Wajerumani Walificha Mali Nyingi Kwenye Ardhi ya Tanzania

Wajerumani Walificha Mali Nyingi Kwenye Ardhi ya Tanzania

Mtaalamu alisema kuna vito vya kutosha sana, tulipofiikia kuna vigaae vikubwa vimefunika na pembeni yake kuna ukuta wa mawe umejengwa,sasa kuna ngema juu imeninginia na kuna kiwe, inafaa lilipuliwe na litolewe.

Tulikutana na mauza uza kibao lakini tyliyashinda,kubwa ilikuwa nyoka wa kutisha wa kutosha, tuliambiwa hapana kumuuwa hata mmoja,mbinde ilikuwa kuwatoa humo shimoni.

Sent using Jamii Forums mobile app
Hahahaha sasa akiwaua nyie je??

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna sehemu moja nilienda maeneo ya kamsamba wilaya momba mkoa mbeya saiz song we wamejenga kanisa zuri sana linapendeza sana h alafu nipolini kwelikweli sasa nikawa najiuliza why waliamua kujenga huku nahisi kuna vitu kanisa limgine wamelijenga chunya poleni kweli kweli halafu zuri kwelikweli

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wadau haya mambo nimeshiriki sana kweli vitu vipo nimefika ktk eneo husika sema kutoa mzigo ni shughuli na mpaka niliamua kuacha kwasababu unapoteza muda mwingi na pesa kufuatilia but kuna eneo najua kuna mzigo ila kuchukua sasa ni kugumu nimekutana na huo.ugumu

Sent using Jamii Forums mobile app
Ugumu wake upi mkuu kwamba ukichimba hupati au kunamambo ya giza

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hiyo ni kweli pia na Mm nineshuhudia kuna mzee mmoja kama wa miaka 89 au 90 alikuwa na ramani ya hazina kubwa sana iliyopo around Mwadui Shinyanga.

Sent using Jamii Forums mobile app

Ramani na uwepo wa hazina ni vitu viwili tofauti kabisa. Anyway nimetahadharisha kwakuwa nafahamu ninachokiandika. Nasubiri ushuhuda kwa aliyepata hizo hazina.Haya mambo ni ya kufikirika zaidi fanyeni utafiti wa kina mtanielewa ninachokimaanisha hapa.
 
Ramani na uwepo wa hazina ni vitu viwili tofauti kabisa. Anyway nimetahadharisha kwakuwa nafahamu ninachokiandika. Nasubiri ushuhuda kwa aliyepata hizo hazina.Haya mambo ni ya kufikirika zaidi fanyeni utafiti wa kina mtanielewa ninachokimaanisha hapa.
Kuna baadhi ya hazina ni ngumu kupatikana bila ya kuwepo kwa mwongozo maana kama Mwadui kuna sehemu ukionekana lazima wazee wakuulize kuwa umekwenda kufanya nini huko

Sent using Infinix hot 4
 
Na kwanini WaGermany wafiche ????? Yaani upike chakula kizuri,halafu uweke mvunguni (usile Wala usiondoke nacho) eti.... Use common sense !!!
 
Achana na story za mtaani, nenda kamtafute huyo mtu kama utampata zaidi utajikuta kila mtu hamfahamu, tuache ujinga hakuna mambo kama hayo
Kuna mmoja kyela eneo lake inasemekana chini kuna pango huko masanduku na gari moja lipo wazungu wakaomba wampe gari na wamjengee nyumba nzuri ilo eneo wapewe wao jamaa akakataa akasema atachimba yeye..

kitu cha kushangaza kila lipokua anachimba vile vitu vinashuka chini... Akatengeneza mashimo makubwa matatu na maji kwake bila mafanikio

Hivyo vitu vya kishirikina hatari

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kubali kwa hili ndugu wewe ni mbumbumbu, mambo haya yapo,na wenye bahati zao wanatusua,mie nimeona kwa macho yangu, na mwisho ilikuwa ni singida, bibi kizee aliuza pasi kwa Muizraeli, alikuja na helicopter akachukua pasi yake na akaondoka na ajuza huyo na mjukuu wake,japo walipewa pesa kiduchu sana, mil 30 na ushee hivi.

Wapo wanaochemka kutokana na mauzauza hayo,wengine wanakutana na maiti na wengine wachache pia wanabahatika. Utajiri baba unanjia nyingi.

