Wajamaa mnisaidie, hivi Nyerere aliwezaje kuvumilia haya?

Wajamaa mnisaidie, hivi Nyerere aliwezaje kuvumilia haya?

Mifumo siyo tatizo, tatizo ni matokeo na jinsi watawala wanavyoyapokea. Ilifahamika kabisa kwamba Tanzania haiwezi kujikwamua kiuchumi bila wananchi kuwa na hisa kwenye uchumi wao. Tunasingizia vita vya Kagera, ila ukweli ni kwamba Tanzania ilianza kuumia miaka ya 70's kipindi kina Mtei wanamshauri Nyerere lakini hataki kusikia. Kukosea viongozi wote duniani hukosea, tatizo huja pale ambapo kiburi chako cha kukataa matokeo kinagharimu maisha ya mamilioni ya watu waliokuwa wanakuamini.

Hivi kwanini hakukubali mapema kwamba nchi ilimshinda hadi asubiri jeshi na waasi wamtumie ujumbe kwamba amechokwa ?​
Hulka ya Baba wa taifa ilikuwa ya ujuaji zaidi, ndio maana walimuita "Bwana haambiliki"hii ililetwa na tabia yake ya kuto sikiliza ushauri wa mtu,bali maono yake tu,kinyume na hapo ni tatizo kubwa sana.Mpaka kufikia hatua ya watu kuwekwa vizuizini na wengine kukimbia taifa hali ilikuwa mbaya sana.
 
Huwa najiuliza sana lakini sipati majawabu, lakini naomba wasomi wa humu ndani mnisaidie.

Hivi Mzee Nyerere alikuwa ana roho ya namna gani kuona mambo kama haya yakitokea kwa wananchi lakini bado hataki kubadilika na akaendelea kutumia mkono wa chuma kuhakikisha anasigina kabisa uwezo binafsi wa mtanzania kuweza kujikwamua kiuchumi. Ujamaa wa Tanzania hakuleta matokeo yoyote makubwa na ya kuchangaza ukilinganisha na kule Asia na Ulaya ambako walau walifanya mapinduzi ya sayansi na teknolojia.

Uchina walifanikiwa sana baada ya Raisi Deng Xiaping kuanza kuwaonea huruma raia wake akifahamu kabisa kwamba njia waliyokuwa wanaenda ilikuwa siyo sahihi. Aliruhusu watu waanze kumiliki mali zao binafsi na kufanya biashara. Najiuliza sana, miaka yote 18 ya Ujamaa, yalifanyika na kutokea mambo mengi mno kwa watanzania, kiasi kwamba kiongozi yoyote mwenye huruma na wananchi ni lazima angekaa chini na kujifanyia tathmini, lakini Raisi Nyerere hakufanya hivyo, aliendelea kuwa na moyo mgumu kama Farao. Hebu tuzingatie haya:

1. Sera ya utaifishaji wa mali, ilileta umasikini mkubwa sana kwa watu.
2. Kufuta vikundi ya ushirika (Cooperatives) na kuweka vile vya TANU kulididimiza mno sekta ya kilimo.
3. Kupiga marufuku watu binafsi kuagiza bidhaa nje ya Tanzania kulipelekea uhaba wa bidhaa na huduma muhimu.
4. Kuweka ugumu katika kusafiri (Travelling Restrictions) kulisababisha ukosefu wa ujuzi kwa watanzania.
5. Kuminya uhuru wa mawazo na kutumia nguvu ya dola kunyamazisha watu kulidumaza ukomavi wa demokrasia.

Mpaka kufika miaka ya 80's Ujamaa ulikuwa umefeli vibaya mno. Tanzania tulikuwa hatuna hata unga wa kupikia, mafuta, wala sukari. Mtaa mzima mlikuwa mnaenda kwa mwenyekiti kuomba sukari au sabuni kutoka maduka ya ushirika. Ukikamatwa na mafuta, sabuni au dawa za binadamu zilizolanguliwa kutoka Kenya lazima ushughulikiwe na dola. Kama ulisoma miaka ya 80's unaweza kukumbuka kwamba hata sare za shule zilikosa rangi, watu tukawa tunavaa vitu vya ajabu vilivyochakaa kama vile vichaa. Ukibahatika kukutana na wamishionari au taasisi za kidini ndiyo ulikuwa unaweza kupewa hata nguo, mahitaji na wazungu.

