Wajamaa mnisaidie, hivi Nyerere aliwezaje kuvumilia haya?

Wajamaa mnisaidie, hivi Nyerere aliwezaje kuvumilia haya?

Kiongozi lazima awe na principles zake, kusimamia kile anachokiamini mpaka mwisho, kiongozi asiye na msimamo ndie chanzo cha kuyumba kwa taifa lolote hapa duniani, leo atashika hiki atakiacha, kesho atashika kile nacho atakiacha...

Kulalamika miaka yote ya Nyerere kuwepo madarakani halafu bado hali ya maisha ya mtanzania ikaendelea kuwa mbaya, kwangu sioni kama kuna mantiki yoyote, kwasababu siku zote mabadiliko hayaji kwa usiku mmoja, ni mchakato.

Sasa ndani ya kipindi hicho cha mchakato ndicho kinamfanya kiongozi aendelee kusimamia kile anachokiamini, akiamini atafikia malengo, kama kikija kuwa na matokeo tofauti hayo ni mambo ya kibinadamu, kwamba alikosea, na ndio maana akawapisha wengine.

- Lakini unaposema Nyerere hakuwa na huruma na watu wake unakosea, alikuwa na huruma kupitiliza.

1. Hakujilimbikizia mali yoyote, licha ya madini na kila aina ya rasilimali tulizonazo.

2. Aliwahi kukaririwa akisema; "kiongozi unapita barabarani, unaona hali ya mtanzania ilivyo mbaya, unajua hili ni jukumu langu kumuondoa hapo alipo".

3. Hakuna hata mtoto wake mmoja tunayesikia amewahi kuhusishwa na wizi/ufisadi wa aina yoyote.

Mpaka hapo naamini utapata picha Nyerere alikuwa kiongozi wa aina gani, kwamba licha ya sera yake ya ujamaa kufeli, lakini dhamira ya dhati ya kumkomboa mtanzania toka kwenye lindi la umasikini alikuwa nayo tofauti na ulivyoandika.

Above all, hivi umewahi kujiuliza baada ya Nyerere kuondoka madarakani nini kilifuatia?

Kilichofuatia ndicho kile ambacho Nyerere alikipiga vita na wewe unaonekana kukifurahia, binafsi nchi hii naamini hakuna mabadiliko yoyote ya maana kiuchumi zaidi ya kuwepo pengo kubwa kati ya walio nacho na wasio nacho, hili Nyerere na Sokoine ndio walikuwa wakilipinga.

- Hii kwangu ni sawa na kusema, licha ya kumuona Nyerere alifeli, lakini hata hao waliofuatia baada yake nao wamefeli pia, hatuna cha maana cha kujivunia, mgao wa umeme, ukosefu wa maji safi na salama, wanafunzi kukosa matundu ya vyoo shuleni na madawati, mambo ni mengi...

Labda uniambie tu kwa sasa unafurahia uwepo wa unga, sabuni, mchele na mahitaji mengineyo mitaani, lakini ukweli wa mambo ni kwamba, licha ya uwepo wa vitu hivyo, bado hali ya mtanzania kiuchumi ni mbaya na ndio maana mpaka leo bado wapo ndugu zetu vijijini wakisubiri kampeni zianze, ili wagaiwe t-shirts na kofia za CCM ziwastiri.

Hivyo kwangu, kumlaumu Nyerere kwa kufeli bila ya kunionesha yule aliyefaulu hapa ndani kwetu sikuelewi, na kutumia mifano ya nje kumhukumu Nyerere bila kunionesha nani aliyefuatia wa hapa ndani akafaulu, umemuonea, that's unfair comparison.

Unless uniambie mahitaji yetu siku zote yangebaki yale yale ya unga, mchele na sabuni kupatikana madukani, jambo ambalo kwangu halina mantiki, naamini mahitaji hubadilika kulingana na wakati, na pale unaposhindwa kuwapa watu wako kile wanachohitaji kwa wakati husika, basi umefeli, there is no way out.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
 
Hata wakimtangaza kuwa ni mungu hilo halinihusu hata kidogo, ila ntakachouliza ni kwanini huyu mnayemuita mungu wenu alikuwa na moyo mgumu, wa jiwe kama Firahuni ? Alikuwa anapata faida gani kutuona sisi tunaishi vile ?
Sasa hivi tunaishi vizuri sana kwenye mahekalu yetu na tunatembelea mavieite yetu makubwa makubwa huku tumepiga tinted !
Huku tunawazoom wale mamilioni kwa mamilioni wanaokimbizana na maisha ili mkono uende kinywani !
Maisha kweli yamebadilika sana !

