Wajerumani Walificha Mali Nyingi Kwenye Ardhi ya Tanzania

Wajerumani Walificha Mali Nyingi Kwenye Ardhi ya Tanzania

Katika uingereza ya kale, siku moja mtabiri mmoja alitabiri kuwa, ndani ya mwaka mmoja ujao kutatokea upepo mkubwa sana... Upepo huo utaangamiza mji wote ule... .. Upepo huo utavuma usiku mida ya saa 2 .... Upepo huo utavuma kutokea bondeni... Mtabiri huyo akashauri kuwa watu wachukue tahadhari, upepo ukianza watu wakimbilie mlimani kwani ndio itakuwa salama yao.

Basi kweli muda huo ulipita, siku hiyo jioni mida ya saa mbili. Bwana mmoja alimuona mama akikimbia akitimua mbio kuelekea mlimani. Haikupita muda mwanaume alikuwa nyuma yake.. Bwana yule akakumbuka kuwa mtabiri alitabiri. Na wakati ndio huo, naye akatoka mbio na familia yake, majirani nao wakafuata, majirani wa majirani wakakimbia wakipiga kelele cha kimbunga huku wakielekea mlimani.

Wakiwa kule mlimani, wakaanza ulizana juu ya ukubwa wa kimbunga hicho.. Kila mmoja akasema alimuona jirani anakimbia naye akafuata. Hatimaye yule bwana wa kwanza kukimbia akasema mimi nilimuona mama anakimbia nikajua ndio utabiri wa mtabiri umefika...

Yule mama kuulizwa akasema yeye alikimbia baada ya mumewe kutaka kumpiga usiku ule, na mume naye akawa anamkimbiza mkewe ili amkamate wala hawajaona kimbunga.

Swali, mlishawahi ziona hizo mali? Au ni hadithi kama za kimbunga au samaki mtu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna ankali wangu kateseka sana na hizi mambo na hadi leo huenda bado yuko huko "mgodini", kama ni mauza uza basi itakuwa kuna namna kichwa kinavurugwa unakuwa unaamini umezikaribia mali..... Pia hapo ulivyotaja Lumbira (kama ndo ile ya Mbeya) nimesoma shule moja maeneo yale nakumbuka kuna bweni hata walimu walichangia kulivunja eti kuna mali.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu, ni hatariii.....Ngoja nikupe kisa changu kilichonipata katika hizo pilika.

Kwanza nilivutiwa na jamaa fulani hivi tukiwa Mbeya huko wilaya XYZ,jamaa walifankkiwa kuopoa sanduku la dhahabu kwa Style hyhy ya kusaka Mali za wajerumani. Walikula bata sana na hadi muda huu ni malordilofa,yaani pesa bado wanayo.

Basi bhana,nikasafiri hadi wilaya kwa wajomba zangu baada ya kujifunza Code chache ambazo wajelumani walitumia kama alama na nikagundua hivi vitu nilivionaga kwa wajomba zangu nikiwa nachunga ng'ombe milimani.

Nilipofika kwa babu,nikanyoosha msituni kwenda kuhakiki kama zile alama kwenye miti,mawe na michoro kama ipo, bahati nzuri bhana nikavikuta kama vilivyo,wala havijaharibiwa sana na waharibifu wa mazingira. Nikashauriana na vijana wa pale tukaanza utaratbu wa kuchimba.

Huku tukiendelea kukutana na code na ninazisoma vizuri na kusonga mbele,baada ya siku 6 hatimaye tukalifikia sanduku bhana....!! Tulichokiona humo......mmamaye ,nikikumbuka huwa hata sijielewagi,maana ni hatari.

Tulikutana na marehemu mzungu humo.....ashamong'onyoka kawa unga tu,sijui walimtia nini hakuoza,kawa vumbi tu na mifupa, hilo vumbi likaingia vifuani, tulikohoa karibia ya kunya......!!!!

Aisee.....tulirudi nyumbani tukatengeezwa kienyehi ndio mambo yakawa sawa, lakini kuna mzee akasema mgetoa lile sanduku ndio mgekutana na mzigo wenyewe....!! Alinistua mbaya,lakini cha ajabu,nasema tena chaa ajabu niliporudi kule porini ile sehemu sijaikuta na wala sikuiona tena hadi leo, nilienda takribani mara 6 kwa siku tofauti lakini mpaka leo sipajui eti.....!!

Kuna sehemu tena nipo ugenini,nilikwenda kucheki shamba la kununua nimekutana na code tena za ajabu aisee.....!!! Sasa sijajua nini wameficha...!!

Kwanza nilikuta Mti mkubwa una mzizi upo nje,mzizi huo umetobolewa,nikaufuatilia kidogo nikakuta tobo la pili, nikaendelea kufukua nikakuta nikakuta tena mzizi umekunjwa kuelekea direction ya kusini,nikaendelea kuufuata, mbele ya huo mzizi kulikuwa na jiwe kubwa sana kama tani 30 hivi, nilipolizoom vizuri kabisa na kulichunguza,nikagundua kuwa huyo ni picha iliyojchongwa picha ya bundi...!!!! Nikafukuafukua kuzungua hilo hiwe nikakuta ramani aisee.....!!! Bahati mbaya sijui kijerumani .

