Pre GE2025 Wajumbe Mkutano Mkuu CCM wapitisha Rais Samia, Dkt. Mwinyi kugombea Urais 2025
Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimemteua rasmi Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kuwa mgombea wa urais kwa uchaguzi mkuu wa mwaka 2025.

Uamuzi huu wa kihistoria unaonyesha imani kubwa na matumaini makubwa ambayo CCM inayo kwa uongozi thabiti na wa kimkakati wa Rais Samia, pamoja na dhamira yake isiyotetereka ya kutekeleza Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020-2025.

Katika kipindi chake cha uongozi, Tanzania imeshuhudia mafanikio makubwa katika ukuaji wa uchumi, ujenzi wa miundombinu, maboresho ya huduma za afya, na kukuza demokrasia kupitia falsafa yake ya “4Rs.”

Akiwa Rais wa kwanza mwanamke katika historia ya Tanzania, Rais Samia si tu kwamba amevunja vikwazo vya kijinsia, bali pia ameweka viwango vipya vya uongozi shirikishi na wa maono.

Uteuzi wa CCM ni hatua muhimu ya kuhakikisha maendeleo yanayoendelea na mustakabali wa neema kwa Watanzania wote.
IMG-20250119-WA1485.jpg


#Samia2025 #TanzaniaKwanza #CCM2025 #UongoziBora
 
Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimemteua rasmi Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kuwa mgombea wa urais kwa uchaguzi mkuu wa mwaka 2025.

Uamuzi huu wa kihistoria unaonyesha imani kubwa na matumaini makubwa ambayo CCM inayo kwa uongozi thabiti na wa kimkakati wa Rais Samia, pamoja na dhamira yake isiyotetereka ya kutekeleza Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020-2025.

Katika kipindi chake cha uongozi, Tanzania imeshuhudia mafanikio makubwa katika ukuaji wa uchumi, ujenzi wa miundombinu, maboresho ya huduma za afya, na kukuza demokrasia kupitia falsafa yake ya “4Rs.”

Akiwa Rais wa kwanza mwanamke katika historia ya Tanzania, Rais Samia si tu kwamba amevunja vikwazo vya kijinsia, bali pia ameweka viwango vipya vya uongozi shirikishi na wa maono.

Uteuzi wa CCM ni hatua muhimu ya kuhakikisha maendeleo yanayoendelea na mustakabali wa neema kwa Watanzania wote.

#Samia2025 #TanzaniaKwanza #CCM2025 #UongoziBora
 

Attachments

  • IMG-20250119-WA0034.jpg
    IMG-20250119-WA0034.jpg
    111.6 KB · Views: 1
Na ili kujia kuwa walipangwa ni kwamba mtoa hoja ni kimbisa lakini naona katambuliwa mwana dada mwasi
Mbona ni mambo ya kawaida hayo CCM tunapoitaji kuchomekeza Agenda . Na kwa wale watakopinga wanapewa Nafasi yao ya kunyoosha mikono pia 😀
 
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dodoma, Adam Kimbisa amewasilisha hoja kwa mkutano mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuwa Mwenyeiti wa chama hicho, Rais Samia Suluhu Hassan awe mgombea urais wa Tanzania katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025.

Pia, Kimbisa amesema Makamu Mwenyekiti Zanzibar wa CCM, Dk Hussein Mwinyi awe mgombea urais wa Zanzibar.

Baada ya kutoa hoja hiyo leo Jumapili, Januari 19, 2025 katika kikao hicho kinachoongozwa na Rais Samia, wajumbe wote wa mkutano huo wakasimama kushangilia na kuunga mkono hoja hiyo.

Hoja kama hiyo imetolewa wakati wajumbe wa mkutano huo wakichangia taarifa za utekelezaji wa Ilani ya CCM ya mwaka 2020/25 kwa upande wa Zanzibar na Tanzania Bara.

Hoja za wachangiaji wote zinaeleza kuwa ni kutokana na ubora na ufanisi wa utekelezaji wa ilani wakisema hakuna mbadala wa wawili hao kuwania Urais.