Nyerere alituchelewesha !!
RIP Mwalimu Nyerere 🙏🙏
 
Haya mengine ya kisiasa ntayazungumzia siku ingine panapo majaaliwa. Ila kilichonileta hapa ni kuuliza kwanini bado aliendelea kutumia mabavu na kulazimisha sera zake hata pale ambapo mamilioni ya watanzania walikuwa wanapitia kipindi kigumu mno kimaisha. Najiuliza kwanini hakuwa hata na chembe ya huruma pale ambapo watanzania wengine walikosa chakula hadi kuchemsha pumba na huku wengine wakilala njaa ? Najiuliza sana, lengo lake haswa lilikuwa ni nini, lakini sipati majibu?​
Sasa mzee wangu, majibu utayapataje wakati muhusika ameshafariki? Ilipaswa awe hai kisha umuulize mwenyewe uso kwa macho
 
Sikuwepo duniani kipindi cha Nyerere,lakini kupitia maandiko mbalimbali unaweza kuona utawala ule ulikua na ahueni kwa wananchi licha ya changamoto mbalimbali zilizojitokeza.waliokuwepo enzi hizo wanasema hakukua na mgao wa umeme,elimu ilikua bora zaidi,huduma mbalimbali za kijamii pamoja na kwamba zilikua chache lakini zilitolewa kwa wakati na bila upendeleo wowote na tena kwa kiwango cha juu, utu wa Mtanzania ulikua ni kipaumbele cha serikali, serikali iliwajibika kisawasawa.je tujiulize miaka 38 sasa tangu Nyerere atoke madarakani zaidi ya kuongezeka majengo marefu kwenye miji mikubwa kama Dar nini cha maana serikali zilizopita zimefanya ambacho hakikufanywa na serikali ile ya Nyerere?
Kilichoongezeka kwa sasa ni watu wachache kuwatambia watu wengi ambao ni hohehahe !
 
Nyerere alikuwa ni mtu mwenye utu,kipindi cha msiba wake Maalim Seif alinukuliwa akisema Mwl alikuwa ni mkweli.Sasa jiulize yule mliyekuwa mnamuona alionewa na mwl anasema alikua mkweli which means ni kama ali-REGRET kuhusu ugomvi wao.Kushindwa kwa ujamaa dhidi ya ubepari ni sawa na kushindwa kwa utu dhidi ya unyama na kuonesha kwamba hakukubaliana na ubepari aling'atuka ili asiingize nchi matatizoni kwa shinikizo la wenye makucha(aliipenda nchi yake)kipi cha ajabu cha sasa hivi ukiachana teknolojia ambayo ni lazima tucheze nayo?
Kwamba ubepari ni unyama na ujamaa ni utu ?

Chagua kuishi USA au North Korea, kisha jibu lako litakuambia wapi kuna utu wapi kuna unyama
 
Kwenye hili Nyerere alikuwa ndiye bingwa. Alikuwa kila anayemkosoa anahama nchi. Ni vile tu ukweli hausemwi na bahati mbaya Nyerere katawala ktk kipindi ambacho media outlets zilikuwa hakuna.

Redio ya taifa ilikuwa inaandikiwa nn cha kusema kuhusu rais kwenye taarifa ya habari.

¶ Nyerere ndiye aliyefanya Kambona kuishi ukimbizini maisha yake yote.
¶ Nyerere ndiye aliyechana vyeti vya Tuntemeke Sanga.
¶ Nyerere ndiye aliyemfunga kifungo cha nyumbani (alimuweka kizuini) Kasangatumbo
¶ Nyerere ndiye alimuondoa kwenye urais Abdul Jumbe halafu akamuweka kizuizini hapo Kigamboni mpk umauti.
¶> Nyerere ndiye aliyetunga hili katiba bovu lililomfanya yeye kujipa umungu wa Tanzania.

Nyerere ni dikteta asiyesemwa.
Nyerere pia ndiye aliyetuepusha na udini, ukabila na ukanda mambo ambayo yalilitafuna sana bara la Africa kipindi hicho.
 
Kiongozi lazima awe na principles zake, kusimamia kile anachokiamini mpaka mwisho, kiongozi asiye na msimamo ndie chanzo cha kuyumba kwa taifa lolote hapa duniani.