Sent using Jamii Forums mobile app

Nakubali mimi ni mbumbumbu Muizaeli aje na helkopta Singida kufuata pasi milioni 30 na ushee .... alikuja lini? kijiji gani? huyo "ajuza" alikuwa na nguvu ya kuchimba? alikuwa na utaalamu wa kusoma ramani? alikuwa na manguvu ya kupambana na "mauza uza" wewe ulikuwa wapi kipindi hicho?

Anyway haya ni maswali ya kimbumbumbu endelea kuamini unachokiamini lakini usiwashawishi watu waingie mkenge. BTW mbona unatumia nguvu kubwa sana kwenye hii issue? kuna ajenda nyingine?
 
Ndugu zangu wanajamvi.
Nimekuwa katika utafiti wa mali kale na mambo ya asili kwa muda mrefu.
Katika utafiti wangu nimekuja kugundua wajerumani wameficha mali nyingi sana kawenye ardhi ya Tanzania.
View attachment 1022278

Wakati wa utawala wa wajerumani kulikuwa na fedha ambazo zilikuwa zikitumiaka.
Heller na Rupee zilikuwa zikitumiaka. Coin hizo zilikuwa na madini mengi sana tofauti na coin za sasa.
Kwa mfano 1 Heller kwa sasa inauzwa kwa $900 - $1000.
View attachment 1022271

View attachment 1022276

Kwenye vita vya kwanza vya dunia wajerumani walizichimbia hizo mali sehemu mbalimbali kwenye ardhi ya Tanzania kwa ustadi mkubwa.

Katika tafiti nilizozifanya mpaka hivi leo. Maeneo yafuatayo na mengine mengi ndiko zilipogichwa mali hizo. Inatakiwa kujua sasa ni eneo gani masanduku yenye mali yalichimbiwa:-

  1. Ikombe
  2. Mibirizi
  3. Kasanga
  4. Ilembule
  5. Rombo
  6. Nyakanazi
  7. Uvinza
  8. Mlalo
  9. Kisarawe
  10. Kazimzumbwi
  11. Kirondatal
  12. Tukuyu
  13. Leganga
  14. Igulwa
  15. Ushetu
  16. Mnazi
  17. Mikese
  18. Shume
  19. Lumbira
  20. Mbulu
  21. Nansio
  22. Sekenke
  23. Galula
  24. Liuli
  25. Manda
  26. Lushoto
Hizi ni sehemu kadhaa zinazohitajika utafiti wa kina ili kujua ni sehemu zipi mali hizo zilifichwa.

Asanteni
Ukitaka kufirisika na kupata uchizi ingia kwenye hiyo biashara. Kila mali kale utakayopata utaambiwa siyo. Ukipata hiyo Heller watakuambia mwaka siyo tunataka ya 1890, ukiipata utaambiwa hapana hii imechubuka, mara ilihusisha kifo nk. Utaambiwa kuna pasi, ukiipata watakuambia aah! siyo hii ya mkaa, ipo ya mvuke... Mara utashangaa unapata stress utaota mvi hadi kwenye nyusi.
 
Kuna jamaa alikuwa anawinda mbugani na baba yake wakapita sehemu wakakuta mawe mengi ya dhahabu yamerundikwa kwenye mti wa mwembe, hawakuyatilia maanani wakaendelea na uwindaji walipo rudi kijijini wakawasimulia watu. Watu walivyo sikia hivyo wakambembeleza kijana awapeleke. Kabla kijana hajawapeleka wakaenda kwa kwa mganga kupiga ramli.

Mganga akawambia waende ila anaona giza mbele ya huyo kijana anayewapeleka. Wakasisitiza japo kijana aliogopa. Basi mganga akawambia wakifika kuna kitu kitatokea ila wasiseme neno lolote.

Story ni ndefu ila nitaifupisha.

Walipokaribia kwenye ule mti kweli waliziona zile dhahabu ghafla kikatokea kimbunga kikali kikamyanyua mzee moja. Mkwe wa yule mzee kuona hivyo akasema "haiwezekani baba mkwe aende"

Ghafla walitokea nyani kusiko julikana wakawapa kichapo si cha nchi hii alafu ikanyesha mvua kubwa hawajawahi kuona. Ikaharibu chakula chote walicho kuwa nacho.

Ilikuwa ni safari ya siku nne kurudi bila msosi

Sent using Jamii Forums mobile app
Hekaya tu hizi za bunuwasi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
  • Thanks
Reactions: R.K
Back
Top Bottom