Wajerumani Walificha Mali Nyingi Kwenye Ardhi ya Tanzania

Asante sana Dada kwa kuliweka wazi hili maana kuna matapeli ya kila aina
Coins zote zinauzwa eBay na bei zake hazivuki $20
Sio kweli kuwa zina madini na zinauzwa $1000 No way

Nazijua sana na nina detector yangu pia ndogo
 
Kuna Mali ila cha ajabu kila mtu akiingia pangoni hatoki!![emoji24]anaishia kupotea ndani ya pango hii nimeshuhudia kabisa
 
Kuna Mali ila cha ajabu kila mtu akiingia pangoni hatoki!![emoji24]anaishia kupotea ndani ya pango hii nimeshuhudia kabisa
Sasa kama kila anaeingia anapotea aliethibitisha kuna mali ni nani?
Yaani alierudi akathibitisha mali fulani ipo ni nani?
Mali gani ipo na sehemu/location gani.

Anyway pango za kupoteza watu kwanza milango yao yote imeelekea jua linapotoka.
Mnatafuta ndama dume mnachinja hapo mlangoni kwa kuomba walinzi waachie.
Kisha mnachoma ubani,harmali,mushtaka na ladhani hapo mlangoni.
Mnakaa siku saba ndo mnaingia kabla jua halijatoka.

Lakini najua huna taarifa sahihi kwa sababu huwa kuna mitego zaidi ya mmoja.
 
Kuna mwaka flani binti kutoka Italy alikuja hapa nchini na akaripoti RC Kisha akapewa wajeda 2 wakampeleka kwenye pango lakini mwenye ramani ni binti walipokaribia binti akawaambia nisubirini hapo, baada ya masaa 3 binti akatoka wakarudi akaenda nao benki akawapa mil 7 Kila mmoja na inasemekana akaenda kumuaga RC ambae pia alipewa kama Dola 8000 akasepa zake.

Wale wajeda wakajadili wakaamua kwenda peke yao Kwa Siri. Walipofika saiti mmoja akatangulia sasa palikuwa na sehem ya kuruka akafeli akadondoka kwenye shimo refu na akawa haonekani kabisa halafu lile shimo hata ukimulika na tochi mwisho hauonekani halafu kimyaaa, jamaa alisubir hakuna kitu ikabidi arudi kambini bila mwenzie ikabidi atoe taarifa na akasema Kila kitu, ikabidi uongozi na wajeda kadhaa wafike eneo husika wakaona mazingira magumu akataarifiwa RC ndipo akachukua hatua ya kumpigia yule binti wa kiitaliano Kwa msaada kwakua aliacha contact.
Wakajibiwa kuwa huko pangoni hata yeye alikuja Kwa codes na alikubaliwa na mizimu baada ya kuchambuliwa kati ya vilembwekezi 167 kutoka Kwa muhenga aliyeficha Mali hiyo na akawaambia huyo Kesha kufa na hata mwili hauwezi patikana wanajeshi wakatumia mbinu zao za sanduku lililojazwa upepo wakapelekea familia na kuzikwa kijeshi hivyo hizo Mali kuzipata iwe bahati lakini siyo kitu chepesi, hata wanaokuja kuchukua kutoka ulaya Kuna kiasi kidogo anachoruhusiwa kuchukua na akivunja sharti hilo hata yeye anaweza ishia kufa huko mapangoni lengo ni kubakiza Mali zitakazo saidia vizazi vijavyo itakapotokea mkwamo wa kiuchumi, mbinu walizotumia kuficha hizi akiba ni mbili.

Mbinu ya kwanza ni uchawi ambao hauingiliani na WA kwetu ndo maana hata ukikusanya waganga na wachawi wa mkoa mzima wanaweza ishia kubamizwa na madondola au nyuki na kupoteana, mbinu ya pili walotumia ni sayansi na teknolojia na chenga za uwanjani, mfano unakuta sehem Kuna sakafu sasa kubomoa mtatumia nyundo zoote ikiwamo fatuma hadi atuganile nyundo hazipasui kumbe jamaa alisaga kwato za wanyama pori na kuchanganya na simenti maalum hivyo ni Bora uanzishe kilimo Cha nyanya kuliko kudili na haya mapango
 
Huu ni utapeli wa kizamani sana... uliopitwa na wakati... asilimia 100 ya mandezi nashangaa bado wanaendelea kupigwa tu... mara pasi ya mjerumani, mecury nyekundu[hii im not so sure- pengine ipo] ila rupia na takataka zinginezo.....ni utapeli!!!

Kiufupi ni scam iliyosukwa enzi hizo kiustadi...na bado inaliza watu hadi waleo!.

Stuka shee wangu...muda haurudi nyuma!...masaa yanasogea!....endelea kupoteza muda huko...uzeekee huko ukiwa maskini wa kutupwa!!!

Dont say i did'nt warn you!
 
Peleka ujinga wako huko, labda hujui mfumo wa ibada Wala viongozi wa kanisa Katoliki. Kwamba Padri atoke ujerumani aumbe kuwa anasali kanisa Fulani?
 
Soma post #830
 
Mjerumani hajaficha chochote. We si unajua fumbo hufumbiwa nani?
 
Asilmia 95 huwa hawafanikiwi ,ila wanaojihusisha na kilimo cha nyanya asilimia 80 hufanikiwa
Wewe jamaa wee. Ebu faster pita hapo kwa mangi agizia chochote ntapita baadaye kulipa na range yangu.
 
kweli "mandezii 😆😆😆
ati fufuma sijui nn..
yaani "undezi" mtupu wa mipopoma inayoamini katika "shortcut" na mambo ya kusadikika!
 
27 maeneo mengi ya tarime walificha pia. kuna maeneo walichimbia vitu wakasakafia kabisa hilo shimo
 
Mali nyingi walificha au walikuja kuchukua mali nyingi ?

Anyway mali nyingi bado tunayo ndio maana kila siku so called wawekezaji hawaishi kuja kwenye shamba la bibi
 

Wangekuwa wasenge sana waache kupeleka kwao wakajenge nchi wafiche kwenye mapango uliyoyataja! Karne hii bado kuna watu wana akili hizi za kutafuta rupia? Kweli bongo nyoso wandugu!
 

Hukupiga kapicha Mkuu
 
Rubbish
 
Upuuzi mtupu!.
Mali nihuomuda unaopoteza kuangaika navitu visivyo eleweka.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…