Wahubiri wangu wa mfano Tanzania

Wahubiri wangu wa mfano Tanzania

Kimsingi umewataja wa mtandaoni na wanaosikika sana kwenye media ila bado wapo watumishi wazuri tu humu duniani. Kuna mzee mmoja nilimkuta huko Iringa niliendaga na kuiishi kikazi mwezi mmoja huko Vijijini Dabaga nikawa naabudu kanisa la TAG Kilolo Christian Centre lipo pale Kilolo Wilayani Anaitwa Mzee Lucas Mkuye. Huyo ndio Mtume wa kwanza wa kweli kumuona maishani mwangu.

Mzee alianza huduma 1979 kipindi hiko ukanda wote wa Dabaga hauna kanisa lolote la kipentecoste na alikuwa akitembea kwa miguu hadi Mapanda huko Mufindi na akaanzisha na kusimamisha makanisa ya TAG ukanda huo. Zaidi ya makanisa 60 yametokea mikononi mwake.

Kwa Walutheri tunaoishi au kukulia ulutheri Morogoro au kwa wale tuliosoma Lutheran Junior Seminary miaka ya 1990's tuna mkumbuka Marehemu Mchungaji Hebert Hafferman. Huyu ndio Mtume wa Pili wa kweli kumuona kwa macho yangu achana na akina Bashando na Daudi Mashimo.

Mzee yule alikuwa mzungu na alikuja TZ miaka ya 1950's na alisambaza Ulutheri kwa kiasi kikubwa kwenye jamii ya kimasai. Aliwekeza kwenye huduma ya Neno na masuala ya kijamii ikiwemo kuwasomesha wamasai wengi wa Morogoro. Zao lake mmojawapo ni Richard Mameo Askofu wa Lutheran hapa Morogoro. R.I.P HEBERT HAFFERMAN, tutakutana katika pambazuko lile katika siku ile ya kalamu ya mwanakondoo.

Picha ya Marehemu mzee Hebert Hafferman akiwa na mtoto wa mchungaji mmoja wa Kimasai Marehemu Lucas.
View attachment 2818389
✅🙏🙏🙏
 
Mkuu, nilieleza kuwa hao niliowaweka ni ambao kwa namna Moja ama nyingine nimebarikiwa na huduma zao.

Nilivisoma vitabu kadhaa vya Uebert Angel, japo kuna baadhi ya mambo ambayo mwanzoni vilinitia mashaka kuhusu huduma yake, niliamua kupuuzia baada ya kubaini kuwa mentor wake ni Pastor Chris.

Pastor Chris naye nilikuwa nina mashaka naye, lakini mashaka yaliisha nilipogundua kuwa rafiki yake wa karibu ni Benny Hinn.

Hata Benny Hinn, nilikuja kumkubali vilivyo baada ya kugundua ukaribu alikokuwa nao na Reinhard Bonnke.

Unauona mnyororo ulivyo? Bonnke, Benny Hinn, Pastor Chris, Uebert Angel.

Lakini sivyo tu, huwa nina "falsafa" yangu kwa habari ya watumishi. Kwamba, katika mafundisho yao, nitatofautisha chuya na wali. Nikikutana na chuya, nitatema lakini wali nitaumeza.

"Sibugii" kila kitu kisemwacho na mtumishi. Nikijiridhisha kuwa akisemacho kipo nje ya Biblia, nakiweka kando nasubiria kingine.

Acha kumuhusisha Bonke na matapeli.
 
Acha kumuhusisha Bonke na matapeli.
Mkuu, fahamu kuwa imeandikwa, USIHUKUMU USIJE UKAHUKUMIWA.

Kama Bonnke aliamini kuwa Benny Hinn ni mtumishi wa Mungu, si vizuri wewe kumwita tapeli.

Angalia video Bonnke akimwombea Benny Hinn na mkewe.
 

Attachments

  • Reinhard_Bonnke_Prays_For_Benny_Hinn(240p).mp4
    15.5 MB
Fr Titus Amigu, namsikilizaga radio maria Tanzania , jamaa anahubiri na ana logic kubwa sana kwenye mafundisho yake.
Ni Mwandishi wa vitabu? Kama vile nilishawahi kukiona kitabu chake vile! Kilikuwa kama cha Kisaikolojia hivi.

Ni Mwandishi wa vitabu?
 
Kwa Mungu hakuna huyu mtumishi ndio Bora kuliko wengine. Mungu amempatia kila mmoja karama yake, na huwezi kushindanisha karama na kuanza kuwashindanisha watumishi.