Kulalamika miaka yote ya Nyerere kuwepo madarakani halafu bado hali ya maisha ya mtanzania ikaendelea kuwa mbaya, kwangu sioni kama kuna mantiki yoyote, kwasababu siku zote mabadiliko hayaji kwa usiku mmoja, ni mchakato.

Sasa ndani ya kipindi hicho cha mchakato ndicho kinamfanya kiongozi aendelee kusimamia kile anachokiamini, kama kikija kuwa na matokeo tofauti hayo ni mambo ya kibinadamu, kwamba alikosea, na ndio maana akawapisha wengine.

- Lakini unaposema Nyerere hakuwa na huruma na watu wake unakosea, alikuwa na huruma kupitiliza.

1. Hakujilimbikizia mali yoyote, licha ya madini na kila aina ya rasilimali tulizonazo.

2. Aliwahi kukaririwa akisema; "kiongozi unapita barabarani, unaona hali ya mtanzania ilivyo mbaya, unajua hili ni jukumu langu kumuondoa hapo alipo".

3. Hakuna hata mtoto wake mmoja tunayesikia amewahi kuhusishwa na ufisadi wa aina yoyote.

Mpaka hapo naamini utapata picha Nyerere alikuwa kiongozi wa aina gani, licha ya sera yake ya ujamaa kufeli, lakini dhamira ya dhati ya kumkomboa mtanzania toka kwenye lindi la umasikini alikuwa nayo.

Above all, hivi umewahi kujiuliza baada ya Nyerere kuondoka madarakani nini kilifuatia?

Kilichofuatia ndicho kile ambacho Nyerere alikipiga vita na wewe unaonekana kukifurahia, binafsi nchi hii naamini hakuna mabadiliko yoyote ya maana kiuchumi zaidi ya kuwepo pengo kubwa kati ya walionacho na wasionacho, hili Nyerere na Sokoine ndio walikuwa wakilipinga.

- Hii kwangu ni sawa na kusema, licha ya kumuona Nyerere alifeli, lakini hata hao waliofuatia baada yake nao wamefeli, hatuna cha maana cha kujivunia, mgao wa umeme, ukosefu wa maji safi na salama, wanafunzi kukosa matundu ya vyoo shuleni na madawati, mambo ni mengi...

Labda uniambie tu kwa sasa unafurahia uwepo wa unga, sabuni, mchele na mahitaji mengineyo mitaani, lakini ukweli wa mambo ni kwamba, licha ya uwepo wa vitu hivyo, bado hali ya mtanzania kiuchumi ni mbaya na ndio maana mpaka leo bado wapo ndugu zetu vijijini wakisubiri kampeni zianze ili wagaiwe t-shirts na kofia za CCM ziwastiri.

Hivyo kwangu, kumlaumu Nyerere kwa kufeli bila ya kunionesha aliyefaulu hapa ndani kwetu sikuelewi, na kutumia mifano ya nje kumhukumu Nyerere bila kunionesha nani aliyefuatia wa hapa ndani alifaulu, umemuonea, hukumu yako kwake sio ya haki.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
Wamesahau vita vya kagera vilivyo turudisha nyuma.
 
Kwamba ubepari ni unyama na ujamaa ni utu ?

Chagua kuishi USA au North Korea, kisha jibu lako litakuambia wapi kuna utu wapi kuna unyama
Ubepari ni ushetani. Wewe una njaa lakini mwenzako anasaza bila huruma ndivyo tunaishi hivyo kwa sasa. Ujamaa unataka wote muende pamoja hata mtu wa mwisho kabisa naye awezeshwe ndio maana tunaita ujamaa ni utu. Hamuoni licha ya matatizo tuliyonayo lakini mtu yupo radhi awe na fedha ambazo hatomaliza milele? Watu wanamiliki magari na majumba ya kifahari na ni viongozi wa serikali na kulipwa fedha nyingi ukiachia mbali kuiba lakini watu wanakosa huduma muhimu?
 
Wamesahau vita vya kagera vilivyo turudisha nyuma.
Hii nayo ni mojawapo na setbacks kwenye uongozi wa Nyerere, mleta mada badala ya kutumia muda mwingi kuhukumu tena kwa kutumia mifano nje, nadhani angejielekeza pia kwenye changamoto za kila awamu ili tupime awamu ipi ilikuwa na changamoto nzito zaidi ya nyingine, kisha tuone yupi alikuwa mzembe zaidi.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
 
Watu ni wajinga sana kama umegundua viongozi wengi wenye maono na mtazamo mwema kwa wananchi na ambao wamekuwa tayari kujitoa kwa ajili ya wananchi huishia kuitwa madikteta alafu wale wanao ruhusu ufisadi na wizi serikalini wanapewa sifa za kijinga.