Yote haya yanafanyika, Mzee Nyerere na Sokoine wakaingia mtaani kuanza kushughulikia maelfu ya watanzania ambao wanahujumu uchumi. Ila ukifuatilia zile kesi nyingi, utafahamu kwamba hao wahujumu uchumi ni wale watanzania wenye akili za haraka ambao walijiongeza na kuweza kupata mahitaji muhimu ili kuhudumia familia zao. Wahujumu uchumi kwelikweli, ambao wengi walikuwa ni vigogo wa serikalini hawakuguswa. Kiukweli, kama nchi ina kiongozi mwenye huruma haya yote yasingetokea bila yeye kujirudi.

Hivi kwanini MTAKATIFU na MWENYEHERI, Raisi Nyerere hakuwa na chembe ya huruma moyoni ?
Kuna mambo nikikumbuka huwa naumia sana na nakosa majawabu. Hivi alikuwa anapenda kutuona sisi vile ?​
Kule kwnye history

Point zilikuwa kama ifuatavyo

Poor science and technology in simplifying the process of renewals

ideological from other leaders


imitate without being sure in the revolution so that we destroy the confusion

Nyerere's knowledge in everything...here he saw himself as knowing everything in the country, even his advisors were considered fools

Wazee wa history mnirekebishe



Sent from my SM-A047F using JamiiForums mobile app
 
Sawa kabisa ila hii ni history lazima ipewe hakiyake watu wajue nini kilikuwa kinaendelea ilikuwa kama Misukule watanzania suruali viraka viatu matairi ya gari. Hakika inasikitisha..
Ukiwaambia watu hili, wengi wanaweza wasiamini. Nguo za viraka, makobaz, kupanga mstari kununua sukari, halafu hapo bado bwana Moringe hajakusweka ndani kisa tuhuma za uhujumu uchumi. Kuna baadhi ya mambo tulikosewa na kunyanyaswa mno sisi watanzania. Hivi hadi chakula uende ukaombe kwa Mwenyekiti kweli ?​
 
Huwa najiuliza sana lakini sipati majawabu, lakini naomba wasomi wa humu ndani mnisaidie.

Hivi Mzee Nyerere alikuwa ana roho ya namna gani kuona mambo kama haya yakitokea kwa wananchi lakini bado hataki kubadilika na akaendelea kutumia mkono wa chuma kuhakikisha anasigina kabisa uwezo binafsi wa mtanzania kuweza kujikwamua kiuchumi. Ujamaa wa Tanzania hakuleta matokeo yoyote makubwa na ya kuchangaza ukilinganisha na kule Asia na Ulaya ambako walau walifanya mapinduzi ya sayansi na teknolojia.

Uchina walifanikiwa sana baada ya Raisi Deng Xiaping kuanza kuwaonea huruma raia wake akifahamu kabisa kwamba njia waliyokuwa wanaenda ilikuwa siyo sahihi. Aliruhusu watu waanze kumiliki mali zao binafsi na kufanya biashara. Najiuliza sana, miaka yote 18 ya Ujamaa, yalifanyika na kutokea mambo mengi mno kwa watanzania, kiasi kwamba kiongozi yoyote mwenye huruma na wananchi ni lazima angekaa chini na kujifanyia tathmini, lakini Raisi Nyerere hakufanya hivyo, aliendelea kuwa na moyo mgumu kama Farao. Hebu tuzingatie haya:

1. Sera ya utaifishaji wa mali, ilileta umasikini mkubwa sana kwa watu.
2. Kufuta vikundi ya ushirika (Cooperatives) na kuweka vile vya TANU kulididimiza mno sekta ya kilimo.
3. Kupiga marufuku watu binafsi kuagiza bidhaa nje ya Tanzania kulipelekea uhaba wa bidhaa na huduma muhimu.
4. Kuweka ugumu katika kusafiri (Travelling Restrictions) kulisababisha ukosefu wa ujuzi kwa watanzania.
5. Kuminya uhuru wa mawazo na kutumia nguvu ya dola kunyamazisha watu kulidumaza ukomavi wa demokrasia.

Mpaka kufika miaka ya 80's Ujamaa ulikuwa umefeli vibaya mno. Tanzania tulikuwa hatuna hata unga wa kupikia, mafuta, wala sukari. Mtaa mzima mlikuwa mnaenda kwa mwenyekiti kuomba sukari au sabuni kutoka maduka ya ushirika. Ukikamatwa na mafuta, sabuni au dawa za binadamu zilizolanguliwa kutoka Kenya lazima ushughulikiwe na dola. Kama ulisoma miaka ya 80's unaweza kukumbuka kwamba hata sare za shule zilikosa rangi, watu tukawa tunavaa vitu vya ajabu vilivyochakaa kama vile vichaa. Ukibahatika kukutana na wamishionari au taasisi za kidini ndiyo ulikuwa unaweza kupewa hata nguo, mahitaji na wazungu.