Na mara nyingi tunapotoka kwa kulazimisha kwamba watumishi maarufu ndio waziri kuliko wengine. Mtumishi akisha kuwa na you tube channel au redio basi ndio anaitwa Bora.

Kuna siku nilikuwa nasikiliza Mwalimu Mwakasege, akasema Kuna siku Mchungaji wa Kanisa alimfuata akamwuliza , Kama Mwakasege akiwa kwenye ibada huwa anafuatilia mahubiri ya watumishi wengine. Mwakasege akamjibu kuwa huwa anafuatilia Sana na Kuna mambo mengi anayapata.

Point ya Mwakasege ni kwamba kila mtumishi kawekewa kitu chake tofauti hivyo huwezi kuanza kuwarank huyu ni Bora huyu sio Bora ( hii happy kwa manabii matapeli).

Mimi miaka ya Nyuma nilikuwa najua Askofu Kulola ndio mwanzilishi wa Upentekoste, ila nilipokuja kusoma historia ya Upentekoste nikagundua kumbe kulikuwa Kuna watumishi wakubwa miaka ya nyuma walioanzisha Upentekoste, tatizo hawakuwa maarufu.

Kwa mfano miaka ya 1935 kipindi Cha ukoloni kulikuwa na mwinjilisti mkubwa Sana alihubiri maeneo mengi Sana alikuwa anaitwa Harris Kapiga. Na wengine wengi akiwemo Mzee Andrea shimba ila hawakuwa maarufu. So nashauri tuachane na roho ya mashindano ndani ya kanisa , na kila mmoja afanye kwa kadri alivyopewa na Mungu.
 
Mkuu, fahamu kuwa imeandikwa, USIHUKUMU USIJE UKAHUKUMIWA.

Kama Bonnke aliamini kuwa Benny Hinn ni mtumishi wa Mungu, si vizuri wewe kumwita tapeli.

Angalia video Bonnke akimwombea Benny Hinn na mkewe.

Mkuu sio kwamba nahukumu. Tofautisha hukumu na maoni. Anayeweza kuhukumu ni Mungu tu. Hukumu maana yake kutoa maamuzi ya mwisho kwamba huyu anaenda motoni au mbinguni. Ndio maana hiyo kazi ya kuhukumu ni ya Mungu pekee sio mwanadamu.

Mwanadamu akisema Fulani haendi mbinguni, hiyo ni dhambi na atahukumiwa kwa kuingilia kazi ya Mungu maana yeye Hana mamlaka hayo. Mungu pekee ndio mwenye kuhukumu.

Mimi nimetoa maoni yangu ya kwamba usimhusishe Bonke na matapeli haikumaanisha kwamba Nina wahukumu Bali natoa maoni kwa jinsi ninavyowafahamu. Lazima ujue Benny Hinn na Pastor Chris waliwahi kuachana na wake zao kwa tuhuma mbalimbali, mke wa pastor Chris alidai mumewe ana mchepuko. Ndio maana nikawaita matapeli.

Mchungaji asiyeweza kuitunza ndoa yake utamwitaje?. Unanifundisha kuhusu ndoa wakati wewe umeshindwa kulinda ndoa yako?. Kwangu Mimi Bonke hafananii kuwa na hao watu. Halafu kuombea sio Jambo baya, unaweza kumwombea yeyote. Bonke amewahi kumwombea mtu aliyempinga kuhusu wokovu, sembuse kumuombea huyo Benny Hinn.

Bonke level zake ni akina Cerrullo, Billy Graham, Osborn, Don Double etc.
 
Kwa Mungu hakuna huyu mtumishi ndio Bora kuliko wengine. Mungu amempatia kila mmoja karama yake, na huwezi kushindanisha karama na kuanza kuwashindanisha watumishi.

Na mara nyingi tunapotoka kwa kulazimisha kwamba watumishi maarufu ndio waziri kuliko wengine. Mtumishi akisha kuwa na you tube channel au redio basi ndio anaitwa Bora.

Kuna siku nilikuwa nasikiliza Mwalimu Mwakasege, akasema Kuna siku Mchungaji wa Kanisa alimfuata akamwuliza , Kama Mwakasege akiwa kwenye ibada huwa anafuatilia mahubiri ya watumishi wengine. Mwakasege akamjibu kuwa huwa anafuatilia Sana na Kuna mambo mengi anayapata.