Hata Yesu alikuwa mwema lakini akaishia kuuliwa bila kosa lolote. Binadamu ni wajinga na wapuuzi sana. Badala ya kumlinda mtu anayejali, sisi tunampiga mawe.
 
Wewe,you are quite mistaken. Unadhabi Ujamaa umekufa.
Ujamaa haujakuja.
By God! Tunazitamani sana hizo video zenu,na tutakuja kuwapora hizo video ili na sisi tuzitazame.
 
Huwa najiuliza sana lakini sipati majawabu, lakini naomba wasomi wa humu ndani mnisaidie.

Hivi Mzee Nyerere alikuwa ana roho ya namna gani kuona mambo kama haya yakitokea kwa wananchi lakini bado hataki kubadilika na akaendelea kutumia mkono wa chuma kuhakikisha anasigina kabisa uwezo binafsi wa mtanzania kuweza kujikwamua kiuchumi. Ujamaa wa Tanzania hakuleta matokeo yoyote makubwa na ya kuchangaza ukilinganisha na kule Asia na Ulaya ambako walau walifanya mapinduzi ya sayansi na teknolojia.

Uchina walifanikiwa sana baada ya Raisi Deng Xiaping kuanza kuwaonea huruma raia wake akifahamu kabisa kwamba njia waliyokuwa wanaenda ilikuwa siyo sahihi. Aliruhusu watu waanze kumiliki mali zao binafsi na kufanya biashara. Najiuliza sana, miaka yote 18 ya Ujamaa, yalifanyika na kutokea mambo mengi mno kwa watanzania, kiasi kwamba kiongozi yoyote mwenye huruma na wananchi ni lazima angekaa chini na kujifanyia tathmini, lakini Raisi Nyerere hakufanya hivyo, aliendelea kuwa na moyo mgumu kama Farao. Hebu tuzingatie haya:

1. Sera ya utaifishaji wa mali, ilileta umasikini mkubwa sana kwa watu.
2. Kufuta vikundi ya ushirika (Cooperatives) na kuweka vile vya TANU kulididimiza mno sekta ya kilimo.
3. Kupiga marufuku watu binafsi kuagiza bidhaa nje ya Tanzania kulipelekea uhaba wa bidhaa na huduma muhimu.
4. Kuweka ugumu katika kusafiri (Travelling Restrictions) kulisababisha ukosefu wa ujuzi kwa watanzania.
5. Kuminya uhuru wa mawazo na kutumia nguvu ya dola kunyamazisha watu kulidumaza ukomavi wa demokrasia.

Mpaka kufika miaka ya 80's Ujamaa ulikuwa umefeli vibaya mno. Tanzania tulikuwa hatuna hata unga wa kupikia, mafuta, wala sukari. Mtaa mzima mlikuwa mnaenda kwa mwenyekiti kuomba sukari au sabuni kutoka maduka ya ushirika. Ukikamatwa na mafuta, sabuni au dawa za binadamu zilizolanguliwa kutoka Kenya lazima ushughulikiwe na dola. Kama ulisoma miaka ya 80's unaweza kukumbuka kwamba hata sare za shule zilikosa rangi, watu tukawa tunavaa vitu vya ajabu vilivyochakaa kama vile vichaa. Ukibahatika kukutana na wamishionari au taasisi za kidini ndiyo ulikuwa unaweza kupewa hata nguo, mahitaji na wazungu.

Yote haya yanafanyika, Mzee Nyerere na Sokoine wakaingia mtaani kuanza kushughulikia maelfu ya watanzania ambao wanahujumu uchumi. Ila ukifuatilia zile kesi nyingi, utafahamu kwamba hao wahujumu uchumi ni wale watanzania wenye akili za haraka ambao walijiongeza na kuweza kupata mahitaji muhimu ili kuhudumia familia zao. Wahujumu uchumi kwelikweli, ambao wengi walikuwa ni vigogo wa serikalini hawakuguswa. Kiukweli, kama nchi ina kiongozi mwenye huruma haya yote yasingetokea bila yeye kujirudi.

Hivi kwanini MTAKATIFU na MWENYEHERI, Raisi Nyerere hakuwa na chembe ya huruma moyoni ?
Kuna mambo nikikumbuka huwa naumia sana na nakosa majawabu. Hivi alikuwa anapenda kutuona sisi vile ?​
Kosa lilianzia kwenye mifumo ya kuabudu, MUNGU WETU HARISI, keshatukataa, hatuchagulii viongozi wa kutuvusha, hatufumbui kuhusu raslimali alizotuwekea ardhin kwetu, ametufanya kuwa watumwa wa kudum
 
Huwa najiuliza sana lakini sipati majawabu, lakini naomba wasomi wa humu ndani mnisaidie.

