MAONI NA HITIMISHO
Sisi wote ni watoto wa Mungu, kwa tofauti zetu ukuu wa Mungu ndipo unapodhihirika Mungu amependa tuwe tofauti, ndiyo maana kuna warefu, wafupi, wembamba, wanene, weupe, weusi, wazungu, waafrika, waarabu, wachina na wahindi.
Wote tunafanya ibada na kumcha Mungu kwa namna tofauti na hilo ndilo kusudio lake Mungu, je kuna haja yoyote ya kujistahilisha mema au ukuu mbele za Mungu? Sisi wakristu tunaonywa kwamba, tusijifanyie utukufu.
Methew 23:12
Whoever exalt himself will be humbled and whoever humble himself will be exalted
Katika mantiki hii, na kwa kweli nimependa sana uzi huu, kwanza mtoa uzi anakumbusha umma wa kiislamu kutoa shukrani, kwa kuhifadhiwa kielimu na wakristu. Siyo jambo baya unapokarimiwa kutoa shukrani, lakini pili nimeona mtoa uzi ameweka sala nzuri sana ambayo na mimi nitachukua sehemu kidogo ili nianze kusali.
Naomba nikiri, ukiachilia tofauti ya lugha, lakini sala nyingi za kikristu na kiislamu zina maudhui yanayo fanana. Wakatoliki tunayo masifu ya asubuhi na jioni, na sehemu kubwa ni kuomba toba, reheme, fadhila na ridhiki kutoka kwa Mungu
Hakikia kipande hiki cha sala kitakua sehemu ya moja ya ibada zangu kila siku.
SALA YA KUMUOMBA MSAMAHA MWENYEZI MUNGU NA KUMSHUKURU 24/7
1. EWE MWENYEENZI MUNGU, MWINGI WA REHEMA,
NINAKUOMBA NDANI YA NAFSI YANGU, UNISAMEHE MAKOSA YANGU YOTE NIYOTENDA KWA KUJUA, AU KWA KUTOKUJUA.
EWE MWENYEEZI MUNGU, UNAYAJUA MAKOSA YANGU YOTE
NINAKUOMBA UNISAMEHE. (RUDIA MARA 19)
2. EWE MWENYEENZI MUNGU, MWINGI WA REHEMA
NINAKUSHUKURU KWA NEEMA ZAKO ZOTE JUU YANGU MIMI,
ULIZO NIJAALIA, UNAZO NIJAALIA NA UTAKAZO NIJAALIA.
EWE MWENYEENZI MUNGU KWA DHATI YA NAFSI YANGU, NINAKUSHUKURU. (RUDIA MARA 19)
SIKU YA JUMAMOSI
MUDA WA KUSWALI
USIKU: KUANZIA SAA 5:00 USIKU MPAKA SAA 11:00 ALFAJIR
MCHANA NI KUANZIA SAA 12:30 ASUBUHI MPAKA SAA 12:30 JIONI
Tuendelee kupendana na kushirikisha yale yalioyo meme, ili siku moja tukutane huko mbinguni, wote ni watoto wa Mungu hivyo hatuna budi kuishi tukipendana.