Waimbaji kumi bora wa nyimbo za injili kuwahi kutokea hapa Tanzania mpaka sasa

Kiujumla kwa sasa hii huduma ya uimbaji imeingilia sana,watu wako kipesa zaidi kuliko utumishi...mtu anaalikwa kwenye mkutano wa injili anataja na kiwango cha kumpa,bila kujua NENO linasema mmepewa bure toeni bure,leo watu wanauza huduma ya Mungu...Mungu awabariki wale wote wanaofanya hii Huduma ktk Roho na kweli.
 
Wewe humfahamu Jangalasoni...huyu ni mtumishi wa Mungu ambaye ameimba ktk upako kwa miaka mingi kabla hajaondoka nchini,kizazi cha miaka ya 80' mpk 90' +2000 mwanzon kinamjua vzr
Video nilizoona YouTube anaonekana kijana mdogo. Aliimba tangu miaka ya 80? Basi itakuwa nimepishana naye.
 
Aliyoyapitia hayatupi sisi uhalali wa kum'judge..

Kila mtu ana mapito yake...tunaanguka ila Neema ya Mungu inatunyanyua tena....

Kwanza umeshausikiliza au kuuona wimbo wake wa 'Simba'? She is back like nothing happened.
"-Simbaa...anaungurumaaa-"Inasisimua na kufikirisha na kutia ujasiri pia.Kwangu ni gwiji wa Gospel Tanzania hii...

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 
Kuwepo kwenye imani thabiti ndani ya Kristo!!! Afu unaleta vituko?

1. Huyo Shusho amekuwa mfano mbovu kwa familia na huduma pia

2. Mwaipaja anaishi na mumewe wa ndoa?

Nadhani wote hawa wana makanisa kwa sasa, nani kamwita mwanamke afungue Kanisa?
 
Kuna waimbaji humo kawataji walishaachika kwenye ndoa za kikristo na wakaolewa tena.
 
Kuwepo kwenye imani thabiti ndani ya Kristo!!! Afu unaleta vituko?

1. Huyo Shusho amekuwa mfano mbovu kwa familia na huduma pia

2. Mwaipaja anaishi na mumewe wa ndoa?

Nadhani wote hawa wana makanisa kwa sasa, nani kamwita mwanamke afungue Kanisa?
Maisha binafsi ya mtu hakuna anayeweza kuyafahamu asilimia mia moja isipokuwa Mungu mwenyewe. Hapa tunaangalia general public life na kufuata maadili ya kikristo.

Kufungua kanisa? Hapa tutaenda kwenye theological arguments ambazo ni nje ya mjadala huu. Ndani ya Kristo hakuna myahudi wala myunani, mwanaume au mwanamke, wote ni mwili wa Kristo.
 
Kuna waimbaji humo kawataji walishaachika kwenye ndoa za kikristo na wakaolewa tena.
Kuachika kwenye ndoa ni jambo pana sana pengine linahitaji mjadala wake. Hata suala la kuoa/kuolewa upya nalo ni pana na lina theological perspectives nyingi hivyo tusiende sana huko.

Kifupi biblia imeruhusu kutengana na ukifanya hivyo ukae kwa kutulia. Na imeruhusu kumwacha yule anayeenda nje ya ndoa. Huyo ukitengana naye unaweza kuoa tena.

Msingi wa kanisa kukataa watu kuacha na kuoa upya upo zaidi kwenye kuelewa maana ya msamaha. Kwamba kama Mungu anatusamehe kila aina ya dhambi (of course isipokuwa kumkufuru Roho Mtakatifu) ni kwanini sisi nasi tusisamehe watu aina zote za dhambi?
 
1.Fanuel Sedekia
2.Cosmas Chidumule
3.Jangala Son
4.Paul Mwangosi
5.Abiudi Misholi.
6.Apostle Kyande(Kenya)
7.Ambwene Mwasongwe
8.Medrick Sanga
9.
10..........
Hao ni among the best!
 
Unaposema maisha binafsi unamaanisha nini? Yaani ndoa ni maisha binafsi? Na kama unaangalia maisha ya ujumla kwenye jamii basi hawa wanatakiwa maisha yao YAMHUBIRI KRISTO. Je wanafanya hivyo?

Halafu suala ala wanawake kuwa viongozi wala halihitaji theolojia yoyote, niaandiko tu yapo wazi kabisa. Hata hicho ulicho nukuu wala hakisemi hivyo, kina ujumbe tofauti kabisa. Kama ungependa ningefafanua kidogo lakini kwa kuwa umedai tutabadili mada basi naacha hivyo.
 
Katika ujumla wake ninaona maisha yao yanamhubiri Kristo. Hakuna jambo lolote la wazi ambalo linafahamika kiasi kwamba waweze kuhesabika kuwa hawafuati maadili ya kikristo.

Mkuu concept ya kuwa ndani ya Kristo haijaweza kutafsiriwa vyema na matokeo yake wengi wanaona wanaume na wanawake hawawezi kushika majukumu yanayofanana katika kanisa lakini hili sio sahihi. Pengine unaweza kuuleta huo mjadala tupeane elimu na kujengana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…