Yote haya yanafanyika, Mzee Nyerere na Sokoine wakaingia mtaani kuanza kushughulikia maelfu ya watanzania ambao wanahujumu uchumi. Ila ukifuatilia zile kesi nyingi, utafahamu kwamba hao wahujumu uchumi ni wale watanzania wenye akili za haraka ambao walijiongeza na kuweza kupata mahitaji muhimu ili kuhudumia familia zao. Wahujumu uchumi kwelikweli, ambao wengi walikuwa ni vigogo wa serikalini hawakuguswa. Kiukweli, kama nchi ina kiongozi mwenye huruma haya yote yasingetokea bila yeye kujirudi.

Hivi kwanini MTAKATIFU na MWENYEHERI, Raisi Nyerere hakuwa na chembe ya huruma moyoni ?
Kuna mambo nikikumbuka huwa naumia sana na nakosa majawabu. Hivi alikuwa anapenda kutuona sisi vile ?​
Ndio maana tuko hapa tulipo.....Nyerere alijali san Tanu kuliko Tanzania
 
Huwa najiuliza sana lakini sipati majawabu, lakini naomba wasomi wa humu ndani mnisaidie.

Hivi Mzee Nyerere alikuwa ana roho ya namna gani kuona mambo kama haya yakitokea kwa wananchi lakini bado hataki kubadilika na akaendelea kutumia mkono wa chuma kuhakikisha anasigina kabisa uwezo binafsi wa mtanzania kuweza kujikwamua kiuchumi. Ujamaa wa Tanzania hakuleta matokeo yoyote makubwa na ya kuchangaza ukilinganisha na kule Asia na Ulaya ambako walau walifanya mapinduzi ya sayansi na teknolojia.

Uchina walifanikiwa sana baada ya Raisi Deng Xiaping kuanza kuwaonea huruma raia wake akifahamu kabisa kwamba njia waliyokuwa wanaenda ilikuwa siyo sahihi. Aliruhusu watu waanze kumiliki mali zao binafsi na kufanya biashara. Najiuliza sana, miaka yote 18 ya Ujamaa, yalifanyika na kutokea mambo mengi mno kwa watanzania, kiasi kwamba kiongozi yoyote mwenye huruma na wananchi ni lazima angekaa chini na kujifanyia tathmini, lakini Raisi Nyerere hakufanya hivyo, aliendelea kuwa na moyo mgumu kama Farao. Hebu tuzingatie haya:

1. Sera ya utaifishaji wa mali, ilileta umasikini mkubwa sana kwa watu.
2. Kufuta vikundi ya ushirika (Cooperatives) na kuweka vile vya TANU kulididimiza mno sekta ya kilimo.
3. Kupiga marufuku watu binafsi kuagiza bidhaa nje ya Tanzania kulipelekea uhaba wa bidhaa na huduma muhimu.
4. Kuweka ugumu katika kusafiri (Travelling Restrictions) kulisababisha ukosefu wa ujuzi kwa watanzania.
5. Kuminya uhuru wa mawazo na kutumia nguvu ya dola kunyamazisha watu kulidumaza ukomavi wa demokrasia.

Mpaka kufika miaka ya 80's Ujamaa ulikuwa umefeli vibaya mno. Tanzania tulikuwa hatuna hata unga wa kupikia, mafuta, wala sukari. Mtaa mzima mlikuwa mnaenda kwa mwenyekiti kuomba sukari au sabuni kutoka maduka ya ushirika. Ukikamatwa na mafuta, sabuni au dawa za binadamu zilizolanguliwa kutoka Kenya lazima ushughulikiwe na dola. Kama ulisoma miaka ya 80's unaweza kukumbuka kwamba hata sare za shule zilikosa rangi, watu tukawa tunavaa vitu vya ajabu vilivyochakaa kama vile vichaa. Ukibahatika kukutana na wamishionari au taasisi za kidini ndiyo ulikuwa unaweza kupewa hata nguo, mahitaji na wazungu.

