denoo JG
JF-Expert Member
- Oct 27, 2023
- 2,701
- 9,759
Kiongozi lazima awe na principles zake, kusimamia kile anachokiamini mpaka mwisho, kiongozi asiye na msimamo ndie chanzo cha kuyumba kwa taifa lolote hapa duniani, leo atashika hiki atakiacha, kesho atashika kile nacho atakiacha...
Kulalamika miaka yote ya Nyerere kuwepo madarakani halafu bado hali ya maisha ya mtanzania ikaendelea kuwa mbaya, kwangu sioni kama kuna mantiki yoyote, kwasababu siku zote mabadiliko hayaji kwa usiku mmoja, ni mchakato.
Sasa ndani ya kipindi hicho cha mchakato ndicho kinamfanya kiongozi aendelee kusimamia kile anachokiamini, akiamini atafikia malengo, kama kikija kuwa na matokeo tofauti hayo ni mambo ya kibinadamu, kwamba alikosea, na ndio maana akawapisha wengine.
- Lakini unaposema Nyerere hakuwa na huruma na watu wake unakosea, alikuwa na huruma kupitiliza.
1. Hakujilimbikizia mali yoyote, licha ya madini na kila aina ya rasilimali tulizonazo.
2. Aliwahi kukaririwa akisema; "kiongozi unapita barabarani, unaona hali ya mtanzania ilivyo mbaya, unajua hili ni jukumu langu kumuondoa hapo alipo".
3. Hakuna hata mtoto wake mmoja tunayesikia amewahi kuhusishwa na wizi/ufisadi wa aina yoyote.
Mpaka hapo naamini utapata picha Nyerere alikuwa kiongozi wa aina gani, kwamba licha ya sera yake ya ujamaa kufeli, lakini dhamira ya dhati ya kumkomboa mtanzania toka kwenye lindi la umasikini alikuwa nayo tofauti na ulivyoandika.
Above all, hivi umewahi kujiuliza baada ya Nyerere kuondoka madarakani nini kilifuatia?
Kilichofuatia ndicho kile ambacho Nyerere alikipiga vita na wewe unaonekana kukifurahia, binafsi nchi hii naamini hakuna mabadiliko yoyote ya maana kiuchumi zaidi ya kuwepo pengo kubwa kati ya walio nacho na wasio nacho, hili Nyerere na Sokoine ndio walikuwa wakilipinga.
- Hii kwangu ni sawa na kusema, licha ya kumuona Nyerere alifeli, lakini hata hao waliofuatia baada yake nao wamefeli pia, hatuna cha maana cha kujivunia, mgao wa umeme, ukosefu wa maji safi na salama, wanafunzi kukosa matundu ya vyoo shuleni na madawati, mambo ni mengi...
Labda uniambie tu kwa sasa unafurahia uwepo wa unga, sabuni, mchele na mahitaji mengineyo mitaani, lakini ukweli wa mambo ni kwamba, licha ya uwepo wa vitu hivyo, bado hali ya mtanzania kiuchumi ni mbaya na ndio maana mpaka leo bado wapo ndugu zetu vijijini wakisubiri kampeni zianze, ili wagaiwe t-shirts na kofia za CCM ziwastiri.
Hivyo kwangu, kumlaumu Nyerere kwa kufeli bila ya kunionesha yule aliyefaulu hapa ndani kwetu sikuelewi, na kutumia mifano ya nje kumhukumu Nyerere bila kunionesha nani aliyefuatia wa hapa ndani akafaulu, umemuonea, that's unfair comparison.
Unless uniambie mahitaji yetu siku zote yangebaki yale yale ya unga, mchele na sabuni kupatikana madukani, jambo ambalo kwangu halina mantiki, naamini mahitaji hubadilika kulingana na wakati, na pale unaposhindwa kuwapa watu wako kile wanachohitaji kwa wakati husika, basi umefeli, there is no way out.
Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
Kulalamika miaka yote ya Nyerere kuwepo madarakani halafu bado hali ya maisha ya mtanzania ikaendelea kuwa mbaya, kwangu sioni kama kuna mantiki yoyote, kwasababu siku zote mabadiliko hayaji kwa usiku mmoja, ni mchakato.
Sasa ndani ya kipindi hicho cha mchakato ndicho kinamfanya kiongozi aendelee kusimamia kile anachokiamini, akiamini atafikia malengo, kama kikija kuwa na matokeo tofauti hayo ni mambo ya kibinadamu, kwamba alikosea, na ndio maana akawapisha wengine.
- Lakini unaposema Nyerere hakuwa na huruma na watu wake unakosea, alikuwa na huruma kupitiliza.
1. Hakujilimbikizia mali yoyote, licha ya madini na kila aina ya rasilimali tulizonazo.
2. Aliwahi kukaririwa akisema; "kiongozi unapita barabarani, unaona hali ya mtanzania ilivyo mbaya, unajua hili ni jukumu langu kumuondoa hapo alipo".
3. Hakuna hata mtoto wake mmoja tunayesikia amewahi kuhusishwa na wizi/ufisadi wa aina yoyote.
Mpaka hapo naamini utapata picha Nyerere alikuwa kiongozi wa aina gani, kwamba licha ya sera yake ya ujamaa kufeli, lakini dhamira ya dhati ya kumkomboa mtanzania toka kwenye lindi la umasikini alikuwa nayo tofauti na ulivyoandika.
Above all, hivi umewahi kujiuliza baada ya Nyerere kuondoka madarakani nini kilifuatia?
Kilichofuatia ndicho kile ambacho Nyerere alikipiga vita na wewe unaonekana kukifurahia, binafsi nchi hii naamini hakuna mabadiliko yoyote ya maana kiuchumi zaidi ya kuwepo pengo kubwa kati ya walio nacho na wasio nacho, hili Nyerere na Sokoine ndio walikuwa wakilipinga.
- Hii kwangu ni sawa na kusema, licha ya kumuona Nyerere alifeli, lakini hata hao waliofuatia baada yake nao wamefeli pia, hatuna cha maana cha kujivunia, mgao wa umeme, ukosefu wa maji safi na salama, wanafunzi kukosa matundu ya vyoo shuleni na madawati, mambo ni mengi...
Labda uniambie tu kwa sasa unafurahia uwepo wa unga, sabuni, mchele na mahitaji mengineyo mitaani, lakini ukweli wa mambo ni kwamba, licha ya uwepo wa vitu hivyo, bado hali ya mtanzania kiuchumi ni mbaya na ndio maana mpaka leo bado wapo ndugu zetu vijijini wakisubiri kampeni zianze, ili wagaiwe t-shirts na kofia za CCM ziwastiri.
Hivyo kwangu, kumlaumu Nyerere kwa kufeli bila ya kunionesha yule aliyefaulu hapa ndani kwetu sikuelewi, na kutumia mifano ya nje kumhukumu Nyerere bila kunionesha nani aliyefuatia wa hapa ndani akafaulu, umemuonea, that's unfair comparison.
Unless uniambie mahitaji yetu siku zote yangebaki yale yale ya unga, mchele na sabuni kupatikana madukani, jambo ambalo kwangu halina mantiki, naamini mahitaji hubadilika kulingana na wakati, na pale unaposhindwa kuwapa watu wako kile wanachohitaji kwa wakati husika, basi umefeli, there is no way out.
Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app