moi wa kitaa
JF-Expert Member
- May 3, 2015
- 931
- 940
Umejuaje!?Tukikaa kimya mnatutaka tuongee, tukiongea mnataka tukae kimya.
Ukweli ni kwamba mashehe wote wanamiliki majini. Muislamu asiyewasiliana na majini labda ni wa level ya chini.
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Umejuaje!?Tukikaa kimya mnatutaka tuongee, tukiongea mnataka tukae kimya.
Ukweli ni kwamba mashehe wote wanamiliki majini. Muislamu asiyewasiliana na majini labda ni wa level ya chini.
Swadakta Al habibShida ipo sehemu moja tu wakristo wengi hawana elimu juu ya uislam kwaiyo wanamezeshana propaganda sana juu ya uislam.
Lakini bado sioni tatizo kuitwa wafuga majini kama ufugi uwezi chukia kitu ukiona unakasilika ujue unayafuga.
Nimekaa tanga, tabora na lindi hivyo nafahamu kazi za mashehe kupunga pepo.Umejuaje!?
Endeleeni kufundishana wala msiogope.Kweli unaweza kusoma andiko na usielewe,hapa nawatahadharisha wakae mbali na majini nawe uelewa wako tufundishane tena?
Hapo ndo umedhihirisha kweli we ni konki mropokaji
Mwenyezi mungu ndio mjuzi zaidiMajini wanatupa utajiri bwashee, kwann tusishirikiane nao?
Wao pia ni viumbe wa Allah
Mbn wengine wanafuga kuku na ng'ombe?
Shukrani kwa darsa👏Kumekuwa na dhana kwamba waislamu wanafuga majini kitu ambacho si kweli kabisa na hata Dini hairuhusu hivyo.
Mwenyezi Mungu anasema hakuumba majini na watu Ila isipokuwa wamwabudu Mola wao,ebu tuangalie Maandiko;
((Nami sikuwaumba majini na watu ila waniabudu Mimi.))
51:56
Kwahiyo Majini na wanadamu waliumbwa Kwa lengo moja Tu la kumwabudu Mola wao na sio vinginevyo.
Lakini bahati mbaya Sana kuna baadhi ya waislamu ambao hushirikiana na majini katika mambo Yao,na hii sio waislamu Tu hata baadhi ya watu ambao sio waislamu hufanya hivyo pia,iwe Kwa kupiga ramli,kufanya miujiza huko kwenye nyumba za ibada na kadhalika.
Ila mazungumzo yangu Leo hapa nazungumza na waislamu, kuna baadhi ambao huwa na haya maruhani/majini ambayo wenyewe huyaita majini Waziri kwakuwa Tu yanawasaidia katika mambo Yao. Naomba niwaambie kuwa hakuna majini mazuri ambayo yanakaa mwilini mwa mtu hata kidogo,hayo ni mabaya na machafu,jini ambaye ameumbwa ili kumwabudu Mola wake hawezi kuja kufanya makazi katika mwili WA mtu kwakuwa hayo ni makosa na amekiuka sababu ya kuumbwa kwake kabisa.
Wanao mwabudu Mola wao wapo kwenye makazi Yao ya kijini na wanaendesha Maisha Yao huku wanamwabudu Mola wao,kwahiyo acheni kuwa watumwa WA hayo majini,kwani hakika mwisho wenu utakuwa sio mzuri.
Ebu tuangalie maongezi haya ya majini kama yalivyoelezwa katika Qur'an ;
((Na hakika walikuwako wanaume katika watu walio kuwa wakitafuta kujikinga kwa wanaume wa kijini; kwa hivyo wakawazidisha madhambi.))
72:6
Haya ni maongezi ya Majini baada ya kusikia Qur'an na kumwamini Mola wao,ndio wanahadithia kuwa kuna wanadamu wanaume ambao walikuwa wanatafuta hifadhi toka Kwa majini lakini matokeo yake wakazidishiwa madhambi. Na huo ndio ukweli kuna watu ambao wanaamini majini kuwa ndio watawalinda hapa duniani,na huwa hawafanyi Jambo lolote mpaka washaurieni na majini wao,hakika hiyo ni kufuru kubwa kumwamini kiumbe wa Mwenyezi Mungu kuwa ndio anakuwezesha kufanikiwa Kwa mambo hapa duniani.