Hivi Mzee Nyerere alikuwa ana roho ya namna gani kuona mambo kama haya yakitokea kwa wananchi lakini bado hataki kubadilika na akaendelea kutumia mkono wa chuma kuhakikisha anasigina kabisa uwezo binafsi wa mtanzania kuweza kujikwamua kiuchumi. Ujamaa wa Tanzania hakuleta matokeo yoyote makubwa na ya kuchangaza ukilinganisha na kule Asia na Ulaya ambako walau walifanya mapinduzi ya sayansi na teknolojia.

Uchina walifanikiwa sana baada ya Raisi Deng Xiaping kuanza kuwaonea huruma raia wake akifahamu kabisa kwamba njia waliyokuwa wanaenda ilikuwa siyo sahihi. Aliruhusu watu waanze kumiliki mali zao binafsi na kufanya biashara. Najiuliza sana, miaka yote 18 ya Ujamaa, yalifanyika na kutokea mambo mengi mno kwa watanzania, kiasi kwamba kiongozi yoyote mwenye huruma na wananchi ni lazima angekaa chini na kujifanyia tathmini, lakini Raisi Nyerere hakufanya hivyo, aliendelea kuwa na moyo mgumu kama Farao. Hebu tuzingatie haya:

1. Sera ya utaifishaji wa mali, ilileta umasikini mkubwa sana kwa watu.
2. Kufuta vikundi ya ushirika (Cooperatives) na kuweka vile vya TANU kulididimiza mno sekta ya kilimo.
3. Kupiga marufuku watu binafsi kuagiza bidhaa nje ya Tanzania kulipelekea uhaba wa bidhaa na huduma muhimu.
4. Kuweka ugumu katika kusafiri (Travelling Restrictions) kulisababisha ukosefu wa ujuzi kwa watanzania.
5. Kuminya uhuru wa mawazo na kutumia nguvu ya dola kunyamazisha watu kulidumaza ukomavi wa demokrasia.

Mpaka kufika miaka ya 80's Ujamaa ulikuwa umefeli vibaya mno. Tanzania tulikuwa hatuna hata unga wa kupikia, mafuta, wala sukari. Mtaa mzima mlikuwa mnaenda kwa mwenyekiti kuomba sukari au sabuni kutoka maduka ya ushirika. Ukikamatwa na mafuta, sabuni au dawa za binadamu zilizolanguliwa kutoka Kenya lazima ushughulikiwe na dola. Kama ulisoma miaka ya 80's unaweza kukumbuka kwamba hata sare za shule zilikosa rangi, watu tukawa tunavaa vitu vya ajabu vilivyochakaa kama vile vichaa. Ukibahatika kukutana na wamishionari au taasisi za kidini ndiyo ulikuwa unaweza kupewa hata nguo, mahitaji na wazungu.

Yote haya yanafanyika, Mzee Nyerere na Sokoine wakaingia mtaani kuanza kushughulikia maelfu ya watanzania ambao wanahujumu uchumi. Ila ukifuatilia zile kesi nyingi, utafahamu kwamba hao wahujumu uchumi ni wale watanzania wenye akili za haraka ambao walijiongeza na kuweza kupata mahitaji muhimu ili kuhudumia familia zao. Wahujumu uchumi kwelikweli, ambao wengi walikuwa ni vigogo wa serikalini hawakuguswa. Kiukweli, kama nchi ina kiongozi mwenye huruma haya yote yasingetokea bila yeye kujirudi.

