Waislam waruhusiwe kwenda Msikitini leo Ijumaa

Malaria 2

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2023
Posts
6,846
Reaction score
10,288
Baadhi ya waislam siku kama ya Leo saa 7 wapo ktk vikao badala ya kwenda msikitini . Saa 7 vikao visitishwe Vikao virudi tena saa 8 mpaka usiku wa manane
Baadhi ya mabosi huanzisha vikao siku kama ya Leo wakijua waislam wanatakiwa waende msikitini. Vikao vitoe fursa saa 7 msiktini saa 8 na kuendee virejee mezani.

"Enyi mlioamini! Iwapo mtaadhiniwa kwa ajili ya Swala siku ya Ijumaa, kimbilieni kumtaja Mwenyezi Mungu na acheni biashara. Hayo ni bora kwenu, ikiwa mnajua."
(Surat Al-Jumu'ah, 62:9)
 
Mbona siku za Jumamosi na Jumapili kuna matukio ya kiTaifa hufanyika?, mfano kesho na kesho kutwa nimesikia kuna mafunzo elekezi ya wasimamizi wa uchaguzi wa serikali za mitaa.

Hauoni hata hao waabudu Jumamosi na Jumapili watalalamika kwa nini ipangwe hivyo na siyo siku za katikari mwa juma?.

Wakoloni walituachia athari mbaya sana vichwani mwetu.
 
Wakiristo kwenda kanisani ni option. Muislam ni lazima kwenda msikitini
 
Kwani kuna anayewakataza kwenda kumuabudu allah ijumaa? Waende tu. Halafu we jamaa acha basi uchochezi wa kidini. Umewahi kusikia au kusoma wakristo wakijibagua na kutaka matakwa yao binafsi katikati ya jamii kubwa mchanganyiko nchini Tanzania? huo ni ubaguzi wa kidini na ni upuuzi na ushenzi
 
Umekasirika? Mbona ukiona neno islam unaumia sana? Halafu mbona unahasira? Uislam hata uuuchukie utakuwa tu
 
Waislam wenyewe wanasemaje kwani?
 
Nendeni acheni kulia lia....kila siku ni lawama na kulalamika tu. Nani kakukataza kwenda? Au wewe ulizaliwa njiti?kwa ulalamishi huu.
 
Ukishakuwa wa kulalama, kila siku na kila kitu utakilalamikia..!! LAST BORN
 
Dini.
Siasa.
Mpira.

Bora nijifungie ghetto nahesabu mavuzi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…