Point ya Mwakasege ni kwamba kila mtumishi kawekewa kitu chake tofauti hivyo huwezi kuanza kuwarank huyu ni Bora huyu sio Bora ( hii happy kwa manabii matapeli).

Mimi miaka ya Nyuma nilikuwa najua Askofu Kulola ndio mwanzilishi wa Upentekoste, ila nilipokuja kusoma historia ya Upentekoste nikagundua kumbe kulikuwa Kuna watumishi wakubwa miaka ya nyuma walioanzisha Upentekoste, tatizo hawakuwa maarufu.

Kwa mfano miaka ya 1935 kipindi Cha ukoloni kulikuwa na mwinjilisti mkubwa Sana alihubiri maeneo mengi Sana alikuwa anaitwa Harris Kapiga. Na wengine wengi akiwemo Mzee Andrea shimba ila hawakuwa maarufu. So nashauri tuachane na roho ya mashindano ndani ya kanisa , na kila mmoja afanye kwa kadri alivyopewa na Mungu.
1. Uko sahihi mkuu! Kwa Mungu wote ni sawa. Hakuna aliye bora kuliko mwingine.

2. Hakuna mtumishi anayejua kila kitu, hata Paulo kaandika, TUNAJUA KWA SEHEMU. Ndiyo maana ni hatari mtu kuamini kuwa ni Kanisani kwao pekee ndiko kuliko na mafundisho sahihi, na si sahihi sana kwa mtumishi kukataa kusikiliza mafundisho au kusoma vitabu vya watumishi wengine.

3. Hao niliowataja, simaanishi kuwa ndiyo bora kuliko wengine, ila ni ambao nimebarikiwa kupitia huduma zao. Na ujue, si kila mtumishi anaweza akawa msaada kwa kila mtu.

Paulo alipewa Injili ya wasiotahiriwa. Petro alipewa Injili ya waliotahiriwa. Kila mmoja alipewa watu wa kuwahudumia. Hata sasa, si kila mtumishi ni kwa ajili ya kila mtu. Inawezekana hao niliowataja ni miongoni mwa wale walio na "vitu" vyangu kutoka kwa Mungu.

Ukiona, kwa mfano, unavutiwa sana na mahubiri ya mtumishi fulani, inawezekana ni kwa sababu ana "kitu" chako. Ni muhimu kumfuatilia mtu kama huyo.

Lakini ukiona mtu mwingine havutiwi naye, usimhukumu. Inawezekana huyo si kwa ajili yake. Lakini akikutana na aliye na kitu chake, atavutiwa kumsikiliza.
 
Mkuu sio kwamba nahukumu. Tofautisha hukumu na maoni. Anayeweza kuhukumu ni Mungu tu. Hukumu maana yake kutoa maamuzi ya mwisho kwamba huyu anaenda motoni au mbinguni. Ndio maana hiyo kazi ya kuhukumu ni ya Mungu pekee sio mwanadamu.

Mwanadamu akisema Fulani haendi mbinguni, hiyo ni dhambi na atahukumiwa kwa kuingilia kazi ya Mungu maana yeye Hana mamlaka hayo. Mungu pekee ndio mwenye kuhukumu.

Mimi nimetoa maoni yangu ya kwamba usimhusishe Bonke na matapeli haikumaanisha kwamba Nina wahukumu Bali natoa maoni kwa jinsi ninavyowafahamu. Lazima ujue Benny Hinn na Pastor Chris waliwahi kuachana na wake zao kwa tuhuma mbalimbali, mke wa pastor Chris alidai mumewe ana mchepuko. Ndio maana nikawaita matapeli.

Mchungaji asiyeweza kuitunza ndoa yake utamwitaje?. Unanifundisha kuhusu ndoa wakati wewe umeshindwa kulinda ndoa yako?. Kwangu Mimi Bonke hafananii kuwa na hao watu. Halafu kuombea sio Jambo baya, unaweza kumwombea yeyote. Bonke amewahi kumwombea mtu aliyempinga kuhusu wokovu, sembuse kumuombea huyo Benny Hinn.

Bonke level zake ni akina Cerrullo, Billy Graham, Osborn, Don Double etc.
Bora tu sijakurupuka kukusahihisha kuhusu Don Double. Nilifikiri ulimmaanisha Don Gossett, ambaye kimsingi, ni kama mtoto wa kiroho wa E. W. Kenyon.

Nimejisahihisha. Don Double si Don Gossett.

Hao ni watu wawili tofauti ingawa wote ni watumishi wa Mungu.
 