Yote haya yanafanyika, Mzee Nyerere na Sokoine wakaingia mtaani kuanza kushughulikia maelfu ya watanzania ambao wanahujumu uchumi. Ila ukifuatilia zile kesi nyingi, utafahamu kwamba hao wahujumu uchumi ni wale watanzania wenye akili za haraka ambao walijiongeza na kuweza kupata mahitaji muhimu ili kuhudumia familia zao. Wahujumu uchumi kwelikweli, ambao wengi walikuwa ni vigogo wa serikalini hawakuguswa. Kiukweli, kama nchi ina kiongozi mwenye huruma haya yote yasingetokea bila yeye kujirudi.

Hivi kwanini MTAKATIFU na MWENYEHERI, Raisi Nyerere hakuwa na chembe ya huruma moyoni ?
Kuna mambo nikikumbuka huwa naumia sana na nakosa majawabu. Hivi alikuwa anapenda kutuona sisi vile ?​
Nyerere aliondoka madarakani mwaka 1985 baada ya kuwa madarakani kwa miaka 24 wakati wa vita baridi. Leo hii ni miaka zaidi ya 38 tangu aondoke madarakani, na vita baridi ilikufa takriban miaka 32 iliyopita. Dunia imebadilika sana baada ya vita baridi kuisha na ukuaji wa information technology. Kwa nini una interest na revisionisim ya mambo ambayo siyo relevant ten katika dunia ya leo?
 
Ukiwaambia watu hili, wengi wanaweza wasiamini. Nguo za viraka, makobaz, kupanga mstari kununua sukari, halafu hapo bado bwana Moringe hajakusweka ndani kisa tuhuma za uhujumu uchumi. Kuna baadhi ya mambo tulikosewa na kunyanyaswa mno sisi watanzania. Hivi hadi chakula uende ukaombe kwa Mwenyekiti kweli ?​
Mkuu wanaokumbuka adha hiyo ni wachache, na hao ni wale walioishi na kukulia mijini na hasa jiji la Dar es salaam.
Wengi wenye umri kama wako wakati huo walikuwa shule vijijini, ambako vyakula walikuwa wanalima wenyewe.
Na vitu kama dawa ya meno, siagi, sabuni, sukari, kandambili nk kwenye maeneo ya vijijini vilikuwa ni anasa tu. Hawakuhisi adha ya kukosekana kwake.
Vinginevyo wangekuelewa unasema nini.

Binafsi sijasahau mateso niliyopitia nikiwa mvulana mdogo kufuatilia gari ya ugawaji kwenye mitaa niliyoishi.
Kwenye foleni ya kupata bidhaa adimu na muhimu tulikuwa tunapanga mawe kusubiri gari.
Haya yalisababishwa na sera mbaya za ujamaa na utekelezaji wake kupitia Azimio la Arusha.
 
Nyerere alikuwa ni mtu mwenye utu,kipindi cha msiba wake Maalim Seif alinukuliwa akisema Mwl alikuwa ni mkweli.Sasa jiulize yule mliyekuwa mnamuona alionewa na mwl anasema alikua mkweli which means ni kama ali-REGRET kuhusu ugomvi wao.Kushindwa kwa ujamaa dhidi ya ubepari ni sawa na kushindwa kwa utu dhidi ya unyama na kuonesha kwamba hakukubaliana na ubepari aling'atuka ili asiingize nchi matatizoni kwa shinikizo la wenye makucha(aliipenda nchi yake)kipi cha ajabu cha sasa hivi ukiachana teknolojia ambayo ni lazima tucheze nayo?
 
Sikuwepo duniani kipindi cha Nyerere,lakini kupitia maandiko mbalimbali unaweza kuona utawala ule ulikua na ahueni kwa wananchi licha ya changamoto mbalimbali zilizojitokeza.waliokuwepo enzi hizo wanasema hakukua na mgao wa umeme,elimu ilikua bora zaidi,huduma mbalimbali za kijamii pamoja na kwamba zilikua chache lakini zilitolewa kwa wakati na bila upendeleo wowote na tena kwa kiwango cha juu, utu wa Mtanzania ulikua ni kipaumbele cha serikali, serikali iliwajibika kisawasawa.je tujiulize miaka 38 sasa tangu Nyerere atoke madarakani zaidi ya kuongezeka majengo marefu kwenye miji mikubwa kama Dar nini cha maana serikali zilizopita zimefanya ambacho hakikufanywa na serikali ile ya Nyerere?
 
Back
Top Bottom