania, ni hawa wafuatao:
1. Aaron B. C. Mabondo
Kwa sasa ni marehemu. Alikuwa katibu Mkuu wa Kanisa la Pentekoste Tanzania. Nilimfahamu kwa mara ya kwanza mwaka 2003, mwezi June, nilipohudhuria Camp iliyoandaliwa na NEW LIFE BAND ya jijini Arusha na kufanyikia katika shule ya Sekondari Moshi mkoani Kilimanjaro.

Nilibarikiwa na masomo yake ya Imani na jinsi alivyokuwa akiishi Imani yake. Baada ya kuaga dunia, nilifanikiwa kukisoma kitabu cha Historia ya maisha yake. Nimevutiwa na misimamo yake ya kiimani, kiasi cha kutokukubali kuwekewa mipaka ya kidhehebu.

Inasemekana, kupitia mafundisho yake, alichochea "uamsho" kwenye Makanisa yasiyokuwa ya Kipentekoste, kama Moravian, Anglikana, n.k. Huwa ninabarikiwa sana na wahubiri wanaolisambaza Neno la Mungu bila kuzingatia mipaka ya madhehebu yao. Msimamo wa Mabondo ulikuwa kwamba hakutumwa kuyahubiria madhehebu, bali kila kiumbe. Kwa hiyo alikuwa yupo tayari kuhubiri popote, bila kujali dhehebu litakalomwalika.

2. Dr. Mosses Kulola
Aliifanya huduma yake kwa uaminifu mkubwa sana. Hakuwa akitafuta maslahi yake binafsi. Alikuwa tayari kuhubiri hata katika mazingira magumu. Alikuwa ni mtu wa lengo moja tu maishani mwake, KUHUBIRI INJILI.

3. Mwl Christopher Mwakasege
Tokea aanze huduma, amekuwa "focused" kwenye hiyo huduma. Angeweza kufanya shughuli zingine za kiuchumi, hasa ukizingatia kuwa ni msomi wa Uchumi, lakini kwa kuwa ameukubali wito wa KULIFUNDISHA Neno la Mungu, ameamua kuachana na vingine vyote na kubaki na kimoja tu, huduma aliyoitiwa.

Kingine ninachompendea, ni tabia yake ya kutokuendekeza "udini". Timu ya huduma yake inadhihirisha hilo. Ina wahudumu kutoka madhehebu mablimbali yaliyopo Tanzania.

Kwa ufahamu wangu, yeye ni miongoni mwa wahubiri wachache walioweza kukivuka kiunzi cha udhehebu nchini Tanzania.

4. Mch. Elyona Kimaro
Japo sijamfuatilia sana, lakini kwa vipindi vyake vichache nilivyovitazama kupitia Upendo TV, amenibariki kwa kweli. Ni kiongozi mzuri. Kiongozi huona hitaji na kutafuta kulitimiza kabla ya kuambiwa. Ndivyo alivyofanya Kimaro kwenye Kanisa analoliongoza, ametafuta jinsi ya kukata kiu ya kiroho ya watu wake.

5. Dr. Augustine Mpemba
Ni Mtanzania anayeishi Marekani. Alikuwa Askofu wa Kanisa la TFE Jijini Mwanza, lakini sijui kama angali kiongozi wa hilo Kanisa kwa sasa. Nilishakisoma kitabu chake kimoja, na nilishasikiliza mtandaoni mafundisho yake kadhaa. Ana uelewa mpana wa mambo ya kiroho na kijamii. Madhalani, yupo vizuri sana kwenye masomo ya IMANI, masomo ambayo ni adimu sana katika Makanisa mengi ya Tanzania.

6. Prosper Ntepa
Sijawahi kusikiliza mahubiri yake, lakini nimevisoma vitabu kadhaa alivyoviandika. Kuna kimoja kinachohusiana na uponyaji, nilikipenda sana. Ni Mwalimu mzuri sana kwenye somo la Imani. Na kama ilivyo kwa tabia ya walimu wengi, yeye naye ni msomaji mzuri sana wa Vitabu.

7. Pastor Famous
Huyu ni Mchungaji wa Winners Chapel Jijini Mwanza. Nafikiri ni Mnigeria, alikuwa akiliongoza Kanisa la Winners Chapel lililopo Pasiansi jijini Mwanza. Sijui kama bado yupo pale au la.

8. Dr. Barnaba Mtokambali
Ni Askofu Mkuu wa TAG na pia ni Rais wa Makanisa ya Assemblies barani Afrika. Kama hiyo haitoshi, ni Mwenyekiti wa Makanisa ya Kipentekoste Tanzania.

Ana maono ya kiuongozi. Si bure CPCT wamempa Uenyekiti.

NB. Naweza nisiwe nakubaliana na kila kitu kwa baadhi ya hao watumishi wa Mungu, lakini kwa kuamua kuwataja kama miongoni mwa wahubiri wangu wa mfano, ni kwa sababu kuna maeneo wamenibariki.

Na, katika wahubiri woote, "my favourite" ni KENNETH HAGIN. Japo alishaaga dunia tokea mwaka 2003, vitabu vyake vimenisaidia sana , hasa katika eneo la IMANI.

Hatujawahi kukutana ana kwa ana, lakini kupitia vitabu vyake, amekuwa kama baba kwangu. Nimeshavisoma zaidi ya vitabu vyake hamsini. Nimeshavisoma karibia vitabu vyote alivyoviandika. Ni vichache sana ndiyo bado.

Tuwekee na wewe watumishi au viongozi wa dini unaowachukulia kama watumishi wa Mungu au viongozi wa mfano kwako.

Karibu!!!
Mzee wa Neema Pastor Ceasar Masisi

Anahuburi kweli ya Kristo
 
huyo Uebert Angel, umepotea. mwalimu wenu pia ni mhubiri mzuri ila huwa hajui hata anachohubiri kwasababu hajawahi kuexperience wokovu wa kweli. the same kwa kimaro. mwenye kuelewa ameelewa.
Uebert Angel alinijibu swali ambalo niliwauliza watalaamu wa theologia wakatoa majibu ambayo sijawahi kuridhika ,huyu mwamba alifundisha "the origin of God ".Toka nikiwa mdogo nilikuwa nauliza Mungu alitoka wapi na anakaa wapi.Huyu mwamba alijibu haya maswali mawili nikanyanyua mikono juu .
 
Back
Top Bottom