Bishop Dicskon Kabigumila
Kijana yuko vizuri na anakuja speed anajua kulea
Anamiaka 33 tu ila ameshafanikiwa kusimamisha makanisa 7 mikoa tofauti tofauti

Siku utakayoanza kumsikiliza hutaacha kamwe
 
1. Uko sahihi mkuu! Kwa Mungu wote ni sawa. Hakuna aliye bora kuliko mwingine.

2. Hakuna mtumishi anayejua kila kitu, hata Paulo kaandika, TUNAJUA KWA SEHEMU. Ndiyo maana ni hatari mtu kuamini kuwa ni Kanisani kwao pekee ndiko kuliko na mafundisho sahihi, na si sahihi sana kwa mtumishi kukataa kusikiliza mafundisho au kusoma vitabu vya watumishi wengine.

3. Hao niliowataja, simaanishi kuwa ndiyo bora kuliko wengine, ila ni ambao nimebarikiwa kupitia huduma zao. Na ujue, si kila mtumishi anaweza akawa msaada kwa kila mtu.

Paulo alipewa Injili ya wasiotahiriwa. Petro alipewa Injili ya waliotahiriwa. Kila mmoja alipewa watu wa kuwahudumia. Hata sasa, si kila mtumishi ni kwa ajili ya kila mtu. Inawezekana hao niliowataja ni miongoni mwa wale walio na "vitu" vyangu kutoka kwa Mungu.

Ukiona, kwa mfano, unavutiwa sana na mahubiri ya mtumishi fulani, inawezekana ni kwa sababu ana "kitu" chako. Ni muhimu kumfuatilia mtu kama huyo.

Lakini ukiona mtu mwingine havutiwi naye, usinihukumu. Inawezekana huyo si kwa ajili yake. Lakini akikutana na aliye na kitu chake, atavutiwa kumsikiliza.

Ubarikiwe
 
Unamfahamu Aaron B. C. Mabondo? Hebu dadavua kidogo mkuu! Ni kati ya watumishi wa Mungu niliowakubali sana.

~ Alimpenda sana Mungu

~ Aliwaheshimu watumishi wenzake bila kujali utofauti wa madhehebu yao

~ Alikuwa mnyenyekevu sana

~ Alikuwa na imani katika NENO la Mungu. Japo hakuwa mtu wa media na hakupenda kujitangaza, kuna watu wengi walisaidika sana kupitia huduma yake, mfano:
1. Kumfufua Kanali wa JWTZ mkoani Arusha. Siku hiyo alikuwa Arusha katika Kanisa la KLPT Kaloleni alipopigiwa simu na mke wa marehemu ili akamsaidie kuupeleka mwili mochwari. Lakini alipofika, alimwamuru ainuke na ikawa hivyo, tena, akiwa hana hata chembe ya maumivu.

2. Dar Es Salaam nako pia alimfufua mtu.

3. Alipopelekwa hospitalini baada ya kivunjika mguu kwa ajali ya gari, daktari alipomwambia atakaa hospitalini mwezi mmoja alikataa. Alisema ana kazi nyingi hivyo atatoka baada ya siku tatu. Na kweli, siku ya tatu iligundulilka kuwa mguu ulishaunga na akaruhusiwa kwenda nyumbani.

Alikuwa ni mtu wa imani hasa. Alimwombea mwanamke aliyekuwa katolewa kizazi na hatimaye akaweza kubeba mimba, alimwombea muathirika wa VVU akapona, n.k.

Ukiweza, soma kitabu cha Historia yake, kinaitwa A WALK OF FAITH.
Aiseeh, wewe n mshirika wake?
 
Bora tu sijakurupuka kukusahihisha kumhusu Don Double. Nilifikiri ulimmaanisha Don Gossett, ambaye kimsingi, ni kama mtoto wa kiroho wa E. W. Kenyon.

Nimejisahihisha. Don Double si Don Gossett.

Hao ni watu wawili tofauti ingawa wote ni watumishi wa Mungu.

Kweli kabisa. Don Double zaidi yupo kwenye uinjilisti chini ya huduma ya Good News Crusade
 
Kwa Tanzania Mwl Mwakasege, nje ya Tanzania Chris Oyakhilome, na mwamba mmoja toka Ghana anaitwa Pastor Mensa Otabil. Huyu Otabil fanya kutafuta seminar zake YouTube ni [emoji91][emoji91]
Mensa aliwafundisha somo moja. 21 principles of success.

Ile ni course ambayo inatakiwa ifundishwe chuoni kwa miezi 3
 
Back
Top Bottom