Na mwisho wa siku shetani/ hayo majini machafu ambayo yameacha kusudio la kuumbwa kwao na kuja kushirikiana na wanadamu,mwisho wa siku yatawakana na kuwaambia ukweli, tuangalie Aya ifuatayo;
((Na Shet'ani atasema itapo katwa hukumu: Hakika Mwenyezi Mungu alikuahidini ahadi ya kweli. Nami nalikuahidini; lakini sikukutimizieni. Na sikuwa na mamlaka juu yenu, isipo kuwa nilikuiteni, nanyi mkaniitikia. Basi msinilaumu mimi, bali jilaumuni wenyewe. Mimi siwezi kuwa mtetezi wenu, wala nyinyi hamwezi kuwa watetezi wangu. Hakika mimi nilikataa tangu zamani kunishirikisha na Mwenyezi Mungu. Hakika madhaalimu watakuwa na adhabu chungu.))
14:22
Hakika kuna Aya nyingi Sana juu ya majini kuwapotosha wanadamu na kuwaingiza Motoni,kubwa ni kujua kwamba hakuna majini ambao wanatakiwa kushirikiana na binadamu kwani wao Wana Maisha Yao na wanadamu tuna yetu,ushirikiano wowote baina yetu ni upotovu na mwisho wake ni jehenamu.
Mambo mengi na Mda ni mchache!
Ni hayo Tu!
mwenyezi mungu anasema anayetaka maisha ya dunia atampa na atakuacha ujilie raha ya mchongo ya dunia ila tambua ahera huna chako, kupanga ni kuchagua mkuuMajini wanatupa utajiri bwashee, kwann tusishirikiane nao?
Wao pia ni viumbe wa Allah
Mbn wengine wanafuga kuku na ng'ombe?
Aaah kasema wapi hii?mwenyezi mungu anasema anayetaka maisha ya dunia atampa na atakuacha ujilie raha ya mchongo ya dunia ila tambua ahera huna chako..kupanga ni kuchagua mkuu
Mimi nna Rafiki yangu wa kijini, ila yeye Ni wa ibada Sana, na hakai mwilini mwangu, ila huwa anakuja kwa umbo la kibidamu baadae anatoweka, Ni mshakaji tunapiga story Sana, kila alhamisi ndio inakuwa siku yake yakuja kibindamu ,na ijumaa, nimeegundua kumbe chakula chao Ni mifupa pia,na mabaki ya vyakula walioacha binadamu baadhiNi Kama dhambi zingine tu,ukute anayeshitikiana na jinni hanywi pombe,hazini,hachezi kamari...Ila hakuna uchawi usiohusisha jinni,wengine wanaita mizimu,Ila ndiyo jinni haohao
Majini Kama ilivyo binadamu, Kuna wema na wabayaSi tulikubaliana kuna majini wazuri na wabaya..leo wewe unasema majini wote wabaya..utakua muislamu wa mchongo wewe.
#MaendeleoHayanaChama
Asalam alaykumMimi nna Rafiki yangu wa kijini, ila yeye Ni wa ibada Sana, na hakai mwilini mwangu, ila huwa anakuja kwa umbo la kibidamu baadae anatoweka, Ni mshakaji tunapiga story Sana, kila alhamisi ndio inakuwa siku yake yakuja kibindamu ,na ijumaa, nimeegundua kumbe chakula chao Ni mifupa pia,na mabaki ya vyakula walioacha binadamu baadhi
Majini wazur na wabaya Kwa matendo Yao ni wao katika Maisha Yao, kuna wema na wabaya kama binadamu.Si tulikubaliana kuna majini wazuri na wabaya..leo wewe unasema majini wote wabaya..utakua muislamu wa mchongo wewe.
#MaendeleoHayanaChama
Huo mtihani ndugu yangu, lazima mtakuwa na mapatano FulaniMimi nna Rafiki yangu wa kijini, ila yeye Ni wa ibada Sana, na hakai mwilini mwangu, ila huwa anakuja kwa umbo la kibidamu baadae anatoweka, Ni mshakaji tunapiga story Sana, kila alhamisi ndio inakuwa siku yake yakuja kibindamu ,na ijumaa, nimeegundua kumbe chakula chao Ni mifupa pia,na mabaki ya vyakula walioacha binadamu baadhi
Mimi huwa mkweli katika Jambo la ukweli,sikatai kwamba hakuna masheikh ambao wanafanya hivyo,wapo na hao ni Wale wanao fanya uganga.Nimekaa tanga, tabora na lindi hivyo nafahamu kazi za mashehe kupunga pepo.