Majini sio ishu ukipatwa ni mpaka zipote siku 3 ndo ufe.kuna ugumu fulani wa kupata hizo mali kwasababu maeneo ambayo wajurumani walificha hizo mali yamekuwa ni makazi ya kudumu ya majini na majoka makubwa ya kutisha.
ili kupata hizo mali inabidi ujizatiti kweli kweli. vinginevyo utaishia kupata ukichaa au kufa kifo cha ajabu.
Watu wanapata tatizo ni moja tuNi nani aliyefanikiwa kuchimba na kupata hiyo hazina? Mkuu hii kitu nimeufuatilia kwa karibu sana zaidi ya miaka ishirini. Nilichokiandika nakifahamu fika. na ukweli ni wale wanaotaka utajiri kwa ganda la ndizi ndio wanafanya hii ishu au wanahamasisha wengine nao wafanye. Inauma sana lakini bahati mbaya ukishakolea inakuwa kama umelishwa uganga.
No hazina ya Mjerumani full stop.
Uongo.kila muafrika anaetumwa kuficha Mali ilikuwa lazima afie kule kule mafichoni.Wajerumani walikua wanamchukua muafrika mmoja halafu wanachukua kichwa cha chatu wanamuwekea mdomoni kisha wanafunika pamoja na Mali
Sent using Jamii Forums mobile app
Alikuwa na elimu hiyo juu ya hazina.Vipi kuhusu maeneo ambayo kuna alama (handaki,misaraba, zege n.k)ziliwekwa na hao hao wajerumani zilikua za nini? Ninao ushahidi alikuja Padre mmoja mjerumani akaondoka na mzigo na wala hakuchimba umbali mkubwa ,walitumia jembe tu ilikuwa 2016
Sent using Jamii Forums mobile app
Mlikuwa mnakutana na kizuizi gani?Wadau haya mambo nimeshiriki sana kweli vitu vipo nimefika ktk eneo husika sema kutoa mzigo ni shughuli na mpaka niliamua kuacha kwasababu unapoteza muda mwingi na pesa kufuatilia but kuna eneo najua kuna mzigo ila kuchukua sasa ni kugumu nimekutana na huo.ugumu
Sent using Jamii Forums mobile app
Ni kweli kwa sababu taarifa zinakuwa si sahihi unajiendea tu.Hapa ukiingia unapoteza pesa na muda wako bila wewe kujua
Umeona!Kuna ankali wangu kateseka sana na hizi mambo na hadi leo huenda bado yuko huko "mgodini", kama ni mauza uza basi itakuwa kuna namna kichwa kinavurugwa unakuwa unaamini umezikaribia mali..... Pia hapo ulivyotaja Lumbira (kama ndo ile ya Mbeya) nimesoma shule moja maeneo yale nakumbuka kuna bweni hata walimu walichangia kulivunja eti kuna mali.
Sent using Jamii Forums mobile app
Unachukua mkuu.Hata utumie waganga na wachungaji na mashehe hizo mali huchukui kabisa mkuu. Unaweza kuingia hasara tu. Ila wao huwa wanakuja wanazichukua kwa mtindo kama kujenga kanisa au kuwajengea shule. Na wanahakikisha sehemu walipochagua kujenga hilo kanisa, hospital au shule ni ile ile karibia na mahala walipochimbia hizo mali.
Rejea hospital ya Ilembula. Hospital ya Ifisi ya mzungu Lena mbalizi mbeya pale ilipojengwa kwenye korongo hivi. Hospital ya Ikonda,makete ilijengwa polini,mlimani,mbali kabisa na makazi ya watu. Hizo ni baadhi tu. Wazungu ni wachawi kitambo sio huu uchawi wa kiafrica. Na hizo mali ni nyingi sana za matrilion ya pesa
Ni wapi mkuu.Mbulu inajulikana ni wapi zimechimbiwa
Si anafanya jambo bila taarifa kwa maneno ya wabongo lazima aliwe tu.Kuna mzee mmoja kamaliza kiinua mgongo chake kisa hizo ishu Hadi Leo hajafanikiwa
Kweli?Unachukua mkuu.
Toa taarifa sahihi eneo husika na kizuizi gani ulikutana nacho toa hapa hapa nikupe jibu.
Huu nao ndio ujinga..nimekua sasikia hivyo, Hadi watu kwenda Kwa wagangaNikajua umeshapata Mali kwenye mojawapo ya hivyo Vijiji kumbe unatupa usimulizi wa vijiweni [emoji16][emoji16]
Taja kizuizi nimekwambia mkuu.Kweli?
Hadithi hii..anaanzaje kuchimba kanisani ambalo kila siku watu wanaingia...Lina walinzi, viongozi Wa ngazi ZA chininimepanda bajaji siku mbili zimepita kuna dada alikua ana sali kanisa fulani la Rome pale Iringa kuna padri akaja akawa anasali pale akaomba awe anafunga na kuomba usiku wakamruhusu kumbe pale madhabahuni pana mali usiku ana chimba anafunika na mkeka Siku kadhaa akapotea kimya kimya kuja kugunudua wamekuta shimo kubwa sana chini na mzigo ushatolewa na wabongo tunakuaga wazembe magetin hatukazi kukagua mtu kasepa na mzigo
Kwenda kwa waganga sio shidaHuu nao ndio ujinga..nimekua sasikia hivyo, Hadi watu kwenda Kwa waganga
BInafsi sijawahi kutamani wala kufikiria kuhusu haya mambo ya mali kale,lakini naamini na nathibitisha kabisa zipo
Babu yangu alishawahi kuniadithia sana kuhusu haya mambo maana yeye ndo alikuwa anajishughulisha na haya mambo
Na anasema enzi za ujana wake, walifanikiwa kupata mali nyingi sana na walikuwa matajiri kweli,sema walianza kufilisika taratibu baada ya kukosea miongozo flani
Kipindi ananiadithia alikua akinificha baadhi ya Siri kubwa kubwa kuhusu haya mambo,kwasababu alishanisoma ndani ya moyo wangu kuwa sina interest kabisa na hayo mambo.
Anasema kama ningeonyesha interest kidogo,basi angenifungukia siri zooote na kunirithisha rasmi nyenzo zake za kufanya izo kazi.
Anasema lengo lake kuu alitaka mimi nizitafute izo mali ili niweze kuukomboa ukoo wangu na umaskini,maana yeye alipewa iyo nafasi akaichezea...( yeye naye alifundishwa na baba ake,yaaan baba wa babu yangu)
Babu yangu alifariki 2014 akiwa na miaka 98...kuna sehemu moja uko kijijini kwetu katika mashamba yake,aliacha usia kwamba pasichimbwe ,wala kupandwa kitu chochote kile juu ya ile ardhi mpaka pale atakapotokea mteule katika ukoo wetu na atapewa ishara maalumu
Iyo sehemu katika shamba,kwa juu kuna mchanga mweupee ambao ni mkavu kipindi chote hata mvua inyeshe namna gani hapaloi
Ukoo wote unaamini pengine ilo eneo ndo sehemu alipohifadhia nyenzo zake za kufanya izo kazi za kutafuta mali za kale.
Ulikuwa nao?Hii stori ya uongo.