Mzee nikaazimia kazi, tukaenda kwa mchawi wetu akasema kuna mzigo wa kufa jamaa....vizuri vyote ruby,gold na sapphire akasema zipo. Akatupa masharti tukaingia mzigoni...!!

Baba tumefungua ardhi huku tukifuata masharti makamanda tulikuwa 6, tuliikosea ramani kidogo tukajikuta kuna mwamba una ninginia juu yetu.

Tulichokifikia ni kwanza kuna vigae vya mawe vimefunika kitu tusichokijua hapo chini, pili kuna ukuta umejengwa kwa mawe ya kupondekezwa hapo chini shimoni...!!

Tuliogopa kupondwa na tulikuwa tumechoka sana,maana kazi ilikuwa ya ngumu na ilituchukua miezi 3,tukasema labda tusake katapila.


Sasa tumeliacha tu na tumeamua tulime tu kwanza lakini tukiwa na matumaini kwamba ipo siku.
Sasa najiuliza,au tutakuta marehemu mzungu tena au la ....nakaribisha wadau,kama unaweza kuleta Scaveta njoo tujaribu bahati.





Sent using Jamii Forums mobile app
Duuu..mzeebaba!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nakubali mimi ni mbumbumbu Muizaeli aje na helkopta Singida kufuata pasi milioni 30 na ushee .... alikuja lini? kijiji gani? huyo "ajuza" alikuwa na nguvu ya kuchimba? alikuwa na utaalamu wa kusoma ramani? alikuwa na manguvu ya kupambana na "mauza uza" wewe ulikuwa wapi kipindi hicho?

Anyway haya ni maswali ya kimbumbumbu endelea kuamini unachokiamini lakini usiwashawishi watu waingie mkenge. BTW mbona unatumia nguvu kubwa sana kwenye hii issue? kuna ajenda nyingine?
Kakojoe ukalale,jambo usilolijua wala usihangaike nalo....waache wanaojua vitu hivi.

Kwa akili yako unadhani kila kitu ni cha kuchimba,kuna vingine waliachiwa watu, hata hizo heller,zingine wanazo wakongwe ,,,.!!

Hizi akili za darasani wakati mwingine huwafanya watu more mbumbumbu....!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kakojoe ukalale,jambo usilolijua wala usihangaike nalo....waache wanaojua vitu hivi.

Kwa akili yako unadhani kila kitu ni cha kuchimba,kuna vingine waliachiwa watu, hata hizo heller,zingine wanazo wakongwe ,,,.!!

Hizi akili za darasani wakati mwingine huwafanya watu more mbumbumbu....!!

Sent using Jamii Forums mobile app

Maswali hujajibu unasisitiza umbumbu wangu. Anyway the motion is closed na sorry kwa kuwaharibia biashara.
 
Kuna mahali huko Tanga Korogwe kijiji cha Lutindi Wajerumani wamejenga kanisa na hospitali ya vichaa.
Ukipanda huko juu kuna kilele cha mlima hao wajerumani wameweka zinga moja ya msalaba wa zege sa sijui na hapo kuna mali au vipi.
Mleta uzi kama upo tayari kunilipa ntakupeleka tukachimbe mana hali ngumu.
 
Kuna mahali huko Tanga Korogwe kijiji cha Lutindi Wajerumani wamejenga kanisa na hospitali ya vichaa.
Ukipanda huko juu kuna kilele cha mlima hao wajerumani wameweka zinga moja ya msalaba wa zege sa sijui na hapo kuna mali au vipi.
Mleta uzi kama upo tayari kunilipa ntakupeleka tukachimbe mana hali ngumu.
Ukiuchimba huo msalaba wa zege, kilichomo ndani ni kajitabu kadogo ka rangi ya njano na kijani.. Kana maneno yasomekayo "ILANI YA CCM"

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Haiwezekani Hawa wazungu mbumbumbu wa leo wakina BARICK waweze kuja kubeba mali nyingi namna hiyo ya dhahabu halafu watu kenye akili kama wajerumani wasiwe wamechukua dhahabu kutoka bongo!! Wajerumani walisomba madini mengi sana na yale ambapo yaliwashinda kubeba baada ya vita ndio hayo waliyoyaficha sehemu mbali mbali nchini.

Nakumbuka wazee wazamani wakisimulia habari hizi! Kule TUKUYU kwa mfano inasemekana wajerumani walitupa mali nyingi sana kwenye mto Kiwira sehemu moja inaitwa KIJUNGU [ sehemu hii ina kina kirefu sana]. Kuna mzee mmoja sasa marehemu inasemekana yeye alikuwa anaweza kuzama sehemu hiyo sasa sijui kama kuna mtu anaweza shuhuri hiyo hivi leo, kwani inasemekana kuzama sehemu hiyo kuna matambiko yake!!
Kaka nimefika kijungu na daraja la mungu. Nimepaona kwa macho yangu. Majo ya mto yanaingia kwenye hicho kijungu. Na kuna kijisehem cha kupita na unaambiwa shart unapopita utangulize mguu wa kushoto.

sent using [emoji85]
 
Back
Top Bottom