Hivi kwanini MTAKATIFU na MWENYEHERI, Raisi Nyerere hakuwa na chembe ya huruma moyoni ?
Kuna mambo nikikumbuka huwa naumia sana na nakosa majawabu. Hivi alikuwa anapenda kutuona sisi vile ?​
Mtoa mada nadhani unakosea kwa kusema Nyerere hakuwa na huruma hata kidogo. Umechambua upande wa udhaifu wake ndio maana unaona hakua na huruma hata kidogo.
Chambua na upande wa mazuri yake ndipo utaiona huruma ya Nyerere kwa wananchi wake.
1. Nyerere kwa kipindi alichoongoza alikua na nafasi ya kuiba mali za umma na kujilimbikizia kadri atakavyo na asingekuwepo wa kumpigia kelele lakini hakufanya hivyo.
2. Mwl. J.K. Nyerere angetaka kutoa madaraka makubwa kwa watoto wake angefanya hivyo lakini mpaka sasa nadhani Makongoro Nyerere ndio kakumbukwa juzi hapa kuwa Mkuu wa Mkoa angalia hao wengine wanavyowapaisha watoto wao.
Inakua rahisi kumchambua udhaifu wake kwa kuwa kimepita kipindi kirefu inakua rahisi kuona makosa yake.
Kumbuka:
3. Mwl. Nyerere alitoka madarakani Nchi ikiwa na viwanda vingi sana lakini kutokana na ubinafsi na Ubepari leo hii viwanda karibu vyote vimeuzwa na kutelekezwa matokeo yake ajira nyingi sana zimepotea.
4.Harakati za kuunganisha Nchi unaweza kuzichukulia rahisi kwa kuwa unaona matokeo tu lakini mchakato wake sio wa kubeza. Pale ilifanyika kazi kubwa sana kuwaungansha watanzania na kuondoa ukabila na udini.
5. Nadhani nia ya Mwl.ilikua nzuri sana ila matokeo ndio hayakua mazuri.
Kitu kingine matokeo ya vita ya Kagera kwa uchumi wetu ilileta athari kubwa sana.
Vile vile Mwl.alijihusisha sana na ukombozi wa Nchi nyingine za Afrika. Hivyo alikua na mambo mengi sana ya kupigania katika lindi la ufukara wa Taifa.
Tujiulize
Miaka 38 tangu Mwl. Nyerere atoke madarakani ni eneo gani kama Taifa tunalifanya kwa ufanisi ndani ya Ubepari.
Nadhani sekta ya uchawa tu ndio tuko njema zaidi.
Mwl.apewe heshima yake
 
Kwamba ubepari ni unyama na ujamaa ni utu ?

Chagua kuishi USA au North Korea, kisha jibu lako litakuambia wapi kuna utu wapi kuna unyama
Namba 9 ina maajabu !
Upande moja inonekana ni 6 lakini upande mwingine ni 9.
Maisha yenye furaha ni mindset ya kila mtu alivyojitengenezea !!
Wapo watu wanayafurahia maisha huko Korea na wapo watu wanayachukia maisha huko USA !
 
Sikuwepo duniani kipindi cha Nyerere,lakini kupitia maandiko mbalimbali unaweza kuona utawala ule ulikua na ahueni kwa wananchi licha ya changamoto mbalimbali zilizojitokeza.waliokuwepo enzi hizo wanasema hakukua na mgao wa umeme,elimu ilikua bora zaidi,huduma mbalimbali za kijamii pamoja na kwamba zilikua chache lakini zilitolewa kwa wakati na bila upendeleo wowote na tena kwa kiwango cha juu, utu wa Mtanzania ulikua ni kipaumbele cha serikali, serikali iliwajibika kisawasawa.je tujiulize miaka 38 sasa tangu Nyerere atoke madarakani zaidi ya kuongezeka majengo marefu kwenye miji mikubwa kama Dar nini cha maana serikali zilizopita zimefanya ambacho hakikufanywa na serikali ile ya Nyerere?
Huo umeme ambao haukuwa kwenye mgao ulikuwa kwenye miji mingapi,

Unakumbuka maduka ya ushirika,?
 
Ubepari ni ushetani. Wewe una njaa lakini mwenzako anasaza bila huruma ndivyo tunaishi hivyo kwa sasa. Ujamaa unataka wote muende pamoja hata mtu wa mwisho kabisa naye awezeshwe ndio maana tunaita ujamaa ni utu. Hamuoni licha ya matatizo tuliyonayo lakini mtu yupo radhi awe na fedha ambazo hatomaliza milele? Watu wanamiliki magari na majumba ya kifahari na ni viongozi wa serikali na kulipwa fedha nyingi ukiachia mbali kuiba lakini watu wanakosa huduma muhimu?
Kwa io unaamini kwenye ujamaa, Mkuu wa mkoa anaishi sawa na mkulima wa nanjilinji?

Au unahisi Nyerere familia yake nayo ilipanga folen kwenye maduka ya ushirika? Au unadhani na Nyerere aliishi kama wakulima wa Namtumbo?

Duniani hakuna usawa, ila ni bora kwenye ubepari mana doors are open ila kwenye ujamaa doors are closed
 
Back
Top Bottom