Kikwete Azungumza na Wajumbe Kuhusu Rais Samia Kugombea Urais 2025

"Azimio liwe Rais Samia amechaguliwa kuwa mgombea Rais wa CCM 2025"

Rais mstaafu na Mwenyekiti mstaafu wa CCM, Jakaya Kikwete, alilazimika kutoa busara zake baada ya wajumbe wa mkutano mkuu maalum wa CCM kutaka kuanzisha mjadala kuhusu wagombea wa urais katika Uchaguzi Mkuu ujao kupitia chama hicho.

Katika kikao hicho, ilikubalika kuwa Rais Samia Suluhu Hassan atakuwa mgombea urais wa CCM kwa uchaguzi wa 2025, huku Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar, Dkt. Hussein Ali Mwinyi, pia akijitokeza kama mgombea mwenye nguvu.


Safi sana.Mama anaendelea kuupiga mwingi
 

𝐖𝐀𝐉𝐔𝐌𝐁𝐄 𝐖𝐀𝐏𝐈𝐓𝐈𝐒𝐇𝐀 𝐀𝐙𝐈𝐌𝐈𝐎 𝐋𝐀 𝐊𝐔𝐖𝐀𝐏𝐈𝐓𝐈𝐒𝐇𝐀 𝐃𝐊𝐓. 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐍𝐀 𝐃𝐊𝐓. 𝐌𝐖𝐈𝐍𝐘𝐈 𝐊𝐔𝐆𝐎𝐌𝐁𝐄𝐀 𝐍𝐀𝐅𝐀𝐒𝐈 𝐙𝐀 𝐔𝐑𝐀𝐈𝐒 𝐓𝐀𝐍𝐙𝐀𝐍𝐈𝐀 & 𝐙𝐀𝐍𝐙𝐈𝐁𝐀𝐑

𝑾𝒂𝒋𝒖𝒎𝒃𝒆 𝒘𝒂𝒎𝒆𝒇𝒂𝒏𝒚𝒂 𝒎𝒂𝒂𝒎𝒖𝒛𝒊 𝒉𝒂𝒚𝒐 𝒌𝒘𝒂 𝒌𝒖𝒛𝒊𝒏𝒈𝒂𝒕𝒊𝒂 𝑲𝒂𝒕𝒊𝒃𝒂 𝒚𝒂 𝑪𝑪𝑴 𝒊𝒃𝒂𝒓𝒂 𝒚𝒂 100 𝒌𝒊𝒇𝒖𝒏𝒈𝒖 𝒌𝒊𝒅𝒐𝒈𝒐 𝒄𝒉𝒂 2 𝒊𝒏𝒂𝒚𝒐𝒆𝒍𝒆𝒛𝒂 𝒌𝒖𝒘𝒂 𝑴𝒌𝒖𝒕𝒂𝒏𝒐 𝑴𝒌𝒖𝒖 𝒏𝒅𝒊𝒐 𝒌𝒊𝒌𝒂𝒐 𝒌𝒊𝒌𝒖𝒖 𝒄𝒉𝒂 𝑪𝑪𝑴 𝒄𝒉𝒆𝒏𝒚𝒆 𝒎𝒂𝒎𝒍𝒂𝒌𝒂 𝒚𝒂 𝒎𝒘𝒊𝒔𝒉𝒐

Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) wameridhia kwa kauli moja kuwapitisha Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan na Makamu Mwenyekiti wa CCM (Zanzibar) Rais wa Zanzibar Dkt. Hussein Mwinyi, kuwania tena nafasi hizo katika uchaguzi wa mwaka huu 2025.

Hayo yametokana na mapendekezo waliyoyatoa wakati wa michango yao baada ya kutazama na kusikiliza utekelezaji wa Ilani ya CCM.

Hivyo, Sekretarieti ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa imeketi na kuandaa Azimio hilo na kuwasilishwa kwa Wajumbe wa Mkutano Mkuu katika ukumbi wa JKCC Jijini Dodoma leo tarehe 19 Januari, 2025 ambapo kwa pamoja wameridhia kwa asilimia 100.

#MkutanoMkuuCCM2025
#CCMImara
#VitendoVinaSauti
#KaziIendelee
 

Attachments

  • Screenshot 2025-01-19 at 14-44-58 Instagram.png
    Screenshot 2025-01-19 at 14-44-58 Instagram.png
    851.6 KB · Views: 1
Back
Top Bottom